Mchumia Rungu
JF-Expert Member
- Apr 26, 2013
- 1,434
- 821
Na aliyepita kwa rushwa ni lazima afikishwe mahakamani yeye pamoja na wajumbe. Kwasababu mtoa rushwa na anayepokea rushwa, wote ni wakosaji kisheria.Na hapo ndipo mchakato mzima wa kura za maoni unapo kuwa hauna maana. Sasa Kama maoni ya wengi yanaonesha wanamkubali zaidi mgombea fulani, kwa nini apitishwe ambaye hakubaliki na wengi? Kamati zilitakiwa ziangalie kama mchakato ulifuata taratibu walizo jiwekea mfano kuhakikisha mgombea hakupita kwa kutoa rushwa. Siyo kukataa chaguo la wengi kutokana na mtu mmoja kuamka vibaya siku hiyo.