Maoni yatolewayo na wanasiasa wajulikanao hapa JF yalindwe vipi?

Kichuguu

Platinum Member
Oct 11, 2006
15,293
18,888
Ndugu wanaJF, najua mada hii siyo siasa lakini bado ina maudhui ya siasa, hivyo nimeamua kuiweka hapa badala ya kuipeleka kule kwenye hoja mchanyiko au kwenye udaku.

Nitatoa background information ambayo ineonekana kuwa ndefu kidogo kwa sababu sipendi kufupisha quotes ninazofanya hapa ili kuepusha lile ninalotaka kuongelea, yaani upotoshaji wa post za wachangiaji mbalimbali. Msomaji anaweza kurukia moja kwa moja kwenye paragraph ya mwisho iliyo katika herufi nzito na kuepuka kusoma hii background information iliyoko katikati.


Kule Google Groups kuna discussion group ya Watanzania ijulikanayo kama wanabidii na website yao ni wanabidii.net. kwa wale wasioifahamu discussion group ile ni kwamba inajadili mada moto moto za kisiasa kama hii JF. Ila wachangiaji wengi pale wanatumia majina yao moja kwa moja badala ya aliases. Kinachonifanya niandike hapa ni kuhusiana na mjadala wa juzi uliofanyika pale ukiwa na kichwa cha habari kisemacho "Nionavyo Mimi....Uchaguzi wa Rais na wabunge vitenganishwe." Ingawa sikuomba wahusika ruhusa kutumia mjadala ule hapa JF, hata hivyo nitachomoa posts zilivyokuwa bila kuzifanyia editing yoyote ili kuzia nisipotoshe nia za wachangiaji wale. Katika mjadala huo niliotaja hapo juu, Mheshimwa Zitto alitoa maoni yake kama ifuatavyo

Hoja hii inaweza kuwa na maana sana ikijadiliwa kwa mapana yake. Nchi kadhaa Duniani zenye kufuata mfumo kama wetu mchanyato wa Rais na Waziri Mkuu mwenye madaraka kidogo wametengnisha Uchaguzi wa Rais na Wabunge. Rwanda, Rais anakaa Madarakani miaka 7 na anaweza kuoongeza mara moja na Bunge miaka 5. Hivyo hakuna kipindi ambacho kimoja kati ya Bunge na Urais havipo. Hii inatumika kwa nchi nyingi zilizokuwa chini ya Mfaransa. Marekani Useneta ni miaka 6, Ubunge miaka 2 na Urais miaka 4. katika uchaguzi ni nusu tu ya maseneta ndio huingia katika uchaguzi na hivyo Taasisi za taifa kuwepo muda wote licha ya kwamba kuna uchaguzi. Kila baada ya miaka 2 kuna uchaguzi Marekani ama wa wabunge, au rais au Maseneta. Mwaka 2008 katika uchaguzi
Mkuu wao walichagua nusu ya seneti na Rais. mwaka 2006 wakati democrats walipochukua Bunge na Pelosi kuwa Spika hapakuwa na Uchaguzi wa Urais.

Mfumo huu unahahakisha kuwa Dola ipo - Mihimili- muda wote kwa mbili kati ya taasisi kutokuwa katika ucahaguzi na kuondoa uncertainty zozote.

Mjadala kama huu Tanzania nina mashaka hautakuwa na tija kwani watanzania huwa tunajikuta tunajadili watu badala ya masuala. Hoja kama hii ni rahisi sana kwa wanasiasa kuonyesha kana kwamba ama unataka wabunge waongezewe muda au Rais Kikwete aongezewe Muda. Na kwa kuwa sasa tumekosa statemen ambao wangeweza kuangalia mambo juu ya siasa kama Mwalimu Nyerere, mjadala kama huu utakufa kibudu.

Hata hivyo ni hoja nyeti sana katika kulinda Demokrasia ya vyama vingi na
katika kuhakikisha nyakati za uchaguzi Taifa halitetereki kwani Asasi za
Dola 2/3 zinakuwapo.

I would go for 6 years Urais and 4 years Ubunge.

Wanasayansi ya Siasa wanaweza kutusaidia faida na hasara za mfumo ambao tunaujadili na tukafanya mjadala huu mpaka mwisho na kutoa ripoti maalumu ya wanabidii kwa umma na mamlaka husika. Labda tunaweza kuwa chachu ya marekebisho ya mfumo wetu wa uchaguzi.

Zitto
baadaye mcahangiaji Lingsona akajibu Zito ifuatavyo
Kaka Zito
Shukrani kwa maelezo ya kina zaidi kuhusu suala hili. Ni wajibu wetu kuhuisha mijadala yenye tija kwa taifa letu hata kama kwa kuanzia haitakuwa popular!

Ili kuepuka kujadili watu, kama ulivyosema, tunaweza kusema lini utaratibu huo uanze, mathalani kwa rais atakayeingia madarakani baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Vivyo kwa wabunge, utaratibu mpya utumike baada ya bunge hili kumaliza muda wake, au hata baada ya uchaguzi wa mwaka 2015. Kwa kuweka benchmark tunaweza kuepuka hoja za kisiasa kwamba tuna agenda ya siri kumwongezea muda mtu fulani. Gharama ya muda na mchakato si kitu iwapo tija ya kufanya mabadiliko tunayoyatazamia na kuyaamini ni kubwa.

Pamoja na mjadala huu, suala la kurejesha uchaguzi wa madiwani kwenye chaguzi za serikali za mitaa halina budi kuhuishwa. Haileti maana, madiwani kuchaguliwa katika uchaguzi mkuu wakati wenyeviti wa mitaa/vijiji na vitongoji wanachaguliwa tofauti.

Nachangia.
Zito naye akajibu ifuatavyo

Lingson,
Tunaweza kuwa na utaratibu ambao mfano, 2014 tunafanya uchaguzi wa Vijiji, Mitaa na Madiwani. 2015 Uchaguzi Mkuu wa Wabunge na 2016 Uchaguzi Mkuu wa Rais. Hivyo tunaweza kusema kuwa tunaanzia watakaochaguliwa mwaka 2010.

