Mkuu Gsana, wewe ulimsikia kwa masikio yako mwenyewe Mama Fatma Karume akiongea hayo?.Fatma,mama Karume ameeleza kuwa wakati wamelala na Mzee karume alikuwa akisikia risasi nje na wao hawakuwa na taarifa yoyote ya mapinduzi na wala Karume hakujua mapinduzi yatakuwa lini,lakini mpango wa kupindua ulikuwepo pia naye Karume alikuwa anajua kuwa siku moja yatakuwepo.
Mama Karume kaeleza mengi sana yanayoonesha kuwa Karume hakuhusika,ila baada ya mapinduzi kuna watu walifika kwa karume wakiwa na gari ya kijani na nyingine ya manjano walikuwa wamefunga shoka juu ndo walipofika kwa karume na kupitia mlango wa nyuma waligonga mlango na mama karume alipofungua mlango aliona sura ambazo hakuzikariri wala hakuziona tena,walifika wakasema wanamtaka mzee na kisha waliondoka nae baada ya kukamilisha mapinduzi! Nadhani mama amemaliza utata uliokuwepo hapa Jamvini.
OKELO ALIRUDI KWAO UGANDA NA KUFIA HUKO KWA WACHOLI WENZAKE, NYERER ALIMZAWADIA GARI NA PESA ZA MAFUTA ILI ARUDI NYUMBANI SALAMA ,LAKINI ALIPATA AJALI NJIANI NA AKANUSURIKA KUFA ILA GARI IKAWA RIGHT OFF,HAPO AKALA BODA KWA MABASI HADI ACHOLI.
Tafuta vizuri,waacholi wako Ugandaokelo alikua mkenya
sawa sawaKwadwo. Unataka watu wa Unguja na watu wa Pemba wamtambuwe Okello? Okello hakutambuliwa na ASP wala TANU leo atatambuliwa na Wazanzibari. Hebu nioneshe wapi alipotajwa na vyama hivyo kwamba yeye ndie shujaa. Okello alikua mdini na ndio kilichomponza eti anasema kwamba kapindua kwaajili ya Ukristo?.
ev uyu chegevara nimtu ainagan mwalabu mcyopia auPhilemon umesema ukweli,
Historia ya Tanzania imekuwa na tabia ya kufuta michango ya wale ambao hawakupendwa na wakubwa: John Okello akiwa mmoja wao.
Ingawa sijasoma maandiko yaliyopo kuhusu historia ya Tanzania kwa muda mrefu ukweli wa kuwa majina kama ya Okello, Kambona, na Kanali Mahafudhi yamefutika kabisa katika historia ya Tanzania. Bibi Titi Mohammed alipata bahati baada ya kurudi CCM na hivyo kurudisha jina lake katika historia lakini nalo lilikuwa limeshapotea.
Tutafute utaratibu wa kutunza historia kamilifu ya nchi bila kujali uhusiano wa wahusika na "ukoo wa mfalme" ulikuwaje.
Kumbe?Kwadwo. Unataka watu wa Unguja na watu wa Pemba wamtambuwe Okello? Okello hakutambuliwa na ASP wala TANU leo atatambuliwa na Wazanzibari. Hebu nioneshe wapi alipotajwa na vyama hivyo kwamba yeye ndie shujaa. Okello alikua mdini na ndio kilichomponza eti anasema kwamba kapindua kwaajili ya Ukristo?.
OKELO ALIRUDI KWAO UGANDA NA KUFIA HUKO KWA WACHOLI WENZAKE, NYERER ALIMZAWADIA GARI NA PESA ZA MAFUTA ILI ARUDI NYUMBANI SALAMA ,LAKINI ALIPATA AJALI NJIANI NA AKANUSURIKA KUFA ILA GARI IKAWA RIGHT OFF,HAPO AKALA BODA KWA MABASI HADI ACHOLI.
Phillemon,
Tafuta kile kitabu aliandika Okello juu ya mapinduziya Zanzibar. Utaanza kujiuliza Karume alikuwa na role gani pale. Pia ya kusikitisha zaidi, alipofukuzwa Zanzibar hakuruhusiwa hata kuchukua mizigo yake--achilia mbali malipo/compesation yake.
Kikubwa ni shinikizo kutoka jumuiya za kiwataifa na mashirika mbalimbali ya haki za kibinadamu, wanadai kuwa ule ulikuwa ni unyama (genocide) dhidi ya wanawake watoto na wazee wa kiarabu hasa wenye asili ya Oman, maana watu wenye asili ya Uajemi wawakuguswa hata kidogo.
Wengi waliuwa cold blooded yani unaambiwa walikuwa wanapanga mstari msururu mrefu na wote wanauwawa kwa upanga maana hata risasi zilikuwa chache yaani kifupi yale yalikuwa mapinduzi ya mapanga
Makaburi ya watu wengi(mass grave's) yalitapakaa maana ilikuwa ni ngumu kuzika watu wote kwa muda huo mfupi, sasa kutokana na pressure za media ndio kina Karume wakamrushia mpira Okelo na wao kwa kukwepa mkono wa jumuiya hizo za kibinadam wakaamua kujificha nyuma ya mgongo wa kaka mkubwa Tanganyika,
Na wao ndio waliomshinikiza mkapitalisti Nyerere aliolesoma Marekani na Ulaya na Missionary schools za haohao makapitalisti kugeukia upande wa wakomunisti chini ya uangalizi wa Abrahaman Babu(huyu jamaa unaambiwa ni hatari kuliko hata huyo Okelo mliemtia umaridadi)
Vitu vingi juu ya historia ya mapinduzi ya Zanziba havipo wazi, yani unaambiwa Okelo alikuja akadai ametumwa na Mungu cjui yesu kwenye nchi ambayo 99% ni waislam na kufanikiwa kupata sapoti ya wazawa bado haiingii akilini hata kidogo,
Kuna kitabu alikuwa nacho mwalimu wangu wa historia zamani hizo sidhani kama nnaweza kukipata nikiweke hapa, ila kuna documentary iliokwenye mfumo wa video ilirekodiwa na muitaliano mmoja akiwa kwenye helicopter inaonesha watu wanapanga mstari kwenda kuuliwa na pia inaonesha makaburi ya watu wengi na kuna mizoga ya watu wengine baharini wakijaribu kutoroka kwa kuogelea
OKELLO BABA WA TAIFA LA ZANZIBAR .ALIYEWAOKOA WAZANZIBAR TOKA ITUMWANI NA BADO HAWAMTAMBUI.