Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,299
- 33,080
Mapishi ya firigisi za kuku
Mahitaji
Firigisi za kuku gramu 200, pilipili mboga moja, tangawizi gramu 5, pilipili manga gramu 2, vitunguu saumu gramu 5, mchuzi wa chaza gramu 5 Njia 1. chemsha maji, halafu weka firigisi ya kuku kwenye maji ya moto, halafu zipakue, na uziweke kwenye maji ya baridi. Kata firigiri ya kuku iwe vipande. 2. kata tangawizi, vitunguu saumu, pilipili mboga iwe vipande. 3. washa moto tia mafuta kwenye sufuria, tia vipande vya tangawizi, vitunguu saumu na pilipili manga kwenye sufuria, korogakoroga, tia firigisi za kuku kwenye sufuria, pilipili mboga, korogakoroga, mimina mchuzi wa chaza, korogakoroga. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa. |
Mapishi ya kamba-mwakaje na vitunguu saumu
Mahitaji Kamba-mwakaje gramu 500, limao moja, vitunguu saumu gramu 10, vitunguu maji gramu 5, mchuzi wa sosi vijiko viwili, mvinyo wa kupikia vijiko viwili, mafuta ya ufuta kijiko kimoja, sukari kijiko kimoja, wanga wa pilipili manga kijiko kimoja Njia 1. osha kamba-mwakaje, ondoa vichwa vyake. 2. washa moto, tia mafuta kwenye sufuria, tia vipande vya vitunguu saumu na vitunguu maji, korogakoroga, mimina juisi ya limau, mchuzi wa sosi, mvinyo wa kupikia, korogakoroga, tia wanga wa pilipili manga, sukari, mimina mafuta ya ufuta, korogakoroga, mimina maji yasiyo ya baridi, korogakoroga halafu weka kwenye kamba-mwakaje. 3. chemsha maji kwenye sufuria, weka kamba-mwakaje kwenye sufuria, chemsha kwa mvuke kwa dakika 10. mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa. Mapishi ya samaki na mafuta
|