Mapinduzi baridi ndani ya chama kongwe, iliyokuwa CCM Mpya ya mwendazake yafukiwa rasmi

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,247
24,108
Mapinduzi baridi ndani ya chama kongwe, iliyokuwa CCM Mpya ya mwendazake yafukiwa rasmi


Hakika sasa chama kikongwe chama dola kimefanya mabadiliko na kurudisha safu, makada na itikadi iliyokuwa imefukiwa na mwenyekiti mwendazake (revered) hayati (late) John Pombe Joseph Magufuli.


Yanayoendelea kimya kimya ndani ya CCM ni hatua ya kuondokana na wale walioonekana kama 'wageni ' na sasa wale waliokulia ndani ya chama sasa wamerudi na kuchukua hatamu.

Nini tutegemee kwa taifa kuhusu mabadiliko haya ya ndani kwa ndani ya chama kongwe ambacho kilikuwa na uvumilivu wa vyama vingine vingi vya siasa Tanzania tangu kuasisiwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992.


Historia inaonesha mwalimu Nyerere aliyechagiza mfumo huo wa vyama vingi viwepo ingawa wahafidhina wachache ndani ya CCM waliuogopa.

Ali Hassan Mwinyi aliulea mfumo huo na kupokewa na Benjamin Mkapa na kisha jukumu hilo la kitaifa likamwendea Jakaya Kikwete. Mambo yalienda kwa kiasi mazuri baina ya mwaka 1992 mpaka 2015 ambapo ghafla kukatokea mkakati wa kuua vyama na mfumo mzima wa vyama vingi.

Mwaka 2015 aliposhinda urais kuoitia chama cha CCM na kisha baadaye kama desturi ya CCM mwrndazake hayati rais John Pombe Joseph Magufuli kujizatiti kwa kuwa pia meenyekiti wa CCM alianza harakati za kufuta mfumo wa vyama vingi na pia kuwaweka pembeni wenye CCM yao.

Mbali ya kuiathiri CCM na pia kwa kiwango kikubwa vyama vingine vya siasa kugandamizwa, chaguzi kuchafuliwa na wageni kukaribishwa katika iliyoitwa CCM Mpya ya Magufuli, kelele na mayowe yakaanza kusikika ndani ya chama dola kongwe cha CCM vipi waliokipigania, waliokulia ndani ya chama tangu jumuiya ya chipukizi ya CCM, UVCCM vyuoni na kisha kuwa watu wa makamo ndani ya CCM wakatupwa nje ya shughuli za chama na nafasi zao kupewa wasio wanasiasa na pia ni mamluki toka vyama vingine walionunuliwa kwa fedha wakawa sasa wanaendesha chama na serikali chini ya John Pombe Joseph Magufuli.
 
TOKA MAKTABA:
LEO Desemba 05, 2021

WAKUMBUSHANA NYIMBO ZA USHINDI VITA YA UGANDA

LEO Desemba 05,2021 wazee wa CCM walio wanajeshi akiwemo Rais mstaafu wa awamu wa Nne, Jakaya Kikwete (Lt. Colonel mstaafu) na viongozi Abdulrahman Kinana (Colonel mstaafu), Yusuf Makamba (Luteni mstaafu), Capt Ditopile Mzuzuri wengine wa serikali wameshiriki katika kumbukumbu ya kifo cha baba mzazi wa Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye, Hayati Brigedia Moses Nnauye.. na kutoboa siri ya jinsi walivyoishi kwa ...

 
Ali Hassan Mwinyi aliulea mfumo huo na kupokewa na Benjamin Mkapa na kisha jukumu hilo la kitaifa likamwendea Jakaya Kikwete. Mambo yalienda kwa kiasi mazuri baina ya mwaka 1992 mpaka 2015 ambapo ghafla kukatokea mkakati wa kuua vyama na mfumo mzima wa vyama vingi

Furaha furaha upande wa vyama vingi kuona mabadiliko yanayoendelea ndani ya chama dola kongwe. Inaashiria siasa za kabla ya 2015 kurudi Tanzania

15 October 2013


Rais Dk. Jakaya Kikwete akisalimiana na Mbunge wa Singida kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu. Nyuma ni James Mbatia NCCR Mageuzi, Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi
 
Profesa wa siasa za Tanzania Dr. Jakaya Mrisho Kikwete na ushawishi wake anastahili kupewa nishani ya kutukuka katika medani za siasa za vyama vingi nchini Tanzania na kanda nzima ya Afrika Mashariki na nchi za Maziwa Makuu barani Afrika

TOKA MAKTABA :

LEO Desemba 05, 2021

NILIFUNDISHWA Kuishi na VIONGOZI Wenzangu, UPENDO Ndio KILA KITU"



LEO Desemba 05, Rais mstaafu wa awamu wa Nne, Jakaya Kikwete na viongozi wengine wa serikali wameshiriki katika kumbukumbu ya kifo cha baba mzazi wa Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye, Hayati Brigedia Moses Nnauye..
 
Mwaka 2015 aliposhinda urais kuoitia chama cha CCM na kisha baadaye kama desturi ya CCM mwrndazake hayati rais John Pombe Joseph Magufuli kujizatiti kwa kuwa pia meenyekiti wa CCM alianza harakati za kufuta mfumo wa vyama vingi na pia kuwaweka pembeni wenye CCM yao.


Je mabadiliko ya sasa ndani ya CCM ni baada ya wakongwe kutoridhishwa na yaliyoanza kutokea toka October 2015 ?

Wazee wenye chama kuamua inatosha wabadilishe safu kuanzia katibu mkuu wa chama, katibu wa uenezi na kukirudisha chama mikononi mwa makada kindakindaki waliokulia chamani !

TOKA MAKTABA :


13 July 2015
Dodoma

Rais Kikwete alipoendesha vikao vya CCM vya uteuzi wa Mgombea Urais Dodoma



Rais Kikwete alipoendesha vikao vya uteuzi wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ukumbi wa Dodoma Convention Centre mjini Dodoma Julai 12-13, 2015
 
2022 CCM Muendelezo wa kujivua gamba 2.0 ?

TOKA MAKTABA :

Wednesday, April 13, 2011​

KATIBU MPYA WA CCM BAADA YA KUVUA GAMBA LA KALE​


Mrithi wa Makamba aingia na moto
Tuesday, 12 April 2011 22:20

Katibu Mkuu mpya wa CCM Wilson Mukama
Waandishi Wetu, Dar na Dodoma

UPEPO wa kisiasa ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM), unazidi kuvuma kwa kasi baada ya Katibu Mkuu mpya wa chama hicho, Wilson Mukama, kutangaza kiama kwa mafisadi akitaka wajiuzulu mapema, huku Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa wa Chama hicho, Makongoro Nyerere akitajwa kuchochea maamuzi magumu dhidi ya genge hilo.


Kauli hizo nzito za vigogo hao dhidi ya genge la mafisadi ambalo lina nguvu za fedha ndani na nje ya chama hicho tawala, ni sehemu ya mpango mkakati wa Mwenyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete, wa kukivua magamba.Mukama ambaye ndiye Mtendaji Mkuu wa chama hicho aliyetangazwa mjini Dodoma usiku wa kuamkia jana, alisema ili chama hicho kiweze kurudisha heshima yake kinatakiwa kuwa na watu safi wasiotiliwa mashaka kabisa katika jamii.


Akizungumza na Mwananchi ofisini kwake muda mfupi baada ya kumaliza kikao na watendaji wa mikoa wa chama hicho, Katibu huyo alisema hana jipya atakalopeleka CCM isipokuwa yeye atasimamia weledi na misingi iliyokuwapo tangu kuanzishwa kwa CCM.


“CCM inatakiwa kujengwa upya kabisa na ili hayo yaweze kufanikiwa, kuna kila sababu za kuwa na watu safi, hivyo mimi nawataka ndugu zangu wasimame katika misingi ya zamani tuliyokuwa nayo katika chama chetu,” alisema Mukama na kuongeza:
“Nawataka wote wenye tuhuma za rushwa na ufisadi ndani ya chama waanze kujiuzulu mapema ili kulinda heshima yao, kwani tunaingia kujenga chama sio kukibomoa.”


Katibu Mkuu huyo ambaye ana kibarua kigumu cha kusafisha chama na kukirejesha katika misingi ya waasisi wake tangu enzi TANU na CCM ya mwaka 1977, alisema mwelekeo wa CCM pamoja na sera zake bado unakubalika kwa wananchi na kuongeza: "Kinachotakiwa sasa ni kuwa na usimamizi na maamuzi magumu kwa kila mtu atakayekabidhiwa dhamana hiyo".


Akizungumzia juu ya chama kujengwa upya alisema: "Ili tuweze kufanikiwa katika hilo mimi nitasimamia maamuzi ya Kamati Kuu ya CCM ya kukirudisha chama kwa wanachama ngazi ya chini ili wao ndio wakafanye maamuzi.”


Mukama ambaye alikuwa akizungumza kwa kujiamini alisema atasimamia kikamilifu itikadi ya Ujamaa na Kujitegemea, kwa kuwa ndio sera kubwa ya CCM tangu kuanzishwa kwake.


Jambo lingine alilosisitiza kiongozi huyo ni pamoja na kukiongoza chama katika kupata ushindi ambao hautakuwa ukitiliwa mashaka na watu wengine.“Jambo kubwa na la msingi hapa ni kukiongoza chama katika kufikia malengo makubwa ya kupata ushindi usiokuwa na manung’uniko, kwani mbinu za kivita hupatikana katika medani sio uwanja wa vita,” alitamba Mukama. Hata hivyo, alisifia hatua ambayo imechukuliwa na chama ambayo imesaidia kukijenga hadi sasa.


Aliyataja mafanikio ya hatua hiyo kuwa ni pamoja na kuwa viti vingi bungeni, kwani zaidi ya asilimia 78 ya wabunge wanatoka CCM.

Abeza nguvu ya upinzani
Akizungumzia nguvu za upinzani, Mukama alibeza na kusema hilo haliwezi kumsumbua yeye wala kumfanya asilale usingizi, kwani anatambua ni wapi panatakiwa kusimamiwa na ni wapi panatakiwa kutolewa maelekezo yake.


“Kwenye siasa hata siku moja ni kubwa sana huwezi kuidharau. Leo tutazungumzia miaka minne ili tuingie katika Uchaguzi Mkuu mwingine, hivyo bado kuna muda mzuri na wa kutosha kufanya maandalizi, ndio maana siwezi kutaja moja kwa moja chama kinachonipa tabu bali kitajulikana mbele ya safari,” alitamba Mukama

Ofisini siku ya kwanza
Kutwa nzima jana, Mukama akiwa na wasaidizi wake John Chiligati (Bara), Vuai Alli Vuai (Zanzibar) pamoja na Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, walifanya vikao na makatibu wa mikoa na watumishi wa CCM Makao Makuu.


Awali, Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Kikwete, alizungumza na watumishi makao makuu na baadhi ya makada wa chama kwa lengo la kuitambulisha Sekretarieti mpya na kuweka mikakati.

Makamba ataka aachwe
Kwa upande wake Katibu Mkuu aliyeachia ngazi, Yusuph Makamba, alisema huu ni wakati wake wa kupumzika kwani amechoka.Akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu jana kuhusu uamuzi mgumu wa kujiuzulu aliouchukua mjini Dodoma hivi karibuni alisema, "Naomba mniache nipumzike... Nimechoka."


Alifafanua kwamba ametumikia nchi kwa zaidi ya miaka 50, hivyo huu ni wakati wake kupumzika na watu wengine kufanya kazi na yeye aachwe apumzike.


"Nimetumikia nchi hii kwa miaka mingi, nimekuwa mkuu wa wilaya, mkoa na baadaye chama, sasa ni wakati wangu wa kupumzika kwani kazi niliyofanya ni kubwa," alisisitiza.


