Benjamini Netanyahu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2014
- 80,710
- 93,456
Nashauri viongozi wafanye yafuatayo kuondoa omba omba kwenye miji mikubwa, si ungi mkono kuwa na omba omba lakini kuna omba omba wa aina mbili, Omba omba wa kweli na wa uongo. Wa kweli ni wale ambao unakuta mtu kweli anamatatizo na hana namna ya kujikimu, kama ugonjwa na uzee, lakini wa uongo ni wale ambao wamefanya kuwa njia ya kujikimu na wananguvu za kufanya kazi lakini hawataki kufanya kazi.
Watanzania kwa umoja wetu na upendo tukiamua tunaweza kuwasaidia hawa ndugu zetu na kubadilisha hali zao za kimaisha.
Watanzania tupo milioni 45 na kila mtanzania akatoa shilingi elfu 1 tu yaani 45,000,000 x 1,000 = 45,000,000,000. Ambazo ni fedha nyingi sana, nimesema kila mtu elfu 1 tu, kuna wengine ni watoto siyo wote watatoa, lakini kuna wengine watatoa milioni 1 hapo anakuwa amewatolea watu elfu 1. Hii elfu moja kwa kila mtu ni wastani. Hizi fedha zikagawanywa kwa kila kanda 4 billion 8 = billion 32 baki billion 13 kwa ajili ya kanda ya pwani sababu ina omba omba wengi.
Hizi fedha zikifanya yafuatavyo:-
i. Kununua hekari 200 kwa kila kanda (Kaskazini, Ziwa Victoria, Kati, Kusini na Pwani) yaani hekari 1,000 x 2,000,000 = 2,000,000,000
ii. Kujenga mabweni ya kisasa kwa ajili ya kulala watu, kuchimba visima na wale ombaomba wenye nguvu kutumika kufanya kazi hapo kambini.(skim za umwagiliaji)n.k
iii. Kujenga shule kwa ajili ya watoto wa omba omba na wa mazingira magumu.
iv. Kujenga zahanati kwa ajili ya kuwahudumia.
v. Kujenga nyumba kwa ajili ya watumishi (walimu, wataalamu wa afya, wataalamu wa kilimo, uvuvi, walinzi na wengineo).
vi. Kununua trecta za kisasa kwa kila kanda kwa ajili ya kilimo.
vii. Kununua mifungo(Ng’ombe, Mbuzi, Kuku, samaki, nyuki nk).
Fedha hizi zikisimamiwa vizuri omba omba watapata mazingira bora na watafundishwa kujitengemea na wazee wasiojiweza watahamishiwa huko hatimaye tutakuwa na taifa lenye maadili mazuri.
Hapa tutakuwa tumewawezesha kujitegemea kupitia miradi yao wenyewe.
Viongozi wakizisimamia hasa kwa utawala huu wa hapa kazi tu, mambo yataenda vizuri badala ya kuwafukunza tu mjini na hawajui wanaenda wapi.
Viongozi wakifanya kampeni/kuhamasisha fedha hizi zitapatikana, mimi nitalipia watu 30 yaani elfu 30 nitatoa kwa kuanza. Tunaweza kuchangia kupitia Vodacom, tigo pesa, Airtel money nk.
Kampeni hii inaweza kufanyika ndani ya mwezi mmoja tu.
Angalizo
Fedha zisimamiwe na Raisi au Waziri Mkuu.
Mambo yapo mengi lakini nimeamua kuandika machache kulingana na muda naamini kuna wachumi wazuri Tanzania wanaweza kuandika andiko zuri zaidi yangu.
Naomba kuwasilisha kutoka Babati Manyara.
Tuwasiliane
0715-163816
Isack
Babati – Manyara.
Watanzania kwa umoja wetu na upendo tukiamua tunaweza kuwasaidia hawa ndugu zetu na kubadilisha hali zao za kimaisha.
Watanzania tupo milioni 45 na kila mtanzania akatoa shilingi elfu 1 tu yaani 45,000,000 x 1,000 = 45,000,000,000. Ambazo ni fedha nyingi sana, nimesema kila mtu elfu 1 tu, kuna wengine ni watoto siyo wote watatoa, lakini kuna wengine watatoa milioni 1 hapo anakuwa amewatolea watu elfu 1. Hii elfu moja kwa kila mtu ni wastani. Hizi fedha zikagawanywa kwa kila kanda 4 billion 8 = billion 32 baki billion 13 kwa ajili ya kanda ya pwani sababu ina omba omba wengi.
Hizi fedha zikifanya yafuatavyo:-
i. Kununua hekari 200 kwa kila kanda (Kaskazini, Ziwa Victoria, Kati, Kusini na Pwani) yaani hekari 1,000 x 2,000,000 = 2,000,000,000
ii. Kujenga mabweni ya kisasa kwa ajili ya kulala watu, kuchimba visima na wale ombaomba wenye nguvu kutumika kufanya kazi hapo kambini.(skim za umwagiliaji)n.k
iii. Kujenga shule kwa ajili ya watoto wa omba omba na wa mazingira magumu.
iv. Kujenga zahanati kwa ajili ya kuwahudumia.
v. Kujenga nyumba kwa ajili ya watumishi (walimu, wataalamu wa afya, wataalamu wa kilimo, uvuvi, walinzi na wengineo).
vi. Kununua trecta za kisasa kwa kila kanda kwa ajili ya kilimo.
vii. Kununua mifungo(Ng’ombe, Mbuzi, Kuku, samaki, nyuki nk).
Fedha hizi zikisimamiwa vizuri omba omba watapata mazingira bora na watafundishwa kujitengemea na wazee wasiojiweza watahamishiwa huko hatimaye tutakuwa na taifa lenye maadili mazuri.
Hapa tutakuwa tumewawezesha kujitegemea kupitia miradi yao wenyewe.
Viongozi wakizisimamia hasa kwa utawala huu wa hapa kazi tu, mambo yataenda vizuri badala ya kuwafukunza tu mjini na hawajui wanaenda wapi.
Viongozi wakifanya kampeni/kuhamasisha fedha hizi zitapatikana, mimi nitalipia watu 30 yaani elfu 30 nitatoa kwa kuanza. Tunaweza kuchangia kupitia Vodacom, tigo pesa, Airtel money nk.
Kampeni hii inaweza kufanyika ndani ya mwezi mmoja tu.
Angalizo
Fedha zisimamiwe na Raisi au Waziri Mkuu.
Mambo yapo mengi lakini nimeamua kuandika machache kulingana na muda naamini kuna wachumi wazuri Tanzania wanaweza kuandika andiko zuri zaidi yangu.
Naomba kuwasilisha kutoka Babati Manyara.
Tuwasiliane
0715-163816
Isack
Babati – Manyara.