omtiti
JF-Expert Member
- Jun 19, 2019
- 1,022
- 1,590
Kama mwana ccm mkereketwa naomba uongozi wa juu hasa kamati kuu ya ccm, ambayo itahusika na uchujaji wa majina ya wagombea watakao peperusha bendera ya ccm kwenye uchaguzi mkuu October mwaka huu kwa nafasi ya ubunge jimbo la Kigamboni yafuatayo
Nashauri na kupendekeza Jina la Makonda ndio lirudi na lipeperushe bendera ya ccm jimbo la kigamboni, ni kijana ambae anaijua vizuri Dar, fitina zote anazijua, pia anaimudu vizuri kasi na maelekezo ya Rais Magufuli, hii itakua ni chachu nzuri kwa utawala huu ikiwa Makonda atapata uteuzi kwa nafasi ya uwaziri, sipati picha huku Makonda kule Alexander Mnyeti, Jaffo, Kigwa, Bashe, Bashungwa mchakamcha wa hatari. Hakuna kulala, vijana wana ndoto na matamanio ya utumishi uliotukuka.
Baraza la mawaziri lijalo linahitaji vijana zaidi kukimbiza, isipokua kwa nafasi ya waziri mkuu, waziri wa fedha, waziri wa mambo ya nje na waziri wa sheria wawe watu wazima kutokana na unyeti wa wizara hizo.
Ndugulile ateuliwe kuwa balozi nchi yoyote huko Ulaya, na aachwe kipindi chote cha miaka mitano, asitumbuliwe, cha msingi atimize majukumu yake kwa ufanisi wa hali ya juu.
Ni maoni yangu tu, si lazima kuyazingatia
Nashauri na kupendekeza Jina la Makonda ndio lirudi na lipeperushe bendera ya ccm jimbo la kigamboni, ni kijana ambae anaijua vizuri Dar, fitina zote anazijua, pia anaimudu vizuri kasi na maelekezo ya Rais Magufuli, hii itakua ni chachu nzuri kwa utawala huu ikiwa Makonda atapata uteuzi kwa nafasi ya uwaziri, sipati picha huku Makonda kule Alexander Mnyeti, Jaffo, Kigwa, Bashe, Bashungwa mchakamcha wa hatari. Hakuna kulala, vijana wana ndoto na matamanio ya utumishi uliotukuka.
Baraza la mawaziri lijalo linahitaji vijana zaidi kukimbiza, isipokua kwa nafasi ya waziri mkuu, waziri wa fedha, waziri wa mambo ya nje na waziri wa sheria wawe watu wazima kutokana na unyeti wa wizara hizo.
Ndugulile ateuliwe kuwa balozi nchi yoyote huko Ulaya, na aachwe kipindi chote cha miaka mitano, asitumbuliwe, cha msingi atimize majukumu yake kwa ufanisi wa hali ya juu.
Ni maoni yangu tu, si lazima kuyazingatia