Mapambano dhidi ya Mafisadi

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Hawa kweli ni vigogo au vibua tu!!? IPPMEDIA ni aibu kwenu kwa kushindwa kuyaweka majina ya wahusika kwenye article hii.

JK amwaga vigogo sita

2008-08-23 15:43:59
Na Mwandishi Wetu, Jijini

Wale vigogo wanaotuhumiwa kuchota mapesa ya umma kwa manufaa yao, waliodhani Rais Jakaya Kikwete atawakingia kifua, sasa wameula wa chuya kwani JK kawanawa kama hawajui vile.

Katika kudhihirisha kwamba hivi sasa kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe, imedaiwa kuwa, JK ameapa kutoingilia kwa namna yoyote mamlaka ya kisheria kuchukua mkondo wake, hata kama watuhumiwa ni watu walio karibu naye.

Taarifa kutoka kwa chanzo cha gazeti hili, zinadai kuwa ni kutokana na msimamo huo ambapo JK ametoa baraka zake ili watuhumiwa wote wa sakata la ufisadi, waburuzwe kortini ili kukabiliana na tuhuma zinazowakabili.

``Hali sasa ni ngumu kwa baadhi ya waheshimiwa maana mzee (rais) amesema hatamlinda mtu yeyote, japokuwa baadhi ya watuhumiwa ni watu wanaofahamiana vizuri,`` kimedai chanzo chetu kutoka Serikalini.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, kila kigogo ambaye ushahidi utaonyesha zipo hoja za msingi za kumburuza kortini, JK hataingilia kwa namna yoyote.

``Wale watuhumiwa sita aliosema mzee katika hotuba yake juzi kwamba watafikishwa kortini, ni mwanzo tu, wengine watafuata,`` chanzo hicho kimedai.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, Rais Kikwete amefikia uamuzi huo wa kuacha watuhumiwa hata kama ni vigogo waumbuke mahakamani, kwa lengo la kufanikisha vita dhidi ya rushwa na kuiletea heshima Serikali yake.

``Unajua siku zilizopita kuna watu walidhani sheria inafanya kazi kwa watu wadogo tu, sasa hilo halipo. Yeyote ambaye kuna ushahidi wa kutosha wa kumburuzwa kortini, atabebwa tu,`` kimeongeza chanzo hicho.

Akihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juzi, Rais Kikwete alisema Taasisi ya Kupambana na Kuzuia rushwa nchini, TAKUKURU inakusudia kufikisha mahakamani kesi sita za rushwa kubwa.

``Kesi nyingine sita uchunguzi wake umekamilika... ziko mbioni kufikishwa kortini,`` alisema Rais Kikwete.

Akizungumzia hatua nyingine za mapambano dhidi ya rushwa ambazo tayari zimeshughulikiwa na Serikali, Rais Kikwete alisema kesi zilizofikishwa kortini zimeongezeka kutoka kesi 50 mwaka 2005 hadi kufikia kesi 156 mwaka huu.

Akasema TAKUKURU ambayo ndiyo inayosimamia kesi hizo tayari imeshinda kesi 35 kutoka kesi sita tu ilizokuwa imeshinda mwaka 2005.

Aidha akasema ili kuimarisha vita dhidi ya rushwa, Serikali imeajiri vijana 442 katika Taasisi ya kupambambana na Kuzuia Rushwa, TAKUKURU kwa ajili ya kuwadaka wala rushwa.

SOURCE: Alasiri
 
Hawa kweli ni vigogo au vibua tu!!? IPPMEDIA ni aibu kwenu kwa kushindwa kuyaweka majina ya wahusika kwenye article hii.

JK amwaga vigogo sita

2008-08-23 15:43:59
Na Mwandishi Wetu, Jijini

Wale vigogo wanaotuhumiwa kuchota mapesa ya umma kwa manufaa yao, waliodhani Rais Jakaya Kikwete atawakingia kifua, sasa wameula wa chuya kwani JK kawanawa kama hawajui vile.

Katika kudhihirisha kwamba hivi sasa kila mtu ataubeba mzigo wake mwenyewe, imedaiwa kuwa, JK ameapa kutoingilia kwa namna yoyote mamlaka ya kisheria kuchukua mkondo wake, hata kama watuhumiwa ni watu walio karibu naye.

