Mapenzi Yanataabu

Game Theory

JF-Expert Member
Sep 5, 2006
8,545
833
GetAttachmentaspx.jpg



Mapenzi yantaaabu,

Usiku kucha silali

nikaapo hukuonaaa

Imeniruka akili

Upita kwa lako jina

kumbe chako kivuli

mwenyewe sinaye sinawe tenaa
 
Shukran mwinyi.

lakini nilitaka kukufahamisha tuu kuwa hiyo ni shairi la nyimbo nyimbo iliyopigwa na Culture.
 
Nimekupata mpenzi , Mpenzi wangu wa ndani
Mi mwenzio sijiwezi Sina raha duniani
Nataka yako mapenzi Uliyonipa zamani

Mapenzi ni kikohozi Kuyaficha huwa kazi
Nina kiu ya mapenzi Tokea enzi na enzi
Nimekupata mpenzi Nakuomba unienzi

Ulinionjesha raha Raha zako za ajabu
Imekua ni karaha Moyoni napata tabu
Mapenzi sio karaha Nitoe hii aibu

Ni macho yaonapo Moyo huwa mashakani
Yasingelionapo Moyo usingetamani
Moyoni bado upo Japo kua huamini
 

Mpenzi njoo kwa haraka,
Sijamaliza mapenzi bado nakutaka!

Mbona ulipoondoka hukuniaga mpenzi,
Mwenzako nakukukumbuka yananitoka machozi,
Rudi wangu muhibaka unifutie simanzi!

Tangu ulipoondoka moyoni sina tabasamu,
Kuwaza na kukumbuka mapenzi yako matamu,
Na iwapo hutafika ninahiari kunywa sumu!

Toka ulipoondoka sina furaha moyoni,
Kuwaza na kukumbuka la kutenda silioni,
Rudi wangu nyonda nami niwe furahani!
Njoo kwa haraka!!!

 
"hakuna mwingine kuliko wewe,
nakonda kwa maradhi ya mapenzi nilokuwa nayo!"
 
"mapenzi ni hayawani avumaye kama gharika kuu"
"upepo ukipita ananywea na kusinyaa kama nungunungu aliyeshituliwa"
 
Sabalkheri mpenzi waonaje hali yako....
Sabal'Ain habibi, hali yangu kama yako.....
Wawaonaje wazazi nyumbani utokeako.....


Haya na mtu apokee hapo jamani....
 
Nikitembea mbele naiona sura yako,
Nipo tayari nife nikikukosa wewe,
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom