VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Ndugu Bernard Membe jana amenena. Ya kuwa Tanzania ipo tayari kupeleka wanajeshi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ili kuwadhibiti Waasi wa March 23 Movement almaarufu kama M23 ambao wanaendelea kumnyima usingizi Rais Joseph Kabila wa nchi hiyo. Baada ya kuteka Goma,Waasi hao wamefanikiwa kuuteka Mji mwingine wa Sake wakielekea katikati ya Bukavu.
Kwa mujibu wa Membe,Tanzania inasubiri 'ruhusa' ya Umoja wa Mataifa ili kuwapeleka wanajeshi wake huko Kongo-DRC.Sasa,nchi yetu itafaidikaje: kisiasa,kiuchumi na kiutamaduni? Kwani tumeombwa na Kabila/Umoja wa Mataifa au ni uamuzi wetu binafsi?
Kwa mujibu wa Membe,Tanzania inasubiri 'ruhusa' ya Umoja wa Mataifa ili kuwapeleka wanajeshi wake huko Kongo-DRC.Sasa,nchi yetu itafaidikaje: kisiasa,kiuchumi na kiutamaduni? Kwani tumeombwa na Kabila/Umoja wa Mataifa au ni uamuzi wetu binafsi?