Taarifa kutoka kwa chanzo cha gazeti hili, zinadai kuwa ni kutokana na msimamo huo ambapo JK ametoa baraka zake ili watuhumiwa wote wa sakata la ufisadi, waburuzwe kortini ili kukabiliana na tuhuma zinazowakabili.

``Hali sasa ni ngumu kwa baadhi ya waheshimiwa maana mzee (rais) amesema hatamlinda mtu yeyote, japokuwa baadhi ya watuhumiwa ni watu wanaofahamiana vizuri,`` kimedai chanzo chetu kutoka Serikalini.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, kila kigogo ambaye ushahidi utaonyesha zipo hoja za msingi za kumburuza kortini, JK hataingilia kwa namna yoyote.

``Wale watuhumiwa sita aliosema mzee katika hotuba yake juzi kwamba watafikishwa kortini, ni mwanzo tu, wengine watafuata,`` chanzo hicho kimedai.

Kwa mujibu wa chanzo hicho, Rais Kikwete amefikia uamuzi huo wa kuacha watuhumiwa hata kama ni vigogo waumbuke mahakamani, kwa lengo la kufanikisha vita dhidi ya rushwa na kuiletea heshima Serikali yake.

``Unajua siku zilizopita kuna watu walidhani sheria inafanya kazi kwa watu wadogo tu, sasa hilo halipo. Yeyote ambaye kuna ushahidi wa kutosha wa kumburuzwa kortini, atabebwa tu,`` kimeongeza chanzo hicho.

Akihutubia Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania juzi, Rais Kikwete alisema Taasisi ya Kupambana na Kuzuia rushwa nchini, TAKUKURU inakusudia kufikisha mahakamani kesi sita za rushwa kubwa.

``Kesi nyingine sita uchunguzi wake umekamilika... ziko mbioni kufikishwa kortini,`` alisema Rais Kikwete.

Akizungumzia hatua nyingine za mapambano dhidi ya rushwa ambazo tayari zimeshughulikiwa na Serikali, Rais Kikwete alisema kesi zilizofikishwa kortini zimeongezeka kutoka kesi 50 mwaka 2005 hadi kufikia kesi 156 mwaka huu.

Akasema TAKUKURU ambayo ndiyo inayosimamia kesi hizo tayari imeshinda kesi 35 kutoka kesi sita tu ilizokuwa imeshinda mwaka 2005.

Aidha akasema ili kuimarisha vita dhidi ya rushwa, Serikali imeajiri vijana 442 katika Taasisi ya kupambambana na Kuzuia Rushwa, TAKUKURU kwa ajili ya kuwadaka wala rushwa.

SOURCE: Alasiri


Alasiri bwana .Yaani hili gazeti ni kwamba halina waandishi ama kuna matatizo gani hapo ?
 
Hivi kama mali zimekamatwa hazina majina?????????????? unajua vitu vingine vinachekesha sana.
 
Mlimwona Slaa Jana aliposhusha Nondo kwenye Kipindi cha Tuongee Asubuhi cha Star Tv Jumamosi? aliingia hadi na nakala ya Ripoti ya uchunguzi wa Kasha ya EPA na kuonesha tuhuma za Kampuni ya Kagoda. Lakini mgeni wa pili Chitalilo yeye aliishia kumsifia JK na kumwita Baba akionya kuwa ni Utovu wa Nidhamu kumkosoa baba baada ya kutoa (Kuhutubia) maelekezo kwa wototo wake (Bunge).

Kwa kauli hii ya Chitalilo - Mbuneg wa Buchosa - sikushangaa kusikia CCM wanaandamana kumpongeza JK kwa hotuba nzuri.

end
 
yaani slaa na phd yake anafanya mdahalo na chitalilo! kweli ccm wajua kumdhihaki mtu.
 
Mlimwona Slaa Jana aliposhusha Nondo kwenye Kipindi cha Tuongee Asubuhi cha Star Tv Jumamosi? aliingia hadi na nakala ya Ripoti ya uchunguzi wa Kasha ya EPA na kuonesha tuhuma za Kampuni ya Kagoda. Lakini mgeni wa pili Chitalilo yeye aliishia kumsifia JK na kumwita Baba akionya kuwa ni Utovu wa Nidhamu kumkosoa baba baada ya kutoa (Kuhutubia) maelekezo kwa wototo wake (Bunge).

Kwa kauli hii ya Chitalilo - Mbuneg wa Buchosa - sikushangaa kusikia CCM wanaandamana kumpongeza JK kwa hotuba nzuri.

end

Hakika huko CCM kuna viongozi mabwege. Kwa nini anajaribu ku-patronise watu. Serikali inajihusisha na WIZI wa mali za umma, halafu anawaita wanaokosoa ni watovu wa nidhamu?? Na hao watu wa Buchosa, wenye Mbunge kama huyu, wana raha gani?
 
yaani slaa na phd yake anafanya mdahalo na chitalilo! kweli ccm wajua kumdhihaki mtu.
Sidhani kama Slaa ndio yeye anachangua nani ajadiliane naye,ni hao tv programmers ambao wanaandaa programs ndio wa kulaumu.Isitoshe Slaa kufanya mijadala na chitalilo sio kosa kwani unataka kusema mtu mwenye phd hana haki ya kujadiliana na mtu mwenye elimu ya bachelors,kidato cha nne, anu kidato cha sita au hata darasa la saba?kwenye siasa kila kitu kinawezekana.Pia walikuwa wamemweka chitalilo pale huwezi kujua azma yao,labda ilikuwa ni kuendelea kuwaonesha umma who chitalilo is.
 
Kwa kweli mimi nanona mambo ambayo Rais Kikwete alipaswa kuwafanyia watanzania wakaridhika na utendaji wake na hivyo kuifanya kasi mpya ionekane kwamba ni dhahiri zaidi ya uwa ni dhana tu,yalitolewa kwa ufupi na Mheshimiwa Sitta mara baada ya Rais kumaliza hotuba yake. Yale mambo makuu matatu ambayo sitta alimweleza Rais kama yakichambuliwa na Rais kuyafanyia kazi,bas ndoto zake,za kukomesha ufisadi,kuleta maisha bora nk ingeweza kufikiwa hata kabla ya mwaka 2015

Sio siri ukitaka kupambana na haya mambo ya ufisadi lazima kutumia multi-approach lakini la muhimu zaidi ni kwa kutumia legal reform,maana ni kwa sheria tu unaweza kukabiliana na mambo mengi, lakini iwapo sheria zilizopo bado zina mianya ya kukumbatia mafisadi hataubwabwaje vipi bado watakuwa na nafasi ya kupeta tu. Mfano halisi ni Rais mwenyewe ambaye amekiri wazi kuwa moja ana madaraka makubwa pili,kuwa vyombo vya dola havina uhuru kamili ndio maana anaweza kuviingilia kwa kusema "kamata Dr.slaa" wakishakamata wanarudi kwake kumuuliza "tumeshamkamata tumfanyeje?" yaani hii inaonesha zaidi hawawezi hata kumuuliza mkuu kwa nini Dr.slaa akamatwe. Kwa mtaji huu ndio maana kila mtuhumiwa wa ufisadi jina linapelekwa kwa Rais ili yeye aamue cha kufanya,hali inayotafsiriwa kuwa vyombo vyetu vya dola kila wakati vinasubiri kuambiwa na Rais nini cha kufanya.Haviwezi kwa vyenyewe kutumia utashi wao,lakini hii haiishii hao tu inakwenda hadi kwenye idara nyingine za utendaji,matokeo yake Rais anaonekana nafanya kazi peke yake,na sote tunajua kidole kimoja hakivunji chawa,je mkuu wa kaya kwa mtindo huu anadhani atafanikiwa?
 
Nadhani jf hamfahamu chitalilo, huyu alitumika kumwondoa mzee shindika kwenye ulingo wa siasa, ni huyuhuyu alitumika kuhakikisha dr.tizeba (mhandisi mipango miji) hakanyagi bungeni. Kumbuka star tv nimali ya diallo, Hivyo kuwepo kwenye mdahalo haikuwa bahati mbaya, dr.slaa hakuwa nasabubu ya kukaa mezamoja na huyu jamaa.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom