Waungwana,
Hii habari ikoje? Naona inaniogopesha, nani wanagharamia ujenzi wa hiyo reli? Mbona inaonekana kama hao Wazungu ndio wame initiate hii project?
Tuangalie, tusije tukaibiwa kama kwenye umeme. naomba wenye taarifa zaidi tusaidieni hii project ikoje? Idea yenyewe nimeipenda mno ila tu ninahisi kunaweza kuwa na mafisi yanatuzengea tena.
na Mwandishi Wetu
UJENZI wa reli itakayounganisha mji wa Isaka nchini na mji mkuu wa Rwanda, Kigali, umepangwa kuanza mwakani, Rais Jakaya Kikwete alielezwa jana.
Ujenzi wa reli hiyo ni moja ya mikakati ya kuboresha miundombinu nchini ambayo itahusisha pia ukarabati mkubwa katika njia nyingine za reli, ikiwemo Reli ya Kati.
Ujumbe wa Kampuni ya Barlington Northern Santa Fe (BNSF) kutoka Marekani, ambayo ndiyo itakayofanya kazi hiyo, ulimweleza Rais Kikwete kuwa ujenzi huo unatarajiwa kukamilika mwaka 2013.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu jana, ilieleza kuwa ujumbe huo pia ulimwambia rais kuwa kazi ya ujenzi wa reli hiyo mpya, utakwenda sambamba na matengenezo makubwa na upanuzi wa Reli ya Kati, kati ya Isaka na Dar es Salaam.
Upanuzi huo utalenga kuiwezesha Reli ya Kati kufikia kiwango cha kimataifa cha reli, kuongeza nguvu ya reli hiyo kuweza kubeba mabehewa zaidi, na kubeba mizigo mikubwa zaidi na kupunguza muda wa safari, ilisema taarifa hiyo ya Ikulu.
Katika mazungumzo kati ya ujumbe huo na Rais Kikwete, yaliyofanyika Ikulu, ujumbe huo pia ulimwambia kuwa maandalizi yote muhimu kwa ajili ya ujenzi wa reli kati ya Isaka na Kigali karibu yanakamilika.
Ujumbe huo uliwajumuisha Daniel Cooper na mshirika wake, Tom Vegh, kutoka kampuni ya masuala ya fedha ya Fox River Financial Resources, ambayo inahusika na masuala ya fedha kwa ajili ya ujenzi wa reli hiyo, pamoja na John Orrison kutoka Kampuni ya BNFS.
Mazungumzo hayo pia yalihudhuriwa na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge na Waziri wa Mipango, Uchumi na Uwezeshaji, Dk. Juma Ngasongwa.
Wakati maandalizi yanaendelea kwa ajili ya ujenzi wa reli ya Isaka-Kigali, na upanuzi wa Reli ya Kati, maandalizi pia yanafanyika kwa ajili ya kuangalia uwezekano wa ujenzi wa reli kati ya Isaka-Kigali-Bujumbura.
Mbali na hiyo, mipango pia inaandaliwa na kuangalia uwezekano wa kuunganisha Isaka na mji wa Mwanza, na kuunganisha Tabora na Kigoma kwa reli bora zaidi.
Rais ameuelezea ujumbe huo kuhusu furaha yake kusikia habari hizo, na kusema kuwa serikali yake inaiunga mkono mipango hiyo kwa asilimia 150.
Ujumbe wangu ni mfupi tu tunataka njia ya reli. Na tunaunga mkono juhudi zenu asilimia 150, Rais Kikwete aliuambia ujumbe huo.
Rais pia alitaka kuangaliwa kwa uwezekano wa kuunganisha Reli ya Kati na Reli ya TAZARA, na hivyo kuwezesha mizigo kutoka kusini mwa Afrika kusafirishwa hadi Tanzania, na mizigo ya nchi jirani za kaskazini mwa Tanzania, kusafirishwa kwa urahisi kwenda kusini mwa Afrika.
Aliuambia ujumbe huo kuwa, serikali imejipanga kuhakikisha kuwa upanuzi na matengenezo makubwa katika Reli ya Kati unakwenda sambamba na upanuzi mkubwa wa Bandari ya Dar es Salaam
Hii habari ikoje? Naona inaniogopesha, nani wanagharamia ujenzi wa hiyo reli? Mbona inaonekana kama hao Wazungu ndio wame initiate hii project?
Tuangalie, tusije tukaibiwa kama kwenye umeme. naomba wenye taarifa zaidi tusaidieni hii project ikoje? Idea yenyewe nimeipenda mno ila tu ninahisi kunaweza kuwa na mafisi yanatuzengea tena.
Mapinduzi makubwa yaja kwenye reli nchini
na Mwandishi Wetu
UJENZI wa reli itakayounganisha mji wa Isaka nchini na mji mkuu wa Rwanda, Kigali, umepangwa kuanza mwakani, Rais Jakaya Kikwete alielezwa jana.
Ujenzi wa reli hiyo ni moja ya mikakati ya kuboresha miundombinu nchini ambayo itahusisha pia ukarabati mkubwa katika njia nyingine za reli, ikiwemo Reli ya Kati.
Ujumbe wa Kampuni ya Barlington Northern Santa Fe (BNSF) kutoka Marekani, ambayo ndiyo itakayofanya kazi hiyo, ulimweleza Rais Kikwete kuwa ujenzi huo unatarajiwa kukamilika mwaka 2013.
Taarifa iliyotolewa na Ikulu jana, ilieleza kuwa ujumbe huo pia ulimwambia rais kuwa kazi ya ujenzi wa reli hiyo mpya, utakwenda sambamba na matengenezo makubwa na upanuzi wa Reli ya Kati, kati ya Isaka na Dar es Salaam.
Upanuzi huo utalenga kuiwezesha Reli ya Kati kufikia kiwango cha kimataifa cha reli, kuongeza nguvu ya reli hiyo kuweza kubeba mabehewa zaidi, na kubeba mizigo mikubwa zaidi na kupunguza muda wa safari, ilisema taarifa hiyo ya Ikulu.
Katika mazungumzo kati ya ujumbe huo na Rais Kikwete, yaliyofanyika Ikulu, ujumbe huo pia ulimwambia kuwa maandalizi yote muhimu kwa ajili ya ujenzi wa reli kati ya Isaka na Kigali karibu yanakamilika.
Ujumbe huo uliwajumuisha Daniel Cooper na mshirika wake, Tom Vegh, kutoka kampuni ya masuala ya fedha ya Fox River Financial Resources, ambayo inahusika na masuala ya fedha kwa ajili ya ujenzi wa reli hiyo, pamoja na John Orrison kutoka Kampuni ya BNFS.
Mazungumzo hayo pia yalihudhuriwa na Waziri wa Fedha, Zakia Meghji, Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge na Waziri wa Mipango, Uchumi na Uwezeshaji, Dk. Juma Ngasongwa.
Wakati maandalizi yanaendelea kwa ajili ya ujenzi wa reli ya Isaka-Kigali, na upanuzi wa Reli ya Kati, maandalizi pia yanafanyika kwa ajili ya kuangalia uwezekano wa ujenzi wa reli kati ya Isaka-Kigali-Bujumbura.
Mbali na hiyo, mipango pia inaandaliwa na kuangalia uwezekano wa kuunganisha Isaka na mji wa Mwanza, na kuunganisha Tabora na Kigoma kwa reli bora zaidi.
Rais ameuelezea ujumbe huo kuhusu furaha yake kusikia habari hizo, na kusema kuwa serikali yake inaiunga mkono mipango hiyo kwa asilimia 150.
Ujumbe wangu ni mfupi tu tunataka njia ya reli. Na tunaunga mkono juhudi zenu asilimia 150, Rais Kikwete aliuambia ujumbe huo.
Rais pia alitaka kuangaliwa kwa uwezekano wa kuunganisha Reli ya Kati na Reli ya TAZARA, na hivyo kuwezesha mizigo kutoka kusini mwa Afrika kusafirishwa hadi Tanzania, na mizigo ya nchi jirani za kaskazini mwa Tanzania, kusafirishwa kwa urahisi kwenda kusini mwa Afrika.
Aliuambia ujumbe huo kuwa, serikali imejipanga kuhakikisha kuwa upanuzi na matengenezo makubwa katika Reli ya Kati unakwenda sambamba na upanuzi mkubwa wa Bandari ya Dar es Salaam