Katibu Mkuu huyo mstaafu aliyetuhumiwa kukigawa chama, alisema kama ni chama kimepata uongozi mpya ambao anaamini utaweza kusimamia ajenda zake kwa ufanisi.

Makongoro Nyerere amchochea JK
Mtoto wa Baba wa Taifa ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara, Makongoro Nyerere, amemshauri Mwenyekiti wake Rais Kikwete, kuwabwaga wote wanaotuhumiwa kwa ufisadi hata kama ni maswahiba wake kisiasa.


Habari kutoka ndani ya kikao cha NEC, zilidokeza gazeti hili kwamba Makongoro alimweleza Rais Kikwete wakati wa kikao kuwa hana budi kuchukua uamuzi utakaowaumiza marafiki zake, ili kukinusuru chama.


“Vitabu vitakatifu vinatueleza kuwa awali Mungu alikuwa akishirikiana kwa karibu na shetani, lakini shetani alipoanza ushetani wake, Mungu akamtimua na kumtupa uwanjani. Mungu hakai na shetani,” mpasha habari wetu alimnukuu Makongoro.


Makongoro anadaiwa kumweleza Rais Kikwete kwamba, watu wa Dar es Salaam walipokwenda kuhiji katika kaburi la baba yake, walipata jibu la kuwa Kikwete ndiye anayefaa, hivyo asivurugwe na watu wachache.


Makongoro alimtahadharisha rais kuwa kama atachukua uamuzi wa kuilipa Kampuni ya Dowans Sh94 bilioni, hakuna Mtanzania atakayemwelewa.
Katika hatua nyingine, uamuzi wa kuvunjwa kwa Sekretarieti na Kamati Kuu ya CCM, kumechochea wanachama kudai mabadiliko yafanyike haraka katika ngazi ya mikoa.
Mbunge wa Kinondoni (CCM), Iddi Azzan, alisema mabadiliko yaliyofanywa ndani ya chama hicho ni mazuri.


Hata hivyo, Azzan alisema mabadiliko hayo yanatakiwa kufanyika katika ngazi za mikoa na wilaya ambako alidai kuwa kumeoza.
Aliitaka Sekretarieti ya Mkoa wa Dar es Salaam kujiuzulu kama walivyofanya wa Sekretarieti ya Taifa.
Sekretarieti ya CCM, Mkoa wa Dar es Salaam inaundwa na Katibu wa CCM Mkoa, Kilumbe Ng'enda, Katibu Mwenezi, Juma Simba, Katibu wa Uchumi, Abbas Tarimba, Katibu wa Wazazi, Mustafa Yakub, Katibu wa UWT, Tatu Mariaga na Katibu wa UVCCM, Omar Mwanag’alu.

January Makama ajiuzulu Kamati ya Bunge
Katika tukio lingine, Katibu wa Siasa na Uhusiano wa Kimataifa wa CCM, Januari Makamba, anatakiwa kujiuzulu nafasi yake ya Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini.


Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, John Chiligati, alisema January Makamba anatakiwa kupima uzito wa kazi aliyopewa na ile ya Bunge. Anatakiwa kubaki na ubunge kwa sababu sio kazi ya kuwajibika kila siku.


Katika mkutano wake Nec iliamua kuwa watumishi wa chama wanatakiwa kuwapo kila siku kwa ajili ya utendaji na kwamba wanatakiwa kutenganisha viongozi wa Serikali na chama.

Habari hii imeandikwa na Habel Chidawali na Midraj Ibrahim, Dodoma, Ramadhan Semtawa, Dar
 
Mapinduzi baridi ndani ya chama kongwe, iliyokuwa CCM Mpya ya mwendazake yafukiwa rasmi


Hakika sasa chama kikongwe chama dola kimefanya mabadiliko na kurudisha safu, makada na itikadi iliyokuwa imefukiwa na mwenyekiti mwendazake (revered) hayati (late) John Pombe Joseph Magufuli.


Yanayoendelea kimya kimya ndani ya CCM ni hatua ya kuondokana na wale walioonekana kama 'wageni ' na sasa wale waliokulia ndani ya chama sasa wamerudi na kuchukua hatamu.

Nini tutegemee kwa taifa kuhusu mabadiliko haya ya ndani kwa ndani ya chama kongwe ambacho kilikuwa na uvumilivu wa vyama vingine vingi vya siasa Tanzania tangu kuasisiwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992.


Historia inaonesha mwalimu Nyerere aliyechagiza mfumo huo wa vyama vingi viwepo ingawa wahafidhina wachache ndani ya CCM waliuogopa.

Ali Hassan Mwinyi aliulea mfumo huo na kupokewa na Benjamin Mkapa na kisha jukumu hilo la kitaifa likamwendea Jakaya Kikwete. Mambo yalienda kwa kiasi mazuri baina ya mwaka 1992 mpaka 2015 ambapo ghafla kukatokea mkakati wa kuua vyama na mfumo mzima wa vyama vingi.

Mwaka 2015 aliposhinda urais kuoitia chama cha CCM na kisha baadaye kama desturi ya CCM mwrndazake hayati rais John Pombe Joseph Magufuli kujizatiti kwa kuwa pia meenyekiti wa CCM alianza harakati za kufuta mfumo wa vyama vingi na pia kuwaweka pembeni wenye CCM yao.

Mbali ya kuiathiri CCM na pia kwa kiwango kikubwa vyama vingine vya siasa kugandamizwa, chaguzi kuchafuliwa na wageni kukaribishwa katika iliyoitwa CCM Mpya ya Magufuli, kelele na mayowe yakaanza kusikika ndani ya chama dola kongwe cha CCM vipi waliokipigania, waliokulia ndani ya chama tangu jumuiya ya chipukizi ya CCM, UVCCM vyuoni na kisha kuwa watu wa makamo ndani ya CCM wakatupwa nje ya shughuli za chama na nafasi zao kupewa wasio wanasiasa na pia ni mamluki toka vyama vingine walionunuliwa kwa fedha wakawa sasa wanaendesha chama na serikali chini ya John Pombe Joseph Magufuli.

Hii ni CCM timu ufisadi imeingia tena kazini. Ni ile ile ya Kikwete legevu. Kipya sana sana ni ufisadi na madawa ya kulevya kuongezeka. Umesikia wameanza kutolewa jela ili waingie kazini?
 
Mapinduzi baridi ndani ya chama kongwe, iliyokuwa CCM Mpya ya mwendazake yafukiwa rasmi


Hakika sasa chama kikongwe chama dola kimefanya mabadiliko na kurudisha safu, makada na itikadi iliyokuwa imefukiwa na mwenyekiti mwendazake (revered) hayati (late) John Pombe Joseph Magufuli.


Yanayoendelea kimya kimya ndani ya CCM ni hatua ya kuondokana na wale walioonekana kama 'wageni ' na sasa wale waliokulia ndani ya chama sasa wamerudi na kuchukua hatamu.

Nini tutegemee kwa taifa kuhusu mabadiliko haya ya ndani kwa ndani ya chama kongwe ambacho kilikuwa na uvumilivu wa vyama vingine vingi vya siasa Tanzania tangu kuasisiwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992.


Historia inaonesha mwalimu Nyerere aliyechagiza mfumo huo wa vyama vingi viwepo ingawa wahafidhina wachache ndani ya CCM waliuogopa.

Ali Hassan Mwinyi aliulea mfumo huo na kupokewa na Benjamin Mkapa na kisha jukumu hilo la kitaifa likamwendea Jakaya Kikwete. Mambo yalienda kwa kiasi mazuri baina ya mwaka 1992 mpaka 2015 ambapo ghafla kukatokea mkakati wa kuua vyama na mfumo mzima wa vyama vingi.

Mwaka 2015 aliposhinda urais kuoitia chama cha CCM na kisha baadaye kama desturi ya CCM mwrndazake hayati rais John Pombe Joseph Magufuli kujizatiti kwa kuwa pia meenyekiti wa CCM alianza harakati za kufuta mfumo wa vyama vingi na pia kuwaweka pembeni wenye CCM yao.

Mbali ya kuiathiri CCM na pia kwa kiwango kikubwa vyama vingine vya siasa kugandamizwa, chaguzi kuchafuliwa na wageni kukaribishwa katika iliyoitwa CCM Mpya ya Magufuli, kelele na mayowe yakaanza kusikika ndani ya chama dola kongwe cha CCM vipi waliokipigania, waliokulia ndani ya chama tangu jumuiya ya chipukizi ya CCM, UVCCM vyuoni na kisha kuwa watu wa makamo ndani ya CCM wakatupwa nje ya shughuli za chama na nafasi zao kupewa wasio wanasiasa na pia ni mamluki toka vyama vingine walionunuliwa kwa fedha wakawa sasa wanaendesha chama na serikali chini ya John Pombe Joseph Magufuli.
Another , hujui usemalo wewe!
 
31 March 2022
Helsinki, Finland 🇫🇮

KUREJEA KWA BERNARD MEMBE NA COL. MST. KINANA KUNA MAANA GANI? (1)




Bernard Membe ambaye alifukuzwa uanachama wa CCM Februari 2020 leo amerejeshewa uanachama wake. Abdulrahman Kinana ambaye amewahi kuwa katibu mkuu wa CCM, na ambaye aliponea chupuchupu kufukuzwa uanachama mwaka 2020, ameteuliwa kuwa Makamu mwenyekiti wa CCM. Huu ni utangulizi wa uchambuzi juu ya maana ya kurejea kwa vigogo hawa katika siasa za CCM.

Source : SK media Online TV
 
Mapinduzi baridi ndani ya chama kongwe, iliyokuwa CCM Mpya ya mwendazake yafukiwa rasmi


Hakika sasa chama kikongwe chama dola kimefanya mabadiliko na kurudisha safu, makada na itikadi iliyokuwa imefukiwa na mwenyekiti mwendazake (revered) hayati (late) John Pombe Joseph Magufuli.


Yanayoendelea kimya kimya ndani ya CCM ni hatua ya kuondokana na wale walioonekana kama 'wageni ' na sasa wale waliokulia ndani ya chama sasa wamerudi na kuchukua hatamu.

Nini tutegemee kwa taifa kuhusu mabadiliko haya ya ndani kwa ndani ya chama kongwe ambacho kilikuwa na uvumilivu wa vyama vingine vingi vya siasa Tanzania tangu kuasisiwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1992.


Historia inaonesha mwalimu Nyerere aliyechagiza mfumo huo wa vyama vingi viwepo ingawa wahafidhina wachache ndani ya CCM waliuogopa.

Ali Hassan Mwinyi aliulea mfumo huo na kupokewa na Benjamin Mkapa na kisha jukumu hilo la kitaifa likamwendea Jakaya Kikwete. Mambo yalienda kwa kiasi mazuri baina ya mwaka 1992 mpaka 2015 ambapo ghafla kukatokea mkakati wa kuua vyama na mfumo mzima wa vyama vingi.

Mwaka 2015 aliposhinda urais kuoitia chama cha CCM na kisha baadaye kama desturi ya CCM mwrndazake hayati rais John Pombe Joseph Magufuli kujizatiti kwa kuwa pia meenyekiti wa CCM alianza harakati za kufuta mfumo wa vyama vingi na pia kuwaweka pembeni wenye CCM yao.

Mbali ya kuiathiri CCM na pia kwa kiwango kikubwa vyama vingine vya siasa kugandamizwa, chaguzi kuchafuliwa na wageni kukaribishwa katika iliyoitwa CCM Mpya ya Magufuli, kelele na mayowe yakaanza kusikika ndani ya chama dola kongwe cha CCM vipi waliokipigania, waliokulia ndani ya chama tangu jumuiya ya chipukizi ya CCM, UVCCM vyuoni na kisha kuwa watu wa makamo ndani ya CCM wakatupwa nje ya shughuli za chama na nafasi zao kupewa wasio wanasiasa na pia ni mamluki toka vyama vingine walionunuliwa kwa fedha wakawa sasa wanaendesha chama na serikali chini ya John Pombe Joseph Magufuli.

