Mapendekezo ya kutatua tatizo la wanafunzi kujiunga kidato cha kwanza bila kujua kusoma & kuandika

ENANTIOMER

JF-Expert Member
Sep 22, 2014
1,419
804
Wakuu habari za usiku.
Ntumaini sisi sote tunafahamu kuhusu hili swala la elimu msingi ambayo inamtaka kila mwanafunzi kusoma kuanzia elimu ya awali mpaka kidato cha nne bila malipo (maarufu kama elimu bure). Hi elimu msingi haitaki mwanafunzi aishie njiani, bali amalize kidato cha nne na ikibidi aendelee na masomo kama akifaulu. Kiufupi hii itakua elimu ya lazima kwa kila mtanzania kama ilivyo lazima kwa elimu ya mpaka darasa la saba kwasasa.

Pamoja na kua kuna mambo memngi ya kuangaliwa ktk elimu msingi, ila tuangalie hili moja la jinsi ya kutatua tatizo la wanafunzi kuingia kidato cha kwanza bila kujua kusoma wala kuandika. Kwa kuzingatia kua, lengo la mwanafunzi kujiunga na shule ni kwa ajili ya kujifunza na sio kukua, napendekeza jambo lifuatalo.

*** Napendekeza iwekwe sheria ya kuwabana walimu wakuu wahakikishe kua asiyejua kusoma na kuandika haruhusiwi kujiunga darasa la tano hata kama alitazamia majibu na kufaulu. Tena akiruhusu mwanafunzi asiyejua kusoma na kuandika kuingia darasa la tano, basi achukuliwe hatua za kisheria na mamlaka zinazohusika. kama hajui kuosma na kuandika, akariri darasa mpaka ajue.

kama mwanafunzi akifaulu kuingia kidato cha kwanza huku hajui kusomaa wala kuandika, sheria imuwajibishe mwalimu mkuu wa shule aliyotoka kwa kosa la kumruhusu mwanfunzi huyo kuingia darasa la tano bila kujua kusoma wala kuandika.

Mwalimu mkuu asijitete kua mimi nilihamia tu ktk ile shule nikakuta huyo mwanafunzi yuko darasa la 5, 6 au 7. Ikitokea mwalimu mkuu akahamia ktk shule fulani na akakuta kuna mwanafunzi yuko darasa la 5, 6 au 7 huku hajui kusoma wala kuandika, basi amrudishe mwanafunzi huyo darasa la nne akakae huko mpaka ajue kusoma na kuandika. Tena ikibidi mwalimu wa darasa husika ( darasa la 5, 6 au 7) awajibishwe kwa kuruhusu mwanafunzi huyo kuingia ktk daarasa analolisimamia yeye (darasa la 5, 6 au 7) huku akiwa hajui kusoma wala kuandika.

Tujiulize. Tunamvusha mwanafunzi asiyejua kusoma wala kuandika kuingia darasa la tano aende kufanya nini huko wakati hata kusoma wala kuandika hajui? Mwanaaunzi anapata faida gani kwa kuingia darasa la tano huku akiwa hajui hata kusoma na kuandika?

Nahitimisha kwa kusema kua lengo la mwanafunzi kujiunga na shule ni kwa ajili ya kujifunza na sio kukua, hivyo mwanafunzi asiyejua kusoma wala kuandika akariri darasa la nne mpaka ajue kusoma na kuandika.


Yangu ni hayo tu. Kama kuna marekebisho au nyogeza, basi ni vyema ukayaweka ili yajadiliwe.
Asanteni sana.
 
Umetoa ushauri mzuri sana ingawa umekaa kinadharia zaidi naamanisha hauwez kutekelezeka kirahc,
Kama msomi uliyeelimika ulitakiwa kubuni mipango ambayo serikali itaitumia katika kutatua tatizo la ajira nchini ili kuleta hamasa zaidi kwa vijana ya kusoma kwa bidii kuliko kuleta mada ambazo unajua kabisa hata miaka 100 ijayo hakiwez kutekelezeka try to think twice man
 
Umetoa ushauri mzuri sana ingawa umekaa kinadharia zaidi naamanisha hauwez kutekelezeka kirahc,
Kama msomi uliyeelimika ulitakiwa kubuni mipango ambayo serikali itaitumia katika kutatua tatizo la ajira nchini ili kuleta hamasa zaidi kwa vijana ya kusoma kwa bidii kuliko kuleta mada ambazo unajua kabisa hata miaka 100 ijayo hakiwez kutekelezeka try to think twice man
Kumbe unasubiri ajira!!! Pole sana kwa kua muathirika wa ukata wa pesa za kuajiri unaoikumba nchi yetu.