Ukishakuwa na daftari la kudumu la wapiga kura na Tume Huru ya Uchaguzi, gharama za uchaguzi huwa haziwi kubwa sana kama iwapo hakuna daftari na Tume ya uchaguzi mbovu kujaribu kupata fedha nyingi wawezavyo. Chaguzi za madiwani na wenyeviti wa serikali za mitaa z5naweza kabisa kuendeshwa na Kamati huru za Uchaguzi katika ngazi za Wilaya. Tatizo hatuna uaminifu katika masuala haya na ndio maana hata huu uchaguzi wa mitaa tumetaka usimamiwa na tume.

tatizo kubwa katika taifa letu hatuna mijadala ya kina na yenye kufika
mwisho kuhusu masuala yenye masilahi kwa taifa kwa ujumla wake.

Mjadala uendelee
Jambo la kushangaza, ni kuwa gazeti la Tanzania Daima limetumia mjadala ule na kuandika habari yenye kichwa cha habari kisemacho

"Zitto: JK aongezewe Muda"

katika habari ile siyo tu kuwa mwandishi alipotosha mchango uliokuwa umetolewa na Zitto pale wanabidii.net, bali pia alitumia habari ile bila kuomba kibali cha Zitto mwenyewe au kwa moderator wa Wanabidii.net unless kama yeye mwenywe mwandishi ndiye moderator. Kitendo kile kimafnaya Zitto atangaze kujitoa katika group ile, na mpaka sasa ninapoandika bado wanajadiliana na kumwomba Zitto afikirie tena uamuzi wake. Kilichionishangaza ni pale mhariri wa Tanzania Daima bwana Absalom Kibanda (ambaye pia ni mwanachama wa Wanabidii.net) aliposema kuwa hakubaliani na tafsiri ya mwandishi wake kuhusu maneno yaliyotolewa na Zito lakini bado akamlaumu Zito kwa kusababisha maneno yake yawe yatafsiriwe vibaya na yule mwandishi; hakujilaumu kama mhariri kuwa aliruhusu kuchapishwa kwa habari isiyothibitika!!! na mbaya zaidi kwa maoni yangu ni kuwa mhariri hakukubali hata kuomba radhi kutokana kosa la mwandishi wake, badala yake kumtaka Zito atoe maelezo ya kufafanua alikuwa na maana gani katika post ile kama nilvyoonyesha hapa chini

Wanabidii

Ndugu zangu wasomaji wa mtandao huu ambao hakuna shaka hata kidogo umekuwa na mchango mkubwa katika kuendeleza utamaduni wa mijadala na utoaji wa mawazo tofauti.

Mimi ndiye Mhariri Mtendaji wa Tanzania Daima, Absalom Kibanda ambaye leo asubuhi nilizungumza na Zitto Kabwe kuhusu habari iliyochapishwa katika gazeti letu leo hii na kimsingi nikaungana naye kusikitika kwamba alikuwa amenukuliwa kwa makosa.

Katika mazungumzo yetu na baadaye katika mawasiliano ya simu, Zitto alinieleza wazi kwamba alikuwa na mashaka kuwa habari hiyo iliandikwa kwa nia mbaya dhidi yake na kimsingi akafikia hatua ya kufikiria kwamba, habari hiyo huenda ikawa na mkono wa viongozi wenzake ndani ya Chadema ambao amekuwa akivutana nao kwa muda mrefu.

Tukiwa katika mazungumzo nilimueleza wazi kwamba habari ile ilionekana wazi ikijenga taswira kwamba yeye alikuwa ameshaanza kula njama na viongozi wa CCM ili kumruhusu Kikwete aendelee kuwa rais hadi mwaka 2016 chini ua utaratibu wa kugombea kwa miaka sita hali ambayo inaweza kutafsiriwa na wengi kuwa itamuwezesha yeye Zitto kupata fursa ya Kikatiba kugombea urais kwani atakuwa amefanikiwa kutimiza umri wa miaka 40 inayotakiwa kikatiba.

Nilimtaka anipe muda wa kujadiliana na mwandishi wa habari ile, mhariri aliyekuwa katika dawati jana ambaye ingawa alinibrief kuhusu habari hiyo na kunihakikishia kuwa Zitto alikuwa ameyasema maneno hayo jana nilipaswa kuzungumza naye na kisha kupima hoja za pande zote mbili kuhusu suala hilo.

Baada ya kufanya majadiliano na wenzangu, nilikuwa ndiyo kwanza najipanga kuzungumza na Zitto na kumpa taarifa za upande wa pili kuhusu kile kilichoandikwa na namna ambavyo tungefanya kurekebisha kasoro hii.

Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba Zitto anaonekana kukosa subira na ameamua kurusha malalamiko dhidi ya habari ile jambo ambalo kimsingi ni haki yake lakini akaenda mbele kusema wazi kwamba habari ile iliandikwa kwa nia mbaya dhidi yake na hakuishia hapo akasema hii si mara ya kwanza kwa gazeti hili kuandika habari ambazo anasema 'hazina ukweli wa kutosha'.

Napenda kuwahakikishia wanabidii na Watanzania wenzangu kwa ujumla kwamba, hitimisho la Zitto kuwa habari ile iliandikwa kwa nia mbaya dhidi yake si za kweli hata kidogo na Zitto mwenyewe analitambua hilo sana kwani ni mmoja wa watu wanaoufahamu vyema utendaji kazi wa gazeti hili pengine kuliko ilivyo kwa mwanasiasa mwingine yeyote.

Lakini kilichonisikitisha zaidi ni uamuzi wake wa kufikia hatua ya kutaka kujitoa katika wanabidii kwa sababu ya kuwapo kwa kile alichodai kwamba kuna watu wenye nia mbaya dhidi yake. Sentensi hii ni ushahidi wa wazi kwamba hadi sasa Zitto anaendelea kuamini kwamba gazeti lile liliandika habari kwa nia mbaya. Haiingii akilini hata kidogo.

Binafsi kama mhariri baada ya kumsikiliza Zitto na kisha kuipitia taarifa ya wanabidii alikotuma maneno yake, niliona wazi kuwapo kwa uwezekano mkubwa wa maneno ya Zitto kutafsiriwa kuwa yanamlenga Kikwete kama alivyotafsiri mwandishi na mhariri aliyesimamia uchapaji wa gazeti la jana. Zitto anatambua vyema namna nilivyo mvumilivu sana ninapopingwa kwa hoja ambazo ninazisimamia.

Kwa sababu hiyo basi kwa kuwa ninaheshimu uhuru wa watu kufikiri pasipo kuvunja sheria za nchi, ninamruhusu Zitto kuwasiliana ama na gazeti hili kufafanua kile alichotaka kusema akiondoa hoja yake kwamba habari ile imeandikwa kwa nia mbaya dhidi yake na/ au kuwasiliana na gazeti jingine analoloona litafanikisha azma yake ya kuisahihisha habari aliyoiandika.

Lakini zaidi ya hilo wakati bado tukiendelea kutafakari nini cha kufanya katika Tanzania Daima kumtendea Zitto haki ambazo tunaona hakutendewa katika gazeti hili, napenda kusema bayana kwamba anao uhuru wa kuchukua hatua zozote anazoona zinafaa kusafisha jina lake.

-
Zitto

Nimekusoma na nimekuelewa. Mobini Sarya ni mwanabidii na nimelihakikisha hilo, na yeye ndiye aliyeandika habari hiyo. Sikubaliani kabisa na tafsiri yake ingawa naiheshimu kwani naweza kuona waziwazi alikoitoa kutokana na maandishi yako. Acha nikuonyeshe ushahidi wa maneno yako wewe mwenyewe.

"Tunaweza kuwa na utaratibu ambao mfano, 2014 tunafanya uchaguzi wa Vijiji, Mitaa na Madiwani. 2015 Uchaguzi Mkuu wa Wabunge na 2016 Uchaguzi Mkuu wa Rais. Hivyo tunaweza kusema kuwa tunaanzia watakaochaguliwa mwaka 2010."

"Mjadala kama huu Tanzania nina mashaka hautakuwa na tija kwani watanzania huwa tunajikuta tunajadili watu badala ya masuala. Hoja kama hii ni rahisi sana kwa wanasiasa kuonyesha kana kwamba ama unataka wabunge waongezewe muda au Rais Kikwete aongezewe Muda".

Kaka maeneo haya mawili ni rahisi sana mtu kama Mobini na wengine kuyageuza au kuyatafsiri kuwa yalikuwa na lengo la kumtengenezea njia Kikwete. Nadhani unatambua duniani kote kwamba wanasiasa mnashauriwa kuwa makini sana kwa chochote kile mnachotamka kwani kinaweza kutafsiriwa kinyume cha kile mlichokimaanisha.

Ukweli wa namna hii mara nyingi huwa ni mchungu kwa wanasiasa wengi na ndiyo maana wengi wamekuwa waangalifu sana kutoa maoni hadharani na kila wakati. Wewe mwenyewe ni shahidi mzuri kwamba maneno ya Dk. Slaa dhidi ya Kafulila kwamba kijana yule ni 'dagaa' yamemgarimu kiasi gani mzee yule na kwa kiasi gani maadui wa Slaa na Chadema wanayatumia kumvuruga Slaa na chama chenu.

Kumbuka maneno kama yale ya Kikwete aliposema kuwa "Urais wangu hauna ubia" yalivyotafsiriwa na kila mtu kwa namna na kwa tafsiri yake. Tanzania Daima kwa maelekezo ya mhariri wake ambaye ni mimi tumekuwa na desturi ya kufanya 'analysis' na wakati mwingine 'analysis' huwa zinafanyika katika mitazamo ambayo si sahihi.

Kwa sababu hiyo basi, majibu yangu kwako hayakubeba arrogance ya aina yoyote ingawa nilisikitishwa na uamuzi wako wa kulishambulia Tanzania Daima katika misingi isiyo sahihi (kwa mtazamo wangu). Naamini kwa dhati kabisa kuwa unatambua vyema kwamba habari ile hata kama ina kasoro ya tafsiri, haikuandikwa kwa nia mbaya hata kidogo. Tanzania Daima kama gazeti siku zote limekuwa likisimamia ukweli pasipo kujali machungu ya ukweli huo kwa ndugu, marafiki na jamaa zetu.

Najua na kutambua kuwa, umejijengea taswira ya kipekee kisiasa ambayo hautakuwa tayari kuona ikiharibiwa na mtu yeyote yule kwa namna yoyote ile. Na msimamo wako huu ambao ni wa msingi kabisa naamini kuwa ndiyo unaokusukuma kila mara kuipigania haiba yako hiyo ya kisiasa. Hivyo hivyo Tanzania Daima ni brand ambayo nimepambana sana kuifikisha hapa ilipo leo kwani inajenga taswira yangu binafsi na ya wenzangu wengine kama mimi.

Ni kwa sababu hiyo siku zote nimekuwa sina sababu hata moja ya kumhurumia mtu yeyote ambaye kwa kujua au kutokujua anaamua kuidhalilisha brand hii (Tanzania Daima) kwa kuipachika sifa za uongo na za kuipaka matope. Ni kwa sababu hiyo kwa nyakati tofauti nimekabiliana ana kwa ana na yeyote anayejaribu kufanya kosa hilo kwa namna na njia ambazo wakati fulani huwa zinaniweka katika mazingira magumu.

Ninafanya hivyo kwa kuwa natambua kwamba baadhi ya watu, akiwamo wewe Zitto ni watu ambao brand hii (Tanzania Daima) imewapigania kwa wema na kuchangia mafanikio yao ya kisiasa kwa kiwango kikubwa pengine kuliko brand nyingine zote. Naweza kusema wazi kwamba, ni gazeti hili ambalo katika masuala ya msingi lilisimama na litaendelea kusimama nawe bega kwa bega hata kama kwa kufanya hivyo tutatofautiana na ndugu zetu, marafiki zetu na wakati mwingine wamiliki wetu. Tumelifanya hilo mara nyingi na tuombe maisha tutaendelea kulifanya hilo mbele ya safari.

Ni mwandishi na mhariri mpumbavu tu ambaye atashindwa kutambua mchango mkubwa wa Zitto katika maendeleo ya siasa za ushindani na demokrasia ya kweli ya vyama vingi. Ni mwanahabari mwehu ambaye anaweza akasimama leo na kupinga ukweli kwamba Zitto ni chachu kuu ya mchango wa kipekee wa viongozi vijana katika taifa hili.

Zitto na wanabidii wenzangu wengine wanapaswa kutambua hilo na ushahidi upo kwamba Tanzania Daima limekuwa na desturi ya kuomba radhi katika kila jambo kubwa ambalo hudhani tumelikosea na kwa kufanya hivyo wakati mwingine tumekuwa tukiingia katika matatizo makubwa ya kimtazamo. Wako waliotuita waoga, wanafiki, wazushi na kila aina ya majina. Na hata katika hili, tupo tayari kuomba radhi iwapo tutajiridhisha pasipo shaka kwamba tumefanya makosa.

Utabakia kuwa mwanasiasa wa mfano na wa kipekee kwangu. Ni kwa sababu ya kukuheshimu wewe binafsi ndiyo maana marafiki na maadui zako ndani na nje ya Chadema wanaheshimu na kutambua ukaribu wetu kwa kuwa nimekataa kuwa mnafiki.

Hata hivyo wewe unalitambua hili, kwa sababu ya dhamira safi ya kukujenga, kukukomaza na kukutakia mema nitakuwa wa kwanza kukunyoshea kidole pale ambapo mtazamo wangu na uchambuzi wangu utanithibitishia kuwa umekosea na hivyo hivyo nitakuwa wa kwanza kukutetea na kukupigania katika mambo ya msingi utakayofanya na kuyasimamia. Nimeyafanya hayo na historia itanilinda. Utabikia kuwa ndugu yangu, rafiki yangu na mwanasiasa wa mfano japo utakapoteleza au kuanguka sintakaa kimya.

Absalom Kibanda
Mhariri Mtendaji
Tanzania Daima
Mimi pamoja na kuwa sina elimu ya uandishi wa habari, nilisoma thread ile yote na kuona kuwa Zito alikuwa akitoa mawazo pana ambayo hayakuwa yanamhusu mwanasiasa yeyote specific, i.e. Kikwete kama ilivyoripotiwa na tanzania daima. Na alikuwa ni mchangiaji tu kama ambavyo huwa tunachangia hapa mada mbalimbali zinazoanzishwa na watu mbalimbali.


Baada ya kusoma hayo huko Wanabidii.net, nikastuka kidogo kuwa hata sisi tuna wanachama wanasiasa hapa JF ambao hutumia majina yao kutoa mada mbalimbali na wanaweza na kuja kujikuta katika hali kama iliyomkuta Zito: post zao zikachukuliwa out of context na kuwekwa kwenye headline za magazeti. Ingawa nimewahi kuona mada zinatolewa hapa na kuwekwa kwenye forum nyingine lakini sijawahi kuthibitisha posts za wachangiaji wetu zikipotoshwa huko nje.

Swali langu, je hapa JF tuna utaratibu gani wa kulinda michango original ya wanachama wetu (hasa wale wanaojulikana kwa majina yao halisi) isipotoshwe kwenye print media au kwa njia nyingine yoyote?

 
Sifikirii kama upo utaratibu wowote wa kulinda maandishi ya wanachama. Tatizo liko kwenye commitment kufanya hiyo kazi inachukua muda na pesa vile vile.
 
Zito alikuwa anatoa tu maoni yake, inahuzunisha sana hasa gazeti kama la Tanzania daima,

Zitto anaonekana kuyaingizia pesa magazeti mengi sana nchi hii, na mijadala mingi imekuwa kumwaribia yeye na kumuathiri kisaikolojia very same waandishi huwa tunawasifu wanafanya kazi vizuri

mtoa maada, kuzuia ni vigumu, because they can write in other language! wanachotaka wao ni pesa.

Kibanda unajua malengo yako, wewe ni mhariri wa hilo gazeti, tumeshakujua usipate shida sana kujitetea. wala kuandika lugha za kilaghai! Haujaanza leo na huyo mwandishi siyo mtoto !
 
Kwa nini yalindwe? Kwa nini watoa maoni wasisimamie maoni yao?

Omega Psi Phi? 'wewe ni mtu wa Kibanda nini', unaweza kutoa tafsiri sahihi ya neno aliloandika mtu pasipo kumuuliza??

Unaweza kucopy mananeo ya mtu, ukamchafua halafu ukarudi na kusema tulifikiri ulisema hivi???

Zito anailisha familia ya Kibanda, period! huo nao ni uanaume!

Umeona hiyo sentensi ya kwanza niliyoibold? imekaa sawa? iko wrong, siwezi kabisa kukujudge na kutoa tamko kwa watu milioni 40 kwa sababu Omega umendika kitu ambacho nadhani kinaendana na ninavyofikiri mimi!! This is insane! you can feel that,
 
Kwa nini yalindwe? Kwa nini watoa maoni wasisimamie maoni yao?

Kumbuka kuwa forum siyo press conference; hivyo siyo mahali ambapo mchangiaji anatoa maoni ambayo yana-reflect msimamo wake rasmi wa kuweka kwenye headlines. Michango minine hutolewa kulingana na flow ya discussion; siyo vizuri ku-single out jibu la mchangiaji mmoja na kulifanya kuwa habari kamili bila ya kuonyesha jinsi gani maoni yake yalivyokuwa ana-interact na ya wachangiaji wengine. Kufanya hivyo ndiko kunakoweza kusababisha upotoshaji wa mawazo ya wachangiaji kama ilivyotokea kwenye hili la Tanzania Daima na Zito kama nilivyoeleza huko juu ambapo gazeti lilishindwa kuona kuwa maneno ya Zito waliyoquote yalikuwa ni generic kujibu swali la Lingason na wala hakuwa specific kuwa anataka sasa hivi JK aendelee kama walivyoripoti.
Tunaweza kuwa na utaratibu ambao mfano, 2014 tunafanya uchaguzi wa Vijiji,
Mitaa na Madiwani. 2015 Uchaguzi Mkuu wa Wabunge na 2016 Uchaguzi Mkuu wa
Rais. Hivyo tunaweza kusema kuwa tunaanzia watakaochaguliwa mwaka 2010.
 
Kumbuka kuwa forum siyo press conference; hivyo siyo mahali ambapo mchangiaji anatoa maoni ambayo yana-reflect msimamo wake rasmi wa kuweka kwenye headlines. Michango minine hutolewa kulingana na flow ya discussion; siyo vizuri ku-single out jibu la mchangiaji mmoja na kulifanya kuwa habari kamili bila ya kuonyesha jinsi gani maoni yake yalivyokuwa ana-interact na ya wachangiaji wengine. Kufanya hivyo ndiko kunakoweza kusababisha upotoshaji wa mawazo ya wachangiaji kama ilivyotokea kwenye hili la Tanzania Daima na Zito kama nilivyoeleza huko juu ambapo gazeti lilishindwa kuona kuwa maneno ya Zito waliyoquote yalikuwa ni generic kujibu swali la Lingason na wala hakuwa specific kuwa anataka sasa hivi JK aendelee kama walivyoripoti.

Inaelekea kuna tatizo la waandishi wetu wa habari na lakini pia wanasiasa hao wanaweza kutumia luxury ya anonymity na kubandika kwa kutumia majina bandia.
 
Kumbuka kuwa forum siyo press conference; hivyo siyo mahali ambapo mchangiaji anatoa maoni ambayo yana-reflect msimamo wake rasmi wa kuweka kwenye headlines. Michango minine hutolewa kulingana na flow ya discussion; siyo vizuri ku-single out jibu la mchangiaji mmoja na kulifanya kuwa habari kamili bila ya kuonyesha jinsi gani maoni yake yalivyokuwa ana-interact na ya wachangiaji wengine. Kufanya hivyo ndiko kunakoweza kusababisha upotoshaji wa mawazo ya wachangiaji kama ilivyotokea kwenye hili la Tanzania Daima na Zito kama nilivyoeleza huko juu ambapo gazeti lilishindwa kuona kuwa maneno ya Zito waliyoquote yalikuwa ni generic kujibu swali la Lingason na wala hakuwa specific kuwa anataka sasa hivi JK aendelee kama walivyoripoti.

- Mkuu Mwalimu Kichuguu, hiii habari yako haijakaa sawa hata kidogo!Halafu wewe unaheshimika sana hapa. Lakini please tizama hapa chini, huko majuu huyu Senator haya maneno hakuyasema kwenye pres. conference lakini yamenukuliwa na tayari ameomba msamaha badala ya kususa na kutafuta visingizio vya kitoto, siasa ni professional kama zingine, zina miiko yake na process zake pamoja na sheria zake, kama huziwezi kuzifuata ni vyema kujitoa na kwenda kwenye field nyingine, soma chini hapa:-


WASHINGTON (Reuters) - The Republican Party chief called on Senator Harry Reid on Sunday to step down as Senate majority leader over racial comments about President Barack Obama, while Democrats tried to put the issue behind them. Both Obama and Reid are Democrats.

Republican National Committee Chairman Michael Steele said Reid should step aside as Senate majority leader, saying if a Republican made the same remarks Democrats would be "screaming for his head.""Oh yeah, there's a big double standard here," Steele, who is black, said on the NBC program "Meet the Press.""There is this standard where the Democrats feel that they can say these things and they can apologize when it ... comes from the mouths of their own. But if it comes from anyone else, it's racism," Steele added on "Fox News Sunday."


Steele said, "Well, if it is, I apologize for it. ... I wasn't intending to say a racial slur at all." Reid's comments, made in private conversations, were quoted in a newly published book about the 2008 U.S. presidential campaign, "Game Change," by Time magazine reporter Mark Halperin and New York magazine writer John Heileman.

'A POOR CHOICE OF WORDS'
Reid on Saturday apologized for "using such a poor choice of words." Obama issued a statement accepting the apology.Reid, 70, has been a close partner of the White House on key Obama "Harry Reid made a misstatement. He owned up to it. He apologized. I think he is mortified by the statement he's made. And I don't think he should step down," Democratic Senator Jack Reed told "Fox News Sunday."Republicans compared Reid's remarks to those made in 2002 by Republican Trent Lott, praising former segregationist presidential candidate and long-time senator Strom Thurmond. Lott stepped down as Senate majority leader over the comments.


"If he (Lott) should resign, then Harry Reid should," Republican Senator Jon Kyl told "Fox News Sunday."

- Sasa Mwalimu, unaona hawa wenzetu wanakubali na kuungama bila visingizio kama sisi!
Huyu Reid hakusema kwenye pres. Conference kama unavyodai iwe ili kunukuliwa, ila kwa kuwa ni politician aliyefikia lelvel ya kuwa kazini kwa taifa 24/7 kila anachosema hata awe wapi ni msimamo wake kama a national politician na ndio maana hapo juu unaona mtumzima hajaleta maneno mengi amekuba rsponsibility na kubeba msalaba!

Respect.


FMEs!
 

- Mkuu Mwalimu Kichuguu, hiii habari yako haijakaa sawa hata kidogo!Halafu wewe unaheshimika sana hapa.


Respect.


FMEs!


Mkuu imekaa sawa kabisa labda kama unataka nifafanue zaidi.

Katika forum hii wakati mwingine tunajibizana kulingana na premises zilizoko mbele yetu, hasa waanzisha mada au waunganisha mada. Mara kadhaa tumwahi kuandika post ambazo baadaye tunagundua kuwa premises tulizoletewa mbele yetu hazikuwa sahihi. Ndiyo maana nasema majibu ya mchangiaji mmoja katika forum siyo rasmi ya kuchukuliwa na kuwekwa kwenye headlines unless kuna uhakika kuwa premise waliyotumia ni sahihi kabisa. Kuna haja ya kumuuliza mchangiaji hata kwa PM kabla hujaziandika gazetini hasa kama unataka kutumia jina lake moja kwa moja. Personally nimewahi kuombwa ruhusa na watu kadhaa kuthibitisha post zangu na kutoa ruhusu wazitumie katika articles zao, nina imani kuwa hata wewe FMEs umeshawai kuombwa kuthibitisha na kutoa ruhusa ya namna hiyo.

Jambo jingine ambalo ndilo kubwa nilioongea hapo juu ni hilo la kusingle out post ya mchangiaji mmoja bila kuangalia jinsi alivyointeract na wachangiaji wengine; hiyo ndiyo recipe kubwa ya distortion.
 
Mkuu imekaa sawa kabisa labda kama unataka nifafanue zaidi.

Katika forum hii wakati mwingine tunajibizana kulingana na premises zilizoko mbele yetu, hasa waanzisha mada au waunganisha mada. Mara kadhaa tumwahi kuandika post ambazo baadaye tunagundua kuwa premises tulizoletewa mbele yetu hazikuwa sahihi. Ndiyo maana nasema majibu ya mchangiaji mmoja katika forum siyo rasmi ya kuchukuliwa na kuwekwa kwenye headlines unless kuna uhakika kuwa premise waliyotumia ni sahihi kabisa. Kuna haja ya kumuuliza mchangiaji hata kwa PM kabla hujaziandika gazetini hasa kama unataka kutumia jina lake moja kwa moja. Personally nimewahi kuombwa ruhusa na watu kadhaa kuthibitisha post zangu na kutoa ruhusu wazitumie katika articles zao, nina imani kuwa hata wewe FMEs umeshawai kuombwa kuthibitisha na kutoa ruhusa ya namna hiyo.

Jambo jingine ambalo ndilo kubwa nilioongea hapo juu ni hilo la kusingle out post ya mchangiaji mmoja bila kuangalia jinsi alivyointeract na wachangiaji wengine; hiyo ndiyo recipe kubwa ya distortion.

- Hivi Mwalimu how sure are you kwamba anayeshuika hakuombwa, pamoja na kwamba sio hoja ya smingi sana, kwani hapo juu huyo Reid wamemuomba? Kwani Tiger woods aliposema maneno yake na wale wanawake alikwua kwenye pres. conference mkuu, ndio maana ninasema habari yako haijakaa sawa hata kidogo na sina mpango wa kulumbana na wewe maana unaheshimika sana hapa,

- Binafsi ninaheshimu sana michango yako hapa, kwenye hizi ishu za quotation za politician ukijali jina hutaweza kua muandishi wa habari hata siku moja!

Respect.


FMEs!
 
Kichuguu hoja yako ipo sawa kabisa..sijui wengine wasichokuelewa ni nini?
Hii ni mara ya pili sasa waandishi wanakuja kuchota news ya mchangiaji mmoja tu kwa maslahi yao binafsi. Kipindi cha nyuma waliwai kuchukua news ya huyo uyo Zitto alipomtetea Dr Idrissa Rashidi. Nionavyo mimi ni muhimu utaratibu ufikiriwe wa kulinda wachangiaji na waandishi ushwara. Vinginevyo JF itakuja kukosa michango ya ndani ya wanasiasa hao. Wao ndio wanaoshiriki siasa-ni vizuri kupata michango yao. Vinginevyo tutaishia kupata michango ya security officers na wabeba mikoba ya wanasiasa ambayo imejaa udaku na sometime wanakuja na issues za kuwalinda babwana zao.
 

- Mkuu Mwalimu Kichuguu, hiii habari yako haijakaa sawa hata kidogo!Halafu wewe unaheshimika sana hapa. Lakini please tizama hapa chini, huko majuu huyu Senator haya maneno hakuyasema kwenye pres. conference lakini yamenukuliwa na tayari ameomba msamaha badala ya kususa na kutafuta visingizio vya kitoto, siasa ni professional kama zingine, zina miiko yake na process zake pamoja na sheria zake, kama huziwezi kuzifuata ni vyema kujitoa na kwenda kwenye field nyingine, soma chini hapa:-



- Sasa Mwalimu, unaona hawa wenzetu wanakubali na kuungama bila visingizio kama sisi!
Huyu Reid hakusema kwenye pres. Conference kama unavyodai iwe ili kunukuliwa, ila kwa kuwa ni politician aliyefikia lelvel ya kuwa kazini kwa taifa 24/7 kila anachosema hata awe wapi ni msimamo wake kama a national politician na ndio maana hapo juu unaona mtumzima hajaleta maneno mengi amekuba rsponsibility na kubeba msalaba!

Respect.


FMEs!

Nafakiri ukiangalia tena kwa kina utaona kuna tofauti kubwa sana baina ya case ya Reid na hii case ya mwandishi wa habari kuchagua post moja au mbili za mchangiaji na kuziweka kwenye headline kama habari kamili huku akiacha interaction ya post hizo na zile za wachangiaji wengine including qualifiers na premises zilizotumiwa na mchangiaji.

Case ya Reid ni habari kamili wakati hii iliyokopiwa kwenye forum siyo habari kamili unless waandishi waipindishe ili kuifanya iwe habari kamili kama walivyofanya, na ndiyo maana wakapotosha.

Kwa kurekebisha tu, nitakubaliana nawe kwa kufuta neno langu la "press conference," lakini hoja yangu kubwa inabaki pale pale kuwa wasichuke post moja na kuifanya habari kamili bila kuiunganisha na premises zake zote na vile vile kupata uthibitisho kutoka kwa mchangiaji. Inawezekana mchangiaji akawa anatoa vipande vipande kabla ya kuungnsiha, wewe mwenyewe FMES umewahi kutuwekea post za namna hiyo na kuacha kuwa tunakufuatilia kwa siku kadhaa hadi unapomaliza mada yako.
 
- Hivi Mwalimu how sure are you kwamba anayeshuika hakuombwa, pamoja na kwamba sio hoja ya smingi sana, kwani hapo juu huyo Reid wamemuomba? Kwani Tiger woods aliposema maneno yake na wale wanawake alikwua kwenye pres. conference mkuu, ndio maana ninasema habari yako haijakaa sawa hata kidogo na sina mpango wa kulumbana na wewe maana unaheshimika sana hapa,

- Binafsi ninaheshimu sana michango yako hapa, kwenye hizi ishu za quotation za politician ukijali jina hutaweza kua muandishi wa habari hata siku moja!

Respect.


FMEs!

Mzee, hebu gngalia tena background information nilizotoa wakati nafungua mada kuhusu Zito kuombwa kuthibistiha habari ile.

Kuhusu case ya Reid habari kuu pale siyo ule ujumbe aliokuwa anataka kutuma bali uchaguzi wa maneno aliyotumia.

encouragement of Obama was unequivocal. He was wowed by Obama's oratorical gifts and believed that the country was ready to embrace a black presidential candidate, especially one such as Obama -- a "light-skinned" African American "with no Negro dialect, unless he wanted to have one," as he said privately. Reid was convinced, in fact, that Obama's race would help him more than hurt him in a bid for the Democratic nomination.
Kama reid angebadilisha maneno hayo akasema an "an eloquent African American" usingesikia habari hapo.

Case ya Tiger nayo huwezi kuiweka katika context ninayoongelea hapa.

Jambo kubwa hapa ni hizo dots kufanywa habari kamili kabla hujaziunganisha
 
Nafakiri ukiangalia tena kwa kina utaona kuna tofauti kubwa sana baina ya case ya Reid na hii case ya mwandishi wa habari kuchagua post moja au mbili za mchangiaji na kuziweka kwenye headline kama habari kamili huku akiacha interaction ya post hizo na zile za wachangiaji wengine including qualifiers na premises zilizotumiwa na mchangiaji.

Case ya Reid ni habari kamili wakati hii iliyokopiwa kwenye forum siyo habari kamili unless waandishi waipindishe ili kuifanya iwe habari kamili kama walivyofanya, na ndiyo maana wakapotosha.

- Muhimu ni kama amesema au hakusema, sijawahi kusikia Zitto akilalama kwamba hakusema, ila nimesikia akilalama kwamba aliyemnukuu hakuwa na nia njema, anyways sina mpango wa kulumbana na wewe na hii kesi maana kwangu ni black and white, either mwanasiasa amesema au hakusema, amesema wapi au amesema nini au kwa nini sio yote aliyosema siamini kwamba ni ishu, ila it is up you kuamini unavyotaka, sielewi mwanasiasa anavyoweza kuja hapa na ksuema maneno ambayo hayaamini just because sio pres. conference, sidhani kama tunahitaji wanasiasa wa namna hiyo bongo!

- Habari ikitolewa ana haki zote kisheria kusema hakusema na kuwafikisha wanaomtuhumu kwenye sheria. Anyways, thanks I am out maana tumeipitia hii ishu siku za nyuma sitaki kuirudia tena!

Respect.


FMEs!
 
Kichuguu hoja yako ipo sawa kabisa..sijui wengine wasichokuelewa ni nini?
Hii ni mara ya pili sasa waandishi wanakuja kuchota news ya mchangiaji mmoja tu kwa maslahi yao binafsi. Kipindi cha nyuma waliwai kuchukua news ya huyo uyo Zitto alipomtetea Dr Idrissa Rashidi. Nionavyo mimi ni muhimu utaratibu ufikiriwe wa kulinda wachangiaji na waandishi ushwara. Vinginevyo JF itakuja kukosa michango ya ndani ya wanasiasa hao. Wao ndio wanaoshiriki siasa-ni vizuri kupata michango yao. Vinginevyo tutaishia kupata michango ya security officers na wabeba mikoba ya wanasiasa ambayo imejaa udaku na sometime wanakuja na issues za kuwalinda babwana zao.
siasa zimeingia stage tofauti nikiwa na maana sasa hivi siasa sio kwenye majukwaa, TV na redio pekee, bali pia online. Website ni vyombo vinavyoaminika kutoa habari. viongozi wanatumia you tube, face book, twitter n.k
mfano kwenye uchaguzi wa Irani viongozi walikuwa wanatumia twitter na facebook kutoa statement.
hamna ubaya wowote kwa mwandishi wa habari kum quote zitto, slaa, mnyika, mbowe, mo na wengine ambao wanatumia majina yao.
kama mtu ataki kuwa quoted then ujue huo mchango unawalakini

hata kama mtu ni security officer mchango wake utaeshimika kutokana na hoja yake lakini sio shughuli yake anayoifanya.
hayo mambo ya kulindana tena, tunarudi nyuma badal ya kwenda mbele
 
Nadhani kuna tatizo la kuelewana hapa tena, sidhani kama ni tatizo mtu kuwa quoted, mimi naona tatizo ni kupindisha ukweli wa kile alichosema huyo muhusika! That is the case kwa waaandishi wetu hapa Tz
 
- Muhimu ni kama amesema au hakusema, sijawahi kusikia Zitto akilalama kwamba hakusema, ila nimesikia akilalama kwamba aliyemnukuu hakuwa na nia njema, anyways sina mpango wa kulumbana na wewe na hii kesi maana kwangu ni black and white, either mwanasiasa amesema au hakusema, amesema wapi au amesema nini au kwa nini sio yote aliyosema siamini kwamba ni ishu, ila it is up you kuamini unavyotaka, sielewi mwanasiasa anavyoweza kuja hapa na ksuema maneno ambayo hayaamini just because sio pres. conference, sidhani kama tunahitaji wanasiasa wa namna hiyo bongo!

- Habari ikitolewa ana haki zote kisheria kusema hakusema na kuwafikisha wanaomtuhumu kwenye sheria. Anyways, thanks I am out maana tumeipitia hii ishu siku za nyuma sitaki kuirudia tena!

Respect.


FMEs!


(1) Mkuu wangu usiniangushe, hatulumbani. Ninachozungumza ni hii tabia ya waandishi kuchukua vipande vya posts na mwishowe kudistort intent ya mchangiaji wa forum. Kama umesikia Zito akilalama kuwa amenukuliwa vibaya basi ndiyo distortion yenyewe ninayoongea; isingekuwapo kama mwandishi angechukua effort ya kuwasiliana na Zito kabla ya kuweka p[ost hiyo kwenye headline.

(2) Nina imani kuwa wewe huko juu ya kuamini kwa mkato tu kuwa mwanasiasa kasema au hapana. Ni lazima unajua kuchukua habari kutoka pande zote mbili kama zipo na kuona kama yaliyosemwa kuhusu mwanasiasa huyo yana ukweli au vipi; ninakufahamu hivyo.


(3) Kilichonifanya niandike hii thread siyo swala la kumtetea mtu mmoja au vipi bali kuhusu health ya forum kama hii yetu. Endapo posts za wachangiaji wa namna hiyo zikindelea kuwa distorted na vyombo vya habari kuna hatari wote wataondoka na kama tunavyojua contribution za wanasiasa hawa kwenye forum hizi zimekuwa zinasaidia sana kwa namna mbalimbali. Hii siyo kwa Zito tu, leo hii tumeona jinsi informatio za Nape zilivyokuwa distorted hapa lakini mwenyewe akaja kuzisahihisha. Ninawaona watu wa aina hii kam hazina kubwa kwenye forum hii.


(4) kama jambo hili lilishajadiliwa, that is fine. I was just concerned kuliona kwa mara ya kwanza na ndiyo maana katika opening post yangu niliweka kama swali kwa vile sikuwa na uhakika kama liliwahi kujadiliwa au kuna utaratibu wowote wa kulinda post hizo.


(5) Kusubiri itokee distortion halafu wapelekane mahakamani ndilo jambo nililoongea kwenye aya namba (3) hapo juu.


siasa zimeingia stage tofauti nikiwa na maana sasa hivi siasa sio kwenye majukwaa, TV na redio pekee, bali pia online. Website ni vyombo vinavyoaminika kutoa habari. viongozi wanatumia you tube, face book, twitter n.k
mfano kwenye uchaguzi wa Irani viongozi walikuwa wanatumia twitter na facebook kutoa statement.
hamna ubaya wowote kwa mwandishi wa habari kum quote zitto, slaa, mnyika, mbowe, mo na wengine ambao wanatumia majina yao.
kama mtu ataki kuwa quoted then ujue huo mchango unawalakini

hata kama mtu ni security officer mchango wake utaeshimika kutokana na hoja yake lakini sio shughuli yake anayoifanya.
hayo mambo ya kulindana tena, tunarudi nyuma badal ya kwenda mbele

Issue kubwa siyo kumlinda mtu asiwe quoted bali ninachotaka ni kuwa post za wachangiaji zisiwe damagingly distorted kwenye magazeti yetu.
 
- Hivi Mwalimu how sure are you kwamba anayeshuika hakuombwa, pamoja na kwamba sio hoja ya smingi sana, kwani hapo juu huyo Reid wamemuomba? Kwani Tiger woods aliposema maneno yake na wale wanawake alikwua kwenye pres. conference mkuu, ndio maana ninasema habari yako haijakaa sawa hata kidogo na sina mpango wa kulumbana na wewe maana unaheshimika sana hapa,

- Binafsi ninaheshimu sana michango yako hapa, kwenye hizi ishu za quotation za politician ukijali jina hutaweza kua muandishi wa habari hata siku moja!

Respect.

FMEs!

Kwa mtazamo wangu,nadhani ni vyema watu tukawa careful in every sigle word we write here. Mantiki kwamba michango ichungwe au isiende magazetini haina tija. Kama mtu unaweza kuchangia JF au Forum yeyote basi ni dhahisi ungekuwa tayari kusema the same hata ungekutana na friends in the same non-official discussion pale manzese. Kwa sababu hiyo basi, tunachokisema ni kile tunachofikiria na kinabaki fact, ila tukumbuke "meaning of words are not in words but in people who uses the words". Mwandishi wa Tanzania daima yupo sawa.

Zitto ndugu yangu, kuliko kuhisi kila mtu anakufikiria vibaya, basi wewe SIMAMA NA USEME ULICHOMAANISHA SICHO and that is over kuliko kuendelea kuumia bure.

"Politics is a dirty game....play it careful"
 
Mwanasiasa anayo haki ya kutoa maoni yake juu ya jambo lolote na kutokana na utashi wake na kwa kufuata sheria zilizopo.


Hapa tatizo naweza sema lipo huku kwenye taaluma yenyewe ya uandishi wa habari, hasa kwa sababu kiwango cha waandishi wetu wanaopenda kucopy na kupaste habari kinaongezeka kwa kasi sana na kwa njia hii nchi kama nchi haiwezi kuendelea.

Tunahitaji kuwa na waandishi makini, sitegemei mwandishi wa habari anayeiheshimu na kuijua kazi yake akachukua mawazo ya mtu kutoka kwenye mitandao nakuyafanya kuwa ni habari sahii ya kuiandika na hasa bila kumuhoji muhusika/mchangiaji labda kama hilo ni gazeti la udaku.
Na kama ni gazeti la udaku basi sisi wasomaji tutaipokea habari hiyo kiudaku udaki hivyo tatizo naweza sema linaweza kutokuwepo.

Kwa kusema hayo, sioni haja ya kulinda maoni yatolewayo na wanasiasa wajulikano, tuwaweke huru waongee na wanahabari watusaidie kuheshimu sheria zilizopo na kufuata maadili ya kazi yao.

Nawakilisha


 
Kwa mtazamo wangu,nadhani ni vyema watu tukawa careful in every sigle word we write here. Mantiki kwamba michango ichungwe au isiende magazetini haina tija. Kama mtu unaweza kuchangia JF au Forum yeyote basi ni dhahisi ungekuwa tayari kusema the same hata ungekutana na friends in the same non-official discussion pale manzese. Kwa sababu hiyo basi, tunachokisema ni kile tunachofikiria na kinabaki fact, ila tukumbuke "meaning of words are not in words but in people who uses the words". Mwandishi wa Tanzania daima yupo sawa.

Zitto ndugu yangu, kuliko kuhisi kila mtu anakufikiria vibaya, basi wewe SIMAMA NA USEME ULICHOMAANISHA SICHO and that is over kuliko kuendelea kuumia bure.

"Politics is a dirty game....play it careful"

Nimeanza kuona ugumu wetu katika matumizi ya maneno. Wakati ni kweli kuwa kila mtu analoongea kwenye mtandao lazima litoke moyoni mwake na awe tayari kulisimamia, ndugu yangu unalokosea ni kuchukulia kuwa tunatetea maneno yaliyosemwa na Zito, hapana, tunachoongelea ni ule upindishaji wa yale yaliyosema na ZIto, na kuyachukulia nje kabisa ya mada. Nimekopi hapo ujuu posts zote zilizoandikwa na Zito kwenye forum ile: zilikuwa mbili tu. Hakuna hata moja iinayoonyesha kuwa Zito alisema JK aongezewe muda.

Inapotokea gazeti likaandika kuwa eti Zito alipokuwa kule JF alisema kuwa JK aongezewe muda, ni distrotion ambayo siyo tu inachafua jina la Zito bali pia credibility ya JF yenyewe. Maoni yangu ni kutaka posts za hapa JF zisiwe distorted kwenye media; wakiamua kuzitumia basi wazitumie kama zilivyotolewa na mchangiaji bila kuziwekea chumvi au pilipili yoyote. Sababu ya kuwataka wawasiliane na mchangiaji ni huko kutaka kuhakikisha kuwa wanajua fika kuwa wanalioandika linaendana na nia ya mchangiaji huyo siyo nia yao wenyewe. Ni posts chache sana kwenye forum ambazo ni standalone kwa nyingi hutolewa vikiwa ni vpande vipande vinavyoendana na mtililiko wa mjadala wenyewe, hivyo wakichukua vipande vichache tu inabidi wao ndio wawe waangalifuy siyo mchangiaji.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom