ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,906
- 6,909
Wana bodi habari za jioni,
Nimetafakari mienendo ya kiutawala ya Rais Magufuli naona ukombozi toka kwa minyiroro ya CCM sasa imewadia.
Kama vile FARAO alivyopewa mapigo mbalimbali awaachie wana wa Israel waende zao Kaanani lakini Mungu akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu zaidi na zaidi hadi alipouwa wazaliwa wa kwanza wa mwanadamu na mnyama, ndipo Farao akaamini, akawaruhusu Israel watoke Misri.
Maisha ya Watanzania tangu 2016 yamekuwa na misukosuko ambayo ni sawa na ile ya Wamisri.
Mapigo yalikuwa kama ifuatavyo na uhusiano wake na Tanzania ya sasa.
Tuanze hivi:
Kutoka 4:21 BWANA akamwambia Musa, Hapo utakaporudi Misri, angalia ukazifanye mbele ya Farao zile ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; lakini nitaufanya mgumu moyo wake, naye hatawapa ruhusa hao watu waende zao.
1. Fimbo ya haruni iligeuka nyoka, Farao akaita wachawi wa misiri nao fimbo zao zikawa nyoka, lakini nyoka wa Musa na Haruni wakawameza nyoka wote wa wachawi wa Misri lakini Farao akaona simple tu. Kutoka 7:10-13.
2. Musa akiwa na Haruni, waligeuza maji ya mto nile wote ukawa damu, samaki wote wakafa na kukawa na harufu kali Misri yote na hawakupata maji ya kunywa. Farao akaona poa tu. Kutoka 7:19-22.
3. Pigo la vyura, ambapo vyura walitolewa kwenye moto, maziwa, bahari n.k wakafika hadi kwenye kitanda cha Farao. Farao alilegeza msimamo akiomba vyura watoke awaruhusu Israel, vyura walipokoma, akageuka tena. Soma kutoka 8:1-15.
4. Pigo la nee ni la chawa. Hili halikumshitua Farao japo waganga wake walisalimu amri. Soma Kutoka 8:16-19.
5. Pigo la nzi. Hili nalo Farao alinyoosha mikono lkn alipoombewa nzi wakakoma, akakataa kuwaachia Israel. Soma Kutoka 8:21-32.
6. Pigo la tauni. Mungu alishusha tauni wakashambulia mifugo yote ya kufugwa Misri, ikafa yote lakini mifugo ya waisrel yote ilikuwa salama. Farao akawa jiwe as usual Kutoka 9:1-7.
7. Pigo la nane ni Kutoka 9:8-12. Hili ni pigo la majipu. Wamisri wote walipigwa majipu haya lkn Farao akawa jiwe.
8. Pigo la nane ni pigo la mvua ya mawe na moto, kila chenye uhai kilichokuwa nje kilikufa, Farao akaomba po, lkn yalipokoma tu, hakuwaruhusu, akawa jiwe. Kutoka 9:18-32.
9. Pigo la tisa ni nzige. Nzige walitanda Misri yote hadi jua hulioni. Kila mmea uliosalia kwenye mvua ya mawe na moto uliliwa. Watu wakamwendea farao wakamwambia
*Kutoka 10:7 Ndipo watumishi wa Farao wakamwambia, Mtu huyu atakuwa tanzi kwetu sisi hata lini? Wape hawa watu ruhusa waende zao, wamtumikie BWANA, Mungu wao; hujatambua bado ya kuwa Misri imekwisha haribika?*
Lkn bado Farao akawa jiwe. Kutoka 10:3-19.
10. Pigo la kumi ni la giza siku tatu mfululizo wakati kwenye eneo la waisraeli, mwanga ulikuwepo. Farao akawa jiwe tena. Kutoka 10:22-29.
11. Pigo la mwisho ni la kuua wazaliwa wote wa kwanza wa binadamu hadi wanyama. Mtoto mpendwa wa Farao, alifariki pia. Lkn hakuna kilichokufa kwa upande wa Israel. Huo ndo ukawa mwanzo wa ukombozi kwao na dunia ya sasa kupitia pasaka. Pigo hili ndo lilizaa pasaka. Kutoka 11.
Sasa tangu Magufuli aingie madarakani, yafuatayo yametendeka:
1. Tumbua ya watumishi walioitwa wenye vyeti vya kughushi. Wengi waliokuwa na taaluma mbalimbali, manesi, madaktari, walimu na kada nyingine, walipoteza kazi. Yeye alifurahia kwa kuwashughulikia kwelikweli. Wengine walikaribia kustaafu, wengine walistaafu na mafao yao akazuia. Ni pigo kwa Watanzania, lakini moyo ukawa mgumu. Wengine walicheka kufurahia watumishi kutumbuliwa.
2. Ikaja zamu ya wakulima, mipaka ikafungwa, hakuna nafaka kuuzwa nje, wakulima wakapata hasara kubwa.
3. Likaja suala la njaa, Magufuli akawajibu wenye uhitaji wa chakula, mnataka nije niwapikie? Moyo wa Rais ukawa jiwe kwa Watanzania.
4. Likaja suala la watumishi kukaa miaka mitatu hakuna promotion, hakuna increment. Wengi wamestaafu na maslahi duni. Watanzania tukavumilia.
5. Wakosoaji wake wameteswa sana tangu 2016. Mawazo, Sanane na wengine wengi wameuwawa na wengine kupotea kabisa, hakuna hatua iliyochukuliwa. Lissu kapigwa risasi 30+ Mungu kamnusuru lkn mioyo ya Watanzania ikawa jiwe dhidi ya jiwe.
Kesi zisizo kichwa wala miguu zimeshamiri kipindi hiki kuliko wakati wowote katika historia ya nchi yetu. Bado tumekaa kimya.
6. Miaka 5 imefika lakini hakuna mtumishi aliyeongezwa mshahara. Bado wananchi wamekuwa jiwe kama alivyo jiwe kuu.
7. Tumeona wanasiasa wetu wananunulika kirahisi, wakihama vyama ovyo, waliotoka upinzani kwenda CCM, wakapitishwa kuendelea na uwakilishi, waliotoka CCM kwenda upinzani wakaandamwa. Baadhi wamerudi mfano Sumaye na Lowasa. Katiba imevunjwa kwa maslahi ya CCM, bado wananchi wamefanywa jiwe kama jiwe kuu mwenyewe.
8. Wabunge kuwekwa ndani bila dhamana hata kwa kesi zenye dhamana imekuwa kawaida, bado mioyo imekuwa migumu tu.
9. Matumizi mabaya ya madaraka na pesa ya umma imekuwa kawaida. Pesa zinachotwa kwenda chato na kusikojulikana. Michango mbalimbali ya hisani bado haikuwafikia wahanga. Na DC na RC wakajiona watemi wakisweka watu mahabusu kwa kesi za kijinga tu. Bado tumekuwa na moyo jiwe na jiwe anatuendesha kwelikweli.
10. Uvunjaji mikataba usiozingatia sheria imegharimu nchi, ndege zetu japo zilinunuliwa bila kufuata sheria zikikamatwa mara mbili. Sasa tumepata soko la nyama Belgium, ndege zetu hazina uwezo wa kupeleka shehena hizo tumetumia za RwandaAir. Ni aibu ni aibu sana.
11. Pigo la corona ndo hatari zaidi. Diplomasia imekufa. Watanzania wanaonekana ni wagonjwa, Watanzania wananyanyaswa, tumefurushwa nchi mbalimbali sasa hakuna anayetuamini.
Watumishi wa afya hawana PPE, pesa zimechangwa vifaa hakuna.
Covid inasambaa, hakuna ckrantini sasa vifo vimekuwa balaa.
Mapigo yote haya kama CCM itachomoa, basi Watanzania tujitambue sisi ni wagonjwa wa akili.
Mie naona ukombozi wa taifa hili umewadia. Wasalaaam.
Ongeza na mengine.
Ntamaholo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Nimetafakari mienendo ya kiutawala ya Rais Magufuli naona ukombozi toka kwa minyiroro ya CCM sasa imewadia.
Kama vile FARAO alivyopewa mapigo mbalimbali awaachie wana wa Israel waende zao Kaanani lakini Mungu akaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu zaidi na zaidi hadi alipouwa wazaliwa wa kwanza wa mwanadamu na mnyama, ndipo Farao akaamini, akawaruhusu Israel watoke Misri.
Maisha ya Watanzania tangu 2016 yamekuwa na misukosuko ambayo ni sawa na ile ya Wamisri.
Mapigo yalikuwa kama ifuatavyo na uhusiano wake na Tanzania ya sasa.
Tuanze hivi:
Kutoka 4:21 BWANA akamwambia Musa, Hapo utakaporudi Misri, angalia ukazifanye mbele ya Farao zile ajabu zote nilizozitia mkononi mwako; lakini nitaufanya mgumu moyo wake, naye hatawapa ruhusa hao watu waende zao.
1. Fimbo ya haruni iligeuka nyoka, Farao akaita wachawi wa misiri nao fimbo zao zikawa nyoka, lakini nyoka wa Musa na Haruni wakawameza nyoka wote wa wachawi wa Misri lakini Farao akaona simple tu. Kutoka 7:10-13.
2. Musa akiwa na Haruni, waligeuza maji ya mto nile wote ukawa damu, samaki wote wakafa na kukawa na harufu kali Misri yote na hawakupata maji ya kunywa. Farao akaona poa tu. Kutoka 7:19-22.
3. Pigo la vyura, ambapo vyura walitolewa kwenye moto, maziwa, bahari n.k wakafika hadi kwenye kitanda cha Farao. Farao alilegeza msimamo akiomba vyura watoke awaruhusu Israel, vyura walipokoma, akageuka tena. Soma kutoka 8:1-15.
4. Pigo la nee ni la chawa. Hili halikumshitua Farao japo waganga wake walisalimu amri. Soma Kutoka 8:16-19.
5. Pigo la nzi. Hili nalo Farao alinyoosha mikono lkn alipoombewa nzi wakakoma, akakataa kuwaachia Israel. Soma Kutoka 8:21-32.
6. Pigo la tauni. Mungu alishusha tauni wakashambulia mifugo yote ya kufugwa Misri, ikafa yote lakini mifugo ya waisrel yote ilikuwa salama. Farao akawa jiwe as usual Kutoka 9:1-7.
7. Pigo la nane ni Kutoka 9:8-12. Hili ni pigo la majipu. Wamisri wote walipigwa majipu haya lkn Farao akawa jiwe.
8. Pigo la nane ni pigo la mvua ya mawe na moto, kila chenye uhai kilichokuwa nje kilikufa, Farao akaomba po, lkn yalipokoma tu, hakuwaruhusu, akawa jiwe. Kutoka 9:18-32.
9. Pigo la tisa ni nzige. Nzige walitanda Misri yote hadi jua hulioni. Kila mmea uliosalia kwenye mvua ya mawe na moto uliliwa. Watu wakamwendea farao wakamwambia
*Kutoka 10:7 Ndipo watumishi wa Farao wakamwambia, Mtu huyu atakuwa tanzi kwetu sisi hata lini? Wape hawa watu ruhusa waende zao, wamtumikie BWANA, Mungu wao; hujatambua bado ya kuwa Misri imekwisha haribika?*
Lkn bado Farao akawa jiwe. Kutoka 10:3-19.
10. Pigo la kumi ni la giza siku tatu mfululizo wakati kwenye eneo la waisraeli, mwanga ulikuwepo. Farao akawa jiwe tena. Kutoka 10:22-29.
11. Pigo la mwisho ni la kuua wazaliwa wote wa kwanza wa binadamu hadi wanyama. Mtoto mpendwa wa Farao, alifariki pia. Lkn hakuna kilichokufa kwa upande wa Israel. Huo ndo ukawa mwanzo wa ukombozi kwao na dunia ya sasa kupitia pasaka. Pigo hili ndo lilizaa pasaka. Kutoka 11.
Sasa tangu Magufuli aingie madarakani, yafuatayo yametendeka:
1. Tumbua ya watumishi walioitwa wenye vyeti vya kughushi. Wengi waliokuwa na taaluma mbalimbali, manesi, madaktari, walimu na kada nyingine, walipoteza kazi. Yeye alifurahia kwa kuwashughulikia kwelikweli. Wengine walikaribia kustaafu, wengine walistaafu na mafao yao akazuia. Ni pigo kwa Watanzania, lakini moyo ukawa mgumu. Wengine walicheka kufurahia watumishi kutumbuliwa.
2. Ikaja zamu ya wakulima, mipaka ikafungwa, hakuna nafaka kuuzwa nje, wakulima wakapata hasara kubwa.
3. Likaja suala la njaa, Magufuli akawajibu wenye uhitaji wa chakula, mnataka nije niwapikie? Moyo wa Rais ukawa jiwe kwa Watanzania.
4. Likaja suala la watumishi kukaa miaka mitatu hakuna promotion, hakuna increment. Wengi wamestaafu na maslahi duni. Watanzania tukavumilia.
5. Wakosoaji wake wameteswa sana tangu 2016. Mawazo, Sanane na wengine wengi wameuwawa na wengine kupotea kabisa, hakuna hatua iliyochukuliwa. Lissu kapigwa risasi 30+ Mungu kamnusuru lkn mioyo ya Watanzania ikawa jiwe dhidi ya jiwe.
Kesi zisizo kichwa wala miguu zimeshamiri kipindi hiki kuliko wakati wowote katika historia ya nchi yetu. Bado tumekaa kimya.
6. Miaka 5 imefika lakini hakuna mtumishi aliyeongezwa mshahara. Bado wananchi wamekuwa jiwe kama alivyo jiwe kuu.
7. Tumeona wanasiasa wetu wananunulika kirahisi, wakihama vyama ovyo, waliotoka upinzani kwenda CCM, wakapitishwa kuendelea na uwakilishi, waliotoka CCM kwenda upinzani wakaandamwa. Baadhi wamerudi mfano Sumaye na Lowasa. Katiba imevunjwa kwa maslahi ya CCM, bado wananchi wamefanywa jiwe kama jiwe kuu mwenyewe.
8. Wabunge kuwekwa ndani bila dhamana hata kwa kesi zenye dhamana imekuwa kawaida, bado mioyo imekuwa migumu tu.
9. Matumizi mabaya ya madaraka na pesa ya umma imekuwa kawaida. Pesa zinachotwa kwenda chato na kusikojulikana. Michango mbalimbali ya hisani bado haikuwafikia wahanga. Na DC na RC wakajiona watemi wakisweka watu mahabusu kwa kesi za kijinga tu. Bado tumekuwa na moyo jiwe na jiwe anatuendesha kwelikweli.
10. Uvunjaji mikataba usiozingatia sheria imegharimu nchi, ndege zetu japo zilinunuliwa bila kufuata sheria zikikamatwa mara mbili. Sasa tumepata soko la nyama Belgium, ndege zetu hazina uwezo wa kupeleka shehena hizo tumetumia za RwandaAir. Ni aibu ni aibu sana.
11. Pigo la corona ndo hatari zaidi. Diplomasia imekufa. Watanzania wanaonekana ni wagonjwa, Watanzania wananyanyaswa, tumefurushwa nchi mbalimbali sasa hakuna anayetuamini.
Watumishi wa afya hawana PPE, pesa zimechangwa vifaa hakuna.
Covid inasambaa, hakuna ckrantini sasa vifo vimekuwa balaa.
Mapigo yote haya kama CCM itachomoa, basi Watanzania tujitambue sisi ni wagonjwa wa akili.
Mie naona ukombozi wa taifa hili umewadia. Wasalaaam.
Ongeza na mengine.
Ntamaholo.
Sent using Jamii Forums mobile app