Tukirudi kwenye mada. Aliajiri mheshimiwa JK katika kipindi chake chote, ila wasiojua kusoma na kuandika bado wanaingia kidato cha kwanza. Sasa hapa pamoja na kua wanatakiwa kuajiri, ila kunahaja ya kutafuta njia za kutatua taizo hili kabisa. Nimesema wazi kua, ktk elimu msingi kuna mambo mengi ya kuangalia, ila kwasasa tuangalie jinsi ya kutatua kabisa tatizo la wanafunzi kujiunga na kidato cha kwanza huku wakiwa hawajui kusoma na kuandika. Njia niliyoiona mimi ni hiyo. Unaombwa uboreshe mawazo yangu, au pinge mawazo yangu kwa kutoa sababu zilizo wazi, au utoe wazo jipya ili kutatua tatizo kabisa na ueleze litatulikaje.
 
Mkuu umeanza vizuri sana ila tatizo la watoto kutojua kusoma hakusababishwi na walimu tu serikali hairuhusu mfumo wa kurudia rudia madarasa wanafunzi tofauti na shule za binafsi hakuna mwalimu ambaye hazimtoshi afurahie wakati mwanafunzi hajui kusoma swala lingine kuhusu darasa la saba kufanya mtihani angalia karatasi za kujibia yani mtoto anatia kivuli tu so kuufaulu mtoto ni rahisi sana mana anatia kivuli tu kabla ya kumwajibisha mwalimu lazima serikali iangalie hiyo mithani yani mpaka hisabati kutia kivuli tu
 
First thing shughulika na mwalimu,jamani siyo rahisi kumfundisha mtoto kusoma.
Njia ni moja na ndogo sana. MPE Mwl mshahara wake kikamilifu(quality & quantity ), halafu asipomwezesha mwanafunzi kusoma na kuandika, Mwl afukuzwe kaz nafas yake apewe aliye tayari. Walimu wengi wanafanya bora liende, japo wapo wachache ambao kwa kweli hujituma kwa dhat kabisa na kuwapenda watoto na kuwafundsha kwa upendo.
 
Mkuu umeanza vizuri sana ila tatizo la watoto kutojua kusoma hakusababishwi na walimu tu serikali hairuhusu mfumo wa kurudia rudia madarasa wanafunzi tofauti na shule za binafsi hakuna mwalimu ambaye hazimtoshi afurahie wakati mwanafunzi hajui kusoma swala lingine kuhusu darasa la saba kufanya mtihani angalia karatasi za kujibia yani mtoto anatia kivuli tu so kuufaulu mtoto ni rahisi sana mana anatia kivuli tu kabla ya kumwajibisha mwalimu lazima serikali iangalie hiyo mithani yani mpaka hisabati kutia kivuli tu
sijaongelea kumuwajibisha mwalimu kwa kusababisha mwanafunzi kushindwa kusoma, bali nimependekeza njia rahisi kwa pando zote mbili, serikali na walimu kuhakikisha, za kukomesha tatizo la wanafunzi wasiojua kusoma na kuandika kujiunga kidato cha kwanza. hayo mambo ya kutia kivuli pamoja na udanganyifu yapo tu na sina uhakika kama yataisha, hasa udanganyifu. cha msingi tuangalie hili, hata kama kuna kutia vivuli na udanganyifu, basi asiyejua kusoma asiwe miongoni wa watia vivuli na wadanganyifu. asiojua kusoma atie vivuli vya darasa la nne huko mpaka wjue kusoma.
 
