Maoni ya wasomi juu ya mwitikio hafifu wa wapiga kura (low voters turnout)

Njowepo

JF-Expert Member
Feb 26, 2008
9,711
2,226
Kabla ya wananchi kupiga kura Oktoba 31, kulikuwa na malalamiko mengi kutoka kwa watu tofauti kuhusu uwezekano wa kutoshiriki kwenye zoezi hilo.

Malalamiko hayo yalianzia kwa vyama kutaka nakala za daftari hilo mapema, baadhi ya watu kutaka muda wa kuboresha daftari hilo uongezwe, wanafunzi wa vyuo kutoshiriki kutokana na vyuo kufungwa na majina ya watu kutoonekana kwenye daftari.

Maoni ya Profesa Lipumba dhidi ya Nec yanafanana na ya wasomi na wanazuoni waliozungumzia matokeo ya uchaguzi huo wa nne tangu kuanza kwa vyama vingi baada ya zaidi ya watu milioni 11 waliojiandikisha kupiga kura, kutojitokeza Oktoba 31 kutumia haki yao ya kidemokrasia.

Mhadhiri na mkuu wa kitengo cha sheria kwenye Chuo Kikuu cha Tumaini kilicho mkoani Iringa, Renatus Mgongo alisema ana wasiwasi kwamba daftari la wapigakura halikuhakikiwa ipasavyo na ndiyo sababu kuna idadi ndogo ya watu waliojitokeza kupiga kura ikilinganishwa na wale waliojiandikisha.

Mhadhiri huyo alisema kuwa huenda idadi ya wapiga kura iliyotangazwa na Nec haikuwa sahihi kutokana na ukweli kwamba hakukuwa na uhakiki thabiti wa wapiga kura, waliofariki na wale ambao wamehamishwa vituo ambao majina yao yalionekana na baadhi kukosekana.

"Mfano kuna mtu niliyemfahamu ambaye jina lake nililiona huku na yeye amehamishiwa Kigoma ambako pia alikuta jina lake, sasa hapa nilipata tabu kuelewa imekuwaje mtu mmoja kuonekana mara mbili wakati daftari limehakikiwa," alisema.

Alisema sababu nyingine ni kutojitokeza kwa wananchi wengi kupiga kura kutokana na utendaji kazi wa viongozi waliokuwa madarakani ambao haukuwaridhisha kutokana na vile walivyokuwa wakitarajia.

"Mambo mengi yamesababisha idadi ya waliojitokeza kupiga kura kuwa ndogo... wengi hawakuridhishwa na utendaji kazi wa viongozi ambao haukuwa na impact kwa maisha ya kawaida ya wananchi, hivyo wakaona kwamba hakuna umuhimu kwao kupiga kura," alisema.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Waislamu Morogoro, Ali Nassor alisema matokeo ya tafiti zilizofanywa na taasisi za Redet na Synovet yalichangia kukatisha tamaa wananchi kujitokeza kupiga kura kwa kudhani kwamba mshindi ameshajulikana.

"Tafiti kama vile Redet na Synovet zilionekana kama matokeo halisi ya uchaguzi na wananchi kuona kuwa CCM ndio itashinda. Baadhi ya watu hawakuona umuhimu wa kwenda kupiga kura," alisema Nassor.

Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine(SUA), Clavery Tungaraza alisema ikiwa Tanzania ina wastani wa watu milioni 42, si rahisi waliojiandikisha kufikia watu milioni 19.8.

Alisema kuwa idad hiyo ni kubwa na inatia wasiwasi kuwa huenda takwimu za Nec zinakinzana na uhalisia uliopo katika maeneo ya kupigia kura.

Kuhusu vituo vya kupigia kura, Dk Tungaraza alisema kwa vijijini tume ilijitahidi kuwa na vituo vingi ili kukidhi ongezeko la wapiga kura, lakini bado ni tatizo kwa mijini ambako kumekuwa na vituo vichache na hivyo kusababisha baadhi ya watu kutojitokeza kupiga kura kwa hofu kuwa wangetumia muda mwingi vituoni.

Makamu mkuu wa Chuo Kikuu cha Dodoma (Udom), Profesa Idrisa Kikula alisema miongoni mwa sababu hizo ni kukosekana kwa uhakika wa usalama wa raia.

Profesa Kikula alisema wananchi wengi waliingiwa na hofu wakati wa kampeni kutokana na jazba zilizokuwa zikisababishwa na kauli za baadhi ya wagombea pamoja na wapambe wao, jambo ambalo liliwajengea hofu na kuamua kutojitokeaa kupiga kura.

"Wananchi hawakuhakikishiwa usalama wao; wengi walikuwa na hofu ya kutokea machafuko kutokana na picha iliyojitokeza wakati wa kipindi cha kampeni; vyombo husika vilipaswa viwahakikishie wapigakura kuwa kutakuwepo na usalama wa kutosha, vinginevyo hali hii itaendelea kujirudia," alisema Kikula.

Kikula pia alisema kuwa baadhi ya watu walishindwa kwenda kupiga kura kutokana na kupoteza shahada zao, hivyo elimu ya kuhifadhi nyaraka hizo ilitakiwa itolewe na pia kutafutwa namna itayomwezesha mtu aliyejiandikisha kwenye daftari, apige kura hata kama atakuwa amepoteza shahada yake.

"Sio hapa Tanzania tu, hata huko Ulaya jamii ya watu wanaojiita wamestaarabika imekuwa haijitokezi kwenda kuchagua viongozi kwa visingizio kibao. Wengine wanaona kama ni kupoteza muda; wegine wanasema yeyote atakayechaguliwa ni sawa, lakini jambo kubwa hapa kwetu nasisitiza wananchi wahakikishiwe usalama wao, naamini watajitokeza vya kutosha kupiga kura," alisema Profesa Kikula.

Mkurugenzi wa kituo cha redio cha SAUT, Bulendu Dotto alisema kujitokeza kwa watu wachache kupiga kura kunaweza kuwa na sura tofauti, na kushauri ipo haja ya kufanyika utafiti wa kina.

Alitaja sababu mojawapo ambayo inaweza kuwa imechangia ni kuwepo kwa hofu ya kwa vurugu katika zoezi zima la upigaji kura ambayo ilijengwa na viongozi wa majeshi hapa nchini.

Alisema kauli ambazo zilikuwa zikitolewa na viongozi wa majeshi kuwa watadhibiti vurugu kwa nyakati tofauti, ziliwajenga hofu wapigakura ambao waliamua kutojitokeza kupiga kura kwa kuhofia vurugu.

"Ukiangalia takwimu za tume kuwa waliojiandikisha ni watu milioni 19, na waliopiga ni milioni 7, hapa mie napata shaka kuwa huenda takwimu za Tume zilikuwa zimepikwa na hazikuwa sahihi. Kama waliopiga kura ni milioni 7 ina maana jumla ya watu milioni 12 hawajapiga kura, hii inaweza kuwa takwimu za Tume si sahihi," alieleza mkurugenzi huyo.

Naye mratibu wa uchaguzi wa CCM wa mikoa ya Tanga, Arusha na Kilimanjaro, Stephen Mashishanga alisema kilichochangia kuwa na idadi ndogo ya wapigakura ni ukosefu wa elimu ya uraia.

Alisema kuwa ni wajibu wa Nec na vyama vya siasa kutoa elimu hiyo kabla ya uchaguzi. Alisema vyama vilieleza sera zao tu majukwaa na kusahau kuwa jukumu la kutoa elimu ya uraia pia linavihusu vyama vyote.

Naye mwanafunzi wa Chuo cha Biashara (CBE), Charles Daud tatizo hilo linatokana na Nec kuwa na takwimu zisizo sahihi na kushauri kuwa na kipindi cha maboresho ya daftari wa wapigakura wakati wa kampeni kwa vile wapo ambao walijiandikisha katika maeneo mengine na inapofika wakati wa kupiga kura wanakuwa wamehama.

"Mfano wakati Tume inafanya maboresho, mimi nilikuwa Musoma, lakini wakati wa uchaguzi nilikuwa Mwanza, sasa ningepiga vipi kura wakati nimebadilisha makazi," alieleza.

Naye mkazi wa Mwanza, Fatuma Saidi alisema tatizo hilo linatokana na Nec na serikali kutojali elimu ya uraia kwa wapigakura.

Alisema watu wengi walijiandikisha kwa ajili ya kutumia shahada za kupigia kura kama kitambulisho, lakini hawajitokezi kutokana na kutotambua umuhimu wa kupiga kura.

"Nilijiandikisha lakini sikuona umuhimu wa kupiga kura, kwa vile mara zote mbili nilizompigia kura mtu niliyemtaka, aliangushwa na mgombea wa CCM. Mfano mwaka huu nilimpenda sana mgombea urais wa Chadema, lakini nilijuwa kuwa hata akipigiwa kura, atashinda wa CCM sijui kura tukipiga wanazifanyaje... bora sikupiga," alisema mwanafunzi huyo wa CBE.

Mhadhiri katika Mt Tumaini, Dk Fairles Ilomu alitaja sababu zilizofanya wananchi kutojitokeza kwa wingi kuwa ni sheria mbovu za nchi na kufungwa mapema kwa usahihishaji daftari la kupigia kura.



Imeandaliwa na Petro Tumani, Hidaya Omar, Israel Mgussi, Dodoma, Tumaini Msowoya, Iringa, Frederick Katulanda, Mwanza na Venance George, Morogoro
 
Wakuu tokea mwaka 2010 mpaka sasa nimeshangwaza na idadi ya watu wanaojitokeza kupiga kura ktk chaguzi mbalimbali mfano uchaguzi wa rais kwa mujibu wa tume waliopiga kura ni asilimia 42% tu ya wale waliojiandikisha inamaana 58% hawakupiga, tuje kalenga walioandikishwa na kugakikiwa ni 77000 na kitu waliopiga kura ni kama 29000 na zaifi ya nusu hawajapiga tujiulize nini tatizo?
 
Wakuu tokea mwaka 2010 mpaka sasa nimeshangwaza na idadi ya watu wanaojitokeza kupiga kura ktk chaguzi mbalimbali mfano uchaguzi wa rais kwa mujibu wa tume waliopiga kura ni asilimia 42% tu ya wale waliojiandikisha inamaana 58% hawakupiga, tuje kalenga walioandikishwa na kugakikiwa ni 77000 na kitu waliopiga kura ni kama 29000 na zaifi ya nusu hawajapiga tujiulize nini tatizo?


Ndugu yangu katika nchi yenye mizengwe kama ulivyojionea leo Bungeni ambapo CCM wanafikia mahali pa kumtumia Sita kuvunja Kanuni kwanza siamini kwamba idadi tunayoambiwa kwamba ndiyo iliyoandikishwa si ya kweli. Namba hizo zimewekwa tu kwa ajili ya kuibeba CCM. Kwa hiyo sishangai kwamba Tume ya Uchaguzi inaweza kuboresha Daftari kimya kimya. Cha muhimu ni kuendelea kuwaelimisha wananchi wachukue hatua mara moja.
 
Ndugu yangu katika nchi yenye mizengwe kama ulivyojionea leo Bungeni ambapo CCM wanafikia mahali pa kumtumia Sita kuvunja Kanuni kwanza siamini kwamba idadi tunayoambiwa kwamba ndiyo iliyoandikishwa si ya kweli. Namba hizo zimewekwa tu kwa ajili ya kuibeba CCM. Kwa hiyo sishangai kwamba Tume ya Uchaguzi inaweza kuboresha Daftari kimya kimya. Cha muhimu ni kuendelea kuwaelimisha wananchi wachukue hatua mara moja.

Mi nadhani kuna tatizo zaidi ya hilo
 
Maskini!!!! Watanzania wanatongozwa kwa rushwa ya chumvi, kanga na vikofia vya kijani na kuangushwa kwenye jamvi la ufukara! CCM wanachekelea na kuendelea kuwashughulikia na kuwatia mimba ya umaskini bila huruma!
 
Kuna tatizo kubwa sana ambalo hata litakapokuja suala la kupigia kura za maoni ya katiba mpya litajitokeza tuu we subiri.Tatizo kubwa ni elimu kwa mpiga kura hamna kabisa.Kutokana hamna elimu kila mtu anaona kupiga kura kama kumpa kiongozi ulaji hivi so hata kama kuna lichama limeweka mtu ''Mzigo'' uchache wao wanaenda kupiga kura wanashinda.Hili lakuacha kupiga kura ni janga.
 
ila kule arumeru hukuliona hili tatizo. hivi ukiwa msukule akili zako zinageuka kuwa matope? nauliza!
Wakuu tokea mwaka 2010 mpaka sasa nimeshangwaza na idadi ya watu wanaojitokeza kupiga kura ktk chaguzi mbalimbali mfano uchaguzi wa rais kwa mujibu wa tume waliopiga kura ni asilimia 42% tu ya wale waliojiandikisha inamaana 58% hawakupiga, tuje kalenga walioandikishwa na kugakikiwa ni 77000 na kitu waliopiga kura ni kama 29000 na zaifi ya nusu hawajapiga tujiulize nini tatizo?
 
Vitisho hutumiwa sana,na kitu ambacho wanajiita watetezi wa HAKI za binadamu wamelala wakisubiri pesa za DONORS.Wao haki za binadamu ni raia akipigwa na polisi tu,vingine hakuna kitu.AKina Helen wako wapi kwenye suala la Rose Kamili ,kimya hakuna cha maana wanachofanya.
 
Kila panapo tokea chaguzi fulani tumekua tukishuhudia malalamiko ya kwamba hamasa ya kupiga kura haipo, lakini viongozi hao waliochaguliwa na watu wachache wanapo vurunda ndipo watu wengi hujitokeza kulalamika, nini sababu?
1. Je watu wamechoka na siasa?

Sidhani kama kuna mtu asiyefuatilia siasa kwa sasa, kama wewe ni miongoni mwao unawezaje kumpigia kura mtu usiye mfahamu vizuri? Ili umfahamu ni lazima umfuatilie ndipo umjue kiundani ili kuepuka kuwa bendera!

2. Uwoga!
Kuna watu wanasema wanaogopa kupigwa mabomu, sidhani kama kuna askari aliye tahira kupiga watu mabomu bila chanzo.

3. Kuishiwa sera!
Viongozi wa siku hizi hawana sera wakifika kwenye majukwaa wanatumia masaa mawili kupondana na dakika kumi kutoa sera!

Je, kwanini suala hili lisiwe la kisheria?
Ni vema kuwe na sheria ya kupiga kura kwenye katiba mpya liwekwe hili.

"MY PEN, MY ARMY"
 
Ni sawa ccm wameshinda, na mm ni mwanaccm damu, ila wapiga kura waliotangazwa ni zaidi ya 91,000 lakini wapiga kura hawakuzidi 24,000 sawa na 20%.

Je ni wananchi hawapendi kusikia mambo ya siasa ama ni kukataa tamaa ama ni vile vitisho vinaendelea? Elimu ya kupiga kura izoeshwe kwa wanajamii.
 
Nadhani elimu ya uraia na umuhimu wa kupiga kura ni tatizo kwa watz wengi!!!!
 
ukosefu wa elimu ya uraia kukata tamaa kuona hata nikipga kura haitasaidia kuleta mabadiliko yoyote
 
Kua sababua kadhaa ambazo zinasababisha
moja, Vitambulisho vyao vya kupigia kura vinachukuliwa na Maccm, ni kweli kunahitajika elimu ya uraia ambayo serikali ya CCM haipo tayari kuitoa na kuitekeleza,
mbili, vitisho kutoka CCM na vyombo vyake vya dola,
Tatu Rushwa iliyokithir
Nne, Mfumo mbovu wa Tume ya uchaguzi
 
Hiyo elimu ya uraia haifundishwi darasani, waliowengi hawapigi kura kwakua hawajaona mbadala na wanaona upinzani ni njaa, hasa upinzani wanapogombana wao kwa wao. Na si kwamba wanaopiga kura wanaipenda ccm no! Hakuna mbadala
 
Kua sababua kadhaa ambazo zinasababisha
moja, Vitambulisho vyao vya kupigia kura vinachukuliwa na Maccm, ni kweli kunahitajika elimu ya uraia ambayo serikali ya CCM haipo tayari kuitoa na kuitekeleza,
mbili, vitisho kutoka CCM na vyombo vyake vya dola,
Tatu Rushwa iliyokithir
Nne, Mfumo mbovu wa Tume ya uchaguzi

mkuu just be flexible, hebu toa 7bu zenye ukweli. 7bu zako zimekaa kichama zaidi. Mm nadhani wangejitokeza kwa wingi wakipigie hicho chama chenu. Elimu ipi inahitajika? Mbona kwenye helkopta na chopa wanajaa, nani anawapa elimu ya kufuata chopa?
 
Ni area ya kuifanyia research ila tuu ni kwamba wamechoshwa na siasa za tanzania kwani wanajua fika ccm inaharibu suala zima la demokrasia.Na njaa nayo factor kubwa
 
mkuu just be flexible, hebu toa 7bu zenye ukweli. 7bu zako zimekaa kichama zaidi. Mm nadhani wangejitokeza kwa wingi wakipigie hicho chama chenu. Elimu ipi inahitajika? Mbona kwenye helkopta na chopa wanajaa, nani anawapa elimu ya kufuata chopa?
Unakosoa kishabiki shabiki tu!... na kuleta utumbo utumbo tu!
 
tumechoka tukipiga kura kuwachagua watu tunaowataka wanaiba. tunapiga kura hakuna mabadiliko yeyote bado tu tuendelee kupanga foleni kuungua na jua eti kwa ajili ya kumpa chakula mwingine hiyo kazi nilifanya zamani but not now.
 
Ni sawa ccm wameshinda, na mm ni mwanaccm damu, ila wapiga kura waliotangazwa ni zaidi ya 91,000 lakini wapiga kura hawakuzidi 24,000 sawa na 20%.

Je ni wananchi hawapendi kusikia mambo ya siasa ama ni kukataa tamaa ama ni vile vitisho vinaendelea? Elimu ya kupiga kura izoeshwe kwa wanajamii.

Tukuulize wewe mwana CCM, mfano leo mmewanyang'anya wamasaai wa Chalinze kadi zao za kupiga kura, unategemea nini?

Wakati utakuja ambapo tukiuana ndio tutaheshimiana
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom