Maoni yangu kufukuzwa kwa vijana 854 wa JKT

Abdul Nondo

JF-Expert Member
Oct 28, 2016
515
2,874
Tar 8 Desemba 2020.Aliyekuwa Rais wa JMT hayati John Pombe Joseph Magufuli alipokutana na vijana wa JKT hao 2400 ambao walipewa kazi ya kujenga Ikulu Chamwino-Dodoma.Akawaahidi kupewa ajira akisema watakapo maliza ujenzi wa Ikulu wapewe ajira wawe wanajeshi wasipelekwe sehemu nyingine.

Jana tar.17 Aprili 2021 ,CDF Mabeyo alitoa taarifa kwa Rais kufuta mkataba wa vijana wa JKT 854 miongoni mwa waliokuwa wanajenga Ikulu.Sababu alizozitaja kugoma kufanya kazi na kuandamana kwenda Ikulu kumuona Rais,akisema kugoma au kuandamana Jeshi ni uhaini.

Nakubaliana kwamba Mafunzo makubwa na ya mwanzo Jeshini ni utii.Utii wa amri kutoka kwa mamlaka ya kijeshi.

Bila kutaka kujua kwamba vijana hawa waliandama kweli au laa ,walihoji nini au laa ,waligoma kweli au laa ; sababu Jeshini sio sehemu ya kuhoji au kujitetea ikiwa mkubwa amesema.Nilienda Jeshini Msange JKT OP kikwete nilipata kushuhudia haya hata kwa miezi michache niliyokuwepo ,tuliwahi zuiwa kurudi nyumbani kufanya maombi ya vyuo na mikopo elimu ya juu nilihoji kwanini tunazuiwa ikiwa deadline inakaribia nilijibiwa na Captain Bakari "Hiyo ni Amri hupaswi kuhoji Nondo".

Nakiri utii wa amri ya mamlaka ya juu ni muhimu sana Jeshini .Ila tunawajibu sote kwa pamoja,viongozi wa dini na hata viongozi wa nchi kuwaombea msamaha vijana wenzetu hawa.Kwa kuamini wana nafasi kubwa ya kujirekebisha na kufanya vyema kwa maslahi ya taifa letu.

Vijana hawa wapo tangu 2017 ni OP Mererani na OP Makao ,wamefanya kazi kubwa kwa taifa letu .Ndio waliojenga Jengo la Nec Dodoma,waliojenga Hospital ya Uhuru,Msikiti mkubwa Chamwino,Kanisa kubwa Chamwino,Ukuta wa Ikulu km.34 ,Ndio waliojenga Ikulu Dodoma.

Vijana hawa kwa muda mrefu wamejituma na kuvumilia mengi,ikiwa kuna kosa lolote la kimaadili walilofanya nakiri kusema haikuwa dhamira yao bali katika hali ya kuuliza ahadi yao ya kuajiriwa baada ya ujenzi wa Ikulu,muda mrefu maisha yao yalikuwa ya matumaini ya kesho yao katika kulitumikia taifa.

Mimi nina amini kwamba vijana hawa wakisamehewa na kupewa fursa tena,watajirekebisha na kufanya mengi zaidi kuliko kuvunja mkataba na kuwarejesha nyumbani.Kwa pamoja tusichoke kuwaombea msamaha wasamehewe ili wapate fursa ya kujifunza zaidi.

Abdul Nondo.
 
Haaa jama jeshin hatuend kwa maombi ujue.kama umekiri jesh ni amr bas itoshe kusema vijana wameasi kabla hawajafika jeshini na wamepewa hiyo adhabu kwasabu siyo wanajeshi. Wangekua wanajesh hata wasingerudishwa nyumban tungezungunza mengine kabisa hapa
 
Wafunguliwe Kampuni ya Ujenzi.
Iongozwe na wawe wenyewe kwa kushirikiana na TBA.
Ni vizuri walivyorudishwa mtaani ili waone wenyewe hali ulivyo na jinsi gani walivyopoteza uaminifu na uzalendo wao kwa kukaidi amri na maelekezo waliyoyaapa kuyalinda.
 
Nondo kuna mambo ya kuhoji

Ila unapohoji hiki kitu tunashindwa kuchangia kwani hawa vijana hawakusoma terms na condition za hiyo taasisi kabla hawajaingia huko??

Sasa unapewa nafasi ya kusaini mkataba shule yako itakusaidia nini kama huwezi kusoma na kuelewa??

Tujisahihishe
 
Kilichotokea kwa vijana wa JKT "walioasi" ni utabiri wa yajayo....mfumo wa watu wote kufaidi keki ya taifa umepiduliwa sasa tunarudi kule kwa zamani...kupata nafasi kama hizo lazima uwe unatoka kanda flani, kwa Mzee meja mstaafu, wa Chama flani kikongwe, au umepokelewa ukiwa na kimemo!
Kama kawaida yetu naona issue imebandikwa siasa!
 
