Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wajuao jinsi ya kuuandaa muhogo kwa ajili ya mapishi naomba mjitokeze kuwafundisha na wengine.
Leo niliuandaa muhogo wangu lakini aliyeula alisema umekuwa mchungu sikuuandaa vizuri
Wajuao jinsi ya kuuandaa muhogo kwa ajili ya mapishi naomba mjitokeze kuwafundisha na wengine.
Leo niliuandaa muhogo wangu lakini aliyeula alisema umekuwa mchungu sikuuandaa vizuri
Wakati mwingine inategemea na aina ya muhogo ulio tumia, baadhi ya mihogo ni michungu kiasi, hiyo si mizuri kwani kwenye mihogo ambayo ina uchungu kuna sumu ambao si nzuri kiafya. Mihogo michungu husababisha matatizo mengi ikiwemo kupata goiter, nerve-damaging disorder au ugonjwa unao itwa Konzo.
Jinsi ya kupika Muhogo:
Vipimo.
Muhogo................................. Nusu kilo
Tui La Nazi............................2 vikombe
Chumvi.....................................kiasi
Pilipili mbichi...............................2
Mafuta........................................1 kijiko moja
Kitunguu maji..............................1 kidogo
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
1. Chambua muhogo ukatekate au tumia iliyo tayari.
2. Chemsha muhogo katika sufuria kwa maji kidogo na chumvi, funika uive muhogo.
3. Karibu na kukauka maji tia tui, kitunguu maji ulichokatakata na pilipili mbichi.
4. Unaupika moto mdogo mdogo hadi ukauke tayari kuliwa na samaki au kitoweo chochote kingine.
Kama hajaelewa chukua fimbo chapa kisha rudia tena
Aaah kwa hiyo maganda nitoke kwanza
Mie nilifikiri nikiweka maganda utaungua