Alwaz
JF-Expert Member
- Apr 29, 2010
- 7,055
- 10,723
Ukisoma kitabu cha KWAHERI UKOLONI KWAHERI UHURU cha mwandishi Harith Ghassany unakaribia kulia ukijua kwamba kumbe Mapinduzi ya Zanzibar si kama tunavyoyajuwa.Kwa upande mwengine kumbe uongo ni kitu kibaya sana kinacholeta maangamizi katika jamii.
Mwandishi anastahiki sifa kubwa ya kuwa mtafiti aliyebobea.Amehojiana na watu muhimu walioshiriki kuipindua serikali ya Zanzibar ambao wengi wala si wenye kusikika.
Ukisoma hiki kitabu ushahidi uko wazi kuwa mapinduzi yale yalikuwa ya chuki za kikabila na kidini na hayakufanywa na wazanzibari wenyewe.Kumbe Nyerere ndiye aliyesuka na kugharimia mapinduzi yale akikitumia chama cha TANU.
Viongozi wa mapinduzi wao wenyewe hawakujua kipi hasa kilikuwa kikiwaongoza kufanya mapinduzi,ni kumuondoa mwarabu mwenye rangi nyeupe na kumuweka mwafrika wa rangi nyeusi au ni kuwaweka watu wa bara waiongoze Zanzibar.Kauli zao na matendo ni vyenye kujichanganya.
Waliokuwa wakitawala Zanzibar walikuwa ni waislamu lakini hawakutekeleza uislamu,hili ni moja ya kosa lao kubwa.Ubwanyenye na ujinga wa kiutawala ulitoa fursa kwa maadui zao kuwapindua kirahisi.Hata hivyo nguvu ya adui aliyekuwa ndani yao na nje wasingekuwa na uwezo wa kuhimili tena.
Katika mkanganyiko huu walioathirika zaidi bila kosa ni wazanzibari waliotafsiriwa na viongozi wa mapinduzi kwamba wana asili ya kiarabu,wengi wao wakiwa wala hawako kwenye utawala.
Nyerere alipata kusema kuwa udini na ubaguzi ni kama ukoma lakini kwa hakika alitumia ukabila na ubaguzi kujenga udini.
Nyerere kwa Afrika anaweza kuitwa baba wa Mapinduzi.Yeye aliweza kuongoza Mapinduzi ya Zanzibar,akawapinduwa waislamu ndani ya TANU na hupati taabu kuona kwamba yeye alishiriki kumuua Karume kupitia kamanda wake Ali Mahfudh.Nyerere alikuwa na damu ya kimapinduzi tu lakini si kwamba mapinduzi aliyoyafanya yalikuwa yana umuhimu.
Kwa wakristo Nyerere anaweza kuonekana ni shujaa lakini kwa waislamu ni mtu mbaya mno.
Mwandishi anastahiki sifa kubwa ya kuwa mtafiti aliyebobea.Amehojiana na watu muhimu walioshiriki kuipindua serikali ya Zanzibar ambao wengi wala si wenye kusikika.
Ukisoma hiki kitabu ushahidi uko wazi kuwa mapinduzi yale yalikuwa ya chuki za kikabila na kidini na hayakufanywa na wazanzibari wenyewe.Kumbe Nyerere ndiye aliyesuka na kugharimia mapinduzi yale akikitumia chama cha TANU.
Viongozi wa mapinduzi wao wenyewe hawakujua kipi hasa kilikuwa kikiwaongoza kufanya mapinduzi,ni kumuondoa mwarabu mwenye rangi nyeupe na kumuweka mwafrika wa rangi nyeusi au ni kuwaweka watu wa bara waiongoze Zanzibar.Kauli zao na matendo ni vyenye kujichanganya.
Waliokuwa wakitawala Zanzibar walikuwa ni waislamu lakini hawakutekeleza uislamu,hili ni moja ya kosa lao kubwa.Ubwanyenye na ujinga wa kiutawala ulitoa fursa kwa maadui zao kuwapindua kirahisi.Hata hivyo nguvu ya adui aliyekuwa ndani yao na nje wasingekuwa na uwezo wa kuhimili tena.
Katika mkanganyiko huu walioathirika zaidi bila kosa ni wazanzibari waliotafsiriwa na viongozi wa mapinduzi kwamba wana asili ya kiarabu,wengi wao wakiwa wala hawako kwenye utawala.
Nyerere alipata kusema kuwa udini na ubaguzi ni kama ukoma lakini kwa hakika alitumia ukabila na ubaguzi kujenga udini.
Nyerere kwa Afrika anaweza kuitwa baba wa Mapinduzi.Yeye aliweza kuongoza Mapinduzi ya Zanzibar,akawapinduwa waislamu ndani ya TANU na hupati taabu kuona kwamba yeye alishiriki kumuua Karume kupitia kamanda wake Ali Mahfudh.Nyerere alikuwa na damu ya kimapinduzi tu lakini si kwamba mapinduzi aliyoyafanya yalikuwa yana umuhimu.
Kwa wakristo Nyerere anaweza kuonekana ni shujaa lakini kwa waislamu ni mtu mbaya mno.