Karucee
JF-Expert Member
- Mar 11, 2012
- 18,146
- 34,190
The best advice she could use right now.Amekubikiri halafu akasepa. Na huyu huyu kesho na kesho kutwa utamkuta kwa akina Jokajeusi akilalamika kuwa siku hizi hakuna mabikra wa kuoa!
Kuhusu kuumia hakuna njia ya mkato binti yangu. Ni lazima uumie tu. Ila kwa kadri siku zinavyokwenda maumivu yataanza kupungua, kutaanza kupambazuka na hatimaye jua litachomoza tena, moyo wako utapona polepole; na furaha yako itarudi.
Jitahidi kujiweka bize. Kama una marafiki wa kweli kuwa nao karibu. Ndugu pia na hasa mama. Huu ndiyo wakati wa kumuomba akupe stori za usichana wake...pia soma neno la Mungu na kusali sana (kama ni muumini)
Na usiache kulia. Ukijisikia kulia we lia tu. Hiyo ndiyo tiba yenyewe hasa. Utapona na ukija kuangalia experience yako hii ya kwanza na wanaume utakuwa umejifunza mengi....
Na safari ndo imeanza rasmi sasa. It gonna be a bumpy ride ahead. You better fasten your seat belt. Kila la heri