Uchaguzi 2020 Mapigo matatu kwa Bernard Membe katika harakati zake za kuitafuta Ikulu

Bernard Membe amekuwa akipitia nyakati mbalimbali za machungu makubwa kwake katika harakati zake za muda mrefu za kuitafuta Ikulu ya Chamwino. Mapigo hayo yamezidi kufifisha ndoto yake hiyo ya mchana ambayo amekuwa akiiota kila uchao.

Pigo la Kwanza: Hili pigo alilipata mwaka 2015. Ni dhahiri kuwa mwaka ule alikuwa ameshaanza hata kufanya rehearsal ya kuapishwa, na alikuwa ameshaanza hata kutembea kimapozi kama Rais kwani alikuwa na uhakika kwa asilimia nyingi kuwa angeweza kuwa Rais wa Tanzania. Pigo kwake ilikuwa ni Kamati Kuu ya CCM kumkata jina, na hivyo kumuondoa kwenye orodha ya majina ya Wanachama Watatu ambao majina yao yalipelekwa kwenye Mkutano Mkuu ili kupigiwa kura na hivyo kumpata Mgombea kupitia chama hicho.

Pigo la Pili: Hili pigo alilipata baada ya kuvuliwa uanachama wa CCM. Baada ya kukosa nafasi hiyo, Membe bado aliendelea kuwa na imani kuwa mwaka 2020 atagombea nafasi hiyo. Matokeo yake ni kuwa alikamia sana hata akawa anavunja misingi waliyojiwekea kama chama, na hata mara nyingine akaonekana kuwa ni mtovu wa nidhamu. Hali hiyo ilipelekea chama kumvua uanachama wake, na hivyo likawa ni pigo lake la pili.

Pigo la tatu: Upinzani nao wote wamemkataa mchana kweupe. CHADEMA wamekataa kuungana naye, na hivyo kila chama kimeendelea na mchakato wa uchaguzi kivyake. Membe amebaki na ACT yake ambayo alihamia baada ya CCM kumtema. ACT-Wazalendo walimuahidi kumpa nafasi ya kugombea Urais kupitia chama hicho. Membe kipindi fulani alisema atakuwa tayari kugombea iwapo upinzani wangeamua kuungana na kumsimamisha yeye kama Mgombea wao. Ni dhahiri kuwa alijipa “Face Value” kubwa sana wakati wapinzani aliotaka waungane wanamuona kuwa ana “Actual Value” ndogo sana. Membe alitamani sana Chadema wakubali kumuunga mkono yeye; hivyo kitendo cha Chadema kumtema na kumteua Lissu kuwa Mgombea wao na Salum Mwalimu kuwa mgombea mwenza limekuwa ni pigo jingine kwa ndugu yetu Membe.

Yajayo yanafurahisha, Uko Tayari?
Loud and clear
 
mimi membe sijawahi kumuhamini hata siku moja, namuona kama mCCM damu damu aliyelelewa na CCM tangu enzi za chipukizi aliyeletwa uku upinzani kama ilivyokuwa kwa lowasa, sumaye, akina guninita na ata mzee kingunge kuja kutughiribu tu ili baadae atuhache kama alivyotufanyia Lowasa.

Pia tukumbuke kuna mda Bashiru Ally aliwai kusema kuwa wanaweza kumsamehe ili arudi kundini ikiwa na maana kuwa bado ni mtu wao na uku upinzani ni mpango wao maCCM kuwa akiumaliza tu mpango wake atarejea uko.

Malizia damdam ccm awamu ya 4. maumivu!
 
Ukweli Membe hana mvuto wa kisiasa...mtu pekee wapinzani tunaweza kumtumia na kushinda tukiwa siriazi ni TUNDU ATIPAS LISSU
 
Kwa vyovyote mzee angebaki angejenga imani sana kwa wana upinzani na mashabiki,umenena sawia kabisa.
Kuna mbinu zinafeli. Uchaguzi huu ni mgumu. Kumrudisha mzee wa mabadiliko ccm lilikuwa kosa. Yeye ndo alitakiwa ampokee membe upinzani ila sijui ni woga kuwa watabadili gia wachukue nchi kweli au ni nn kilitokea.
 
Mkuu, lakini endapo matokeo ya uchaguzi hayatatoa mshindi wa zaidi ya 50%, yaani tuseme Membe akipata 38% Lissu 40% na Magufuli 22% itapasa uchaguzi uingie "round" ya pili, na kwa vyovyote vile itampasa Membe apambane na Lissu, na ni lazima wana CCM watamuunga mkono Membe, kwa kuwa zimwi likujualo ....
Daa...hv huwa mnawazaga nn hadi uandike ushuzii kama huu..who is membe by z way??
 
Mkuu, lakini endapo matokeo ya uchaguzi hayatatoa mshindi wa zaidi ya 50%, yaani tuseme Membe akipata 38% Lissu 40% na Magufuli 22% itapasa uchaguzi uingie "round" ya pili, na kwa vyovyote vile itampasa Membe apambane na Lissu, na ni lazima wana CCM watamuunga mkono Membe, kwa kuwa zimwi likujualo ....
Na kwa Mara ya kwanza toka siasa za vyama vingi zianze hili ndilo litakalotokea mwaka huu

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Mkuu, lakini endapo matokeo ya uchaguzi hayatatoa mshindi wa zaidi ya 50%, yaani tuseme Membe akipata 38% Lissu 40% na Magufuli 22% itapasa uchaguzi uingie "round" ya pili, na kwa vyovyote vile itampasa Membe apambane na Lissu, na ni lazima wana CCM watamuunga mkono Membe, kwa kuwa zimwi likujualo ....
Ndoto za mchana siku hizi zakubalika
 
Hesabu kuwa Magu ana 80% hiyo iliyobaki wagawane kina Membe, Lissu, nk
Ngumu sana mkuu. Anzia Kikwete awamu ya kwanza alianza na ngp na ya pili ngap na JPM alianza na ngap asilimia za ushindi hapo ndy utajua hyo negative gradient inaenda wapi. Mwaka huu kampeni lazma ziwe ngumu sana na ushindi utakua Tait sana!!

Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
 
Unaota ndoto za mchana. JPM apate 22% ?
Mkuu, lakini endapo matokeo ya uchaguzi hayatatoa mshindi wa zaidi ya 50%, yaani tuseme Membe akipata 38% Lissu 40% na Magufuli 22% itapasa uchaguzi uingie "round" ya pili, na kwa vyovyote vile itampasa Membe apambane na Lissu, na ni lazima wana CCM watamuunga mkono Membe, kwa kuwa zimwi likujualo ....
 
Bernard Membe amekuwa akipitia nyakati mbalimbali za machungu makubwa kwake katika harakati zake za muda mrefu za kuitafuta Ikulu ya Chamwino. Mapigo hayo yamezidi kufifisha ndoto yake hiyo ya mchana ambayo amekuwa akiiota kila uchao.

Pigo la Kwanza: Hili pigo alilipata mwaka 2015. Ni dhahiri kuwa mwaka ule alikuwa ameshaanza hata kufanya rehearsal ya kuapishwa, na alikuwa ameshaanza hata kutembea kimapozi kama Rais kwani alikuwa na uhakika kwa asilimia nyingi kuwa angeweza kuwa Rais wa Tanzania. Pigo kwake ilikuwa ni Kamati Kuu ya CCM kumkata jina, na hivyo kumuondoa kwenye orodha ya majina ya Wanachama Watatu ambao majina yao yalipelekwa kwenye Mkutano Mkuu ili kupigiwa kura na hivyo kumpata Mgombea kupitia chama hicho.

Pigo la Pili: Hili pigo alilipata baada ya kuvuliwa uanachama wa CCM. Baada ya kukosa nafasi hiyo, Membe bado aliendelea kuwa na imani kuwa mwaka 2020 atagombea nafasi hiyo. Matokeo yake ni kuwa alikamia sana hata akawa anavunja misingi waliyojiwekea kama chama, na hata mara nyingine akaonekana kuwa ni mtovu wa nidhamu. Hali hiyo ilipelekea chama kumvua uanachama wake, na hivyo likawa ni pigo lake la pili.

Pigo la tatu: Upinzani nao wote wamemkataa mchana kweupe. CHADEMA wamekataa kuungana naye, na hivyo kila chama kimeendelea na mchakato wa uchaguzi kivyake. Membe amebaki na ACT yake ambayo alihamia baada ya CCM kumtema. ACT-Wazalendo walimuahidi kumpa nafasi ya kugombea Urais kupitia chama hicho. Membe kipindi fulani alisema atakuwa tayari kugombea iwapo upinzani wangeamua kuungana na kumsimamisha yeye kama Mgombea wao. Ni dhahiri kuwa alijipa “Face Value” kubwa sana wakati wapinzani aliotaka waungane wanamuona kuwa ana “Actual Value” ndogo sana. Membe alitamani sana Chadema wakubali kumuunga mkono yeye; hivyo kitendo cha Chadema kumtema na kumteua Lissu kuwa Mgombea wao na Salum Mwalimu kuwa mgombea mwenza limekuwa ni pigo jingine kwa ndugu yetu Membe.

Yajayo yanafurahisha, Uko Tayari?
Pamoja na maelezo mazuri, lkn pia unaonekana upo mbali kidogo na mambo ya kisiasa au hata kisheria. Nchi yetu haina ushindi wa asilima 50. Nchi yetu inaushindi wa wingi wa kura. Hata kama wamepishana kura moja aliezidi ndo hutangazwa mshindi.
 
Kitendo cha BM kuanzisha ACT akiwa serikalini kinamwondolea uhalali wa kuwa mpizani halisi naona anatumika tuu.
 
Mkuu, lakini endapo matokeo ya uchaguzi hayatatoa mshindi wa zaidi ya 50%, yaani tuseme Membe akipata 38% Lissu 40% na Magufuli 22% itapasa uchaguzi uingie "round" ya pili, na kwa vyovyote vile itampasa Membe apambane na Lissu, na ni lazima wana CCM watamuunga mkono Membe, kwa kuwa zimwi likujualo ....
Utaratibu wa Ushindi katika Chaguzi za Kisiasa Tanzania ni 'First Past the Post' na hakuna threshold ya percentage! Kwa hiyo kwa percentage ulizoweka hapo tayari Tundu Lissu yuko Chamwino.

Kwa dhana nyingine ni kwamba, hata wakiwa wagombe 100, mgombea wa kwanza akaongoza kwa 9% , wengine 99 wakagawana 91% zilizisalia, basi aliyeongoza kwa 9% ndo Rais wako!

Kwa lugha nyepesi, Tanzania mtu anakuwa Rais, hata akikushinda kura moja tu, regardless ni zaidi ya 50% au pungufu ya 50%.

Nawasilisha!
 
Mkuu, lakini endapo matokeo ya uchaguzi hayatatoa mshindi wa zaidi ya 50%, yaani tuseme Membe akipata 38% Lissu 40% na Magufuli 22% itapasa uchaguzi uingie "round" ya pili, na kwa vyovyote vile itampasa Membe apambane na Lissu, na ni lazima wana CCM watamuunga mkono Membe, kwa kuwa zimwi likujualo ....
Ni Membe yupi unayemzungumzia wakupata 38 % ? Akipata 8 % nishitue.
 
Ilishafutwa hiyo na maccm, sasa hivi mshindi ni yule mwenye kura nyingi.
... ndio hiyo simple majority aliyekuzidi hata kwa kura moja ndiye mshindi; yaani wewe una 17% na yeye ana 17.0001% yeye ni mshindi. Mkapa ndiye aliyefuta ile ya at least 50%.
 
Mkuu, lakini endapo matokeo ya uchaguzi hayatatoa mshindi wa zaidi ya 50%, yaani tuseme Membe akipata 38% Lissu 40% na Magufuli 22% itapasa uchaguzi uingie "round" ya pili, na kwa vyovyote vile itampasa Membe apambane na Lissu, na ni lazima wana CCM watamuunga mkono Membe, kwa kuwa zimwi likujualo ....
Siwezi kuota ndoto hii hata nikiwekwa kisiwa cha patimo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom