Mapendekezo yaliyosaulika kwenye Ripoti mbili za makinikia: Serikali Yamulikeni.

Musoma Yetu

JF-Expert Member
Mar 11, 2016
2,629
2,288
Mapendekezo haya yangefaa kama ripoti mbili za makinikia zilipaswa kuyaongeza. Nimeona niongezee mwenyewe. 1. Anzisheni au imarisheni vitengo vya utafiti(research and development) kila wizara au mtakavyoona inafaa na watoe taarifa zao kila robo mwaka. Taarifa hizi mbili ni matunda ya tafiti. 2. Hivi vitengo havipo kabisa kwenye halmashauri wala mikoa yetu.Taarifa zingekuwa zinaanza kutoka huko. 3. Nchi zote zilizoendelea wanafanya maamuzi yao na kutekeleza kulingana na tafiti zilisemaje au zinasemaje.Tuache tabia za kufanya maamuzi ya vikao bila kuwa na tafiti. 4. Wizara zote zinaongozwa na mawaziri na makatibu wakuu wasomi mfano ma professor au madoctor! Mnashindwa nini kuishauri serikali kuimarisha au kuweka vitengo vya tafiti. Mbona huko vyuoni mlikotoka matafiti mlikuwa mnafanya, sasa huku mnashindwa nini? Nawasilisha.
 
Sizonje akipewa Tilioni 100+ kutoka kwenye Kampuni yenye Utajiri wa Tilioni 9+ na yeye ni mwizi tu
 
MKUU TANZANIA YETU TUNAIJUA WENYEWE,WACHA TUJIENDESHE TUJUAVYO
Sawa, lakini sasa ni muda wa kubadilika. Tusitumie ile mifumo ya zamani. Bila research and developments, uchumi wa kati tutakuwa tunausikia kwenye radio tu
 
Sizonje akipewa Tilioni 100+ kutoka kwenye Kampuni yenye Utajiri wa Tilioni 9+ na yeye ni mwizi tu
Ni mzalendo, nanyani kaonyesha njia!! Angezitaka alikuwa na uwezo wa kuzichota, lkni nahisi anapenda awanufaishe watanzania
 
Mapendekezo haya yangefaa kama ripoti mbili za makinikia zilipaswa kuyaongeza. Nimeona niongezee mwenyewe. 1. Anzisheni au imarisheni vitengo vya utafiti(research and development) kila wizara au mtakavyoona inafaa na watoe taarifa zao kila robo mwaka. Taarifa hizi mbili ni matunda ya tafiti. 2. Hivi vitengo havipo kabisa kwenye halmashauri wala mikoa yetu.Taarifa zingekuwa zinaanza kutoka huko. 3. Nchi zote zilizoendelea wanafanya maamuzi yao na kutekeleza kulingana na tafiti zilisemaje au zinasemaje.Tuache tabia za kufanya maamuzi ya vikao bila kuwa na tafiti. 4. Wizara zote zinaongozwa na mawaziri na makatibu wakuu wasomi mfano ma professor au madoctor! Mnashindwa nini kuishauri serikali kuimarisha au kuweka vitengo vya tafiti. Mbona huko vyuoni mlikotoka matafiti mlikuwa mnafanya, sasa huku mnashindwa nini? Nawasilisha.
Hizo tafiti ni kwa ajili ya kufanyia mitihani.
Tafiti nyingi ni copied.
 
Back
Top Bottom