Its Pancho
JF-Expert Member
- Sep 21, 2018
- 14,081
- 22,362
Kwa kweli mapenzi ni upumbavu sijui kwanini yaliletwa duniani .
Nimeshuhudia watu wakiteseka na kudiriki kujiua kisa tu mapenzi. Baba mkubwa huko kijijini alikuwa na mke mkubwa baadae akafariki kwahiyo ikabidi aoe mke mwengine ambaye alikuwa binti mdogo.
Yule binti kazi yake ilikuwa kuwatesa watoto wa mzee mkubwa yule huko kuwatumikisha makazi mengi. Na bado mzee huyo akirudi anapewa kesi za uzushi kuwa wanae wamemtukana huyo mama yao wa kambo
Mara wamegoma kufanya kazi. Kwahiyo anawaadhibu vibaya pasipo kutambua anawaonea wanae wa kuwazaa.
Yule binti kwa kuwa alikuwa ni dam changa na aliolewa kutokana na tamaa ya maisha. Basi akawa anagawa uroda kwa vijana wadogo hapo kijijini na tetesi zinasambaa. Ila baba mkubwa yeye alikuwa alikuwa hasikii wala haoni.
Niishie hapa kwa sasa yule binti yupo morogoro huko kaolewa na kijana mwenzie. Watoto wa baba mkubwa tuliwachukua mmoja kamaliza mtihani wa kidato cha 6.
Baba mkubwa yuko huko kijijini alipoumwa sisi ndo tulimpeleka hospitali wakati alipomuoa yule binti ,aliwahi kuwakana ndugu zake na kusema wanamuharibia ndoa yake kwani ameoa binti mbichi hivyo wanamuonea wivu.
Mapenzi ni ujinga yanaficha vitu hasa uovu mwingi. Na ushetani mwingi. Tusilipize mabaya kwa mabaya .bali tulipe kwa mema kwani hujui kesho yako ni ipi. Na atakuokota nani.
Nimeshuhudia watu wakiteseka na kudiriki kujiua kisa tu mapenzi. Baba mkubwa huko kijijini alikuwa na mke mkubwa baadae akafariki kwahiyo ikabidi aoe mke mwengine ambaye alikuwa binti mdogo.
Yule binti kazi yake ilikuwa kuwatesa watoto wa mzee mkubwa yule huko kuwatumikisha makazi mengi. Na bado mzee huyo akirudi anapewa kesi za uzushi kuwa wanae wamemtukana huyo mama yao wa kambo
Mara wamegoma kufanya kazi. Kwahiyo anawaadhibu vibaya pasipo kutambua anawaonea wanae wa kuwazaa.
Yule binti kwa kuwa alikuwa ni dam changa na aliolewa kutokana na tamaa ya maisha. Basi akawa anagawa uroda kwa vijana wadogo hapo kijijini na tetesi zinasambaa. Ila baba mkubwa yeye alikuwa alikuwa hasikii wala haoni.
Niishie hapa kwa sasa yule binti yupo morogoro huko kaolewa na kijana mwenzie. Watoto wa baba mkubwa tuliwachukua mmoja kamaliza mtihani wa kidato cha 6.
Baba mkubwa yuko huko kijijini alipoumwa sisi ndo tulimpeleka hospitali wakati alipomuoa yule binti ,aliwahi kuwakana ndugu zake na kusema wanamuharibia ndoa yake kwani ameoa binti mbichi hivyo wanamuonea wivu.
Mapenzi ni ujinga yanaficha vitu hasa uovu mwingi. Na ushetani mwingi. Tusilipize mabaya kwa mabaya .bali tulipe kwa mema kwani hujui kesho yako ni ipi. Na atakuokota nani.