Mapinduzi ya Zanzibar: Mchango wa John Okello (Che Guevara wa Afrika Mashariki) umefutwaje?

IFIKE WAKATI WAZANZIBARI NA WAPEMBA WAMTAMBUE RASMI BABA WA TAIFA LA ZANZIBAR NDUGU, JOHN OKELO.
BILA KUFANYA HIVYO, LAANA YA KUTUMIKA NA TANGANYIKA KUBAGUANA NA KUTAFUTA MADARAKA KWA GHARAMA YA KUIANGAAMIZA NCHI YAO ITAENDELEA KUWAANDAMA MILELE
 
IFIKE WAKATI WAZANZIBARI NA WAPEMBA WAMTAMBUE RASMI BABA WA TAIFA LA ZANZIBAR NDUGU, JOHN OKELO.
BILA KUFANYA HIVYO, LAANA YA KUTUMIKA NA TANGANYIKA KUBAGUANA NA KUTAFUTA MADARAKA KWA GHARAMA YA KUIANGAAMIZA NCHI YAO ITAENDELEA KUWAANDAMA MILELE

Ubaba wake ukuepo kwa misingi ipi?
 
John Okello ambaye aliongoza Mapinduzi ya Zanzibar alizaliwa mwaka 1937 huko Uganda katika kabila la Langi ambalo pia ni la Rais wa Zamani wa Uganda Milton Obotte. Alizaliwa akiitwa John Gideon Etuku. Wazazi wake walifariki Akiwa bado mdogo na kulazimika kwenda kulelewa na mjomba wake pamoja na wadogo zake wawili lakini kutokana na utukutu wake hakuweza kuishi kwa mjomba sababu alikuwa akipigwa na akakimbia kwenda kuanza vibarua huko Soroti katika Gineri ya kuchambua pamba. Inasemekana alitaka kwenda kujiunga na jeshi lakini hakufanikiwa kutokana na umri mdogo.


Katika harakati za kutafuta maisha alifika hadi Nairobi nchini Kenya na kuendelea hadi Mombasa ambapo alikuwa ukifanya kazi za vibarua. Alichukia kiuitwa boy , mtumishi, au mtumwa . Mwaka 1955 aliwekwa gerezani huko na akiwa humo alikutana na wapiganaji wa maumau waliokuwa wakipinga Ukoloni nchini Kenya kutoka kwao alipata hamasa ya Kupambana na ukoloni na ukandamizaji.


Mwaka 1959 akiwa na rafiki yake Mluo walienda Pemba katika eneo la Vitongoji na akawa anafanya kazi ya kugonga na kuuza mawe. Huko alipendwa na kuwa na ushawishi na ndipo alipoanza kuonesha nia yake ya kuuondoa utawala wa Sultan. Wakati anaondoka Pemba alipatia chama cha ASP nyumba yake ili waifanye ofisi ya chama.


Mwaka 1963 alihamia Unguja na kuanza kufanya kazi za kupaka rangi nyumba pamoja na kufanya kazi katika kiwanda cha kuoka mikate na akaendelea na vuguvugu la kisiasa.

Kumekuwa na Tetesi kuwa aliwahi kuwa mwanajeshi na askari polisi na askari wa Mau mau lakini pia kuwa aliwahi kupigana wakati wa vita vya pili vya Dunia, dhana zote hizo si za kweli. Ukweli ni kuwa Okello hakuwahi kuwa mwanajeshi au kupata mafunzo ya kijeshi. Majigambo yake kuwa alikuwa na uzoefu wa kijeshi yalikuwa ni mbinu tu ya kumsaidia kuongoza mapinduzi


Alifanikiwa kuanzisha chama cha Mafundi rangi wa Unguja na Pemba na kupitia chama hicho aliweza kupenyeza ushawishi wake wa kufanya mabadiliko ya kumuondoa Sultan


Baada ya kufanikisha Mapinduzi aalimkaribisha Karume kuongoza serikali. Tatizo la Okello hakuwa na back up ya kisiasa na hakuweza kuaminika. Akatupwa na kufukuzwa bila shukrani. Mwanzoni alipelekwa Kenya lakini akafanya jitihada za kutaka kurudi nchini akakamatwa Mwanza na kufungwa. Lakini baadae akarudi Uganda.


Wakati Idd Amini alipompindua Obotte mwaka 1972 alikwenda kumpongeza. Lakini baadae akawa na Mawasiliano na kundi la Obotte lililokuwa Tanzania, katika harakati za kutaka kujiunga na kundi hilo alikamatwa na kuuwawa na Idd Amin.


Kwa hiyo tunaona kuwa Okello alikuwa Mwanamapinduzi. Kuongoza na kushiriki Mapinduzi ya Zanzibar haikuwa kwa ajili ya Mshahara, bali ilitokana na nia yake ya dhati ya kupinga ukoloni na ukandamizaji.





Sent using Jamii Forums mobile app
 
John Okello ambaye aliongoza Mapinduzi ya Zanzibar alizaliwa mwaka 1937 huko Uganda katika kabila la Langi ambalo pia ni la Rais wa Zamani wa Uganda Milton Obotte. Alizaliwa akiitwa John Gideon Etuku. Wazazi wake walifariki Akiwa bado mdogo na kulazimika kwenda kulelewa na mjomba wake pamoja na wadogo zake wawili lakini kutokana na utukutu wake hakuweza kuishi kwa mjomba sababu alikuwa akipigwa na akakimbia kwenda kuanza vibarua huko Soroti katika Gineri ya kuchambua pamba. Inasemekana alitaka kwenda kujiunga na jeshi lakini hakufanikiwa kutokana na umri mdogo.


Katika harakati za kutafuta maisha alifika hadi Nairobi nchini Kenya na kuendelea hadi Mombasa ambapo alikuwa ukifanya kazi za vibarua. Alichukia kiuitwa boy , mtumishi, au mtumwa . Mwaka 1955 aliwekwa gerezani huko na akiwa humo alikutana na wapiganaji wa maumau waliokuwa wakipinga Ukoloni nchini Kenya kutoka kwao alipata hamasa ya Kupambana na ukoloni na ukandamizaji.


Mwaka 1959 akiwa na rafiki yake Mluo walienda Pemba katika eneo la Vitongoji na akawa anafanya kazi ya kugonga na kuuza mawe. Huko alipendwa na kuwa na ushawishi na ndipo alipoanza kuonesha nia yake ya kuuondoa utawala wa Sultan. Wakati anaondoka Pemba alipatia chama cha ASP nyumba yake ili waifanye ofisi ya chama.


Mwaka 1963 alihamia Unguja na kuanza kufanya kazi za kupaka rangi nyumba pamoja na kufanya kazi katika kiwanda cha kuoka mikate na akaendelea na vuguvugu la kisiasa.

Kumekuwa na Tetesi kuwa aliwahi kuwa mwanajeshi na askari polisi na askari wa Mau mau lakini pia kuwa aliwahi kupigana wakati wa vita vya pili vya Dunia, dhana zote hizo si za kweli. Ukweli ni kuwa Okello hakuwahi kuwa mwanajeshi au kupata mafunzo ya kijeshi. Majigambo yake kuwa alikuwa na uzoefu wa kijeshi yalikuwa ni mbinu tu ya kumsaidia kuongoza mapinduzi


Alifanikiwa kuanzisha chama cha Mafundi rangi wa Unguja na Pemba na kupitia chama hicho aliweza kupenyeza ushawishi wake wa kufanya mabadiliko ya kumuondoa Sultan


Baada ya kufanikisha Mapinduzi aalimkaribisha Karume kuongoza serikali. Tatizo la Okello hakuwa na back up ya kisiasa na hakuweza kuaminika. Akatupwa na kufukuzwa bila shukrani. Mwanzoni alipelekwa Kenya lakini akafanya jitihada za kutaka kurudi nchini akakamatwa Mwanza na kufungwa. Lakini baadae akarudi Uganda.


Wakati Idd Amini alipompindua Obotte mwaka 1972 alikwenda kumpongeza. Lakini baadae akawa na Mawasiliano na kundi la Obotte lililokuwa Tanzania, katika harakati za kutaka kujiunga na kundi hilo alikamatwa na kuuwawa na Idd Amin.


Kwa hiyo tunaona kuwa Okello alikuwa Mwanamapinduzi. Kuongoza na kushiriki Mapinduzi ya Zanzibar haikuwa kwa ajili ya Mshahara, bali ilitokana na nia yake ya dhati ya kupinga ukoloni na ukandamizaji.





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu katika Concept ya Historiography of African History yaani jinsi historia ya Africa ilivyo andikwa kuna Theory Nyingi zilitumika kuandika historia ya Africa miongoni mwazo ni

"The Great Man Theory "
Kwa mujibu wa theory hii inasema kwamba historia huwekwa na Mashujaa au Viongozi na hao ndio wanaitwa Makers of History

Kwaiyo kwa mujibu wa Nadharia hii ni kwamba atakaye zingatiwa kuwa ndiyo aliyefanikisha mapinduzi ya Zanzibar ( ZNZ Revolution ) ni Rais Karume na wala sio Okello

Kwaiyo kwenye Vitabu vingi vya historia utakuta Karume ndiye anayetambulika kama Mfanikishaji wa Mapinduzi ya Zanzibar

Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu karume hakua na role yoyote kwenye mapinduzi yale.
 
John Okello ambaye aliongoza Mapinduzi ya Zanzibar alizaliwa mwaka 1937 huko Uganda katika kabila la Langi ambalo pia ni la Rais wa Zamani wa Uganda Milton Obotte. Alizaliwa akiitwa John Gideon Etuku. Wazazi wake walifariki Akiwa bado mdogo na kulazimika kwenda kulelewa na mjomba wake pamoja na wadogo zake wawili lakini kutokana na utukutu wake hakuweza kuishi kwa mjomba sababu alikuwa akipigwa na akakimbia kwenda kuanza vibarua huko Soroti katika Gineri ya kuchambua pamba. Inasemekana alitaka kwenda kujiunga na jeshi lakini hakufanikiwa kutokana na umri mdogo.


Katika harakati za kutafuta maisha alifika hadi Nairobi nchini Kenya na kuendelea hadi Mombasa ambapo alikuwa ukifanya kazi za vibarua. Alichukia kiuitwa boy , mtumishi, au mtumwa . Mwaka 1955 aliwekwa gerezani huko na akiwa humo alikutana na wapiganaji wa maumau waliokuwa wakipinga Ukoloni nchini Kenya kutoka kwao alipata hamasa ya Kupambana na ukoloni na ukandamizaji.


Mwaka 1959 akiwa na rafiki yake Mluo walienda Pemba katika eneo la Vitongoji na akawa anafanya kazi ya kugonga na kuuza mawe. Huko alipendwa na kuwa na ushawishi na ndipo alipoanza kuonesha nia yake ya kuuondoa utawala wa Sultan. Wakati anaondoka Pemba alipatia chama cha ASP nyumba yake ili waifanye ofisi ya chama.


Mwaka 1963 alihamia Unguja na kuanza kufanya kazi za kupaka rangi nyumba pamoja na kufanya kazi katika kiwanda cha kuoka mikate na akaendelea na vuguvugu la kisiasa.

Kumekuwa na Tetesi kuwa aliwahi kuwa mwanajeshi na askari polisi na askari wa Mau mau lakini pia kuwa aliwahi kupigana wakati wa vita vya pili vya Dunia, dhana zote hizo si za kweli. Ukweli ni kuwa Okello hakuwahi kuwa mwanajeshi au kupata mafunzo ya kijeshi. Majigambo yake kuwa alikuwa na uzoefu wa kijeshi yalikuwa ni mbinu tu ya kumsaidia kuongoza mapinduzi


Alifanikiwa kuanzisha chama cha Mafundi rangi wa Unguja na Pemba na kupitia chama hicho aliweza kupenyeza ushawishi wake wa kufanya mabadiliko ya kumuondoa Sultan


Baada ya kufanikisha Mapinduzi aalimkaribisha Karume kuongoza serikali. Tatizo la Okello hakuwa na back up ya kisiasa na hakuweza kuaminika. Akatupwa na kufukuzwa bila shukrani. Mwanzoni alipelekwa Kenya lakini akafanya jitihada za kutaka kurudi nchini akakamatwa Mwanza na kufungwa. Lakini baadae akarudi Uganda.


Wakati Idd Amini alipompindua Obotte mwaka 1972 alikwenda kumpongeza. Lakini baadae akawa na Mawasiliano na kundi la Obotte lililokuwa Tanzania, katika harakati za kutaka kujiunga na kundi hilo alikamatwa na kuuwawa na Idd Amin.


Kwa hiyo tunaona kuwa Okello alikuwa Mwanamapinduzi. Kuongoza na kushiriki Mapinduzi ya Zanzibar haikuwa kwa ajili ya Mshahara, bali ilitokana na nia yake ya dhati ya kupinga ukoloni na ukandamizaji.





Sent using Jamii Forums mobile app

Mkuu hiyo hadithi umeipata wapi? alihamia Unguja 1963 na ndani ya mwaka alifanya mapinduzi. Unafikiria mapinduzi ni jambo la masihara ?
 
maprofessa mahiri wetu mko wapi kwa historia ya kweli,upo wapi haroub othman,proffesa mazrui, baregu na wengine tele wasomi..wanazuoni.

Historia ya mataifa yetu hapa afrika mashariki imepindishwa ,andileni upya.....
kwa nini tunawafundisha watoto ...uwongo..
Hata wakiandika ukweli ulivyo, hautakubalika bado. Lakini ukweli madaraka ndivyo yanavyopatikana. Madaraka ni kama kupata dhahabu au almasi kule mgodini. Ukipata madini hayo halafu uzubaa kidogo watu wenye hila wapo pale watakupora tu pengine hata kupoteza maisha yako. Ndivyo ilivyo kuwa kwa field marshal huyo wa enzi hizo. Hata kwao Uganda, kaburi au taarifa za kifo chake hazipo wazi.
 
maana kuna watu kibao walikuwa mashujaa wa Tanzania waliachwa ka kusudi wakati wanaandika historia sasa hizi kelele za Okello naona haziishi

Iweje watu kama akina Suedi Kagasheki na Dosa Aziz wasipewe kipaumbele wakati Okello mnataka kumfanya Mungu Mtu?

charity begins at home na tunao our sons and daughters ambao walipigania na kumwaga damu zao pale lakini husikii kitu
Kagasheki??? ni nani tena. alifanya nini?
 
Gy
kuna nini hpo sasa
View attachment 458696
“UNGUJA iliipindua Serikali ya Sultani kibaraka, kwa marungu mama, kwa mapanga mama, mwisho wake wakafaulu.”

Kwenye miaka ya 1960 na 1970 ilikuwa ni rahisi kusikia nyimbo za kumbukizi la Mapinduzi ya Zanzibar ambayo leo Januari 12, yanatimiza miaka 53.

Mapinduzi hayo ambayo yalijumuisha mambo mengi baadhi yakiwa kwenye kumbukumbu rasmi za kihistoria lakini baadhi yamekuwa yanawekwa pembezoni na hivyo uelewa juu yake kuwa wa juu juu.

Miongoni mwa mambo hayo ni kukosekana kutajwa au kukumbukwa kwa mshiriki mmojawapo kwenye Mapinduzi hayo hali inayoonesha kugubikwa na mwangwi wa kibaguzi ndani ya kumbukumbu za tukio hilo muhimu ambalo limekuwa linaelezwa kuwa ndio chimbuko la kuondoa utumwa na utwana.

Ambaye anaonekana kuwekwa pembeni ni Field Marshal John Okello ambaye kwenye kumbukumbu za kihistoria inaelezwa kuwa aliingia Zanzibar mwaka 1963 na kuwa na mawasiliano na viongozi wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Afro-Shirazi (ASP).

Vijana hao wa ASP inaelezwa kuwa wakiwa wanapanga mbinu za kuuondoa utawala wa Waarabu, Okello kwa upande wake akiwa mwanachama wa chama cha wapiga rangi – akiwa anapaka rangi majumba mbalimbali, katika muda wake wa ziada aliunda kikundi kidogo cha askari wa Kiafrika.

Kikundi hiki cha kijeshi kilishika na kufuata amri alizozitoa Okello kama kiongozi ambazo ni pamoja na kutojihusisha na masuala ya ngono, kutokula nyama mbichi na kutokunywa pombe.

Inaelezwa kuwa Okello alikuwa muumini mzuri wa dini na aliamini kuwa alipewa amri hizo na Mungu akiwa kwenye ndoto ili aweze kuuondoa utawala wa mabavu wa Waarabu na kuanzisha Serikali ya Mapinduzi ya Unguja na Pemba.

Hali kadhalika inaelezwa kuwa usiku mmoja kabla ya Mapinduzi hayo, Okello aliwaamuru watu wake kuua vijana wote wa Kiarabu waliokuwa na umri kati ya miaka 18 na 25, lakini wasiwadhuru wajawazito na wazee na pia wasifanye ubakaji.

Januari 12, 1964 inaelezwa Okello na kikosi chake waliingia Mji Mkongwe, Zanzibar, maskani ya Sultani, lakini Sultani mwenyewe alikuwa ameshakimbilia mafichoni nchini Uingereza.

Hata hivyo baada ya kufanikiwa kwa Mapinduzi hayo, Okello alitangaza Baraza la Mapinduzi na Sheikh Abeid Amani Karume kuwa Rais. Kiongozi wa Chama cha Umma, Abdulrahman Mohamed Babu, akawa Waziri Mkuu. Baadaye alikuwa Makamu wa Rais.

Sheikh Karume na Babu hawakuwa wamejulishwa kuhusu Mapinduzi hayo ya kijeshi kwani wote walikuwa Tanganyika, lakini walirudi Zanzibar walikokaribishwa na Okello.

Lakini pamoja na shughuli yote aliyoifanya si Karume wala Babu waliomhitaji tena. Okello aliondoka kuelekea Tanganyika na kuanzia wakati huo alizuiwa kurudi Zanzibar na alipigwa marufuku pia asionekane Tanganyika na Kenya.

Hatimaye inaelezwa kuwa alirudi kwao mara ya mwisho alionekana akiwa na kiongozi wa Uganda Idd Amin Dada mwaka 1971 na baadaye alipotea.

Katika kitabu cha ‘Revolution on Zanzibar’ kilichoandikwa na Don Petterson inadhaniwa kuwa Idd Amin alimwona Okello kuwa ni tishio kwake na mara nyingine inaelezwa kuwa baada ya Amin kujipandisha cheo na kuwa Filed Marshal, inaelezwa kuwa Okello alisema kwa dhihaka, “Uganda hivi sasa ina Field Marshal wawili.

Hata hivyo inaelezwa kuwa Idd Amini alipanga mipango ya mauaji dhidi ya Okello, lakini pamoja na hali hiyo kifo chake kimebakia kuwa ni cha utata.

Wapo waliofanya mambo yanayofanana na Okello. Mfano Ernesto Guevara de la Serna maarufu kama Che Guevara, aliyeshiriki kikamilifu kwenye Mapinduzi ya Cuba akiwa ni raia wa Argentina.

Wapo wanaomuona Okello kuwa ni kama askari wa kukodiwa na siku zote askari wa aina hiyo wakimaliza kazi waliyolipwa kufanya huondoshwa haraka.

Yanaweza kuwapo mawazo mengi kinzani kuhusu Mapinduzi lakini yalikuwa muhimu ili kuleta uwiano wa maendeleo kwa jamii ya Zanzibar ndio maana siku zote kauli mbiu mama imekuwa “Mapinduzi Daima.”

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kikubwa ni shinikizo kutoka jumuiya za kiwataifa na mashirika mbalimbali ya haki za kibinadamu, wanadai kuwa ule ulikuwa ni unyama (genocide) dhidi ya wanawake watoto na wazee wa kiarabu hasa wenye asili ya Oman, maana watu wenye asili ya Uajemi wawakuguswa hata kidogo.

Wengi waliuwa cold blooded yani unaambiwa walikuwa wanapanga mstari msururu mrefu na wote wanauwawa kwa upanga maana hata risasi zilikuwa chache yaani kifupi yale yalikuwa mapinduzi ya mapanga

Makaburi ya watu wengi(mass grave's) yalitapakaa maana ilikuwa ni ngumu kuzika watu wote kwa muda huo mfupi, sasa kutokana na pressure za media ndio kina Karume wakamrushia mpira Okelo na wao kwa kukwepa mkono wa jumuiya hizo za kibinadam wakaamua kujificha nyuma ya mgongo wa kaka mkubwa Tanganyika,

Na wao ndio waliomshinikiza mkapitalisti Nyerere aliolesoma Marekani na Ulaya na Missionary schools za haohao makapitalisti kugeukia upande wa wakomunisti chini ya uangalizi wa Abrahaman Babu(huyu jamaa unaambiwa ni hatari kuliko hata huyo Okelo mliemtia umaridadi)

Vitu vingi juu ya historia ya mapinduzi ya Zanziba havipo wazi, yani unaambiwa Okelo alikuja akadai ametumwa na Mungu cjui yesu kwenye nchi ambayo 99% ni waislam na kufanikiwa kupata sapoti ya wazawa bado haiingii akilini hata kidogo,


Kuna kitabu alikuwa nacho mwalimu wangu wa historia zamani hizo sidhani kama nnaweza kukipata nikiweke hapa, ila kuna documentary iliokwenye mfumo wa video ilirekodiwa na muitaliano mmoja akiwa kwenye helicopter inaonesha watu wanapanga mstari kwenda kuuliwa na pia inaonesha makaburi ya watu wengi na kuna mizoga ya watu wengine baharini wakijaribu kutoroka kwa kuogelea







Mwka 1964 siku thelathini baada ya uhuru wa bandia wa Zanzibar, wanamapinduzi kumi na nne wakiongozwa na mpigania uhuru John Okello aliwaongoza kwenye mapinduzi ya Zanzibar yaliyokuwa na umwagaji mkubwa wa damu.

Baada ya mapinduzi kufanikiwa John Okello [kiongozi wa mapinduzi] alichukua jukumu la kutangaza mapinduzi kwenye radio Zanzibar, ikumbukwe pia wakati mapambano yakiendelea ..aliyekuja kuwa rais wa Zanzibar mzee Karume na Babu walikuwa mafichoni na hawakushika wala bisibisi kwenye mapinduzi na hata ukiangalia ile picha ya wanamapinduzi ya kwanza John Okello amevalia kipolisi na amekaa kama kiongozi rasmi.

Baada ya hali kutulia Okello anamtangaza Karume rais na Abdulrahman Babu kuwa Waziri mkuu. Na ndie aliyeenda kumpokea Karume kutoka alikokuwa amejificha kwa siku kadhaa.

Baada ya siku chache mzee Karume akamfukuza Zanzibar kama mbwa John Okello [Field Marshal] na bila kujali mchango wake anatokomea kusikojulikana na historiaa ya mapinduzi ikafutwa na nafasi ya Okello ikaja kuwa mkwezi, mpiga tofali ambaye alibahatika kupiga picha [akiwa amekaa kitini katikati tu kwa sababu ya kuwa na kipaji cha kuongea - (kumbuka kuwa hata kiswahili chake kilikuwa 0kibovu)]

Naomba kuchokoza mada kuhusu nafasi ya John Okello kwenye mapinduzi, kwa nini historia ilifunikwa?

Je aliishia wapi,..wapenda historia ya kweli wameshatamani hata kujua lilipo kaburi lake..kumbukeni wenzetu Kenya baada ya kugundua hila wanahaha kutafuta kaburi la Field Marshal Dedan Kimathi...mbona wapenda hitoria Zanzibar na Tanganyika kwa jumla hamumtendei haki JOHN OKELLO [FIELDMASHAL]?

==============



Video ikimwonesha Okello,Karume na Babu masaa machache baada ya Mapinduzi

 
sasa kipindi ambacho nyie mnataka akina John Okello waandikwe kama mashujaa wa mapinduzi wao watu wa haki za kibinadamu wanataka hao mashujaa wenu wajulikane kama wahalifu wa kivita sasa sijui mna compensation ya kuwalipa hao warab wa Oman
 
Back
Top Bottom