yeddy guyy
JF-Expert Member
- Mar 31, 2015
- 627
- 489
Mambo yanaenda kasi sana hebu ona haya
1. Juma Haji Duni mwaka 2016 alitumia miezi 3 kuhamia Chadema na kurudi CUF. Huku kunaitwa kutokujitambua unataka nini hasa.
2. Lowassa kajiandaa kwa miaka 20 kuingia ikulu na kakosa Magufuli kwa miezi mitatu tu kaingia Ikulu. Huku kunaitwa ni kupoteza muda
3. Mrema anataka Ukawa mpya kati ya CCM na TLP CCM wakakataa rais akamteua kuwa mwenyekiti wa Parole, huku ni kunaitwa kukanyaga ganda la Ndizi.
4. Chadema mwanzoni ilidai Magufuli anatumia sera za Ccm lakini leo sera zile zile zimewabadilikia na wanadai ni udikteta. Huku kunaitwa kusahau kulikopitiliza.
5. Sumaye toka nia ya kugombea uraisi hadi kugombea uenyekiti wa chadema mkoa wa Pwani. Hii ni sawa na mtu aliyeenda kuwinda Tembo akarudi na panya.
6. Mbatia toka kuwa mwenyekiti wa chama hadi kuwa msemaji wa Chadema. Hii ni sawa na mtoto aliyeenda kumsalimia bibi yake akakuta anapika wali akagoma kurudi akalala huko huko.
7. Maalim Seif Toka kumshtaki Shein ICC na kushindwa kufungua mashtaka hayo hadi kukataa kumpa mkono kama adhabu ...... hii ni sawa na kupigwa kelbu na kwa kuwa huna la kumfanya ukaamua kugoma kula.
8.Haina miaka Mingi toka Chadema wawatuhumu cuf kuwa wanaunga mkono ndoa za jinsia Moja (waliberal) nakumbuka walitaka kupigana bungeni hawa leo wameungana. Huku kunaitwa
9. Maalim Seifu toka kuhutubia Maelfu pale Kibanda Maiti huku akiwa na walinzi, ofisi na wapambe hadi kuonekana akitembea na miguu na fimbo mkononi ....... huku kunaitwa kuzurura.
10. Mbowe toka kutangaza operation Ukuta hadi kubomolewa kwa Ukuta wa Bilcanas na operation ikaishia hapo hapo kwa visingizio lukuki..... huku kunaitwa mama mkanye mwanao.
11. Lowasa katoka kuwa Waziri mkuu hadi kuwa raisi wa Facebook. Huku kunaitwa bora liende.
12. Lowassa kazunguka nchi nzima akiwa dhohofu wa Afya kunadi wagombea wa Cuf huku lipumba akimpinga baada ya cuf kuongeza wabunge kutokana na juhudi za lowassa lipumba karudi kuja kula Ruzuku...... huku kunaitwa Timing
13. Watu 14 wa CUF kuwapiga watu 400 kwenye mkutano nalo linapaswa kuingizwa kwenye kitabu cha maajabu ya Dunia..... huku kunaitwa wingi si hoja, hoja ni Weledi.
14.Maalim Seifu kuikimbia ofisi yake buguruni huku akifanyia shughuli zake vichochoroni. Huku kunaitwa woga uliopitiliza.
Mungu ibariki Tanzania Ccm oyeee
1. Juma Haji Duni mwaka 2016 alitumia miezi 3 kuhamia Chadema na kurudi CUF. Huku kunaitwa kutokujitambua unataka nini hasa.
2. Lowassa kajiandaa kwa miaka 20 kuingia ikulu na kakosa Magufuli kwa miezi mitatu tu kaingia Ikulu. Huku kunaitwa ni kupoteza muda
3. Mrema anataka Ukawa mpya kati ya CCM na TLP CCM wakakataa rais akamteua kuwa mwenyekiti wa Parole, huku ni kunaitwa kukanyaga ganda la Ndizi.
4. Chadema mwanzoni ilidai Magufuli anatumia sera za Ccm lakini leo sera zile zile zimewabadilikia na wanadai ni udikteta. Huku kunaitwa kusahau kulikopitiliza.
5. Sumaye toka nia ya kugombea uraisi hadi kugombea uenyekiti wa chadema mkoa wa Pwani. Hii ni sawa na mtu aliyeenda kuwinda Tembo akarudi na panya.
6. Mbatia toka kuwa mwenyekiti wa chama hadi kuwa msemaji wa Chadema. Hii ni sawa na mtoto aliyeenda kumsalimia bibi yake akakuta anapika wali akagoma kurudi akalala huko huko.
7. Maalim Seif Toka kumshtaki Shein ICC na kushindwa kufungua mashtaka hayo hadi kukataa kumpa mkono kama adhabu ...... hii ni sawa na kupigwa kelbu na kwa kuwa huna la kumfanya ukaamua kugoma kula.
8.Haina miaka Mingi toka Chadema wawatuhumu cuf kuwa wanaunga mkono ndoa za jinsia Moja (waliberal) nakumbuka walitaka kupigana bungeni hawa leo wameungana. Huku kunaitwa
9. Maalim Seifu toka kuhutubia Maelfu pale Kibanda Maiti huku akiwa na walinzi, ofisi na wapambe hadi kuonekana akitembea na miguu na fimbo mkononi ....... huku kunaitwa kuzurura.
10. Mbowe toka kutangaza operation Ukuta hadi kubomolewa kwa Ukuta wa Bilcanas na operation ikaishia hapo hapo kwa visingizio lukuki..... huku kunaitwa mama mkanye mwanao.
11. Lowasa katoka kuwa Waziri mkuu hadi kuwa raisi wa Facebook. Huku kunaitwa bora liende.
12. Lowassa kazunguka nchi nzima akiwa dhohofu wa Afya kunadi wagombea wa Cuf huku lipumba akimpinga baada ya cuf kuongeza wabunge kutokana na juhudi za lowassa lipumba karudi kuja kula Ruzuku...... huku kunaitwa Timing
13. Watu 14 wa CUF kuwapiga watu 400 kwenye mkutano nalo linapaswa kuingizwa kwenye kitabu cha maajabu ya Dunia..... huku kunaitwa wingi si hoja, hoja ni Weledi.
14.Maalim Seifu kuikimbia ofisi yake buguruni huku akifanyia shughuli zake vichochoroni. Huku kunaitwa woga uliopitiliza.
Mungu ibariki Tanzania Ccm oyeee