Mapokezi ya Rais Samia: Kwanini watendaji hawajaweka zulia jekundu, kiprotokali hili limekaaje?

Ukipata kiongozi wa kiislam akawa na imani japo nusu ya dini yake hawana tabu na ukamkuta mwenye dini hasa mtaishi kama mbinguni,kifupi luxurious za duniani hazijawahi kumhadaa mcha Mungu kwake maisha ya dunia ni mapito ya muda mfupi sana haoni sababu ya kukera mtu mwingine.

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app

Hivi libya Sudan kusini hakuna waislam au Somalia vipi Yemen? Acheni mambo ya ajabu bana. Mama inaweza kua hulka yake lakini sio dini ndo inasababisha hayo. Nchi za ulaya nyingi ni za kikristo na ndo zinaongoza kwa amani na usawa maisha mazuri. Nao utasema viongozi ni waislam? PASAKA NJEMA
 
Hivi libya Sudan kusini hakuna waislam au Somalia vipi Yemen? Acheni mambo ya ajabu bana. Mama inaweza kua hulka yake lakini sio dini ndo inasababisha hayo. Nchi za ulaya nyingi ni za kikristo na ndo zinaongoza kwa amani na usawa maisha mazuri. Nao utasema viongozi ni waislam? PASAKA NJEMA
Acha jazba mkuu tofautisha muislam na anayeitwa muislam,kwani hawapo waislam wanaokula kitimoto au kunywa pombe lkn dini imekataza,na hayo makundi ya wahuni huko Libya,somalia hawapo ktk misingi ya uislam na uislam haujaelekeza hivyo fuatilia kumbuka si kila mtu anaeitwa Mohammed hassan basi wametimia katika uislam wao wengine ni majina tu

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Mpigie cm umuulize.
Mbona mnawashwawashwa sana...
Mtakuja ingilia hadi ndoa ya Mama muda si mrefu.
Yaani kina watu hawana kazi bali kuleta majungu kila kukicha kwa kufuatilia umbea wa vitu visivyo wahusu

Haya hawajaweka zuria amekufa au kadhurika?

Hawa ndiyo wanaosababisha bundle zipande matako yenu
 
Tumezoea kuona viongozi wakubwa wakipokelewa kwa mazulia mekundu, kwanini kwa mama yetu haikuwa hivyo? Kiprotokali limekaaje hili wanabodi?View attachment 1742740
Inategemea na aina ya ziara, hata magu Kuna nyingi tu kulikuwa hakuna red carpet
Picha chini
Screenshot_20210404-092711_1.jpg
Screenshot_20210404-092917_1.jpg
 
Timu ya itifaki huwa pia inatazama hitaji la Rais, kama yeye ataona siyo la lazima basi huwa na wao huweka kando. Zuria jekundu ni SIFA siyo suala la lazima la kiitifaki, Mama hapendi itifaki za SIFA.
Hapana inategemea na aina ya ziara
Hata magu Kuna ambazo alikuwa haweki
Screenshot_20210404-092711_1.jpg
 
Mama si mpenda sifa za kijinga. Ni mcha Mungu na anajua yupo anayestahili sifa na utukufu. Muacheni apige kazi. Mama mitano na mitano tena.
Sio kweli, itifaki sio matakwa ya mama Samia Bali inategemea na aina ya ziara.
Zipo nyingi tu ambazo magu pia walikuwa hawaweki red carpet
Screenshot_20210404-092711_1.jpg
 
Taifa la Majuha utalijua ndio maana watu wengi wanaipenda Tanzania tunaonekana watu wa ajabu sana tunawashinda hata wale aliyenz
 
Huyo ndo Sa100 hatakagi mbota!! Rais unajaa vitisho mpaka watu wanashindwa Kuapa!!mi nlishindwa hata kumuaga!!!
Sa100 napicha yake hapa ofisini jicho tuu mtu unapata maraha mpaka nyingine nmeweka sebuleni...
 
Tumezoea kuona viongozi wakubwa wakipokelewa kwa mazulia mekundu, kwanini kwa mama yetu haikuwa hivyo? Kiprotokali limekaaje hili wanabodi?View attachment 1742740
Bado mfumo dume wa jiwe haujawatoka. Afukuze wote aanze na timu yake, wale waadilifu wanaomtii wabaki. Jiwe aliharibu kila mfumo! na individuals autuwape/wapewa time to adjust to new situations
 
Madame hana makuu wala kujikweza kweza kama washamba wengine.
Huoni hata mibunduki bunduki kaifyekelea mbali !!

Na hapendi uongo au unafik ndo maana alimwambia CAG ulimi husiwe mzito. Kama shirika bovu au zezeta sema tu husirembe wala kuogopa ...

Huyu hutamuona anagigida mahindi au kunywa alkasus hadharani... au hotuba za kila siku ktk madhabau !!
 
Ukipata kiongozi wa kiislam akawa na imani japo nusu ya dini yake hawana tabu na ukamkuta mwenye dini hasa mtaishi kama mbinguni,kifupi luxurious za duniani hazijawahi kumhadaa mcha Mungu kwake maisha ya dunia ni mapito ya muda mfupi sana haoni sababu ya kukera mtu mwingine.

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
Mkuu relis ,hii comment imenibariki sana Jumapili njema ya leo.
Hakika Kristo amefufuka kweli kweli.
Mungu akubariki.
Mungu ambariki Mh. Rais Samia Suluhu Hassan.
 
Mama asioilindwa sana mnasema mnaona mama hataki mabunduki bunduki safi sana...Akichimbia mkwara mnasema mama kumbe kama Magu tu..polisi wakisema hakuna sherehe za pasaka mnasema oohh CCM ni ile ile inayotesa na kunyanyasa watu..


Asipowekewa zulia nayo ni issue..na mnaenda mbali mpaka mnataka watendaji waulizwe kuna nini...Jameni sisi Watanzania tuna mengi sana hatueleweki wala kamwe hatutaeleweka wala kulidhika kabisa.

hivyo mama yeye afanye kazi yake tu vizuri.
 
4 Reactions
Reply
Back
Top Bottom