CCM imerudi rasmi Pwani
 
31 March 2022
Helsinki, Finland 🇫🇮

KUREJEA KWA BERNARD MEMBE NA COL. MST. KINANA KUNA MAANA GANI? (1)




Bernard Membe ambaye alifukuzwa uanachama wa CCM Februari 2020 leo amerejeshewa uanachama wake. Abdulrahman Kinana ambaye amewahi kuwa katibu mkuu wa CCM, na ambaye aliponea chupuchupu kufukuzwa uanachama mwaka 2020, ameteuliwa kuwa Makamu mwenyekiti wa CCM. Huu ni utangulizi wa uchambuzi juu ya maana ya kurejea kwa vigogo hawa katika siasa za CCM.

Source : SK media Online TV

Sahivi pesa za umma zitapigwa haswa
 
TOKA MAKTABA:
LEO Desemba 05, 2021

WAKUMBUSHANA NYIMBO ZA USHINDI VITA YA UGANDA

LEO Desemba 05,2021 wazee wa CCM walio wanajeshi akiwemo Rais mstaafu wa awamu wa Nne, Jakaya Kikwete (Lt. Colonel mstaafu) na viongozi Abdulrahman Kinana (Colonel mstaafu), Yusuf Makamba (Luteni mstaafu), Capt Ditopile Mzuzuri wengine wa serikali wameshiriki katika kumbukumbu ya kifo cha baba mzazi wa Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye, Hayati Brigedia Moses Nnauye.. na kutoboa siri ya jinsi walivyoishi kwa ...

Mengi bado
 
Je mabadiliko ya sasa ndani ya CCM ni baada ya wakongwe kutoridhishwa na yaliyoanza kutokea toka October 2015 ?

Wazee wenye chama kuamua inatosha wabadilishe safu kuanzia katibu mkuu wa chama, katibu wa uenezi na kukirudisha chama mikononi mwa makada kindakindaki waliokulia chamani !

TOKA MAKTABA :


13 July 2015
Dodoma

Rais Kikwete alipoendesha vikao vya CCM vya uteuzi wa Mgombea Urais Dodoma



Rais Kikwete alipoendesha vikao vya uteuzi wa Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM ukumbi wa Dodoma Convention Centre mjini Dodoma Julai 12-13, 2015
Anguko kubwa la kukumbuka lilikuwa siku hii
 
01 April 2022
Dodoma, Tanzania

"CCM HATUPOKEI MAAGIZO KUTOKA SERIKALINI" - KINANA ALIPUKA MBELE YA RAIS SAMIA...



Mwenyekiti aangalie tu asije akawekwa kwenye siti ya mbele katika mapambano vitani kama Mzee Makamba alivyo tuhadithia ya huko Kagera, akashangalia akifikiri ni kuheshimiwa kumbe kafanywa "an easy target and a shield from a sniper's short.

Kwa kauli hii ya "serikali inatumwa na CCM" Nina pata mashaka inaweza kufanya Rais wa nchi akawa ni Makamu Mkt wa CCM bara ama anaye mtuma. Sijui ushawishi wa hawa...Mh Rais SSH, Makamu Mkt CCM upande wa Visiwani, KM, Mh Rais Mwinyi jR., kama kati yao yuko anaye mshinda/mzidi Mzee Kinana umaarufu na ushawishi ndani na nje ya CCM.

Wahusika mliangalie hilo kwa umakini na mchukue hatua madhubuti. Bila kufanya hivyo Tanzania itakuwa na Rais ambaye si Rais ie Rais wa Makaratasi na kupiga mwikwaju na Rais asiye oneka akawa ndiye anaiongoza nchi. Kwa mabadiliko haya ya CCM ya nafasi ya Makamu mwenyekiti bara Tanzania tunaweza kukutana na kile kule Vatican kiitwacho Black Pope.
 
01 April 2022
Dodoma, Tanzania


Mzee Makamba - "2025 ni 'Simba Vs Yanga', timu zote zina kocha mzuri"

Pia Mzee Yusuf Makamba ametahadharisha kuwa uchaguzi 2025 ni mgumu kwani wote "Simba" na " Yanga" wana viongozi wazuri wenye ushawishi mkubwa ktk siasa za Tanzania ambao ni Mwenyekiti Samia Suluhu Hassan kocha upande wa CCM na upande mwingine pia wana Kocha mzuri pia.

Matumizi ya maneno "Simba" na "Yanga" yaani Rangi ya njano kwa kijana na ile nyekundu na nyeupe aliyotumia Mzee Yusuf Makamba yamezua gumzo kuwa alikuwa ana maana gani kuhusu ukubwa na ushawishi wa kocha wa timu nyingine ya kisiasa ambazo ndizo zinahesabika kuwa ni timu mbili kubwa za kisiasa Tanzania.

Mzee Makamba: Watanzania wameanza kuonja asali awamu ya 6

Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM Mzee Yusuf Makamba amewaambia wajumbe wa mkutano Mkuu Maalum wa Chama hicho kuwa Mgombea wa Urasi wa chama hicho Mwaka 2025 ni Rais wa Sasa Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza katika Mkutano huo, Makamba amesema, Kwa namna kazi zinavyofanyika mpaka sasa hakuna mwingine wa kushika nafasi ya urais katika uchaguzi ujao zaidi ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Mzee Makamba ameeleza kuwa tayari watanzania wameanza kuonja Asali hivyo ni vyema asali hiyo ikaendelea kulambwa na watanzania na mwenye uwezo wa kuwalambisha watanzania asali hiyo ni Samia Suluhu Hassan pekee.

Makamba amewataka wale wote wanaotamani nafasi hiyo wakae kando na wampishe Rais Samia aendelee kujenga nchi kwa uongozi wake aliofananisha na ubatizo wa maji baridi.
 
01 April 2022
Dodoma, Tanzania

Mzee Makamba: Watanzania wameanza kuonja asali awamu ya 6

Katibu Mkuu Mstaafu wa CCM Mzee Yusuf Makamba amewaambia wajumbe wa mkutano Mkuu Maalum wa Chama hicho kuwa Mgombea wa Urasi wa chama hicho Mwaka 2025 ni Rais wa Sasa Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza katika Mkutano huo, Makamba amesema, Kwa namna kazi zinavyofanyika mpaka sasa hakuna mwingine wa kushika nafasi ya urais katika uchaguzi ujao zaidi ya Rais Samia Suluhu Hassan.

Mzee Makamba ameeleza kuwa tayari watanzania wameanza kuonja Asali hivyo ni vyema asali hiyo ikaendelea kulambwa na watanzania na mwenye uwezo wa kuwalambisha watanzania asali hiyo ni Samia Suluhu Hassan pekee.

Makamba amewataka wale wote wanaotamani nafasi hiyo wakae kando na wampishe Rais Samia aendelee kujenga nchi kwa uongozi wake aliofananisha na ubatizo wa maji baridi.

Mzee Makamba - 2025 ni 'Simba Vs Yanga'

Pia Mzee Yusuf Makamba ametahadharisha kuwa uchaguzi 2025 ni mgumu kwani wote "Simba" na " Yanga" wana viongozi wazuri wenye ushawishi mkubwa ktk siasa za Tanzania ambao ni Mwenyekiti Samia Suluhu Hassan kocha upande wa CCM na upande mwingine pia wana Kocha mzuri pia.

Matumizi ya maneno "Simba" na "Yanga" yaani Rangi ya njano kwa kijana na ile nyekundu na nyeupe aliyotumia Mzee Yusuf Makamba yamezua gumzo kuwa alikuwa ana maana gani kuhusu ukubwa na ushawishi wa kocha wa timu nyingine ya kisiasa ambazo ndizo zinahesabika kuwa ni timu mbili kubwa za kisiasa Tanzania.

Niongezee na Ni mfariji msaidizi wa karibu. Yaani Roho Mtakatifu, wawatafute Wachungaji au rafiki wa Mzee Makamba Askofu Gwajima awasaidie kuwa hii imekaa vipi?
 
Back
Top Bottom