Umeandika vizuri bwana nondo ila utii jeshini ni jambo la kwanza. Kwa sababu walikuwa wapo kwenye mafunzo ya awali washukuru tu wamefukuzwa.

Hakuna kitu kinaitwa maandamano jeshini kaka ni kutii tu. Mwanajeshi mtarajiwa unakuwa mwanaharakati wa kuandamana? Okey pole kwao.
 
Namshukuru Mungu hadi leo hiki kikombe namna kilivoniepuka asee

Nilikosa nafac ya kujiunga JKT baada ya vpimo (Nlikua na matatizo ya macho) niliumia lkn nikashukuru.

Juzi nmekutana na mmoja wa wenzangu nliokua nao kwenye vipimo (wao walifanikiwa kwenda) amerudishwa baada kufanya maujenzi ya kutosha,kapoteza mda mwingi hajui aanzie wapi, na mbaya zaidi kakuta geto lake kwao wamepangisha sas anagongea kwa mshkaji wake.

Wngine ndo haoooo wanarudishwa asee

ILA YOTE HAYA YANA MWISHO
 
Kilichotokea kwa vijana wa JKT "walioasi" ni utabiri wa yajayo....mfumo wa watu wote kufaidi keki ya taifa umepiduliwa sasa tunarudi kule kwa zamani...kupata nafasi kama hizo lazima uwe unatoka kanda flani, kwa Mzee meja mstaafu, wa Chama flani kikongwe, au umepokelewa ukiwa na kimemo!
Kama kawaida yetu naona issue imebandikwa siasa!
Hakuna kigogo anapeleka mwanaye jeshini. Jeshini hakuna maslahi.
 
Nondo kuna mambo ya kuhoji

Ila unapohoji hiki kitu tunashindwa kuchangia kwani hawa vijana hawakusoma terms na condition za hiyo taasisi kabla hawajaingia huko??

Sasa unapewa nafasi ya kusaini mkataba shule yako itakusaidia nini kama huwezi kusoma na kuelewa??

Tujisahihishe
Nikuulize jambo kidogo?
Mkataba wa jkt ni miaka miwili ikiisha unarudi kwenu, lakini jeshi lilipojua limepata cheap labour liliamua kuwatumia kwenye miradi ya ujenzi sehemu mbalimbali za nchi ikiwemo ikulu, mirerani n.k
Kwahiyo jeshi halikuheshimu mkataba? Au terms za mkataba zina apply kwa vijana tu?

Jeshi lisitumikishe watu kinyume na mkataba na kuwatafutia sababu za kuwafukuza pale tu linapogundua kazi zake nyingi zimekamilika.

Tuelezane ukweli tuache ile tamaduni yetu ya kuambiana uongo kwa lengo la kuficha ukweli, tusiweke unafiki mbele. Iko hivi Rais aliyepita ndo kaleta yote haya, alianza kuwapa kipaumbele wanaoshiriki kwenye ujenzi na kuacha wale wa vikosini wanaolima na kufuga.

Kutokana na hali hiyo kila kijana alitaka awe kwenye bogi la ujenzi maana lina future ya tpdf, hata vigogo ambao watoto wao walikosa nafasi ya kwenda kwenye ujenzi vimemo vilitumika kuwafikisha huko maana ndiko kuna uhakika wa kutoboa.

Nirudi kwa hao madogo waliofukuzwa na CDF, kumbuka waliahidiwa ajira na Amiri Jeshi Mkuu aliyepita, wakiwa 2400 Amiri Jeshi Mkuu alitoa agizo waajiriwe wote, sasa kazi imeenda inakaribia ukingoni vijana 800+ wanaambiwa nyie rudini kikosini kazi imebaki ndogo, nikuulize mkuu wewe ungekuwa kwenye kundi la watu 800+ wanaorudishwa kikosini ungefikiria nini??

Jeshini kuna ronja yaani tetesi, na askari kwenye majeshi yote huishi kwa ronja, watoto washanusa kuna bogi la ajira linakuja soon ndio maana wamechujwa kimtindo na hiyo ndio sababu ya wao kutaka kujua ile ahadi iliyowafanya wapige kazi kwa morali mbona inapotea kirahisi??

CDF anasema wameasi, hivi watoto wale wanaasi nini? Kama walikuwa askari kwanini wasiuwawe au wafungwe sindo adhabu ya askari anayeasi? Kuwarudisha kwao ni kusolve tatizo kijanja washaona hawawezi kuwaajiri wote 2400 licha ya Rais aliyepita kuwaahidi ajira.

Hapa duniani unaweza kutengenezewa mazingira uonekane umeharibu, watu wanakutengenezea zengwe uki react tu imekula kwako.
 
Back
Top Bottom