Mapendekezo ya muundo wa baraza la mawaziri - 2010-2015

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,463
39,929
MAPENDEKEZO YA MUUNDO WA BARAZA LA MAWAZIRI 2010- NA SABABU ZAKE

Na. M. M. Mwanakijiji

Ni mara chache sana katika kipindi cha utawala tunaweza kupata nafasi ya kutoa mawazo juu ya muundo wa Baraza la Mawaziri. Hakuna wakati mzuri wa kufanya hivyo kama kufuatia uchaguzi mkuu kwani ni wakati huu ndipo mwelekeo wa serikali unaonekana. Wakati mbaya ni wakati ambapo baraza jipya linaundwa katikati ya vipindi vya uchaguzi kufuatia kujiuzulu, kifo cha Waziri Mkuu au kuvunjwa na Rais.

Baraza la Mawaziri ndilo hutoa dalili ya mwelekeo wa serikali inayoingia madarakani. Ilani ya Uchaguzi ya chama na kampeni za siasa ni kwa ajili ya kuomba ridhaa ya kuwaongoza wananchi na baada ya kuchaguliwa chama kilichoshinda hujiandaa kushika madaraka na baada ya taratibu zote za kurasimisha ubunge kukamilika kinachosubiriwa ni kuundwa kwa Baraza la Mawaziri a.k.a Serikali. Baraza la Mawaziri ndicho chombo kikuu cha ushauri kwa Rais na usimamizi wa serikali. Hivyo, kwa kuangalia Baraza lilivyo unaweza kupata picha ya nini kitafanywa na serikali inayokuja. Hakuna haja ya kusikiliza hotuba, kuangalia maneno, semina bali kuangalia baraza limepangwaje ili kutekeleza ilani ya uchaguzi na pili nani anaingia kwenye bara hilo. Timu inaweza kuwa na jina kubwa, bajeti kubwa na kocha mzuri; hata hivyo kazi ipo katika wachezaji wake na mfumo na mikakati yao ya ushindi.

Mapendekezo haya ninayatoa yakiakisi mwelekeo wa serikali ya CCM na Ilani yake. Endapo Dr. Slaa angetangazwa mshindi basi ningetoa mapendekezo yenye kuakisi mabadiliko makubwa ya kimfumo ambacho Chadema ilikuwa imeyaahidi. Kwa vile ajenda ya CCM haikuwa inalenga mabadiliko makubwa ya kimfumo wa utawala mapendekezo yangu basi yameegemea katika mambo makubwa manne tu:

Kupunguza ukubwa wa serikali (lean government)
Kupanga wizara kwa mantiki ya utendaji wake (logical flow of operation)
Kurahisisha mtiririko wa utendaji (streamlining performance)
Kulenga ufanisi wa matokeo kuliko mchakato (result oriented government)

Mapendekezo haya pia yamezingatia mfumo wa baraza la mawaziri ya baadhi ya nchi zinazoendelea na hata zilizoendelea ambazo zimefanya mageuzi makubwa ya mifumo yao ya utawala na kujiweka katika nafasi za kufanikiwa. Nchi ambazo nimepitia mabaraza yake ni:

Indonesia
Korea ya Kusini
Namibia
Botswana
Afrika ya Kusini
Canada
Marekani
Kwa ujumla nimeweza kufikia wizara 23. Kati ya hizi wizara 19 ziko wizara kamili nje za ofisi za Rais, Makamu na Waziri Mkuu. Ina maana ofisi hizo za kiutendaji zinabakia na wizara nne tu au tatu kutegemea na wapi Wizara ya Utumishi wa Umma itawekwa. Kati ya wizara hizo 23 ni saba tu zitakuwa na Manaibu Waziri.

Ninazigawa wizara hizi katika makundi makubwa matano kulingana na mwelekeo wa majukumu yao. Mgawanyo huu hauchori mipaka isiyovukika kati ya wizara na wizara (nyingi zinaingiliana) bali ni mgawanyo wa kuzielewa tu na kuziwezesha kuonekana vizuri katika mwelekeo wa utendaji wake. Ni sawasawa na jinsi wachezaji wa soka wanvyojipanga uwanjani wakati wa mpira kuanza huku kila mmoja akionekana vizuri katika nafasi yake lakini wakianza kucheza tunaweza kuwaona wanavyohusiana, kupishana, kusaidiana na hatimaye kuweza kuleta ushindi.

Wizara za Usalama na Ulinzi
Wizara za Kijamii na Maisha
Wizara za Mambo ya Uchumi na Uzalishaji Mali
Wizara za Utawala na Uwajibikaji
Wizara za Nchi

Katika makala ya mapendekezo ambayo nimeambatanisha hapa nimechangua sababu za kwanini wizara fulani iwe au iko mahali fulani. Hivyo, kabla ya kukosoa nashauri mtu apitie makala hiyo ili kidogo awe ameingia kichwani mwangu kuelewa the reasoning behind ili mtakaponikosoa mnikosoe kwa haki. Kauli ya "mwanakijiji mimi sijasoma makala yako lakini.." ni dalili ya kuwa presumptuous. So, nashauri take time to read halafu kosoa, halafu tujadiliane kwani kwa kufanya hivyo tutakuwa tumegonganisha vichwa (brain storming) na kutoa mchango hata usiozingatiwa au kukubaliwa wa serikali tunayoona itafaa.

WIZARA ZOTE



  1. Wizara ya Ulinzi na JKT - Ministry of Defense & National Service
  2. Wizara ya Mambo ya Ndani, Uhamiaji na Vikosi vya Uokoaji - Ministry of Home Affairs, Immigration and Rescue Forces
  3. Wizara ya Usalama wa Taifa- Ministry of National Security
  4. Wizara ya Afya - Ministry of Health
  5. Wizara ya Elimu - Ministry of Education
  6. Wizara ya Maendeleo ya Jamii - Ministry of Community Development
  7. Wizara ya Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia - Ministry of Science and Technological Development
  8. Wizara ya Ardhi, Nyumba Vijijini na Maendeleo ya Miji - Ministry of Land, Rural Housing and Urban Development
  9. Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo. Ministry of Culture, Arts and Sports
  10. Wizara ya Fedha na Uchumi - Ministry of Finance and Economic Affairs
  11. Wizara ya Biashara, Viwanda, Masoko, na Uwekezaji - Ministry of Trade, Industry and Investments
  12. Wizara ya Nishati na Raslimali za Mafuta - Ministry of Energy and Oil Resources
  13. Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu - Ministry of Infrastructure Development
  14. Wizara ya Mazingira, Utalii na Uhifadhi wa Wanyama Pori - Ministry of Environment, Tourism and Wildlife Conservation
  15. Wizara ya Madini - Ministry of Mining
  16. Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi - Ministry of Agriculture, Livestock and Fisheries
  17. Wizara ya Maji na Usalama wa Chakula - Ministry of Water Resources and Food Security
  18. Wizara ya Mambo ya Nje - Ministry of Foreign Affairs
  19. Wizara ya Haki na Usimamizi wa Sheria - Ministry of Justice and Law
  20. Wizara ya Utumishi wa Umma na Utawala - Ministry of Public Service and Administration
  21. Wizara ya Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Masuala ya Muungano - Ministry of State Vice President's Office - Union Affairs
  22. Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa - Ministry of State Local Governments and Regional Administrations
  23. Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Masuala ya Bunge.
 

Attachments

  • cabinetproposal2010-2015.doc
    42.5 KB · Views: 134
hongera mwanakijiji hii imekaa kiakili sana , i wish jk angepita hapa apate mawazo
 
hongera mwanakijiji hii imekaa kiakili sana , i wish jk angepita hapa apate mawazo

thanks.. huwa tunalalamikiwa mara nyingi kuwa tunapenda kukosoa sana na kuwa hatutoi mapendekezo ya nini kifanyike... well.. kwa mara nyingine tunatoa mawazo na mapendekezo.. hata wakichukua asilimia 50 tu.. ni kuonesha kuwa wanajali. Sasa wakitangaza baraza lao tutakapokosoa watajua tuna reasoning gani.
 
Wewe si miongoni mwa wale wasiomtambua Rais?! Sidhani kama atautambua ushauri wako, kwa sababu huonyeshi kuwa na nia nzuri na Rais wetu.
 
Yaani mimi kumtambua au kutomtambua kunamfanya awe rais au asiwe? Urais wake hautegemei kutambuliwa na watu kama mimi bali na tume ya uchaguzi.
 
Baraza la mawaziri linatangazwa lini?

je wana muda wa kupingia mapendekezo na kufanya change kwa kujilizisha vya kutosha.
 
@Mwanakijiji.

Thanks for taking your time kutoa ushauri wa bure, hili ni jema kwani hata kama kuna mgongano wa kiitikadi, kutoa mawazo hakukatazwi na mimi binafsi kwa sasa naangalia mbele ingawa mwizi wangu namju.. sidhani kama tunahitaji wizara 23, in an efficient and controlled government like ours... 15-16 would suffice...

  • ondoa wizara no 23 huna haja ya wizaya ya PM/Bunge wakati unajua kabisa hiyo ni kuongeza nguvu ya ubakaji wa demokrasia... sioni kwanini
  • wizaras no 4,5,6 na 9 zaweza kuwa mbili tu... hazi na tija wala hazibadili perfomrance kutokana na muundo uliopo
  • unganisha 19-20 (watu kama akina ghasia wanajaza nafasi tu kwenye mawizara
  • nyuma ningeweka na ardhi
  • madini ningeweka na nishati
 
@Mwanakijiji.

Thanks for taking your time kutoa ushauri wa bure, hili ni jema kwani hata kama kuna mgongano wa kiitikadi, kutoa mawazo hakukatazwi na mimi binafsi kwa sasa naangalia mbele ingawa mwizi wangu namju.. sidhani kama tunahitaji wizara 23, in an efficient and controlled government like ours... 15-16 would suffice...

  • ondoa wizara no 23 huna haja ya wizaya ya PM/Bunge wakati unajua kabisa hiyo ni kuongeza nguvu ya ubakaji wa demokrasia... sioni kwanini
  • wizaras no 4,5,6 na 9 zaweza kuwa mbili tu... hazi na tija wala hazibadili perfomrance kutokana na muundo uliopo
  • unganisha 19-20 (watu kama akina ghasia wanajaza nafasi tu kwenye mawizara
  • nyuma ningeweka na ardhi
  • madini ningeweka na nishati

Can you please put up a new list to reflect ur proposal?
 
Kwanza nikushukuru kwa mapendekezo yako mazuri ambayo hat hivi hakuna mtu atashughulika nayo kama ujuavyo viserikali fisadi kama haka ka kwetu!!!!!. Hata hivyo binafsi bado naona umependekeza wizara nyingi kulinganisha uwezo wa serikali hususani kwa kushindwa kukosekana kwa nidhamu katika kusimamia ukusanyaji na matumizi ya pato zima na rasilimali za nchi yetu wote. Tanzania haina uhaba wa mawazo mapya au endelevu! na hata kama tusingekuwa nayo kuna shida kuiga toka kwa wenzetu!?

Nikirudi kwenye wizara pendekezwa hapo juu baadhi ya wizara kwangu mimi bado naona hazihitajiki, kama wizara ya nchi ofisi ya waziri mkuu-bunge,wizara ya madini wizara ya nishati na rasilimali mafuta,hata wizara ya sayansi na tekinolojia bado yaweza kuwa ndani ya wizara ya elimu ni ikafanya vizuuri tu.Tanzania bado ni nchi ndogo sana kkwa upande wa rasilimali na miundo mbinu kuwa na wizara chungu nzima ni wizi tu na kugawana madaraka kusiko kuwa na manufaa kabisaa kwa taifa.
 
hizo wizara naona kama zimekuwa nyingi sana? I hope kuna njia inawezekana kuzi reduce......my view
 
Tujenge consesus ya wizara zipi ziwepo na kwa nini. Tatizo la wizara ya bunge ni kwa sababu mfumo wetu wa kiingereza. Binafsi ningeweza kufuta wizara zote za nchi kwani shughuli zao zingeweza kufanywa na taasisi nyingine. Nitatengeneza orodha nyingine kama tunaweza kuwa na wizara kati ya 16-20. Tuendelee kutoa mawazo.
 
@Mwanakijiji.

Thanks for taking your time kutoa ushauri wa bure, hili ni jema kwani hata kama kuna mgongano wa kiitikadi, kutoa mawazo hakukatazwi na mimi binafsi kwa sasa naangalia mbele ingawa mwizi wangu namju.. sidhani kama tunahitaji wizara 23, in an efficient and controlled government like ours... 15-16 would suffice...

  • ondoa wizara no 23 huna haja ya wizaya ya PM/Bunge wakati unajua kabisa hiyo ni kuongeza nguvu ya ubakaji wa demokrasia... sioni kwanini
  • wizaras no 4,5,6 na 9 zaweza kuwa mbili tu... hazi na tija wala hazibadili perfomrance kutokana na muundo uliopo
  • unganisha 19-20 (watu kama akina ghasia wanajaza nafasi tu kwenye mawizara
  • nyuma ningeweka na ardhi
  • madini ningeweka na nishati
Mapendekezo haya ndiyo yenye tija. Hata Botswana ina wizara 15 tu lakini zimeonyesha ufanisi mkubwa sana katika kufanikisha maendeleo ya Taifa hili linalotegemea zaidi Madini ya Almasi na Utalii pekee kujiendesha. Kuwa na wizara 23 haitasaidia kwani nyingi bado zina majukumu yanayoingiliana mno.
 
Kuna mahala nilipendekeza kama ifuatavyo


...................idadi ya Wizara na Mawaziri.......zisizidi 20...............na ninapendekeza kama ifuatavyo

1. Ministry of Finance and Public Service
2. Ministry of Foreign Affairs (includes EA portfolio)
3. Ministry of Education, Science and Technology
4. Ministry of Health
5. Ministry of Legal Affairs
6. Ministry of Housing, Lands and Surveys
7. Ministry of Agriculture, Livestock and Marine Resources
8. Ministry of Labour and Social Development
9. Ministry of National Security (Polisi, Jeshi, TAKUKURU, UwT, Magereza na Uhamiaji)
10. Ministry of Public Works, Utilities and Transport
11. Ministry of the Environment, Energy, Minerals and Water Resources
12. Ministry of Tourism
13. Ministry of Information,Youths, Sports and Culture
14. Ministry of Trade and Industry
15. Ministry of Local Governments
16. Ministry of Aviation and Telecommunication
 
Ogah.. tatizo la namba 9 ni utofauti wa hizo taasisi kuziweka chini ya mtu mmoja au wizara moja zitaingiliana sana kiasi kwamba hazitakuwa efficient. Kuweka JWTZ na Polisi, Magereza na UwT kwenye eneo moja sidhani kama ni mpangilio mzuri.

Namba 16, 10 na 13 utaona zingeweza labda kuunda wizara mbili na siyo tatu

Sijaelewa mantiki ya kuweka Finance na Public Service mahali pamoja.. ni kwanini?

Na labda kwanini Tourism iwe wizara peke yake?
 
Hakuna haja ya wizara lukuki namna hii...
Kwani wizara kumi haziwezi kufanya kazi?... Wingi wa wizara ni sawa na gharama kubwa kwa Mtanzania.... WE DO NOT NEED IT BE
 
Ogah.. tatizo la namba 9 ni utofauti wa hizo taasisi kuziweka chini ya mtu mmoja au wizara moja zitaingiliana sana kiasi kwamba hazitakuwa efficient. Kuweka JWTZ na Polisi, Magereza na UwT kwenye eneo moja sidhani kama ni mpangilio mzuri.

Sawa sawa

Namba 16, 10 na 13 utaona zingeweza labda kuunda wizara mbili na siyo tatu

Sawa sawa

Sijaelewa mantiki ya kuweka Finance na Public Service mahali pamoja.. ni kwanini?

Moja ya Matumizi makubwa sana ya serikali yako hapo kwenye Public Service.............uwiano wa matumizi ya public service unatakiwa uwe controlled sana na PS wa Finance.................experience iliyopo sasa indhihirisha un-controlled expenditure kubwa kwenye Public service........

Na labda kwanini Tourism iwe wizara peke yake?

Moja ya vyanzo vikuu vya pato la Taifa ni Utalii..............nina imani tuiongeza juhudi/ tukaweka kipaumbele Utalii......unalipa....we need to do more on Utalii....inahitajika focus kubwa.............

Mpanglio mpya baada ya maoni yako nikama ifuatavyo

1. Ministry of Finance, Economic Planning and Public Service
2. Ministry of Foreign Affairs (includes EA portfolio)
3. Ministry of Education, Science and Technology
4. Ministry of Health
5. Ministry of Legal Affairs
6. Ministry of Housing, Lands and Surveys
7. Ministry of Agriculture, Livestock and Marine Resources
8. Ministry of Labour and Social Development
9. Ministry of National Security (Polisi, TAKUKURU, UwT, Magereza na Uhamiaji)
10. Ministry of Public Works, Aviation, Telecommunication and Transport
11. Ministry of the Environment, Energy, Minerals and Water Resources
12. Ministry of Tourism
13. Ministry of Information,Youths, Sports and Culture
14. Ministry of Trade and Industry
15. Ministry of Local Governments
16. Ministry of Defense & National Service

NOTE:
Ukijumuisha na State Ministries i.e. Utawala Bora, Muungano na Bunge hazitakiwi zizidi 20
 
Mwanakijiji,

Nakukubali sana!

We can borrow a leaf from Zanzibar ambapo (Utumishi na Utawala Bora) ni wizara moja chini ya ofisi ya Rais.
7. Mimi naamini Science inatakiwa irudi kwenye elimu... Information iunganishwe na Communication. Mambo ya Science bado yamekaa kishule shule, research research vile... hii information and communication is actual implementations....
 
MAPENDEKEZO YA MUUNDO WA BARAZA LA MAWAZIRI 2010- NA SABABU ZAKE

Na. M. M. Mwanakijiji

Ni mara chache sana katika kipindi cha utawala tunaweza kupata nafasi ya kutoa mawazo juu ya muundo wa Baraza la Mawaziri. Hakuna wakati mzuri wa kufanya hivyo kama kufuatia uchaguzi mkuu kwani ni wakati huu ndipo mwelekeo wa serikali unaonekana. Wakati mbaya ni wakati ambapo baraza jipya linaundwa katikati ya vipindi vya uchaguzi kufuatia kujiuzulu, kifo cha Waziri Mkuu au kuvunjwa na Rais.

Baraza la Mawaziri ndilo hutoa dalili ya mwelekeo wa serikali inayoingia madarakani. Ilani ya Uchaguzi ya chama na kampeni za siasa ni kwa ajili ya kuomba ridhaa ya kuwaongoza wananchi na baada ya kuchaguliwa chama kilichoshinda hujiandaa kushika madaraka na baada ya taratibu zote za kurasimisha ubunge kukamilika kinachosubiriwa ni kuundwa kwa Baraza la Mawaziri a.k.a Serikali. Baraza la Mawaziri ndicho chombo kikuu cha ushauri kwa Rais na usimamizi wa serikali. Hivyo, kwa kuangalia Baraza lilivyo unaweza kupata picha ya nini kitafanywa na serikali inayokuja. Hakuna haja ya kusikiliza hotuba, kuangalia maneno, semina bali kuangalia baraza limepangwaje ili kutekeleza ilani ya uchaguzi na pili nani anaingia kwenye bara hilo. Timu inaweza kuwa na jina kubwa, bajeti kubwa na kocha mzuri; hata hivyo kazi ipo katika wachezaji wake na mfumo na mikakati yao ya ushindi.

Mapendekezo haya ninayatoa yakiakisi mwelekeo wa serikali ya CCM na Ilani yake. Endapo Dr. Slaa angetangazwa mshindi basi ningetoa mapendekezo yenye kuakisi mabadiliko makubwa ya kimfumo ambacho Chadema ilikuwa imeyaahidi. Kwa vile ajenda ya CCM haikuwa inalenga mabadiliko makubwa ya kimfumo wa utawala mapendekezo yangu basi yameegemea katika mambo makubwa manne tu:

Kupunguza ukubwa wa serikali (lean government)
Kupanga wizara kwa mantiki ya utendaji wake (logical flow of operation)
Kurahisisha mtiririko wa utendaji (streamlining performance)
Kulenga ufanisi wa matokeo kuliko mchakato (result oriented government)

Mapendekezo haya pia yamezingatia mfumo wa baraza la mawaziri ya baadhi ya nchi zinazoendelea na hata zilizoendelea ambazo zimefanya mageuzi makubwa ya mifumo yao ya utawala na kujiweka katika nafasi za kufanikiwa. Nchi ambazo nimepitia mabaraza yake ni:

Indonesia
Korea ya Kusini
Namibia
Botswana
Afrika ya Kusini
Canada
Marekani
Kwa ujumla nimeweza kufikia wizara 23. Kati ya hizi wizara 19 ziko wizara kamili nje za ofisi za Rais, Makamu na Waziri Mkuu. Ina maana ofisi hizo za kiutendaji zinabakia na wizara nne tu au tatu kutegemea na wapi Wizara ya Utumishi wa Umma itawekwa. Kati ya wizara hizo 23 ni saba tu zitakuwa na Manaibu Waziri.

Ninazigawa wizara hizi katika makundi makubwa matano kulingana na mwelekeo wa majukumu yao. Mgawanyo huu hauchori mipaka isiyovukika kati ya wizara na wizara (nyingi zinaingiliana) bali ni mgawanyo wa kuzielewa tu na kuziwezesha kuonekana vizuri katika mwelekeo wa utendaji wake. Ni sawasawa na jinsi wachezaji wa soka wanvyojipanga uwanjani wakati wa mpira kuanza huku kila mmoja akionekana vizuri katika nafasi yake lakini wakianza kucheza tunaweza kuwaona wanavyohusiana, kupishana, kusaidiana na hatimaye kuweza kuleta ushindi.

Wizara za Usalama na Ulinzi
Wizara za Kijamii na Maisha
Wizara za Mambo ya Uchumi na Uzalishaji Mali
Wizara za Utawala na Uwajibikaji
Wizara za Nchi

Katika makala ya mapendekezo ambayo nimeambatanisha hapa nimechangua sababu za kwanini wizara fulani iwe au iko mahali fulani. Hivyo, kabla ya kukosoa nashauri mtu apitie makala hiyo ili kidogo awe ameingia kichwani mwangu kuelewa the reasoning behind ili mtakaponikosoa mnikosoe kwa haki. Kauli ya "mwanakijiji mimi sijasoma makala yako lakini.." ni dalili ya kuwa presumptuous. So, nashauri take time to read halafu kosoa, halafu tujadiliane kwani kwa kufanya hivyo tutakuwa tumegonganisha vichwa (brain storming) na kutoa mchango hata usiozingatiwa au kukubaliwa wa serikali tunayoona itafaa.

WIZARA ZOTE



  1. Wizara ya Ulinzi na JKT - Ministry of Defense & National Service
  2. Wizara ya Mambo ya Ndani, Uhamiaji na Vikosi vya Uokoaji - Ministry of Home Affairs, Immigration and Rescue Forces

    [*]Wizara ya Usalama wa Taifa- Ministry of National Security

  3. Wizara ya Afya - Ministry of Health
  4. Wizara ya Elimu - Ministry of Education
  5. Wizara ya Maendeleo ya Jamii - Ministry of Community Development
  6. Wizara ya Maendeleo ya Sayansi na Teknolojia - Ministry of Science and Technological Development
  7. Wizara ya Ardhi, Nyumba Vijijini na Maendeleo ya Miji - Ministry of Land, Rural Housing and Urban Development
  8. Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo. Ministry of Culture, Arts and Sports
  9. Wizara ya Fedha na Uchumi - Ministry of Finance and Economic Affairs
  10. Wizara ya Biashara, Viwanda, Masoko, na Uwekezaji - Ministry of Trade, Industry and Investments

    [*]Wizara ya Nishati na Raslimali za Mafuta - Ministry of Energy and Oil Resources

  11. Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu - Ministry of Infrastructure Development
  12. Wizara ya Mazingira, Utalii na Uhifadhi wa Wanyama Pori - Ministry of Environment, Tourism and Wildlife Conservation

    [*]Wizara ya Madini - Ministry of Mining

  13. Wizara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi - Ministry of Agriculture, Livestock and Fisheries
  14. Wizara ya Maji na Usalama wa Chakula - Ministry of Water Resources and Food Security
  15. Wizara ya Mambo ya Nje - Ministry of Foreign Affairs
  16. Wizara ya Haki na Usimamizi wa Sheria - Ministry of Justice and Law
  17. Wizara ya Utumishi wa Umma na Utawala - Ministry of Public Service and Administration
  18. Wizara ya Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Masuala ya Muungano - Ministry of State Vice President's Office - Union Affairs
  19. Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa - Ministry of State Local Governments and Regional Administrations
  20. Wizara ya Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu - Masuala ya Bunge.

Excellent Mkuu, That is the best picture how our New Government should look like, ila wasiwasi wangu # 12 & # 15 zinaweza kuwa wizara moja, think it again, pia wizara ya Usalama wa Taifa, hapo mkuu kidogo naona hawa jamaa wakiwa ma Mamlaka au Wakala (Agency) na si kuundiwa Wizara nzima, kuna sababu nyingi, ila bila Shaka mm na ww ni mashahidi hawa Usalama wa Taifa jinsi wanavyotumika na CCM, so hawana maana ya kupewa Wizara, otherwise uko sahihi, ila usiwe na wasiwasi JK ni mtu wa kukopy na paste, utaona lazima Serikali itafuata mapendekezo ya Dr (wa Kweli) Slaa, trust me, Good job
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom