Elections 2010 Mapendekezo kwa CCM kufuatia "the Walkout"...

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,460
39,928
Nimefuatilia kwa kina mwitikio wa watu mbalimbali na hususan wa viongozi wa CCM kufuatia the "walkout" a.k.a "kutoka nje" kulikofanywa na wabunge wa Chadema jana. Hata hivyo nimejitolea kutoa ushauri ufuatao kwa viongozi wa CCM maana mwitikio wao hadi sasa unalenga kukoleza (escalate) mgongano wa kisiasa nchini. Ninaamini katika hali iliyopo mzigo wa busara na hekima unawaangukia CCM zaidi kuonesha ukomavu wa kisasa na demokrasia. Nina mambo kadhaa ya kushauri kupunguza (diffuse) hali ya utete iliyopo:

1. CCM itambue mkorogano wa uchaguzi mkuu na hususan matatizo yaliyotokea katika utengazaji wa matokeo. Hadi hivi sasa inaonekana CCM hawajaonesha hata mara moja kutambua utata na mvurugano wa matokeo ya uchaguzi. Hii inawafanya waonekane hawajali jinsi gani uchaguzi unaendeshwa au matokeo yanatangazwa. Hivyo, jambo la kwanza ni kukubali kuwa utangazaji wa matokeo (hata kama umewanufaisha wao) haukuwa katika hali ya kujivunia. Wakubali tatizo ambalo mamilioni ya Watanzania waliliona kufuatia uchaguzi mkuu.

2. CCM ioneshe kutambua tatizo letu la Tume ya Uchaguzi ilivyoendesha utangazaji wa matokeo ya Ubunge na Urais kiasi cha kusababisha maelfu ya vijana wetu kurundikana katika vituo mbalimbali "kulinda kura". Kama Taifa hatuwezi kwenda kwenye uchaguzi mwingine na mfumo huu kwani haumnufaishi yeyote zaidi ya kuweka msukumo katika jamii wakati wa uchaguzi ambao ungeweza kuleta madhara makubwa. CCM ioneshe na yenyewe inataka Tume inayofanya kazi kwa ufanisi, uhuru na uwazi. Ni kwa maslahi ya vyama vyote kuwa na Tume iliyo huru, wazi na ya kisasa.

3. CCM ioneshe kutokana na 1 na 2 hapo juu kuwa ipo haja ya kufanyia mabadiliko ya Katiba hasa kwenye suala la kuzuia au kupinga matangazo ya kura za Rais. Kwa wakati huu mfumo uliopo unaonekana kuinufaisha CCM. Lakini ni mfumo mbaya siku hali ikiwa kinyume na CCM. Kumbe ni kwa maslahi ya CCM na vyama vingine vyote kuweka utaratibu ambapo kura za Rais haziwezi kuonekana zinapandikizwa au Tume kulazimika kutangaza kwa sababu ikishatangaza basi hakuna wa kuhoji na wote wanatakiwa kupiga magoti kukubali matokeo hata kama kuna dalili ya upotofu. Ninaamini kwa chama kikongwe kama CCM ambacho kinajivunia kuwa ni "Baba ya Demokrasia" ni muhimu kuonesha kuwa hakiogopi mfumo mzuri na wa kisasa wa utangazaji wa kura za Urais.

4. CCM isijaribu kwa namna yoyote kutekeleza tishio lake la kuwafukuza wabunge wa Chadema Bungeni. Tayari taifa limeshagawanyika na kitendo chochote kitakachoonekana kuwa ni cha kibabe (wengi tunakumbuka suala la Zitto na Buzwagi) kitakoleza mgongano wa kisiasa nchini. Kuwafukuza CHADEMA hakutasababisha watu wakubali isipokuwa kama watawapeleka mahakamani Watanzania wote ambao hawako tayari kutambua ushindi wa Kikwete na kuwalazimisha kukubali ushindi huo chini ya tishio la kifungo. Vinginevyo, hekima kubwa inatakiwa kutumika na mimi ninaamini hekima hiyo inaanzia na:

- Uongozi wa CCM uanzishe mazungumzo na Uongozi wa CHadema kujaribu kusikilizana. Nilitoa pendekezo la wagombea kukutana kabla ya uchaguzi kwani niliamini wakati ule ndio ulikuwa wakati muafaka wa kufanya hivyo kabla hatujafika hapa tulipofika, na wakiendelea kuringishiana mapembe watajikuta wanalazimishwa kukaa chini huku machozi yanatoka. Tusifike huko.
- Kanuni za makubaliano zitengenezwe ili maridhiano yaanze; lakini ni lazima ziwe kanuni zenye kukubali hali halisi na zenye msingi wa haki na uwazi. Mazungumzo yasifanyike katika masharti kabla ya mazungumzo (pre-conditions).

5: Endapo CCM haitaona ulazima wa kufanyia kazi mapendekezo hayo kwa sababu "wameshinda" na kuwa hawako tayari kukubali kufanya mazungumzo na Chadema kwa kisingizio au sababu yoyote ni wazi kuwa wanalazimisha watu wenye dhamira tofauti kutii dhamira zao kuliko vitisho. Vitisho, mikwara, au hatua ambazo zitaonekana kuwalazimisha watu kupiga magoti kwa kutii kunaweza kuwatisha baadhi ya watu lakini kamwe hazijawahi kufanikiwa mahali popote duniani kuwatiisha watu wote wakati wote. Ndio maana nasema hekima inahitajika kuliko nguvu au vitisho vya nguvu.


6. Ni matumaini yangu kuwa CHadema nao hawajafunga mlango wa mazungumzo na watakuwa tayari kuwasikiliza CCM katika hali ya udugu, na uelewano wa kisiasa. Vinginevyo kidemokrasia ninaamini mgawanyiko uliopo ni mzuri na unakoleza tofauti za kisasa na hivyo kutuletea mapendekezo tofauti kabisa ya mwelekeo wa taifa. Katika demokrasia hatuwezi wote kuimba wimbo mmoja, kucheza ngoma moja na wote kukubaliana mtazamo mmoja. Ni muhimu kutambua kuwa ni katika tofauti zetu ndio demokrasia hukolezwa, na kudumishwa. Lakini ni muhimu tofauti hizo zisifikie uhasama wa kisiasa (political hostility) kitu ambacho ninaamini kinategemea kwa asilimia 100 maamuzi yatakayofanywa na CCM.

Ndiyo hoja zangu na ninazisimamia.
MMM
 
Pamoja na yote CCM watambue kuwa gharama ya kurudia uchaguzi ni ndogo kuliko kurudisha amani ambayo wanataka kuipoteza
 
yote hayo ni zao la katiba ya viraka inayosema taifa letu ni ujamaa na kujitegemea wakati sivyo,inampa rais mamlaka makubwa kama kamungu kadogo,ni muda wa mabadiliko ya katiba,nawaomba hao ccm ambao ndio walioshika dola wayakaribishe hayo mabadiliko kwa amani,kinyume chake ni vurugu
 
acha tu noma iwe noma ndo tunataka sie..hivi hivi hawaelewi hawa wanatakiwa practical sessions ,theory tumepiga nao sana hawaelewi
 
Nimefuatilia kwa kina mwitikio wa watu mbalimbali na hususan wa viongozi wa CCM kufuatia the "walkout" a.k.a "kutoka nje" kulikofanywa na wabunge wa Chadema jana. Hata hivyo nimejitolea kutoa ushauri ufuatao kwa viongozi wa CCM maana mwitikio wao hadi sasa unalenga kukoleza (escalate) mgongano wa kisiasa nchini. Ninaamini katika hali iliyopo mzigo wa busara na hekima unawaangukia CCM zaidi kuonesha ukomavu wa kisasa na demokrasia. Nina mambo kadhaa ya kushauri kupunguza (diffuse) hali ya utete iliyopo:

1. CCM itambue mkorogano wa uchaguzi mkuu na hususan matatizo yaliyotokea katika utengazaji wa matokeo. Hadi hivi sasa inaonekana CCM hawajaonesha hata mara moja kutambua utata na mvurugano wa matokeo ya uchaguzi. Hii inawafanya waonekane hawajali jinsi gani uchaguzi unaendeshwa au matokeo yanatangazwa. Hivyo, jambo la kwanza ni kukubali kuwa utangazaji wa matokeo (hata kama umewanufaisha wao) haukuwa katika hali ya kujivunia. Wakubali tatizo ambalo mamilioni ya Watanzania waliliona kufuatia uchaguzi mkuu.

2. CCM ioneshe kutambua tatizo letu la Tume ya Uchaguzi ilivyoendesha utangazaji wa matokeo ya Ubunge na Urais kiasi cha kusababisha maelfu ya vijana wetu kurundikana katika vituo mbalimbali "kulinda kura". Kama Taifa hatuwezi kwenda kwenye uchaguzi mwingine na mfumo huu kwani haumnufaishi yeyote zaidi ya kuweka msukumo katika jamii wakati wa uchaguzi ambao ungeweza kuleta madhara makubwa. CCM ioneshe na yenyewe inataka Tume inayofanya kazi kwa ufanisi, uhuru na uwazi. Ni kwa maslahi ya vyama vyote kuwa na Tume iliyo huru, wazi na ya kisasa.

3. CCM ioneshe kutokana na 1 na 2 hapo juu kuwa ipo haja ya kufanyia mabadiliko ya Katiba hasa kwenye suala la kuzuia au kupinga matangazo ya kura za Rais. Kwa wakati huu mfumo uliopo unaonekana kuinufaisha CCM. Lakini ni mfumo mbaya siku hali ikiwa kinyume na CCM. Kumbe ni kwa maslahi ya CCM na vyama vingine vyote kuweka utaratibu ambapo kura za Rais haziwezi kuonekana zinapandikizwa au Tume kulazimika kutangaza kwa sababu ikishatangaza basi hakuna wa kuhoji na wote wanatakiwa kupiga magoti kukubali matokeo hata kama kuna dalili ya upotofu. Ninaamini kwa chama kikongwe kama CCM ambacho kinajivunia kuwa ni "Baba ya Demokrasia" ni muhimu kuonesha kuwa hakiogopi mfumo mzuri na wa kisasa wa utangazaji wa kura za Urais.

4. CCM isijaribu kwa namna yoyote kutekeleza tishio lake la kuwafukuza wabunge wa Chadema Bungeni. Tayari taifa limeshagawanyika na kitendo chochote kitakachoonekana kuwa ni cha kibabe (wengi tunakumbuka suala la Zitto na Buzwagi) kitakoleza mgongano wa kisiasa nchini. Kuwafukuza CHADEMA hakutasababisha watu wakubali isipokuwa kama watawapeleka mahakamani Watanzania wote ambao hawako tayari kutambua ushindi wa Kikwete na kuwalazimisha kukubali ushindi huo chini ya tishio la kifungo. Vinginevyo, hekima kubwa inatakiwa kutumika na mimi ninaamini hekima hiyo inaanzia na:

- Uongozi wa CCM uanzishe mazungumzo na Uongozi wa CHadema kujaribu kusikilizana. Nilitoa pendekezo la wagombea kukutana kabla ya uchaguzi kwani niliamini wakati ule ndio ulikuwa wakati muafaka wa kufanya hivyo kabla hatujafika hapa tulipofika, na wakiendelea kuringishiana mapembe watajikuta wanalazimishwa kukaa chini huku machozi yanatoka. Tusifike huko.
- Kanuni za makubaliano zitengenezwe ili maridhiano yaanze; lakini ni lazima ziwe kanuni zenye kukubali hali halisi na zenye msingi wa haki na uwazi. Mazungumzo yasifanyike katika masharti kabla ya mazungumzo (pre-conditions).

5: Endapo CCM haitaona ulazima wa kufanyia kazi mapendekezo hayo kwa sababu "wameshinda" na kuwa hawako tayari kukubali kufanya mazungumzo na Chadema kwa kisingizio au sababu yoyote ni wazi kuwa wanalazimisha watu wenye dhamira tofauti kutii dhamira zao kuliko vitisho. Vitisho, mikwara, au hatua ambazo zitaonekana kuwalazimisha watu kupiga magoti kwa kutii kunaweza kuwatisha baadhi ya watu lakini kamwe hazijawahi kufanikiwa mahali popote duniani kuwatiisha watu wote wakati wote. Ndio maana nasema hekima inahitajika kuliko nguvu au vitisho vya nguvu.


6. Ni matumaini yangu kuwa CHadema nao hawajafunga mlango wa mazungumzo na watakuwa tayari kuwasikiliza CCM katika hali ya udugu, na uelewano wa kisiasa. Vinginevyo kidemokrasia ninaamini mgawanyiko uliopo ni mzuri na unakoleza tofauti za kisasa na hivyo kutuletea mapendekezo tofauti kabisa ya mwelekeo wa taifa. Katika demokrasia hatuwezi wote kuimba wimbo mmoja, kucheza ngoma moja na wote kukubaliana mtazamo mmoja. Ni muhimu kutambua kuwa ni katika tofauti zetu ndio demokrasia hukolezwa, na kudumishwa. Lakini ni muhimu tofauti hizo zisifikie uhasama wa kisiasa (political hostility) kitu ambacho ninaamini kinategemea kwa asilimia 100 maamuzi yatakayofanywa na CCM.

Ndiyo hoja zangu na ninazisimamia.
MMM
mwanakijiji haya maoni yasiishie hapa jf,yapelele mwanahalisi.ni mazuri mno.
 
CCM inakubali kuwa kulikuwa na mapungufu, ndio maana mh. Rais alisema hivyo wakati wa kupokea matokeo. Alisema ni vyema tume ikaangalia jinsi ya kuyaondoa mapungufu hayo in the future.
CCM haikubaliani na hysteria inayoonyeshwa na Chadema. Mazungumzo ni jambo ambalo CCM imelikaribisha kila siku, ila mwenyekiti wa CCM ambaye ndio Rais ya Jamhuri hawezi kuanzisha mazungumzo na chama kisichomtambua.
Kubalidilishwa au kuboreshwa kwa katiba ni wazo sahihi, lakini lina taratibu zake. Among hizo taratibu, kutokumtambua Rais na kususia hotuba zake haipo.
 
siungi mkono hoja ya kuwafukuza wabunge wa Chadema na ninaamini kuwa wabunge wa CCM hawatapeleka hoja hiyo bungeni kama alivyoashiria Mh. Chiligati. Wabunge wa Chadema watajifukuzisha/ kuondoka wenyewe iwapo wataendelea kutokumtambua Rais, kwa sababu swala la kutokumtambua Rais kwa mbunge halitekelezeki - ni mbio za sakafuni.
 
Zemarcopolo.. kwa Chadema kutomtambua Kikwete kama Rais kunamadhara gani kwa Urais wa Kikwete kisheria?
 
CCM inakubali kuwa kulikuwa na mapungufu, ndio maana mh. Rais alisema hivyo wakati wa kupokea matokeo. Alisema ni vyema tume ikaangalia jinsi ya kuyaondoa mapungufu hayo in the future.
CCM haikubaliani na hysteria inayoonyeshwa na Chadema. Mazungumzo ni jambo ambalo CCM imelikaribisha kila siku, ila mwenyekiti wa CCM ambaye ndio Rais ya Jamhuri hawezi kuanzisha mazungumzo na chama kisichomtambua.
Kubalidilishwa au kuboreshwa kwa katiba ni wazo sahihi, lakini lina taratibu zake. Among hizo taratibu, kutokumtambua Rais na kususia hotuba zake haipo.


CCM ndio wana Hysteria plus epilepsy, matokeo ya rais wameiba kura, NEC = CCM unaongea using mdomo use ur brain, think..!!!!!! think.....!!!!!!!!! Katiba hovyo, NEC ya CCM we need change, matokeo ya Rais yahesabiwe upya, think...!!!!!!!
 
Hapa mwanakijiji umenena, laiti kama masikio ya watawala yangefunguka na kuusikia ushauri huu. Wakaingia akilini mwao na kukumbuka majigambo yao ya siku za nyuma kwamba hakuna jambo linaloshindikana kwenye mazungumzo ikiwa milango iko wazi kujadili. Propaganda zenye ushabiki wa kisiasa wa itikadi za vyama ndani ya bunge zitaondoa maana halisi ya bunge letu na kuliondolea pia uhalali wa kuhudumiwa na pesa za kodi zetu. Hivyo basi hatutarajii hoja zisizo za kisheria kwa mujibu wa kanuni za uendeshaji bunge ndani ya bunge kwa mgongo wa wingi wa kura zilizoshinikizwa nje ya bunge kwa kufuata itikadi za chama fulani. Naunga mkono majadiliano ya pande mbili zinazo hasimiana na busara itumike kufikia muafaka mwema. Dhamira Jk aliyoionyesha kumaliza mpasuko wa Zanzibar, ni matumaini yangu kwamba haikuwa ni unafiki. Hivyo basi aitumie kuepusha mpasuko bara. Mungu ibariki Tanzania.
.
 
Zemarcopolo.. kwa Chadema kutomtambua Kikwete kama Rais kunamadhara gani kwa Urais wa Kikwete kisheria?

Kisheria hakuna madhara yoyote.
Ila kisiasa its a gamble. Kutokumtambua kunaweza kuathiri au kunufaisha upande wowote depending on how they handle and communicate the situation. So far, Chadema is more on the loosing side, they need a game changer!
 
CCM inakubali kuwa kulikuwa na mapungufu, ndio maana mh. Rais alisema hivyo wakati wa kupokea matokeo. Alisema ni vyema tume ikaangalia jinsi ya kuyaondoa mapungufu hayo in the future.
CCM haikubaliani na hysteria inayoonyeshwa na Chadema. Mazungumzo ni jambo ambalo CCM imelikaribisha kila siku, ila mwenyekiti wa CCM ambaye ndio Rais ya Jamhuri hawezi kuanzisha mazungumzo na chama kisichomtambua.
Kubalidilishwa au kuboreshwa kwa katiba ni wazo sahihi, lakini lina taratibu zake. Among hizo taratibu, kutokumtambua Rais na kususia hotuba zake haipo.

Mhe. uoni tofauti kati ya mzungumzo kati ya vyama na mazungumzo kati ya chama na serikari?
 
Mhe. uoni tofauti kati ya mzungumzo kati ya vyama na mazungumzo kati ya chama na serikari?

Tofauti ilitakiwa iwepo lakini unfortunatelly kwa CCM mwenyekiti wa chama ndio mkuu wa serikali. Kwahiyo hakuna tofauti hapo, swala la kumtambua kabla ya kuanza mazungumzo haliepukiki.
 
Inasikitisha saana kuona bado Tanzania in watu wajinga na wapumba.... kiasi hiki!!!
Kwa nini watu mnapenda kuhalalisha dhuluma na vitendo vya kihuni vinavyofanywa na hawa watawala uchwala wa
kitanzania? huu upuuzi wote wanaoufanya hauna masilahi kwa taifa la Tanzania hata kidogo even in the long run
hautakuwa na manufaa kwao pia.Tuna matatizo mengi ya msingi yanayohitaji ufumbumbuzi na ccm kwa makusudi
wanaobstruct/deny any move to change things for the betterment of all Tanzanians,halafu kuna wajinga wengine
wanaona ni sawa tu. Cha ajabu wale wanaojiita wasomi ndiyo hasa hovyo kabisa sijui hata hizo elimu zao zinawasaidia
nini?!!!!!
Wabongo acheni ujinga nchi inaangamia.
 
Nadhani tunapozungumzia suala la kutokumtambua Rais na walk out ya Juzi hili kwa wale wanaojua ni tatizo kubwa sana ingawa Kisheria halimuondolei Rais wa nchi madaraka yake.
Ukumbuke kuwa nusu ya Bajeti yetu inaendeshwa na mataifa mengine na haya mataifa hayana issue ndogo so Mkuu wetu popote atakapotua na anavyopenda visafari atakutana na kero ya kufafanua stability ya demokrasia katika nchi yake. Amina usiamini atakereka na hili swali kila atakapokanyaga nje ya nchi.
Pili tukumbuke kuwa vijana wana hasira kubwa na chama tawala na hata EL amelizungumzia hili akimuomba pinda kulichunguza, hawa watu wenye hasira without hope for life wengi wako nyuma ya CDM kama tumaini pekee lililobaki, Kama tusipokuwa makini sasa tutashuhudia Tanzania nyingine kabisa ya mabomu ya machozi, risasi za moto na umwagaji wa damu usiotarajiwa, salama za Mbeya Arusha, na MWanza wakati wa kutangaza matokeo ni vielelezo tosha.
Mimi nadhani huu si wakati wa kusikiliza taarabu za akina Chirigati bali ni wakati wa kuja mezani kutengeneza haya mapungufu for better future of our lovely nation. Tuweke mbali ushabiki na kujipendekeza vitu ambavyo vinaumiza taifa letu na hata mkuu wa nchi. Mara nyingi amezungukwa na watu wanaovizia opportunities na hivyo kutompa ukweli wa hali halisi ya nchi inavyokwenda. Ukitaka kujua Rais wetu anasalitiwa na wapambe angalia kitendo cha msafara wa rais wa nchi kuwa na mipancha, kuchakachua mafuta kwenye magari yake, kufungua hotel kuesho yake kuta zinavunjwa, kurushiwa mawe na kuzomewa kwa mawaziri wake. Hizi na dalili tosha kuwa nchi iko pagumu sana na lazima tuweke misingi mipya
 
Chezo umenifanya nicheke sana eti 'Acha noma na iwe noma'. CCM NI SIKIO LISILOSIKIA DAWA
 
Nadhani tunapozungumzia suala la kutokumtambua Rais na walk out ya Juzi hili kwa wale wanaojua ni tatizo kubwa sana ingawa Kisheria halimuondolei Rais wa nchi madaraka yake.
Ukumbuke kuwa nusu ya Bajeti yetu inaendeshwa na mataifa mengine na haya mataifa hayana issue ndogo so Mkuu wetu popote atakapotua na anavyopenda visafari atakutana na kero ya kufafanua stability ya demokrasia katika nchi yake. Amina usiamini atakereka na hili swali kila atakapokanyaga nje ya nchi.
Pili tukumbuke kuwa vijana wana hasira kubwa na chama tawala na hata EL amelizungumzia hili akimuomba pinda kulichunguza, hawa watu wenye hasira without hope for life wengi wako nyuma ya CDM kama tumaini pekee lililobaki, Kama tusipokuwa makini sasa tutashuhudia Tanzania nyingine kabisa ya mabomu ya machozi, risasi za moto na umwagaji wa damu usiotarajiwa, salama za Mbeya Arusha, na MWanza wakati wa kutangaza matokeo ni vielelezo tosha.
Mimi nadhani huu si wakati wa kusikiliza taarabu za akina Chirigati bali ni wakati wa kuja mezani kutengeneza haya mapungufu for better future of our lovely nation. Tuweke mbali ushabiki na kujipendekeza vitu ambavyo vinaumiza taifa letu na hata mkuu wa nchi. Mara nyingi amezungukwa na watu wanaovizia opportunities na hivyo kutompa ukweli wa hali halisi ya nchi inavyokwenda. Ukitaka kujua Rais wetu anasalitiwa na wapambe angalia kitendo cha msafara wa rais wa nchi kuwa na mipancha, kuchakachua mafuta kwenye magari yake, kufungua hotel kuesho yake kuta zinavunjwa, kurushiwa mawe na kuzomewa kwa mawaziri wake. Hizi na dalili tosha kuwa nchi iko pagumu sana na lazima tuweke misingi mipya

Wahisani hawana interest na true democracy, wanachokifanya ni kutumia kigezo cha democracy kumove agenda zao. Mtu kama Hosni Mubarak asingeweza kuingia White House kama wamarekani wangekuwa wanajiepusha na maadui wa demokrasia. Mfano mwingine ni Musharaf, tulimuoana akienjoy comfortable atmosphere bila vikwazo.

Vilevile tukumbuke kuwa vikwazo vya kiuchumi havijawahi kuwork kwa wanasiasa. Mara nyingi wanaoathirika ni wananchi ambao kura zao zinagombaniwa. Angalia mfano wa Zimbabwe, je vile vikwazo havijamuathiri Mugabe ukifananisha na jinsi walivyoathirika wapiga kura. Kuunga mkono shinikizo kwa njia ya vikwazo vya uchumi na kukatiwa "misaada" ni kuomba hali ngumu ya maisha kwa manufaa ya none.
 
Mzee Mwanakijiji,
Tangu lini sikio la kufa likasikia dawa? Kuipa CCM ushauri kama huo, ingawa unalenga kuinufaisha na kujijenga for the future, ni sawa kummulikia kipofu. Ushauri wanaoutaka wao ni wa jinsi ya kuwahujumu wananchi tu. Ukiwashauri jinsi ya kuwakandamiza wananchi utakuwa rafiki yao, na unaweza hata kupewa ukuu wa wilaya.
 
5: Endapo CCM haitaona ulazima wa kufanyia kazi mapendekezo hayo kwa sababu "wameshinda" na kuwa hawako tayari kukubali kufanya mazungumzo na Chadema kwa kisingizio au sababu yoyote ni wazi kuwa wanalazimisha watu wenye dhamira tofauti kutii dhamira zao kuliko vitisho. Vitisho, mikwara, au hatua ambazo zitaonekana kuwalazimisha watu kupiga magoti kwa kutii kunaweza kuwatisha baadhi ya watu lakini kamwe hazijawahi kufanikiwa mahali popote duniani kuwatiisha watu wote wakati wote. Ndio maana nasema hekima inahitajika kuliko nguvu au vitisho vya nguvu.

CCM watatekeleza hilo hapo juu hadi hapo wafadhili watakaposimamisha misaada yao kama walivyomfanyia Mzee Moi pale kenya..............
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom