Khe!inamaana humu ndani hakuna mtaalamu wa hilo?mbona hamumjibu mwenzenu?Habari za kazi wanajukwaa,naomba mtu yeyote mwenye utaalamu wa kuandaa nundu kwa ajili ya msosi kwa pishi lolote lile anisaidie.
Thanx King'asti.:nod:Kutengeneza mishkaki ya nundu, ikate kama cubes. Weka kitunguu swaumu, tangawizi, chumvi na ndimu. itunge kwenye vijiti. Unaweza kuweka carrot, kitunguu kikubwa ama hoho kika baada ya nyama moja. Ziweke kwenye friji kwa muda unaowezekana hata kama ni kulaza usiku kucha. Usisahau kufunika bakuli na kitambaa ama film ya plastiki.
Choma kwenye moto mdogo huku unageuza geuza. Yaani kukuelezea tu hapa na udenda duh.
Jamani mimi nundu huipikia kwenye ndizi, kwenye supu au kuchoma kama mshkaki, ngoja nikiandaa ntakurushia picha uone mpendwa, But kwa ufupi nundu ni nyama ngumu so haihitaji haraka katika kuindaa mimi baada ya kuikatakata nailoweka kwenye tangawizi kwa dk kama 20 hivi then naiweka katikati ya ndizi ambazo nimeziandaa kwa ajili ya kupika so huwa sichemshi ili kutoa supu huiweka ikiwa mbichi,.sorry nina haraka kidogo but will be back nikupe recipe kidogo katika mojawapo ya ninavyoitumia.best of enjoyment!