Njia ni moja na ndogo sana. MPE Mwl mshahara wake kikamilifu(quality & quantity ), halafu asipomwezesha mwanafunzi kusoma na kuandika, Mwl afukuzwe kaz nafas yake apewe aliye tayari. Walimu wengi wanafanya bora liende, japo wapo wachache ambao kwa kweli hujituma kwa dhat kabisa na kuwapenda watoto na kuwafundsha kwa upendo.
nakubaliana na swala la maslahi ya walimu. mwalimu akilipwa vizuri atajituma zaidi na matokeo yatakua makubwa zaidi ya haya yasasa.
ila hata hivyo mwalimu kulipwa tu hakutaweza kuzuia wanafunzi kuingia kidato cha kwanza wakiwa hawajui kusoma na kuandika. swala la kuingia kidato cha kwanza bila kujua kusoma na kuandika linatokana na udaanganyifu unaofanywa na sisi walimu wenyewe tunaolipwa kidogo kwa kumsaidia mwanafunzi afaulu, ili tupate sifa ya kufaulisha kutoka kwa 'siri kali' inayotulipa kidogo. mapendendekezo yangu ni kwamba, kwakua mwanafuzi anaenda shule kujifunza, basi kama hajui kusoma na kuandika, abaki darasa la nne mpaka ajue kusoma na kuandika. tena ikibidi wale darasa la nne waliobaki kwa kutojua kusoma wandaliwe mazingira ya kipee ya kupikwa kikee. tena sheria iundwe ili kumbana mwalimu mkuu wa shule husika, kutoruhusu asiyejua kusoma kuingia darasa la tano.
 
Hivi wewe unajua mtoto harusiwi kurudia mara mbili shule za serikali au huna taarifa halafu mitihani ya darasa la saba unajua tofauti na jinsi ya kujibu? Unajua sasa unatumia Omr kushade hata asiye jua kusoma anaweza kufaulu kisa kushade herufi?
 
First thing shughulika na mwalimu,jamani siyo rahisi kumfundisha mtoto kusoma.
hilo la mwalimu ni muhimu sana.
polisi anapokea posho ya laki tatu ktkt ya mwezi, huku mwisho wa mwezi anapokea pia laki tatu na kidogo baada ya makato yote. jumla polisi huyo anapokea jumla ya laki sita na kidogo baada ya makato yote.
kipindi polisi anapokea jumla ya laki sita kwa mwezi baada ya makato yote; mwalimu aliyefaulu form 4, kisha kufaulu form 6, kisha kwenda chuo kikuu na kukwepa mishale yote ya sapu na kudisco, analipwa laki tano na kidogo baada ya makato yote.

malipo ya jumla ya laki 6 na kidogo kwa polisi aliyeishia form 4
malipo ya jumla ya laki 5 na kidogo kwa mwalimu aliyefika mpaka chuo kikuu.
hii ni ajabu sana na inavunja moyo.
 
Hivi wewe unajua mtoto harusiwi kurudia mara mbili shule za serikali au huna taarifa halafu mitihani ya darasa la saba unajua tofauti na jinsi ya kujibu? Unajua sasa unatumia Omr kushade hata asiye jua kusoma anaweza kufaulu kisa kushade herufi?
kama haruhusiwi kurudia zaidi ya mara mbili, basi aanze kuruhusiwa kurudia hadi atapoweza kusoma na kuandika. lengo la yeye kwenda shule ni kujiunza na sio kukua, hivyo kama hajui hajui kusoma na kuandika, arudie darasa la nne mpaka wezeze kusoma na kuandika.

mwanafunzi anafaidikaje kwa kuruhusiwa kusonga mbele zaidi huku akiwa akiwa hajui hata kusoma na kuandika?
 
Njia ni moja na ndogo sana. MPE Mwl mshahara wake kikamilifu(quality & quantity ), halafu asipomwezesha mwanafunzi kusoma na kuandika, Mwl afukuzwe kaz nafas yake apewe aliye tayari. Walimu wengi wanafanya bora liende, japo wapo wachache ambao kwa kweli hujituma kwa dhat kabisa na kuwapenda watoto na kuwafundsha kwa upendo.
Ngumu sana mkuu,unamfundisha vp mtoto wa mtu wakati hujui hata utakachokula,utakapolala na basic needs nyingine?Imetosha tulivyowaonea waalimu jamani! They deserve better life.otherwise tutegemee machungu zaidi.
 
Ngumu sana mkuu,unamfundisha vp mtoto wa mtu wakati hujui hata utakachokula,utakapolala na basic needs nyingine?Imetosha tulivyowaonea waalimu jamani! They deserve better life.otherwise tutegemee machungu zaidi.
hivi ni kweli walimu anafundisha huku akiwa hajui hata anachokula? kumbe walimu wanafanya kazi ya kujitolea.

mimi naona utofauti wa kimaslahi kwa walimu mpaka kufikia kushindwa hata na polisi. unakuta mwalimu aliyemaliza chuo kikuu, anashindwa mbali kimaslahi na hata polisi aliyeishia kidato cha nne. hili la kubaguliwa na kudharauiwa kimaslahi ndio linaovunja moyo.
 
Back
Top Bottom