Mapokezi ya Kihistoria aliyoyapata Rais Samia katika ziara yake ni Uthibitisho wa Watanzania wanavyomkubali

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,071
9,478
Ndugu zangu watanzania Rais Samia amepata mapokezi ya Kihistoria, mapokezi ya kishindo, mapokezi ya aina yake, mapokezi yaliyoacha Alama ,mapokezi yaliyotikisa Kanda ya ziwa mpaka mwisho wa reli, mapokezi yaliyo isimamisha Tanzania, Mapokezi yaliyosimamisha kila kitu ,Mapokezi yaliyo tetemesha, Mapokezi yaliyowafanya watu kutimua mbio kuwahi eneo Atakapokuwa Rais ili kumsikiliza.

Mapokezi yaliyomfanya Rais Samia kujiwekea rekodi yake, kujiandikia Ukurasa wake wa Kihistoria ambao umeonyesha ukubwa wake, uzito wake, Nyota yake, mvuto wake, ushawishi wake, kukubalika Kwake na kupendwa kwake na watanzania na namna watanzania wanavyomhitaji Rais Samia Kuendelea kuwatumikia.

Hii inatokana na namna Rais Samia alivyofanya kazi kubwa na ya kutukuka yenye kugusa maisha ya watanzania ndani ya muda mfupi Sana tangia alipoapishwa kuwa Rais wetu,Rais Samia kagusa mioyo ya watanzania, kagusa kila kundi, kaweka mikono yake katika kila kundi, kaweka baraka zake kila eneo, kapelela pesa kila eneo ambako watanzania wapo, kila eneo limetazamwa na kupewa uzito wake, kila eneo limepewa mgao wa keki ya Taifa, mtanzania popote Alipo na anapojishughulisha amefikiwa na Mkono wa Rais Samia, amefikiwa na juhudi za Rais Samia kumuinua mtanzania kiuchumi

Rais Samia kawasha mwanga mahali kwenye Giza kwa kupeleka umeme.kaponya wagonjwa waliokuwa wanahangaika kupata matibabu kwa kuwajengea vituo vya Afya, kupeleka madakitari,vifaa Tiba na madawa kwa wakati. Rais Samia kaleta matumaini kwa wakulima kwa kuhakikisha mbolea zinashuka Bei na soko zuri linapatikana kwa mazao ya mkulima.

Hakuna mtoto anayekaa nyumbani bila kwenda shule kwa kuwa Hana Ada au kwa kuwa katoka familia ya kipato Cha chini maana Rais Samia kafuta Ada mpaka kidato Cha sita na kuongeza mikopo kwa Elimu ya juu, kawagusa wafanyabiashara kwa kuwawekea mazingira mazuri ya kibiashara, vijana nao vivvyo hivyo wamepewa kipaombele Cha kutosha Kama ambavyo Tumeona utoaji wa ajira serikalini Kama alivyotoa ajira zaidi ya elfu 40, japo hawezi kumaliza kuajiri vijana wote lakini juhudi zake zinaonekana katika kutoa nuru kwa vijana ikiwepo kuimarisha secta binafsi na kuvutia wawekezaji ili kusaidia kutengeneza ajira nyingi kwa vijana.

Hii ndio sababu ya mafuriko ya wananchi waliojitokeza kumlaki na kumpokea Rais wetu mpendwa mama Samia, kwa kuwa watanzania Wana imani na matumaini makubwa Sana na Rais Samia kutokana na kuwa Rais wetu Ni kiongozi wa vitendo tu na kila neno litokalo katika kinywa chake linakuwa Ni la kweli na la kuaminika, anahakikisha linatekelezwa na kuleta furaha kwa Watanzania.

Hakika Rais Samia Amejitoa na kujitolea kuwatumikia watanzania, ndio sababu unaona akifanya kazi usiku na mchana bila kupumzika, ndio sababu unamuona wakati wote yupo kutatua matatizo na kero za wananchi, wakati wote yupo kazini kuleta mwanga mahali palipo na Giza, kuleta matumaini palipo na kukata tamaaa, kuleta umoja mahali palipo na utengano, kutoa majibu kwenye maswali na kuleta maendeleo kwa Watanzania.

Usikivu wa Rais Samia umewaridhisha watanzania na kufanya wamuamini Sana na kuwa na Imani na uongozi wake, maana kila Taasisi,kila mtu na kila kundi Lina nafasi sawa katika masikio ya Rais samia, watanzania wote tunasikilizwa katika masikio ya mama Samia, sauti zote Zina nafasi kwake, ndio sababu ya kuona namna makundi yote yakimuunga mkono kumkubali na kumpenda Rais Samia,maana Hakuna anayehisi kupuuzwa Bali kila mtu, kundi au Taasisi zinaona zikisikilizwa na kuheshimiwa maoni au mawazo yake yenye lengo la kujenga Taifa letu.

Kazi iendeleee, mama Ametufikia na kuwafikia Watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti

Lucas Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
 
Hapana silipwi, lakini pia napenda kukwambia kuwa watu wanakwenda kumsikiliza Rais Samia kwa hiyari yao kutokana na upendo wao kwake uliotokana na uchapa kazi wake
Watu walienda kwenye tamasha la bongo fleva.

Hivi Samia anakulipa kumpost kila saa hapa jf?
 
Hapana silipwi, lakini pia napenda kukwambia kuwa watu wanakwenda kumsikiliza Rais Samia kwa hiyari yao kutokana na upendo wao kwake uliotokana na uchapa kazi wake
Mtu mwenye akili timamu hawezi kuacha kazi zake akamsikilize huyo Samia.
 
Mtu mwenye akili timamu hawezi kuacha kazi zake akamsikilize huyo Samia.
Ni mwenye matatizo ya kiafya ndio anaweza akakaa nyumbani bila kwenda kumsikiliza Rais Samia,lakini mwenye utimamu wa kiafya na kiakili lazima atafute namna yoyote Ile kwenda kumpokea na kumsikiliza Rais Samia
 
Back
Top Bottom