johnthebaptist
JF-Expert Member
- May 27, 2014
- 83,850
- 141,770
Kwa namna alivyopita katika tanuru la kisiasa na misukosuko yote ile, namuona Tundu Antipas Lissu akiachana kabisa na mambo ya siasa na kwenda kutoa ushuhuda wa yale Mungu amemtendea. Ni kwa neema ya Mungu tu Lissu alipona katika tukio lile la kijambazi, hivyo ana kila sababu ya kwenda kuihubiri injili ya uponyaji. Chadema wamwache Lissu na familia yake sasa ili wapate fursa ya kuwa na maamuzi yao kama familia na chama kirudi huku duniani kuendelea na shughuli za siasa zilizosimama kwa zaidi ya mwezi sasa!