Maoni yangu katika rasimu ya katiba 2013: viongozi na waliokuwa viongozi wa dini wasiwe wagombea

Lizaboni

JF-Expert Member
Feb 21, 2013
33,894
20,372
wadau, hivi karibuni kumekuwa na wimbi kubwa la viongozi wa dini kuachana na kazi za kiroho na kuingia kwenye siasa. Hilo si tatizo kwani inaruhusiwa kwa mujibu wa katiba tuliyonayo. hata hivyo, pamoja na katiba kutoa mwanya huo, wengi wao wamekuwa wakitumia mwanya huo kutoa upendelea kwa wafuasi wa dini yao au kutumia majukwaa yao ya kisiasa kuponda au kukandamiza imani ya dini nyingine.

Ile dhana ya usichanganye dini na siasa inapotea. pia watu hawa ambao ni viongozi wa kiroho au waliwahi kushika nyadhifa mbalimbali katika jumuiya za kiroho wamekuwa wakitumika na viongozi wa dini au madhehebu yao kukandamiza dini nyingine au kutengeneza mipango michafu ili viongozi wa kisiasa dini au dhehebu jingine waonekane kuwa hawafai au wanatoa upendeleo kwa dini yao.

Kutokana na mkanganyiko huu, ni maoni yangu kuwa viongozi wa kiroho au waliowahi kuwa viongozi wa kiroho pamoja na jumuiya zake wasiruhusiwe kugombea nafasi za kisiasa kwa vile hawataweza kutenganisha nafasi zao za kiroho na za kisiasa. ni hayo tu wakuu kwa leo
 
Mkuu una malengo mema na haya maoni yako?

Wewe unajua fika kinacho wakimbiza viongozi wa kiroho na kuja kwenye siasa ni 'NJAA', sasa katiba mpya ikizuia viongozi wa kiroho kugombea katika nafasi za kisiasa, uoni kama watafilisi wahumini?

Acha waje ili tushikane masharti huku kwenye majukwaa. Ila tu wawe makini na kauli za kiuchochezi kwani zinaleta maafa.
 
Mkuu umesomeka, japo watakuja wafia vyama watoke povu juu ya ukweli huu.... Tumeona namna ambavyo slaa amekuwa akipewa support kubwa na maskoofu mbalimbali katika harakati zake za kisiasa ikiwa ni pamoja na kumkingia kifua kwa dhambi zake za uzinifu wakisema hayo ni maswala binafsi,wapigwe marufuku kabisa watatuletea mambo ya akina kibwetere nchini

Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums
 
Ungekua unatoa na mifano ya kiongozi gani wa kidini kaponda dini nyingine (huyo ambae wewe unasema ni mwasiasa?) Kama kumbukumbu zangu zitakua sahihi akina Kikwete ndio waasisi wa hii kitu, na hawa hawajawahi kua viongozi wa dini, Lipumba hali kadhalika, je wapi kanisa lililo wahi kutuhumiwa (kwa ushahidi na sio hisia) kwamba linataka kusimika kiongozi wa nchi? Ni fikra mgando kutengeza sheria hiyo unayoipendekeza leo eti tu kwasababu yupo Dr. Slaa, kumbuka katiba ni ya zaidi ya miaka 50-100 ijayo, huwezi kutengeza sheria ya kumkoa just one person, huo ni ujinga.

Hata hivyo, kiimani, Wakristo hawana andiko sana lilalo wataka waweke viongozi wa dini yao madarakani, Waislamu wana hiyo historia, rejea kikao kile cha Abuja Nigeria, hayo ndio yalikua mapendekezo, nipio sasa ukaja ule msemo Islam ndugu yake Islam, ni ngumu sana kwa Mwislamu kumponda mwislamu mwenzie hata kama kafanya ujinga wa hali ya juu, leo tunaona hata Zanzibar wanawataka Waarabu warudi, issue sio Uarabu wao, issue ni dini tu, hakika ni ujinga. Dr Slaa kamjataja Mkapa na Daudi Balali (wakatoriki wenzie) kwamba ni mafisadi, kamtaja hadi Sumaye (huyu ni Mluteli) wakati mtu huyu ni wa kabila lake (ongeza Mkristo mwenzie) hapo udini uko wapi?

Nimekua nasikiliza sana mawaidha mbalimbali ya viongozi wa Kislam juu ya Nyerere, ukweli nilicho gundua kuna dini kuongea uongo ili mradi unaempakazi sio Mwislamu mwenzio ni sawa tu, mtu kataifisha shule za kanisa lake ili Wapagani, Waislam n. k wasome halafu eti unamwita mdini, Mh sijui labda Uongo hua nikumsingizia mwislamu tu na sio wengine, kama ni hivyo ifike wakati tufikirie upya hizi imani kama ni kweli zinatoka kwa Mungu aliyetuumba.
 
<p>
<span style="font-size:3;"><span style="font-family: book antiqua;"><span><span><span><span><span><span><span><span>S<strong>asa, unataka nani. Serikali haina dini maana yake nini? Kila mtu ana dini yake anayoamini. Kama hali itakuwa hivyo maana yake kila mtu atapimwa kwanza kwa dini yake na imani yake kabla hajapewa nafasi ya kuongoza. Hoja ya upendeleo sio. Mbona tumeona Zanzibar wakuu wa dini wakiteuliwa na Rais kushika nafasi za maamuzi? Kwani wanapendelea wenye dini yao? Cha msingi ni vyama vyote visiwe vya Kidini hii inaleta mantiki</strong></span></span><strong>.</strong></span></span></span></span></span></span></span></span></p>
 
Kama watu wakipandwa mashetani ya ubaguzi utabadili mengi sana na bado haitosaidia..tangu nimeanza kwenda kanisani sijawahi sikia padri au askofu akiagiza watu wachague wakristo! Lakini wasiokwenda kusali wamewaaminisha watu kwamba kila jumapili watu wanahubiriwa siasa, upuuzi tu
 
Mkuu umesomeka, japo watakuja wafia vyama watoke povu juu ya ukweli huu.... Tumeona namna ambavyo slaa amekuwa akipewa support kubwa na maskoofu mbalimbali katika harakati zake za kisiasa ikiwa ni pamoja na kumkingia kifua kwa dhambi zake za uzinifu wakisema hayo ni maswala binafsi,wapigwe marufuku kabisa watatuletea mambo ya akina kibwetere nchini Sent from my BlackBerry 9360 using JamiiForums

Si lazima uchangie kama huna cha kuandika. We umesikia wapi Dr kaongea hoja ya Udini hata kama alikuwa kiongozi wa dini?

Mbona hujasema ya Prof. ya Msikiti wa Idrissa?

Mambo ya dini si ya kuongozi bali ni kuamua utumikieje watu.
 
Ungekua unatoa na mifano ya kiongozi gani wa kidini kaponda dini nyingine (huyo ambae wewe unasema ni mwasiasa?) Kama kumbukumbu zangu zitakua sahihi akina Kikwete ndio waasisi wa hii kitu, na hawa hawajawahi kua viongozi wa dini, Lipumba hali kadhalika, je wapi kanisa lililo wahi kutuhumiwa (kwa ushahidi na sio hisia) kwamba linataka kusimika kiongozi wa nchi? Ni fikra mgando kutengeza sheria hiyo unayoipendekeza leo eti tu kwasababu yupo Dr. Slaa, kumbuka katiba ni ya zaidi ya miaka 50-100 ijayo, huwezi kutengeza sheria ya kumkoa just one person, huo ni ujinga.

Hata hivyo, kiimani, Wakristo hawana andiko sana lilalo wataka waweke viongozi wa dini yao madarakani, Waislamu wana hiyo historia, rejea kikao kile cha Abuja Nigeria, hayo ndio yalikua mapendekezo, nipio sasa ukaja ule msemo Islam ndugu yake Islam, ni ngumu sana kwa Mwislamu kumponda mwislamu mwenzie hata kama kafanya ujinga wa hali ya juu, leo tunaona hata Zanzibar wanawataka Waarabu warudi, issue sio Uarabu wao, issue ni dini tu, hakika ni ujinga. Dr Slaa kamjataja Mkapa na Daudi Balali (wakatoriki wenzie) kwamba ni mafisadi, kamtaja hadi Sumaye (huyu ni Mluteli) wakati mtu huyu ni wa kabila lake (ongeza Mkristo mwenzie) hapo udini uko wapi?

Nimekua nasikiliza sana mawaidha mbalimbali ya viongozi wa Kislam juu ya Nyerere, ukweli nilicho gundua kuna dini kuongea uongo ili mradi unaempakazi sio Mwislamu mwenzio ni sawa tu, mtu kataifisha shule za kanisa lake ili Wapagani, Waislam n. k wasome halafu eti unamwita mdini, Mh sijui labda Uongo hua nikumsingizia mwislamu tu na sio wengine, kama ni hivyo ifike wakati tufikirie upya hizi imani kama ni kweli zinatoka kwa Mungu aliyetuumba.

Mazindu umeongea vema,ila mtoa mada nimegundua ni kati ya wale wenye kupewa ujira 7000 Lumumba ndio maana anasimamia kucha msuala tata tangu asubuhi!msameheni bure.Kuzuia viongozi wa dini kuwa viongozi wa siasa ni kuliondoa taifa mikononi mwa Mungu na hili gharama yake ni kubwa!
 
Mazindu umeongea vema,ila mtoa mada nimegundua ni kati ya wale wenye kupewa ujira 7000 Lumumba ndio maana anasimamia kucha msuala tata tangu asubuhi!msameheni bure.Kuzuia viongozi wa dini kuwa viongozi wa siasa ni kuliondoa taifa mikononi mwa Mungu na hili gharama yake ni kubwa!

Nyongeza quality za kiongozi hazitajali aliuwa kiongozi wa dini au la!kama ni mbaguzi/mdini anweza kuwa hata kama huko msikitini au kanisani hafiki.
 
Serikali haina dini, labda turekebishe hicho kipengele ili serikali iwe ya kidini!
 
ungekua unatoa na mifano ya kiongozi gani wa kidini kaponda dini nyingine (huyo ambae wewe unasema ni mwasiasa?) kama kumbukumbu zangu zitakua sahihi akina kikwete ndio waasisi wa hii kitu, na hawa hawajawahi kua viongozi wa dini, lipumba hali kadhalika, je wapi kanisa lililo wahi kutuhumiwa (kwa ushahidi na sio hisia) kwamba linataka kusimika kiongozi wa nchi? Ni fikra mgando kutengeza sheria hiyo unayoipendekeza leo eti tu kwasababu yupo dr. Slaa, kumbuka katiba ni ya zaidi ya miaka 50-100 ijayo, huwezi kutengeza sheria ya kumkoa just one person, huo ni ujinga.

Hata hivyo, kiimani, wakristo hawana andiko sana lilalo wataka waweke viongozi wa dini yao madarakani, waislamu wana hiyo historia, rejea kikao kile cha abuja nigeria, hayo ndio yalikua mapendekezo, nipio sasa ukaja ule msemo islam ndugu yake islam, ni ngumu sana kwa mwislamu kumponda mwislamu mwenzie hata kama kafanya ujinga wa hali ya juu, leo tunaona hata zanzibar wanawataka waarabu warudi, issue sio uarabu wao, issue ni dini tu, hakika ni ujinga. Dr slaa kamjataja mkapa na daudi balali (wakatoriki wenzie) kwamba ni mafisadi, kamtaja hadi sumaye (huyu ni mluteli) wakati mtu huyu ni wa kabila lake (ongeza mkristo mwenzie) hapo udini uko wapi?

Nimekua nasikiliza sana mawaidha mbalimbali ya viongozi wa kislam juu ya nyerere, ukweli nilicho gundua kuna dini kuongea uongo ili mradi unaempakazi sio mwislamu mwenzio ni sawa tu, mtu kataifisha shule za kanisa lake ili wapagani, waislam n. K wasome halafu eti unamwita mdini, mh sijui labda uongo hua nikumsingizia mwislamu tu na sio wengine, kama ni hivyo ifike wakati tufikirie upya hizi imani kama ni kweli zinatoka kwa mungu aliyetuumba.

mkuu, sijui kama kinachojadiliwa unakijua? Hakuna mahala mimi nimetaja uislam au ukristo. Kama ungekuwa unalitakia mema taifa hili na kwa kuzingatia kuwa serikali yetu haina dini, basi tuache viongozi wa dini watekeleze majukumu yao ya kidini bila ya serikali kuwaingilia. Vivyo hivyo, viongozi wa kidini wasiingilie mambo ya siasa kwani kwa kufanya hivyo tunakiuka misingi ya kutoingiliana. Tumeona jinsi gani viongozi wa bakwata wanavyotumika kwa maslahi ya wanasiasa. Vivyo hivyo, jumuiya za kikristo kama tec, cct na nyinginezo tumeshuhudia zikitumika na vyama vya siasa na kupelekea kutolea matamko ambayo yanakera katika jamii inayofuata mfumo huru usiofungamana na dini yoyote
 
serikali haina dini, labda turekebishe hicho kipengele ili serikali iwe ya kidini!

mkuu, ukisema kuwa serikali iwe na dini basi ni vema katiba ikatamka kuwa ni dini gani hiyo. Hapo ndipo patakapozua mgogoro mkubwa na hata vita hasa kwa huku tanzania bara ambako idadi ya wakristo na waislam inalingana ingawa hakuna takwimu sahihi zilizowahi kutolewa kwa siku za karibuni
 
Mnapokuwa Lumumba shaurianeni japo vitu vya maana kwa ajili ya uhai wa taifa miaka 100 ijayo.Kwa mtazamo wa Nambalapala anaamini kuingiza hilo litamsaidia kumuondoa anaemlenga!!Jiulize itakuwaje akitokea mwalimu akainyima usingizi CCM kama ilivyo sasa utatoa maoni kurekebisha katiba waalimu asiruhusiwe kuwa viongozi wa siasa kwa kuwa wataifluence wanafunzi wapige kura??
 
Acha kuwalenga viongozi wa Zanzibar. NA hapa Bara mie ni Kionozi wa Jumuiya ndondogo za dini yangu je nisigombee kwa kuwa tu mie ni mwenyekiti wa UWAKA?
 
Timing yenyewe inaonyesha kuwa huu ni "uhamishaji goli" ! miaka mingapi imepita sasa kina Mchungaji Msigwa, Lwakatare na wengineo wapo bungeni na hatujasikia kitu chochote ila kwa vile sasa kumetoka rasimu ya Katiba mpya ambayo kina Sheikh Ponda (Ubungo), Ustadh Ilunga/Basaleh (Kigamboni) na wengineo wanaweza kuingia bungeni ndio tunasikia hoja kama hizi!
 
Nyongeza quality za kiongozi hazitajali aliuwa kiongozi wa dini au la!kama ni mbaguzi/mdini anweza kuwa hata kama huko msikitini au kanisani hafiki.

(a) ni raia wa kuzaliwa wa Jamhuri ya Muungano kwa mujibu wa
Katiba hii na sheria za nchi;
(b) ni mwenye akili timamu;
(c) angalau mmoja kati ya wazazi wake ni raia wa kuzaliwa wa
Jamhuri ya Muungano;
(d) wakati wa kugombea, ana umri usiopungua miaka arobaini;
(e) anazo sifa za kumwezesha kuwa Mbunge wa Bunge la Jamhuri
ya Muungano kwa mujibu wa Katiba hii;
(f) anayo angalau shahada ya kwanza ya chuo kikuu
kinachotambuliwa kwa mujibu wa sheria za nchi;
(g) ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha
siasa au mgombea huru;
(h) sera zake au sera za chama chake si za mrengo wa kuligawa
Taifa kwa misingi ya ukabila, udini, rangi au jinsia;

(i) ni mwadilifu na anafuata maadili ya Taifa;
(j) mwenendo wake binafsi hautiliwi shaka na jamii;
(k) hajatiwa hatiani kwa kosa lolote la jinailinalohusu kukosa
uaminifu; na
(l) katika kipindi cha miaka mitano kabla ya tarehe ya Uchaguzi
Mkuu hajawahi kutiwa hatiani katika Mahakama yoyote kwa
kosa lolote la kukwepa kulipa kodi yoyote ya Serikali.

HAPO PENYE RED KUHUSU IBARA YA 75 RASIMU YA KATIBA JUU YA SIFA ZA MGOMBEA URAIS NDO NDO HASA MAKUSUDI YA THREAD YANGU MAANA SIJUI KWA HAWA WAGOMBEA AMBAO NI VIONGOZI WA KIROHO WATAJITETEA VIPI KWA HILO
 
timing yenyewe inaonyesha kuwa huu ni "uhamishaji goli" ! Miaka mingapi imepita sasa kina mchungaji msigwa, lwakatare na wengineo wapo bungeni na hatujasikia kitu chochote ila kwa vile sasa kumetoka rasimu ya katiba mpya ambayo kina sheikh ponda (ubungo), ustadh ilunga/basaleh (kigamboni) na wengineo wanaweza kuingia bungeni ndio tunasikia hoja kama hizi!

mkuu, waache viongozi wa kiroho wamtumikie Mungu na wanasiasa wafanye siasa
 
mnapokuwa lumumba shaurianeni japo vitu vya maana kwa ajili ya uhai wa taifa miaka 100 ijayo.kwa mtazamo wa nambalapala anaamini kuingiza hilo litamsaidia kumuondoa anaemlenga!!jiulize itakuwaje akitokea mwalimu akainyima usingizi ccm kama ilivyo sasa utatoa maoni kurekebisha katiba waalimu asiruhusiwe kuwa viongozi wa siasa kwa kuwa wataifluence wanafunzi wapige kura??

dah. Nafikiri hujaelewa mantiki. Kila kitu unafikiria uchadema na uccm tu. Tunachotakiwa kufanya ni kuweka msingi imara ambao tanzania tutaendelea kuishi kama dugu moja. Wakati ule viongozi wa kidini walipojitenga na siasa, hatukuwa na malumbano makubwa ya kidini katika taifa. Ila baada ya hawa wanadini kujiingiza kwenye siasa ndotabia ya kunyoosheana vidole na kutoleana matamko imeanza
 
Back
Top Bottom