Mapadri Wakatoliki wavamiwa

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,298
33,083
MAJAMBAZI wenye silaha wiki hii wamevamia nyumba ya Mapadri wa Kanisa Katoliki Changanyikeni, Dar es Salaam na wakarusha risasi kabla ya kutoweka na kompyuta ndogo na baadhi ya nyaraka za padri mmoja, Raia Mwema limethibitisha.
Habari zilizothibitishwa na maofisa wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, zimeeleza kwamba majambazi hao waliokuwa na silaha walivamia nyumba hiyo iliyopo karibu na Chuo cha Takwimu, usiku wa kuamkia juzi Jumatatu.
Imeelezwa kwamba Padri mmoja ambaye eneo lake lilivunjwa na majambazi hao, alinusurika kuuwawa kwa risasi baada ya kuruka na kuangukia katika bonde lilipo kando ya nyumba hiyo, huku majambazi wakiamini kuwa wamekwisha kummaliza kwa risasi.
Akisimulia alivyonusurika, Padri Francis Laswai, wa Parokia ya Kipawa, anayeishi katika nyumba hiyo alisema: “Ni muujiza tu maana nilipovunja mlango wa ghorofani na kurukia bondeni, muda huo huo nikawa nimesikia sauti zikisema mmalize na mlio wa risasi ukafuata. Sikujitambua nilijikuta nikiwa bondeni karibu na maji.”
Nyumba hiyo inayomilikiwa na Shirika la Kikatoliki la Francisca Capchia, ndimo wanamoishi Mapadri wawili, Laswai na mwenzake Damas Mahali, Buruda mmoja na watumishi wawili ambao wote hawakupata madhara yoyote.
Padri Laswai katika sauti iliyokauka, ameliambia Raia Mwema kwamba mbali ya kuchukua kompyuta hiyo ndogo (laptop) na nyaraka zake muhimu zilizokuwa katika begi la laptop hiyo, majambazi hao waliondoka na simu pamoja na saa zake mbili ambazo alisema hata hivyo zilikua mbovu.
Miongoni mwa vitu vilivyoibwa ni leseni ya kufungisha ndoa, vyeti vya elimu na leseni ya udereva ya Padri huyo pamoja na kamera ya mtumishi wake.
Akielezea jinsi majambazi walivyokusudia kumuua, Padri Laswai ambaye yuko chini ya Shirika la Roho Mtakatifu (Holly Ghost Fathers) anasema; “Nilipoangukia bondeni nikasikia mmoja akisema, tayari tumemmaliza, kwa hiyo nikaona nitambae na kuondoka eneo hilo wasije wakagundia niko hai.”
Kabla ya kumvamia Padri Laswai, majambazi hao walimbana mtumishi wa nyumba hiyo, Marceli John, ambaye alitakiwa kuonyesha alipo Padri Laswai, na alipowaambia hajui alipo walisikia sauti ya padri huyo na kuamua kuvunja mlango na kumuingilia kabla ya yeye kutoweka kwa kuvunja mlango mwingine.
Marceli anasema; “Walianza kuniuliza bosi wangu alipo, nikawaambia hayupo.. kwa kweli sikua najua kama amerudi nikajua yuko Kipawa. Wakaniambia niwape laptop yake na pesa. Mara wakaniambia mbona wameliona gari lake jeupe nje, mara nikasikia sauti ya Padri, na wao wakamfuata huko. Ndipo na mimi nikaenda kujificha.”
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Elias Kalinga, hakuweza kupatikana jana lakini wasaidizi wake muhimu waliliambia Raia Mwema kwamba tayari taarifa hizo wamekwisha kumkabidhi kwa kuwa wao si wasemaji wa Mkoa huo.
Imeelezwa kwamba wakati tukio hilo likitokea, eneo la Changanyikeni lililopo karibu kabisa na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam chenye Kituo cha Polisi, hakukuwa na gari la polisi wa doria kama ilivyo kawaida kwa maelezo kwamba gari hilo kwa sasa ni bovu.


http://www.raiamwema.co.tz/news.php?d=2089
hs3.gif
 
UWT wako kazini, nadhani jamaa alikuwa na movement za mashaka hivyo alipaswa kuwa eliminated
 
UWT wako kazini, nadhani jamaa alikuwa na movement za mashaka hivyo alipaswa kuwa eliminated
Kwa hiyo unasema UWT ndio wauaji wenyewe? Makubwa haya..Maelezo yanayopatikana kwenye habari inaonesha kuna kisa kimejificha hapa, na huyo padiri maelezo yake hayajanyooka. Kwanini wamtafute yeye+laptop yake, na 'nyaraka' ?

Lakini lipi ni jpiya hapa ktk jamii hii iliojaa ubinafsi na kupenda ukuu na mali?
 
Inaonekana hiyo Laptop ndiyo ilikuwa inatafutwa haswa, kama huyu padri angesema ilikuwa na nyaraka gani tungeelewa kisa ni nini hasa.,mmh lakini jamaa wamekwenda kuiba laptop kwa mtutu wa bunduki, mbona wametumia nguvu nyingi sana ni sawa na kuua mbu kwa rungu..anyway huyo padri nahisi nae ni mafia...haya ni maoni yangu tu.
 
Kwa hiyo unasema UWT ndio wauaji wenyewe? Makubwa haya..Maelezo yanayopatikana kwenye habari inaonesha kuna kisa kimejificha hapa, na huyo padiri maelezo yake hayajanyooka. Kwanini wamtafute yeye+laptop yake, na 'nyaraka' ?

Lakini lipi ni jpiya hapa ktk jamii hii iliojaa ubinafsi na kupenda ukuu na mali?
mZee ni hao jamaa wa UWT (Usalama wa TAifa), maana ukisoma kisa jamaa walikuwa na haja ya document tu, na huyo padri anaonekana ni mzima kwa sana, maana anakwambia alijirusha kutoka ghorofani na kisa akaanza kutambaa na ukae ukijua risasi zilishamiminwa kwenye uelekeo wake na hao jamaa wakajua tayari wameshamdondosha, (HAPA NAKUMBUKA WILLI GAMBA)
Mkuu hapo kuna mambo mengi mno, Idara yetu ya usalama inaweza kuwa ya kizembe kwenye mambo mengi tu, lakini kwa issue kama hii ya kukudeal nawapa bigup
 
mZee ni hao jamaa wa UWT (Usalama wa TAifa), maana ukisoma kisa jamaa walikuwa na haja ya document tu, na huyo padri anaonekana ni mzima kwa sana, maana anakwambia alijirusha kutoka ghorofani na kisa akaanza kutambaa na ukae ukijua risasi zilishamiminwa kwenye uelekeo wake na hao jamaa wakajua tayari wameshamdondosha, (HAPA NAKUMBUKA WILLI GAMBA)
Mkuu hapo kuna mambo mengi mno, Idara yetu ya usalama inaweza kuwa ya kizembe kwenye mambo mengi tu, lakini kwa issue kama hii ya kukudeal nawapa bigup

Unawapa big-up kwa uuwaji? Dah mkuu uimenistua.

Lakini kipi kipya?
 
mZee ni hao jamaa wa UWT (Usalama wa TAifa), maana ukisoma kisa jamaa walikuwa na haja ya document tu, na huyo padri anaonekana ni mzima kwa sana, maana anakwambia alijirusha kutoka ghorofani na kisa akaanza kutambaa na ukae ukijua risasi zilishamiminwa kwenye uelekeo wake na hao jamaa wakajua tayari wameshamdondosha, (HAPA NAKUMBUKA WILLI GAMBA)
Mkuu hapo kuna mambo mengi mno, Idara yetu ya usalama inaweza kuwa ya kizembe kwenye mambo mengi tu, lakini kwa issue kama hii ya kukudeal nawapa bigup

Na kwa issue kama za Kagoda, wizi wa dhabu na mchanga unaibiwa kila siku unawapa nini?
 
mZee ni hao jamaa wa UWT (Usalama wa TAifa), maana ukisoma kisa jamaa walikuwa na haja ya document tu, na huyo padri anaonekana ni mzima kwa sana, maana anakwambia alijirusha kutoka ghorofani na kisa akaanza kutambaa na ukae ukijua risasi zilishamiminwa kwenye uelekeo wake na hao jamaa wakajua tayari wameshamdondosha, (HAPA NAKUMBUKA WILLI GAMBA)
Mkuu hapo kuna mambo mengi mno, Idara yetu ya usalama inaweza kuwa ya kizembe kwenye mambo mengi tu, lakini kwa issue kama hii ya kukudeal nawapa bigup

Kituko kama unavyojiita nadhani unachoelezea hapa ni kituko cha riwaya tu.

UWT kama unavyowaita wewe kazi yao si kuua bali kulinda usalama wa Taifa kwa kukusanya na kutoa taarifa za kiusalama basi...na pia wana kitengo cha PSU ambacho kazi yake ni ulinzi wa viongozi(body guards), yaani usalama wa watu(Taifa). Usalama wa nchi unalindwa na JWTZ(Yaani ulinzi-Kulinda mipaka na rasilimali zisizokuwa watu za nchi).

Linapokuja suala la kuondosha tishio la taifa kuna jamaa ambao ni tofauti na UWT, hawa wamejifunza kazi moja tu......na wako professional...''when they come for you they know exactly where you are, they see you before you see them, they do not show that you were assassinated, they make it seem a normal death out of natural calamities. Wanaohabarisha juu ya uhatari wa mtu au taasisi kwa maslahi ya taifa ni hao unaowaita wewe UWT(TISS) ambao ni tofauti na hawa professional terminators.

Tukio la hapo juu halina uhusiano kabisa na hawa professionals ambao kwa makusudi kabisa sitakutajia jina lao ili uendelee na dhana na fikra zako za hadithi za kwenye riwaya.

Na ujue kuwa professionals hawa wanaotumwa na taifa hawafanyi ishu za hivyo bila mkubwa wa nchi kuruhusu. Sasa hako kapadri kako na hao mateja walioiba laptop na nyaraka za mkatoliki unawaona wewe kama wana ishu za usalama wa nchi.

Ishu zenyewe nyeti huwa zinakuwa cleaned up, hutakaa uzisikie kwenye vyombo vya habari, na zikitokea huwa zinafunikwa kiasi cha kutofahamika kabisa kilichotokea. Ishu zile huwa zinasimamiwa na wakubwa wa nchi wenyewe kwa hiyo hakuna kuvuja kunakoruhusiwa.

Wale jamaa zangu wale wa kazi...acha TISS unachanganya TISS ni wanahabari tu...tunazungumzia wale......sikwambii jina...wale wanapoua kwa risasi huwa ni lazima wahakikishe umekufa siyo kubahatisha...hapo ndiyo kazi inakuwa imekwisha.

Hao wa changanyikeni vibaka tu hao, wametumwa na jamaa za huyo padre Francis, inaonyesha walikuwa na party ya siri na mademu, jamaa akawapiga picha wenzake akahifadhi kwenye laptop yake, mmoja wao akakumbuka pombe zilipoisha kwa hiyo kulinda hadhi akatuma vibaka wapore laptop na camera kisha wamdedishe jamaa, na hao waliotumwa ni amateurs tu hawana lolote, bila bunduki wanakuwa mbwa tu. Tena hata ukisimama ukamwambia akushoot anaweza akakukosa, hawana shabaha...mateja tu, hakuna UWT hapo wala TAMW!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Kituko kama unavyojiita nadhani unachoelezea hapa ni kituko cha riwaya tu.

UWT kama unavyowaita wewe kazi yao si kuua bali kulinda usalama wa Taifa kwa kukusanya na kutoa taarifa za kiusalama basi...na pia wana kitengo cha PSU ambacho kazi yake ni ulinzi wa viongozi(body guards), yaani usalama wa watu(Taifa). Usalama wa nchi unalindwa na JWTZ(Yaani ulinzi-Kulinda mipaka na rasilimali zisizokuwa watu za nchi).

Linapokuja suala la kuondosha tishio la taifa kuna jamaa ambao ni tofauti na UWT, hawa wamejifunza kazi moja tu......na wako professional...''when they come for you they know exactly where you are, they see you before you see them, they do not show that you were assassinated, they make it seem a normal death out of natural calamities. Wanaohabarisha juu ya uhatari wa mtu au taasisi kwa maslahi ya taifa ni hao unaowaita wewe UWT(TISS) ambao ni tofauti na hawa professional terminators.

Tukio la hapo juu halina uhusiano kabisa na hawa professionals ambao kwa makusudi kabisa sitakutajia jina lao ili uendelee na dhana na fikra zako za hadithi za kwenye riwaya.

Na ujue kuwa professionals hawa wanaotumwa na taifa hawafanyi ishu za hivyo bila mkubwa wa nchi kuruhusu. Sasa hako kapadri kako na hao mateja walioiba laptop na nyaraka za mkatoliki unawaona wewe kama wana ishu za usalama wa nchi.

Ishu zenyewe nyeti huwa zinakuwa cleaned up, hutakaa uzisikie kwenye vyombo vya habari, na zikitokea huwa zinafunikwa kiasi cha kutofahamika kabisa kilichotokea. Ishu zile huwa zinasimamiwa na wakubwa wa nchi wenyewe kwa hiyo hakuna kuvuja kunakoruhusiwa.

Wale jamaa zangu wale wa kazi...acha TISS unachanganya TISS ni wanahabari tu...tunazungumzia wale......sikwambii jina...wale wanapoua kwa risasi huwa ni lazima wahakikishe umekufa siyo kubahatisha...hapo ndiyo kazi inakuwa imekwisha.

Hao wa changanyikeni vibaka tu hao, wametumwa na jamaa za huyo padre Francis, inaonyesha walikuwa na party ya siri na mademu, jamaa akawapiga picha wenzake akahifadhi kwenye laptop yake, mmoja wao akakumbuka pombe zilipoisha kwa hiyo kulinda hadhi akatuma vibaka wapore laptop na camera kisha wamdedishe jamaa, na hao waliotumwa ni amateurs tu hawana lolote, bila bunduki wanakuwa mbwa tu. Tena hata ukisimama ukamwambia akushoot anaweza akakukosa, hawana shabaha...mateja tu, hakuna UWT hapo wala TAMW!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Kwa jinsi ulivyoeleza unaonekana kuwa mmoja wao UWT
 
Lakini mapadre na laptops wapi na wapi?

Huenda kweli kaa bana akashube alivosema huenda walikua wanalewa na makahaba huko wakapigana na mapicha ya ajabu, tena kwenye 'kwalazima' hii sijui saumu wamemwachia nani?

Lakini kipi kipya hapa? Ubazazi na double lives za baadhi ya mapadiri?

Sidhani kaa ni jipya hili.
 
Back
Top Bottom