GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,545
- 108,873
Nadhani kupitia hizi ' Hamasa ' ambazo naziona na nazisikia mara kwa mara kutokea sehemu mbalimbali ' Kiufundi ' kabisa tumewafanya sasa Wachezaji wetu wa Taifa Stars badala wawe ' Watulivu ' na Kujiandaa ' Kisaikolojia ' kwa huo mchezo sasa tumewajengea ' Hofu ' Kubwa ' Mioyoni ' mwao na binafsi naona Watanzania tunaweza kupigwa na ' Butwaa ' kubwa pale Uwanjani na tusiamini kwa kitakachotokea huku tukijutia muda wetu mwingi tulioupoteza katika Kuwahamasisha.
Kwa maoni yangu nadhani masuala ya Kiufundi yangepewa Kipaumbele zaidi kuliko hizi Hamasa na maneno maneno ya hapa na pale ambayo sioni kama yana Tija kwa Timu sana sana naona ni kama vile tunaharibu.
Wachezaji walitakiwa muda mwingi wajengwe Kiufundi na Kisaikolojia na nimesikitika kuona kuwa ni jana tu ndiyo Mwanasaikolojia Nguli nchini Bwana Chris Mauki ndiyo alikuwa na ‘ Session ‘ na Wachezaji wa Taifa Stars wakati kwa mtazamo wangu nadhani Mtaalam huyu alipashwa kuwa nao hata kwa Siku kati ya Tano au Saba.
Na uzuri ni kwamba Wachezaji wetu wengi wa Kitanzania tunawajua na tunashinda nao 24/7 hivyo wanapoanza Kusikia wanasifiwa kupita maelezo na wanaahidiwa ‘ Pesa ‘ nyingi sidhani kama hapo tunawajenga bali ndiyo Kwanza tunawazidishia ‘ Presha ‘ ambayo hatimaye itawafanya wapoteze ‘ Concentration ‘ wakati wa Mchezo na kujikuta wote wanaharibu kila Kitu.
Naheshimu sana na napongeza mno juhudi za Kamati ya Taifa Stars pamoja na Wadau wengine wote hasa Watanzania katika kufanikisha Timu yetu inatinga AFCON Finals 2019 huko Misri mwezi June ila wasiwasi wangu mkubwa GENTAMYCINE uko katika aina ya ‘ Maandalizi ‘ yetu hasa kwa upande wa Wachezaji wetu.
Tumewapa sana ‘ Presha ‘ Wachezaji wetu badala ya kuwaandaa wawe ‘ relaxed ‘ Siku hiyo na kuna uwezekano mkubwa kwa wanayoyaona Mitandaoni na Magazetini na kuyasikia katika Redio na Runinga yakawafanya wawe na wasiwasi mwingi, kuogopa Kukosea au Kuzomewa na hata kutupiwa lawama pale Timu isipofanya vyema.
Huu mtazamo wangu ni wa Kisaikolojia zaidi huku nikichanganya na Uzoefu wangu kidogo wa Mpira nilioucheza japo haukuwa wa Kiwango cha juu ila angalau nami katika Ngazi za Kishule, Kivyuo, Kimtaa, Kindondo na Ligi Daraja la Tatu nimepita huko hivyo mawazo yangu mengi hapa yameakisi yale ambayo nilikuwa nayashuhudia kama Mchezaji wa hizo ngazi za Awali ( za chini tajwa hapo )
Naogopa na nina wasiwasi sana!
Nawasilisha.
Kwa maoni yangu nadhani masuala ya Kiufundi yangepewa Kipaumbele zaidi kuliko hizi Hamasa na maneno maneno ya hapa na pale ambayo sioni kama yana Tija kwa Timu sana sana naona ni kama vile tunaharibu.
Wachezaji walitakiwa muda mwingi wajengwe Kiufundi na Kisaikolojia na nimesikitika kuona kuwa ni jana tu ndiyo Mwanasaikolojia Nguli nchini Bwana Chris Mauki ndiyo alikuwa na ‘ Session ‘ na Wachezaji wa Taifa Stars wakati kwa mtazamo wangu nadhani Mtaalam huyu alipashwa kuwa nao hata kwa Siku kati ya Tano au Saba.
Na uzuri ni kwamba Wachezaji wetu wengi wa Kitanzania tunawajua na tunashinda nao 24/7 hivyo wanapoanza Kusikia wanasifiwa kupita maelezo na wanaahidiwa ‘ Pesa ‘ nyingi sidhani kama hapo tunawajenga bali ndiyo Kwanza tunawazidishia ‘ Presha ‘ ambayo hatimaye itawafanya wapoteze ‘ Concentration ‘ wakati wa Mchezo na kujikuta wote wanaharibu kila Kitu.
Naheshimu sana na napongeza mno juhudi za Kamati ya Taifa Stars pamoja na Wadau wengine wote hasa Watanzania katika kufanikisha Timu yetu inatinga AFCON Finals 2019 huko Misri mwezi June ila wasiwasi wangu mkubwa GENTAMYCINE uko katika aina ya ‘ Maandalizi ‘ yetu hasa kwa upande wa Wachezaji wetu.
Tumewapa sana ‘ Presha ‘ Wachezaji wetu badala ya kuwaandaa wawe ‘ relaxed ‘ Siku hiyo na kuna uwezekano mkubwa kwa wanayoyaona Mitandaoni na Magazetini na kuyasikia katika Redio na Runinga yakawafanya wawe na wasiwasi mwingi, kuogopa Kukosea au Kuzomewa na hata kutupiwa lawama pale Timu isipofanya vyema.
Huu mtazamo wangu ni wa Kisaikolojia zaidi huku nikichanganya na Uzoefu wangu kidogo wa Mpira nilioucheza japo haukuwa wa Kiwango cha juu ila angalau nami katika Ngazi za Kishule, Kivyuo, Kimtaa, Kindondo na Ligi Daraja la Tatu nimepita huko hivyo mawazo yangu mengi hapa yameakisi yale ambayo nilikuwa nayashuhudia kama Mchezaji wa hizo ngazi za Awali ( za chini tajwa hapo )
Naogopa na nina wasiwasi sana!
Nawasilisha.