Maonyesho ya biashara ya 130 ya kimataifa ya Guangdong yaendelea kujenga picha nzuri ya ushirikiano kati ya China na Afrika

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,000
1,019
1634176860970.png


Maonyesho ya kimataifa ya biashara ya Guangdong awamu ya 130 ambayo ni maarufu kwa jina la Canton Fair yamefunguliwa tarehe 15 Oktoba mjini Guangzhou. Maonyesho haya yanatajwa kuwa ni maonyesho ya muda mrefu zaidi na endelevu zaidi kati ya maonyesho yote ya kimataifa ya biashara duniani hadi sasa yakiwa yamefanyika kwa jumla ya miaka 130.

Kwa mara ya kwanza tangu maonyesho haya yaanze mwaka 1957, safari hii kuna vileta bahati (Mascot) vya maonyesho hayo ambavyo ni wanasesere wawili wa umbo la nyuki, mmoja ni wa dume alipewa jina la Haobao (好宝), na mwingine jike akiwa na jina la Haoni (好妮). Nyuki hawa wawili wanabeba maana ya utiifu, umoja na kujitolea. Maana ya vileta bahati hivyo ni kuwa maonyesho haya yanaonyesha nia pana ya China ikiwa ni nchi inayoimarika kiuchumi, ya kuendeleza uchumi ulio wazi na kuwa na mustakbali mzuri wa pamoja kwa binadamu kupitia biashara.

Maonyesho ya awamu hii yanafanyika wakati dunia inaendelea kukabiliana na janga la virusi vya Corona, na wafanyabiashara wengi wanaendelea kukabiliwa na hatua mbalimbali zinazowafanya washindwe kusafiri na kufanya biashara zao. Hata hivyo China imejitahidi kufanya kila linalowezekana kuwawezesha watu kushiriki kwenye maonyesho hayo, iwe ni kwa washiriki kuja wao wenyewe au kwa kushiriki kupitia mtandao wa internet.

Kwa nchi za Afrika hii ni fursa nzuri kwa wafanyabiashara wanaotaka kununua bidhaa za mtaji kama vile mashine na mitambo ya uzalishaji, pamoja na vifaa vingine vingi ambavyo hupatikana China kwa bei nafuu vikiwa na ubora wa juu, lakini pia maonyesho hayo ni fursa ya kuuza bidhaa zao au hata kutafuta fursa za ushirikiano na wawekezaji wa China.

Maonyesho haya huwa yanatajwa pia kama ni kipimo cha hali ya uchumi wa dunia, na mwitikio wa ushiriki kwenye maonyesho hayo sio kama tu huonyesha hali ya uchumi ya nchi wanakotoka washiriki bali pia mwelekeo wa uchumi wa dunia. Kauli mbiu ya maonyesho ya mwaka huu ni “Maonyesho ya kimataifa ya Guangzhou na mchango wake kwa dunia”.

China kwa kutambua umuhimu wake kwa uchumi wa dunia, imekuwa ikijitahidi kuhakikisha inaendelea kufungua zaidi soko lake na mchango wake kwenye kufufua uchumi wa dunia kutokana na athari za janga la COVID-19. Na juhudi hizi sio kama tu zinaonekana kwenye maonyesho haya ya Guangzhou, au maonyesho yaliyofungwa hivi karibuni kati ya China na nchi za Afrika mjini Changsha, Hunan au yale yatakayofanyika mjini Shanghai mwezi Novemba, bali pia kuna majukwaa mbalimbali ya biashara ya mtandao wa internet yanayounganisha moja kwa moja wateja wa China na wauzaji wa bidhaa kutoka nchi mbalimbali duniani.

Lakini pia maonyesho ya safari hii yana mwelekeo mwingine wa kuvutia, sio kama tu bidhaa zilizotengenezwa China zitatangazwa na kuuzwa, lakini pia bidhaa za teknolojia ya hali ya juu zilizotengenezwa China zinazoweza kutumiwa na watu mbalimbali hata watu wa kawaida pia zitatangazwa na kuuzwa. Tofauti na ilivyozoeleka katika miaka iliyopita, kwenye maonyesho ya maendeleo ya uvumbuzi kwenye bidhaa ya China yanatoenekana zaidi na yanatarajiwa kuwa endelevu.
 
View attachment 1973583

Maonyesho ya kimataifa ya biashara ya Guangdong awamu ya 130 ambayo ni maarufu kwa jina la Canton Fair yamefunguliwa tarehe 15 Oktoba mjini Guangzhou. Maonyesho haya yanatajwa kuwa ni maonyesho ya muda mrefu zaidi na endelevu zaidi kati ya maonyesho yote ya kimataifa ya biashara duniani hadi sasa yakiwa yamefanyika kwa jumla ya miaka 130.

Kwa mara ya kwanza tangu maonyesho haya yaanze mwaka 1957, safari hii kuna vileta bahati (Mascot) vya maonyesho hayo ambavyo ni wanasesere wawili wa umbo la nyuki, mmoja ni wa dume alipewa jina la Haobao (好宝), na mwingine jike akiwa na jina la Haoni (好妮). Nyuki hawa wawili wanabeba maana ya utiifu, umoja na kujitolea. Maana ya vileta bahati hivyo ni kuwa maonyesho haya yanaonyesha nia pana ya China ikiwa ni nchi inayoimarika kiuchumi, ya kuendeleza uchumi ulio wazi na kuwa na mustakbali mzuri wa pamoja kwa binadamu kupitia biashara.

Maonyesho ya awamu hii yanafanyika wakati dunia inaendelea kukabiliana na janga la virusi vya Corona, na wafanyabiashara wengi wanaendelea kukabiliwa na hatua mbalimbali zinazowafanya washindwe kusafiri na kufanya biashara zao. Hata hivyo China imejitahidi kufanya kila linalowezekana kuwawezesha watu kushiriki kwenye maonyesho hayo, iwe ni kwa washiriki kuja wao wenyewe au kwa kushiriki kupitia mtandao wa internet.

Kwa nchi za Afrika hii ni fursa nzuri kwa wafanyabiashara wanaotaka kununua bidhaa za mtaji kama vile mashine na mitambo ya uzalishaji, pamoja na vifaa vingine vingi ambavyo hupatikana China kwa bei nafuu vikiwa na ubora wa juu, lakini pia maonyesho hayo ni fursa ya kuuza bidhaa zao au hata kutafuta fursa za ushirikiano na wawekezaji wa China.

Maonyesho haya huwa yanatajwa pia kama ni kipimo cha hali ya uchumi wa dunia, na mwitikio wa ushiriki kwenye maonyesho hayo sio kama tu huonyesha hali ya uchumi ya nchi wanakotoka washiriki bali pia mwelekeo wa uchumi wa dunia. Kauli mbiu ya maonyesho ya mwaka huu ni “Maonyesho ya kimataifa ya Guangzhou na mchango wake kwa dunia”.

China kwa kutambua umuhimu wake kwa uchumi wa dunia, imekuwa ikijitahidi kuhakikisha inaendelea kufungua zaidi soko lake na mchango wake kwenye kufufua uchumi wa dunia kutokana na athari za janga la COVID-19. Na juhudi hizi sio kama tu zinaonekana kwenye maonyesho haya ya Guangzhou, au maonyesho yaliyofungwa hivi karibuni kati ya China na nchi za Afrika mjini Changsha, Hunan au yale yatakayofanyika mjini Shanghai mwezi Novemba, bali pia kuna majukwaa mbalimbali ya biashara ya mtandao wa internet yanayounganisha moja kwa moja wateja wa China na wauzaji wa bidhaa kutoka nchi mbalimbali duniani.

Lakini pia maonyesho ya safari hii yana mwelekeo mwingine wa kuvutia, sio kama tu bidhaa zilizotengenezwa China zitatangazwa na kuuzwa, lakini pia bidhaa za teknolojia ya hali ya juu zilizotengenezwa China zinazoweza kutumiwa na watu mbalimbali hata watu wa kawaida pia zitatangazwa na kuuzwa. Tofauti na ilivyozoeleka katika miaka iliyopita, kwenye maonyesho ya maendeleo ya uvumbuzi kwenye bidhaa ya China yanatoenekana zaidi na yanatarajiwa kuwa endelevu.
Safi sana Ila bado promotion iendelee. wastani wa vikombe sita kwa mwaka ni matumizi madogo mno. mimi peke yangu nakunywa vikombe nane kwa wiki
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom