Mambo Jambo
JF-Expert Member
- Jul 11, 2008
- 1,100
- 81
hapo ulipo Highlight unamaanisha nini ???????aah
MJ = Mambo Jambo
hapo ulipo Highlight unamaanisha nini ???????aah
Nimesoma thread inavoenda nikashindwa hata kuelewa kama kweli kuna ukweli wowote kuhusu shutuma zinazoelekezwa kwa mke za kusababisha kifo cha mume.Kwani ni mara ngapi mke anakufa na mume anaoa hapohapo na hakuna mtu anamshutumu kuwa ameoa haraka haraka bila shaka yeye ndio kamuua mkewe! Ingekuwa hivyo, basi aslimia karibu 80% ya wanawake wanaokufa basi ingesemekana wameuawa na waume zao maana waume huoa punde.
Pamoja na kuwa sishabikii au kufagilia kitendo cha mwanamama huyu kukimbilia kuolewa immediately, nadhani huyu amejaribu kubadilisha mwelekeo kwa kufanya kitu ile roho yake inataka.Wanawake huwa wanajali sana jamii itamfikiria vipi kama ataolewa baada ya mume kufa kama ambavyo hapa huyu anadhaniwa kamuua mumewe ili aolewe. Halafu kitu kingine hatujaambiwa kama mmama huyo ana watoto au la maana hii ni material fact, na je walikuwa na uhusiano vipi na marehemu kwa maana ya maelewano ya mke na mume?...mimi najua cases kadhaa ambapo kwa mfano mume alikuwa na nyumba ndogo baada ya kupata pesa nyingi na kusahau kabisa familia.Alipoishiwa huko nyumba ndogo akarudi main house ambapo mama alishaanza maisha ya kujitegemea kwa kuchacharika na ujasiriamali.Huyo bwana aliporudi hakukaa hata wiki akafariki maana alirudi mgonjwa. Yule mama alichofanya alisafiri na maiti ya mumewe kwenda kuzika na kesho yake akapanda ndege kuelekea kwenye mihangaiko yake na hakujali nani atasema nini.
Nadhani hatupaswi kuhukumu mambo yanayowatokea majirani zetu maana hatujui undani wa maisha yao. KITANDA MTU USICHOKILALIA HUTAJUI KUNGUNI WAKE WANAUMA NAMNA GANI.
issue hapa ni mme alikufa na mke akaolewa ndani ya mwezi ..na kwa sababu ilikuwa very short time ndo maana watu waliwaza wanayojua wao Kwa binadamu mwenye akili timamu hawezi fanya hivi ,,,,hata wewe mdada siamini kama unaweza fanya hivi-no labda unaweza nisiusemee moyo
1.Kuhusu kama naweza kufanya hivyo au la..nadhani post yangu imeanza na disclaimer...kuwa sifagilii wala kuunga mkono hicho kitendo cha kukimbilia kuolewa...
2. HUTUJUI UNDANI WA KILICHOKUA KINAENDELEA BAINA YA HAWA WATU...
kuna ndoa nyingi siku hizi ni keeping up appearances na hakuna ndoa kama ndoa....
Pia sitaki kuamini kuwa huyo mama "alifunga ndoa" kama tunavyoelewa kufunga ndoa.... maana kuna mengi yanayohitajika kabla hujafunga ndoa..in short umeiweka hii mada katika namna simple mno kiasi kwamba inakuwa na maswali mengi zaidi ya majibu na ndio maana kama wachangiaji tunatoa michango simple hivyo hivyo.Umesema huyo mdada ni mkristo.... kweli anaruhusiwa kuolewa kama mume amefariki..lakini usisahau kisheria kuna wiki tatu za kutangaza na mambo mengine...sasa hiyo ndoa ya mwezi mhhhh sijui....labda utufafanulie zaidi.
issue hapa ni mme alikufa na mke akaolewa ndani ya mwezi ..na kwa sababu ilikuwa very short time ndo maana watu waliwaza wanayojua wao Kwa binadamu mwenye akili timamu hawezi fanya hivi ,,,,hata wewe mdada siamini kama unaweza fanya hivi-no labda unaweza nisiusemee moyo
sijui!Wewe ulitaka akae muda gani? Kwahiyo angekaa miaka 2 basi usingemdhania kuwa ameuwa?
sijui!
Komredi kiwanja kipo maeneo ya tegeta huko mwisho mwisho kabisa ni pazuri ijapokuwa sijaend asiku nyingi
FL..ni vema kama tukakubaliana na ripoti ya daktari wa jirani yako, unless kuna ushahidi kuwa alimuua labda kwa kumchoma kisu au kumpiga risasi etc
Ni kisa kilichoniacha mdomo wazi wenzangu ...hivi unaweza penda mpaka ukafikia hatua ya kuua ..??
katika hali ya kutatanisha mama mmoja inasadikika alimuua mmewe mwenye takribani miaka 42 na yeye after 1 month akaolewa na kijana wa miaka 30 wakati yeye alikuwa na miaka 35
Huyu mama ni jirani yangu tukio la kuolewa ndani ya mwezi baada ya kifo cha mmewe limenifanya niamini ni kweli alimuua mmewe
Nini siri ya penzi la hatari na lenye kutisha namna hiii??
FL
una uhakika gani aliuwa?
sawa kabisa hatuhukumu ngoja tusubiri mungu ahukumu mwenyewe
lakini Boss 1 month ni muda mfupi sana kuamua jambo kubwa kama hilo
Firstlady1, Ninavyojua mimi (nakubali kurekebishwa) kwa kawaida huwa wanakaa eda siku 40. Sasa hesabu inaonyesha huyo dada ana less 10 days.
Lazima kuna mazingira yaliyopelekea mama achukue/aolewe mapema.
Mambo yamebadirika sana siku hizi, zamani wifi au shangazi alibaki na mfiwa kwa siku 40. Siku hizi watu hata matanga hawakai, tukizika tu palepale makaburini tunaambiwa shughuli ya msiba imekwisha. Kila mtu anaondokea makaburini kuelekea kwake. Mazingira haya yataleta mabadiriko mengi ktk jamii ya kileo.
Ni bora huyo aliyeonyesha wazi, wapo wengi wanafanya hivyo lakini haiwi issue kwa sababu wanajificha.
Mimi binafsi nampongeza dada kwa kuweka mambo hadharani kwamba hawezi ishi ndani bila kuwa na kichwa. Anahitaji ulinzi.