Maoni yangu kuhusu hali ya uchumi kwa sasa

Mwanahabari Huru

JF-Expert Member
Mar 9, 2015
14,243
34,898
Leo gazeti la Mtanzania limeripoti kufungwa kwa Hotel kadhaa za kifahari kutokana na sababu mbalimbali, lakini SABABU KUU iliyotajwa ni hatua ya serikali kuzuia mikutano yake kufanyika hotelini, badala yake ifanyike kwenye kumbi za serikali na kudaiwa kodi (Mtanzania, Julai 14, 2016, uk.3 na 4).

Nilitamani kufanya uchambuzi wa kina kuhusiana na hali hii lakini nizungumze kwa kifupi kwa sababu niko 'field' huku kwa wanyantuzu natafuta karo ya shule ya mwanangu.

Nionavyo uamuzi huu wa serikali una faida na hasara zake.

#FAIDA_KWA_KIFUPI;

#Mosi; Mzunguko wa fedha utapungua na hivyo kusaidia sana kucontrol inflation rate (mfumko wa bei). Sifa mojawapo ya fedha ni isiwe holela. Pesa inatakiwa ipotee kidogo, iwe adimu lakini si adimu sana (money should be scarce but not very scarce).

Kwahiyo pesa ikipotea kdg hata bei ya bidhaa na huduma itashuka. Maana yake ni kwamba bidhaa zitakuwepo lakini pesa hamna kwa hiyo itabidi zishuke bei. Hii itawaumiza wafanyabiashara lakini itawasaidia sana walaji.

Na hii ni mbinu nzuri sana ya kudhibiti uchumi. Bidhaa na huduma vitapungua bei sana. Kwa mfano Hotel ambayo ulikua ukilala kwa 400,000/= kwa usiku mmoja, muda si mrefu utaanza kulala kwa 100,000/= na zile za 100,000/= zitashuka hadi 40,000/=. Mfuko wa Cement kama unanunua 15,000/= tegemea kununua 8,000/= muda si mrefu. Hii ni habari njema kwa walaji (Consumers) lakini habari mbaya kwa wazalishaji (Producers) na wafanyabiashara.

#Pili; Njia hii itasaidia sana kuleta "nidhamu ya kazi". Kwa kuwa mzunguko wa pesa utakuwa mdogo itawalazimu watu kufanya kazi kwa bidii ili kupata pesa. Enzi za kupata pesa kiulaini zimekufa. Enzi za kumuandikia Mkuu wa Idara "minutes" na kujifanya mlikua na kikao, halafu mkuu wa Idara anasaini mjilipe posho, enzi hizo zimekwisha rasmi. Sasa ni kazi tu.

Kama unataka pesa fanya kazi, kama hutaki utakula jeuri yako. Kwahiyo kuanzia sasa watu watafanya kazi kwa bidii na uchumi wa nchi utakua kwa kasi. Utashangaa kuuziwa mfuko wa Cement 7,000/= lakini utashangaa zaidi kwamba unafanya kazi siku mbili hiyo 7,000/= huipati. Kutakuwa hakuna namna nyingine zaidi ya kuongeza bidii.!

#Tatu; Njia hii itasaidia sana kuimarisha sarafu yetu. Moja ya mambo yaliyokua yakichangia kuporomoka kwa sarafu yetu ni inflation rate kuwa kubwa sana. Sasa kwa utaratibu huu wa JPM inflation itakuwa controled kwa hiyo pesa itapotea mitaani.

Na pesa ikipotea maana yake itatafutwa. Na ikitafutwa means demand yake inaongezeka. Na demand ikiongezeka means thamani yake pia inaongezeka. Kwahiyo usishangae hadi kufika mwaka 2020 Dola 1 ya kimarekani ikauzwa Shilingi 1,000/= au chini ya hapo.

Pia kwa kuwa mzunguko wa pesa utakuwa mdogo watu hawatafanya tena shopping nje ya nchi, kwa hiyo watanunua zaidi bidhaa za ndani na hivyo kusaidia kuimarisha sarafu yetu.

#Nne; Njia hii itasaidia kuleta nidhamu ya matumizi. Yani mtu akipata hela ataitunza vizuri na kufanya saving maana hajui kama kesho atapata tena. Unajua watu hawakuwa na nidhamu kabisa ya matumizi. Ulikua unakuta mtu anaenda bar weekend moja anatumia Milioni moja inaisha.

Wiki inayofuata anaenda tena na milioni bar inateketea. Ananunulia watu pombe, anahonga kila mwanamke anayemrembulia, akienda "Live band" kila jina lake likitajwa anatoa laki moja. Lakini kuanzia sasa nidhamu itakuwepo. Hakuna mtu atakayekua na ujasiri wa kufanya mbwembwe za kijinga tena kama hizo. Nidhamu ya matumizi itaongezeka sana.

#Tano; itasaidia kupunguza ombwe (gap) kati ya wenye nacho na wasiokua nacho. Ngoja nikupe mifano michache. Kuna watumishi ambao mishahara yao haizidi milioni moja lakini walikua na uhakika wa kuingiza milioni 5 hadi 6 kila mwisho wa mwezi kwa "deals" mbalimbali. Mara vikao, mara safari, mara manunuzi (procurement wanakula 10%) etc.

Kwahiyo unakuta mtu ana kipato cha milioni 7 au 8 kwa mwezi, anajiona juu kuliko wewe ambaye kipato chako ni laki 8. Anafanya shoping Nakumat wewe shoping yako Mwenge. Lakini kuanzia sasa ngoma droo. Wote mnaenda kuhemea sokoni Buguruni malapa.

#Sita; Maskini wataanza kumiliki ardhi na bei ya ardhi na viwanja itaanza kuwa "affordable" katika maeneo mengi. Unajua ardhi ilikua inapandishwa na "wapiga dili". Mtu amepata hela zake bila jasho anaenda kununua ardhi kwa mamilioni na kusababisha ardhi ya eneo hilo kupanda thamani. Kama mnakumbuka ile skendo ya boss mmoja wa shirika moja la hifadhi ya jamii aliyenunua ardhi Arusha kwa milioni 5 halafu akaiuza kwa shirika analoliongoza kwa shilingi bilioni 1.

Sasa imagine ardhi imepanda thamani kutoka Milioni 5 hadi nilioni 1 ndani ya mwaka mmoja. Kwahiyo wenye ardhi jirani na hapo wakiona mwenzao kauza Bilioni 1 nao wanapandisha bei. Lakini kuanzia sasa "discipline" itakuwepo. Mfumuko wa bei katika ardhi hautakuwepo tena kwahiyo hata maskini watakuwa na uwezo wa kununua na kumiliki ardhi.

#HASARA_KWA_KIFUPI

#Mosi; watu wengi sana watapoteza ajira kutokana na sekta nyingi za uzalishaji kufungwa. Jiulize mahoteli yote yaliyofungwa wafanyakazi wanaenda wapi? Na sio kwenye mahoteli tu, viwanda vitafungwa, makampuni na mashirika yatapunguza wafanyakazi. Wote hao wataenda kulundikana mtaani na kugeuka kuwa tegemezi.

#Pili; Taasisi nyingi za fedha zitafilisika. Mabenki yaliyozoea kukopesha wafanyabiashara kwa riba kubwa sasa hivi yatakosa wateja, na hivyo "ku-run bankrupt". Kwahiyo tutegemee mabenki mengi kufa, na machache yatakayo-survive yatapunguza wafanyakazi pamoja na kufunga baadhi ya "branches" zake.

#Tatu; Sekta nyingi za uzalishaj na fursa za ujasiriamali zitadumaa. Hii ni kwa sababu hazitakuwa na mitaji na pia wananchi hawatakuwa na purschasing power ya kuweza kumudu gharama ya baadhi ya bidhaa.

Kwamfano mtu alikua anaweza kwenda bank akakopa milioni 500 akaanzisha duka la kuuza vitu vya ndani kama furniture, mafriji, TV set, na akapata wateja wengi ndani ya mwaka mmoja akarudisha mkopo wa benki akaanza kula faida.

Lakimi kuanzia sasa hivi wajasiriamali wengi hawatathubutu kukopa. Na wakikopa hawatakuwa nacuwezo wa kulipa. Kwa hiyo mfanyabiashara akinunua bidhaa za milioni 500 akaziweka dukani, halafu baada ya mwezi mauzo ni laki 6, lazima atafute sumu ya panya atangulie akhera madukani.!

#Nne; Kuyumba kwa bei katika soko la hisa kwa sababu baadhi ya wanahisa katika makampuni mengi wanaweza kuuza hisa zao kufidia mikopo yao benki. Na kwakuwa fedha itakuwa adimu (scarce) watalazimika kuuza hata kwa bei ya hasara hali itakayosababisha soko la hisa kuyumba.

#Tano; kuongezeka kwa vitendo vya kihalifu. Kwa kuwa watu wengi watapoteza kazi, wengine biashara zao, wengine watapoteza dili zao za kuwaingizia kipato, watalazimika kutafuta njia nyingine ya kuishi. Na njia Rahisi ni kujiingiza katika vitendo vya kihalifu. Ujambazi, Ukahaba, Utapeli, Wizi etc.

Kwahiyo tutegemee kusikia matukio mengi ya ujambazi na unyang'anyi wa kutumia silaha katoka maeneo kama benki, super markets, Bureau de change, na hata majumbani. Hakuna mtu atakayekua tayari kukuona unatoa milioni 1 ATM akakuacha hivihivi wakati yeye ana siku ya pili hajala.

#HITIMISHO:
Sisemi Rais aendelee kubana matumizi au aache. Nachotaka kusema ni kuwa apiime kati ya faida na hasara kisha afanye maamuzi kwa maslahi ya nchi. Zipo faida na hasara nyingi zaidi ya hizi. Hapa nimeeleza kwa kifupi tu, lakini najua Rais anao washauri wazuri wa masuala ya kiuchumi watamsaidia kumshauri vizuri kwa maslahi ya "Mama Tanzania"

Malisa G.J
 
Hiyo faida namba moja nina wasi wasi nayo.

Kama uzalishaji wa vitu utabaki vile vile au tutaendelea kuagiza toka nje hiyo tusitegemee mfumuko wa bei utashuka.

Vitu haviwezi kushuka bei kisa pesa zimekuwa hazipatikani kiholela, vitashuka tu kama gharama za uzalishaji zimepungua. Mwisho wa siku uzalishaji utapungua tu kwa kuwa watu hawana pesa za kununua hizo bidhaa.

Namba tatu.. Italeta nidhamu ya matumizi ya pesa ila sio nidhamu ya kazi.
 
Eti uchumi, kwa ubongo upi? Uchumi unafikiri uzushi uliouzoea?

The actual employment impact of removing factor price distortions will depend on the degree to which labor can be substituted for capital in the production processes of various developing-world industries. Economists refer to this as the elasticity of factor substitution and define it roughly as the ratio of the percentage change in the proportion of labor used relative to capital (labor-capital or L/K ratio) compared to a given percentage change in the price of capital relative to labor (PK/PL). Algebraically, the elasticity of substitution, ηLK can be defined as follows:

h
LK =d(L>K)>(L>K) d(PK>PL)>(PK>PL)


For example, if the relative price of capital rises by 1% in the manufacturing sector and the labor-capital ratio rises as a result by, say, 1.5%, the elasticity of substitution in the manufacturing industry will be equal to 1.5. If PK/PL falls by, say, 10% while L/K falls by only 6%, the elasticity of substitution for that industry would be 0.6. Relatively high elasticities of substitution (ratios greater than about 0.7) are indicative that factor price adjustments can have a substantial impact on levels and combinations of factor utilization. In such cases, factor price modifications may be an important means of generating more employment opportunities. In general, most empirical studies of the elasticity of substitution for manufacturing industries in less developed countries reveal coefficients in the range 0.5 to 1.0. These results indicate that a relative reduction in wages (either directly or by holding wages constant while letting the price of capital rise) of, say, 10% will lead to a 5% to 10% increase in employment.
h
LK =
d(L>K)>(L>K) d(PK>PL)>(PK>PL)
 
Hivi suala la Rais kupiga marufuku kufanya mikutano katika hotel lina tatizo lipi? Je, serikali iliingia mkataba na wenye mahotel kuwa jenga mahotel yenu ili semina ziwe zinaenda hotelini? Je, kumbi za serikali zimejengwa kwa sababu zipi? Je, ni sahihi kwa mafunzo kufanyika mahotelini? Let us call a spade a spade!

Mnalalamika serikali kuondoa fedha zake kutoka Mabenki, Je ukiwa na fedha zako unalazimishwa kuziweka katika benki yoyote? Je, na hao wenye mabenki wana mkataba na serikali kuwa fedha zake zitakaa katika hayo mabenki? Nini maana ya Benki kuu? Acha serikali ifanye mambo yake bila kuingiliwa na akina sisi ambao ni wajuzi wa kila jambo.
 
Kozi nyingi za hotel.management kureview silabi zao na kiwafanya mahotelier kuwa wabunifu...tofauti na sasa kivaa vimini kisubiri workshop za serekali...

Tuombe mungu watoka jasho tunaweza pata ahueni...Mungu ibariki tanzania
 
Kwaiyo ili suala la muda au milele? Coz hadi theory ifanye kazi sawa sawa tutafutana,kwasababu ndio kwanza miezi minane ya mheshimiwa
 
Leo gazeti la Mtanzania limeripoti kufungwa kwa Hotel kadhaa za kifahari kutokana na sababu mbalimbali, lakini SABABU KUU iliyotajwa ni hatua ya serikali kuzuia mikutano yake kufanyika hotelini, badala yake ifanyike kwenye kumbi za serikali na kudaiwa kodi (Mtanzania, Julai 14, 2016, uk.3 na 4).

Nilitamani kufanya uchambuzi wa kina kuhusiana na hali hii lakini nizungumze kwa kifupi kwa sababu niko 'field' huku kwa wanyantuzu natafuta karo ya shule ya mwanangu.

Nionavyo uamuzi huu wa serikali una faida na hasara zake.

#FAIDA_KWA_KIFUPI;

#Mosi; Mzunguko wa fedha utapungua na hivyo kusaidia sana kucontrol inflation rate (mfumko wa bei). Sifa mojawapo ya fedha ni isiwe holela. Pesa inatakiwa ipotee kidogo, iwe adimu lakini si adimu sana (money should be scarce but not very scarce).

Kwahiyo pesa ikipotea kdg hata bei ya bidhaa na huduma itashuka. Maana yake ni kwamba bidhaa zitakuwepo lakini pesa hamna kwa hiyo itabidi zishuke bei. Hii itawaumiza wafanyabiashara lakini itawasaidia sana walaji.

Na hii ni mbinu nzuri sana ya kudhibiti uchumi. Bidhaa na huduma vitapungua bei sana. Kwa mfano Hotel ambayo ulikua ukilala kwa 400,000/= kwa usiku mmoja, muda si mrefu utaanza kulala kwa 100,000/= na zile za 100,000/= zitashuka hadi 40,000/=. Mfuko wa Cement kama unanunua 15,000/= tegemea kununua 8,000/= muda si mrefu. Hii ni habari njema kwa walaji (Consumers) lakini habari mbaya kwa wazalishaji (Producers) na wafanyabiashara.

#Pili; Njia hii itasaidia sana kuleta "nidhamu ya kazi". Kwa kuwa mzunguko wa pesa utakuwa mdogo itawalazimu watu kufanya kazi kwa bidii ili kupata pesa. Enzi za kupata pesa kiulaini zimekufa. Enzi za kumuandikia Mkuu wa Idara "minutes" na kujifanya mlikua na kikao, halafu mkuu wa Idara anasaini mjilipe posho, enzi hizo zimekwisha rasmi. Sasa ni kazi tu.

Kama unataka pesa fanya kazi, kama hutaki utakula jeuri yako. Kwahiyo kuanzia sasa watu watafanya kazi kwa bidii na uchumi wa nchi utakua kwa kasi. Utashangaa kuuziwa mfuko wa Cement 7,000/= lakini utashangaa zaidi kwamba unafanya kazi siku mbili hiyo 7,000/= huipati. Kutakuwa hakuna namna nyingine zaidi ya kuongeza bidii.!

#Tatu; Njia hii itasaidia sana kuimarisha sarafu yetu. Moja ya mambo yaliyokua yakichangia kuporomoka kwa sarafu yetu ni inflation rate kuwa kubwa sana. Sasa kwa utaratibu huu wa JPM inflation itakuwa controled kwa hiyo pesa itapotea mitaani.

Na pesa ikipotea maana yake itatafutwa. Na ikitafutwa means demand yake inaongezeka. Na demand ikiongezeka means thamani yake pia inaongezeka. Kwahiyo usishangae hadi kufika mwaka 2020 Dola 1 ya kimarekani ikauzwa Shilingi 1,000/= au chini ya hapo.

Pia kwa kuwa mzunguko wa pesa utakuwa mdogo watu hawatafanya tena shopping nje ya nchi, kwa hiyo watanunua zaidi bidhaa za ndani na hivyo kusaidia kuimarisha sarafu yetu.

#Nne; Njia hii itasaidia kuleta nidhamu ya matumizi. Yani mtu akipata hela ataitunza vizuri na kufanya saving maana hajui kama kesho atapata tena. Unajua watu hawakuwa na nidhamu kabisa ya matumizi. Ulikua unakuta mtu anaenda bar weekend moja anatumia Milioni moja inaisha.

Wiki inayofuata anaenda tena na milioni bar inateketea. Ananunulia watu pombe, anahonga kila mwanamke anayemrembulia, akienda "Live band" kila jina lake likitajwa anatoa laki moja. Lakini kuanzia sasa nidhamu itakuwepo. Hakuna mtu atakayekua na ujasiri wa kufanya mbwembwe za kijinga tena kama hizo. Nidhamu ya matumizi itaongezeka sana.

#Tano; itasaidia kupunguza ombwe (gap) kati ya wenye nacho na wasiokua nacho. Ngoja nikupe mifano michache. Kuna watumishi ambao mishahara yao haizidi milioni moja lakini walikua na uhakika wa kuingiza milioni 5 hadi 6 kila mwisho wa mwezi kwa "deals" mbalimbali. Mara vikao, mara safari, mara manunuzi (procurement wanakula 10%) etc.

Kwahiyo unakuta mtu ana kipato cha milioni 7 au 8 kwa mwezi, anajiona juu kuliko wewe ambaye kipato chako ni laki 8. Anafanya shoping Nakumat wewe shoping yako Mwenge. Lakini kuanzia sasa ngoma droo. Wote mnaenda kuhemea sokoni Buguruni malapa.

#Sita; Maskini wataanza kumiliki ardhi na bei ya ardhi na viwanja itaanza kuwa "affordable" katika maeneo mengi. Unajua ardhi ilikua inapandishwa na "wapiga dili". Mtu amepata hela zake bila jasho anaenda kununua ardhi kwa mamilioni na kusababisha ardhi ya eneo hilo kupanda thamani. Kama mnakumbuka ile skendo ya boss mmoja wa shirika moja la hifadhi ya jamii aliyenunua ardhi Arusha kwa milioni 5 halafu akaiuza kwa shirika analoliongoza kwa shilingi bilioni 1.

Sasa imagine ardhi imepanda thamani kutoka Milioni 5 hadi nilioni 1 ndani ya mwaka mmoja. Kwahiyo wenye ardhi jirani na hapo wakiona mwenzao kauza Bilioni 1 nao wanapandisha bei. Lakini kuanzia sasa "discipline" itakuwepo. Mfumuko wa bei katika ardhi hautakuwepo tena kwahiyo hata maskini watakuwa na uwezo wa kununua na kumiliki ardhi.

#HASARA_KWA_KIFUPI

#Mosi; watu wengi sana watapoteza ajira kutokana na sekta nyingi za uzalishaji kufungwa. Jiulize mahoteli yote yaliyofungwa wafanyakazi wanaenda wapi? Na sio kwenye mahoteli tu, viwanda vitafungwa, makampuni na mashirika yatapunguza wafanyakazi. Wote hao wataenda kulundikana mtaani na kugeuka kuwa tegemezi.

#Pili; Taasisi nyingi za fedha zitafilisika. Mabenki yaliyozoea kukopesha wafanyabiashara kwa riba kubwa sasa hivi yatakosa wateja, na hivyo "ku-run bankrupt". Kwahiyo tutegemee mabenki mengi kufa, na machache yatakayo-survive yatapunguza wafanyakazi pamoja na kufunga baadhi ya "branches" zake.

#Tatu; Sekta nyingi za uzalishaj na fursa za ujasiriamali zitadumaa. Hii ni kwa sababu hazitakuwa na mitaji na pia wananchi hawatakuwa na purschasing power ya kuweza kumudu gharama ya baadhi ya bidhaa.

Kwamfano mtu alikua anaweza kwenda bank akakopa milioni 500 akaanzisha duka la kuuza vitu vya ndani kama furniture, mafriji, TV set, na akapata wateja wengi ndani ya mwaka mmoja akarudisha mkopo wa benki akaanza kula faida.

Lakimi kuanzia sasa hivi wajasiriamali wengi hawatathubutu kukopa. Na wakikopa hawatakuwa nacuwezo wa kulipa. Kwa hiyo mfanyabiashara akinunua bidhaa za milioni 500 akaziweka dukani, halafu baada ya mwezi mauzo ni laki 6, lazima atafute sumu ya panya atangulie akhera madukani.!

#Nne; Kuyumba kwa bei katika soko la hisa kwa sababu baadhi ya wanahisa katika makampuni mengi wanaweza kuuza hisa zao kufidia mikopo yao benki. Na kwakuwa fedha itakuwa adimu (scarce) watalazimika kuuza hata kwa bei ya hasara hali itakayosababisha soko la hisa kuyumba.

#Tano; kuongezeka kwa vitendo vya kihalifu. Kwa kuwa watu wengi watapoteza kazi, wengine biashara zao, wengine watapoteza dili zao za kuwaingizia kipato, watalazimika kutafuta njia nyingine ya kuishi. Na njia Rahisi ni kujiingiza katika vitendo vya kihalifu. Ujambazi, Ukahaba, Utapeli, Wizi etc.

Kwahiyo tutegemee kusikia matukio mengi ya ujambazi na unyang'anyi wa kutumia silaha katoka maeneo kama benki, super markets, Bureau de change, na hata majumbani. Hakuna mtu atakayekua tayari kukuona unatoa milioni 1 ATM akakuacha hivihivi wakati yeye ana siku ya pili hajala.

#HITIMISHO:
Sisemi Rais aendelee kubana matumizi au aache. Nachotaka kusema ni kuwa apiime kati ya faida na hasara kisha afanye maamuzi kwa maslahi ya nchi. Zipo faida na hasara nyingi zaidi ya hizi. Hapa nimeeleza kwa kifupi tu, lakini najua Rais anao washauri wazuri wa masuala ya kiuchumi watamsaidia kumshauri vizuri kwa maslahi ya "Mama Tanzania"

Malisa G.J
Upo viziri
 
Kwa hapo hasara ni hatari zaidi kuliko faida huku mtaani hata watu wamesimamisha ujenzi sasa
 
Back
Top Bottom