Mapumziko siku ya muungano, tangazo la mapumziko lililotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu haliihusu Zanzibar

SubiriJibu

JF-Expert Member
Jun 26, 2009
1,803
1,863
Hatimaye tumetangaziwa kwamba kesho ni siku ya mapumziko na tangazo lenyewe limetolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Lakini Ofisi ya Waziri Mkuu na hata cheo chenyewe cha Uwaziri Mkuu, hakijawahi kuwa mambo ya muungano.

Kulikuwa na Waziri mkuu wa Tanganyika yaani Julius Nyerere mwaka 1961 hadi Feb. 1962 kisha Rashid Kawawa toka Feb. 1962 hadi 1964.

Kule Zanzibar kulikuwa Waziri Mkuu, Mohamed Shamte toka siku ya uhuru December 1963 hadi Jan. 12, 1964.

Baadaye Kawawa akawa Waziri mkuu 1974 na kule Zanzibar mwaka 1984 kukawa na Waziri Kiongozi, Saif Sharrif Hamed.

Hivyo Uwaziri mkuu haujawahi kuwa mambo ya muungano.

Hata Sokoine hakukamata mhujumu uchumi hata mmoja kule Zanzibar.

Hivyo, hili tangazo nina mashaka asilimia nyingi kwamba halina mamlaka Zanzibar. Linaishia kisiwa cha Chumbe.

Zanzibar wanaweza kwenda kivyao. Hata wasipofanya sherehe ni kwa ajili ya utashi wao si kwa nguvu ya tangazo la Ofisi ya Waziri Mkuu.

Jadili, Sahihisha, Elewesha. Usitukane.
 
Nashangaa anaitwa "Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania"
Wakati hana power, instruments wala sauti Zanzibar.
 
Nashangaa anaitwa "Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania"
Wakati hana power, instruments wala sauti Zanzibar.
Tatizo kubwa ni Kitendo cha Bwana Mkubwa kufanya sherehe kwa jinsi anavyojisikia.

Yaani siku akifurahi.... Sherehe. Siku hajisikii.... Hakuna sherehe.
 
Hatimaye tumetangaziwa kwamba kesho ni siku ya mapumziko na tangazo lenyewe limetolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu.

Lakini Ofisi ya Waziri Mkuu na hata cheo chenyewe cha Uwaziri Mkuu, hakijawahi kuwa mambo ya muungano.

Kulikuwa na Waziri mkuu wa Tanganyika yaani Julius Nyerere mwaka 1961 hadi Feb. 1962 kisha Rashid Kawawa toka Feb. 1962 hadi 1964.

Kule Zanzibar kulikuwa Waziri Mkuu, Mohamed Shamte toka siku ya uhuru December 1963 hadi Jan. 12, 1964.

Baadaye Kawawa akawa Waziri mkuu 1974 na kule Zanzibar mwaka 1984 kukawa na Waziri Kiongozi, Saif Sharrif Hamed.

Hivyo Uwaziri mkuu haujawahi kuwa mambo ya muungano.

Hata Sokoine hakukamata mhujumu uchumi hata mmoja kule Zanzibar.

Hivyo, hili tangazo nina mashaka asilimia nyingi kwamba halina mamlaka Zanzibar. Linaishia kisiwa cha Chumbe.

Zanzibar wanaweza kwenda kivyao. Hata wasipofanya sherehe ni kwa ajili ya utashi wao si kwa nguvu ya tangazo la Ofisi ya Waziri Mkuu.

Jadili, Sahihisha, Elewesha. Usitukane.
Usihadaike wewe....waziri mkuu wa jamuhuri ya muungano anayo mamlaka mpaka Zanzibar, tena makubwa sana

Kila kiongozi anayehudumu kwenye serikali ya muungano power zake zina extend mpaka Zanzibar

Ila viongozi wanaohudumu Zanzibar power zao ni kwa Zanzibar tu
 
Back
Top Bottom