Maoni yangu kuhusu Serikali kukataza watu kutoka kwenye nyumba zao kupambana na Covid-19

Kikelelwa

Senior Member
Dec 14, 2010
176
124
Ukweli ni kwamba kuna watu lazima tutoke ndio tupate angalau kidogo cha kulisha familia. Ikatokea serikali imechukua hatua kama za Rwanda, Kenya na nchi nyingine zilizoamua kuchukua hatua ya Lockdown basi ni kiama kwa baadhi yetu.

Majuzi nilikuwa naongea na Dereva daladala mmoja anasema sasa hivi wanapeleka hesabu elfu arobaini halafu wanaishia kugawana elfu tano tano au kumi kumi yeye na konda wake. Hii ni kwasababu tu baadhi ya watu wameamua kuchukua tahadhari wenyewe ya kukaa ndani.

Wenye magari nao wanaona bora kupaki tu.

Ni ukweli usiopingika tunahitaji tahadhari ya hali ya juu sana kwasababu mwisho wa siku tutaishia kufa kama kuku wa kideri

Ila mimi naungana na Mwenzangu Donald Trump lockdown itakuwa na madhara makubwa kuliko ugonjwa wenyewe.

Kama account yako imeshiba na una uwezo wa kulisha familia mpaka huu ugonjwa utakopisha naomba usitukejeli sisi maskini wewe Jipe karantini acha wengine tupambane na hali zetu
 
Usisahau mwenye daladala naye ana mikopo benki na marejesho ya TRA. Bila gari kufanyakazi hiyo hela itatoka wapi? Marekani serikali imetoa ruzuku, kwetu haiwezekani kabisa.

Aidha kwetu tunakula kwa kukopa hivyo tunayopata leo ni kulipa deni la Jana. Achana na watu kama Zitto ati serikali itoe ruzuku!!!!
 
Tangu siku ya kwanza..Siwazi kufa kwa korona nawaza njaa! Kama unavyosema mkuu usipotoka huli watu tunajaa umo kwenye magari tunaendelea na shuguli zetu kama kawaida sio kwamba jeuri ni vile hatuna jinsi... begger cant be choosers!!!
 
Hii mipango ingeanza tangu January wakati China wanapambana tungeanza kuweka unga, mchele, sukari, maharage na vyakula vya makopo ndani. Kusema ukweli self isolation inasaidis sana kuzuia maambuzi mapya.

Wanaotoka wavae baokora kujikinga na kulinda wengine. Ingawa huku kwetu Kwamtogole tunaishi watu 50 nyumba moja. Hii self isolation si self isolation inabidi nivae baokora ninienda chooni au kuchota maji.
 
Hii mipango ingeanza tangu January wakati China wanapambana tungeanza kuweka unga, mchele, sukari, maharage na vyakula vya makopo ndani. Kusema ukweli self isolation inasaidis sana kuzuia maambuzi mapya.

Wanaotoka wavae baokora kujikinga na kulinda wengine. Ingawa huku kwetu Kwamtogole tunaishi watu 50 nyumba moja. Hii self isolation si self isolation inabidi novae baokora ninienda chooni au kuchota maji.

kipato mama
 
Hii mipango ingeanza tangu January wakati China wanapambana tungeanza kuweka unga, mchele, sukari, maharage na vyakula vya makopo ndani. Kusema ukweli self isolation inasaidis sana kuzuia maambuzi mapya.

Wanaotoka wavae baokora kujikinga na kulinda wengine. Ingawa huku kwetu Kwamtogole tunaishi watu 50 nyumba moja. Hii self isolation si self isolation inabidi nivae baokora ninienda chooni au kuchota maji.
baokora=barakoa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom