Maoni ya Thomas Nyimbo kuhusu hotuba ya Kikwete na hatma ya Tanzania

SG8

JF-Expert Member
Dec 12, 2009
3,955
2,125
Mh. Nyimbo kama Mtanzania ana maoni haya kuhusu hotuba ya Rais kikwete- Soma mwenyewe

WATANZANIA TUNAMATATIZO JIBU ATOE NANI?
NALIKO WAPI?
HOTUBA YA MH: RAIS-FEBRUARY 2011.


Mimi ningetegemea, Hotuba yake ingesheheni mambo ambayo yanawatesa waajiri wake (Watanzania) na wanatafuta majibu usiku na mchana hawayapati. Kwa mfano:
1. Mabomu Gongolamboto (Hili nivema lichunguzwe kwa makini) yaweza kuwa hujuma na ufisadi jambo hili ni lakitaalamu;(Ufalme njozi hausaidii)

2. Kupanda kwa gharama za maisha, (Maisha magumu kwa watanzania wote)
v Umeme na Ufisadi (somo hili linaanzia 1998 TANESCO/Net group solutions) Tulishauri kucheza na Umeme ni kaburi letu.
v Mbolea bei juu.
v Mahitaji ya msingi bei juu.
v Elimu bei juu na duni.
v Ongezeko la gharama za Usafiri (Sumatra imetangaza hivi karibuni)
v Hivi kilimo kwanza kwa mimi mwana kijiji nini tafsiri yake?
v I weje “CCM” mgawe Kofia na Tshirts za mamilioni huku shule hazina hata chaki? Hiki ni kiina macho? Au Rushwa? Jee, Uchaguzi huru na wa haki Uwapi?

3. Umeme na Ufisadi (MH. Rais waajiri wake tunapata umasikini wa kutupwa kutokana na Mafisadi Ndani ya CCM (Ref.Mwanahalisi) Katika swala la Umeme.
I. Mh. Rais mpaka leo ameshindwa kueleza kwa nini Bwawa la Mtera halijai huku Mbeya na Makete mvua zinanyesha kila siku (Hivi ninani ameshuhudia kina cha Mtera cha sasa) Kutokana na ufidisadi unaoendelea inawezekana watu wanahamisha kielelezo cha maji na kuonekana hayatoshi (ili Matakwa yao yatekelezeke(CCM na Dowans). Watanzania hatujasahau kuwa Bosi wa Tanesco aliyepita aliitisha Nchi hii kuwa “bila Dowans tutakaa gizani mpaka tukubali”.

II. Mh. Rais anajua Mabwawa yote tuliyo nayo, IPTL, Dowans; Songas na hatua yeyote ile mbali na (Makaa ya Mawe Mchuchuma) ni ufisadi mtupu. Fedha zinazo liwa hivi sasa ni maradufu kuliko gharama za kuzalisha Umeme mkubwa wa Makaa Mchuchuma na mwingine tungekuwa tuna uza nje kufidia gharama za uwekezaji: Pia chuma na madini kadha ya liganga yange zalishwa nakujiletea uchumi mkubwa sana kwa nchi na watu wake. Tatizo nini? Tangu 2000 hadi leo 2011!! Kama si Ufisadi?

III. Naamini Waajiri wa Mh. Rais hatuja pata maelezo kwanini kila kitu bei juu –Mbolea ingekuwa bei nafuu kipato cha mkulima kingemwezesha kumudu gharama kubwa za vitu vya msingi kama Elimu, Dawa, Vifaa vya Ujenzi, Vyakula na kadhalika.

IV. Wanafunzi wanagoma kila leo, haihitaji Usomi kujua kwamba nchi isiyo jali Elimu Duniani ni Nchi inayojenga Matabaka ya watu wake na kusimika umasikini kwa Umma.

waajiri wake Mh. Rais, tunataka kujua hatima ya tatizo la elimu ni nini? na lini mwisho. (Hapa Amani anaivuruga nani? Kama sio “CCM”.)

4. Amani na utulivu ni Matunda ambayo amekuwa akiyaongelea sana Mh. RAis, lakini amesahau kuwa mti wa matunda haya ni:
v Haki na utawala bora (washeria). Ni lazima Haki itangulie kwani sheria zaweza kuwa za kikandamizaji kama zilivyo sasa.
v Utulivu unazaliwa na shibe; Watanzania wana taabu ya njaa; Wana njaa kubwa ya Elimu; Njaa ya Afya; Njaa ya Umasikini, Taabu ya maradhi na Vifo. Jee Mh. Rais kauli yako ya “CHADEMA inataka kupindua Nchi"; una maana gani? Jee tukidai haki zetu maana yake tunataka kunyang’anya ajira yako kwa nguvu? (Mbona wote tuna kutambua Mh. Rais wetu mpendwa) Tunachodai ni haki yetu ya kuishi kwa amani ya kweli.

5. Mh. Rais ni vema ayaone yafuatayo;
Ø Chadema inaongoza mapambano ya kudai Haki ya waajiri wako; Nakumbuka Baba wa Taifa alisema (Haki yako bila kuidai kwa nguvu zote , hakuna takaye kupa haki hiyo kwenye kisahani cha Chai) kudai haki kwa Maandamano ya Amani sio tendo la vita Kamwe.
· Mh. Rais amezoea kuambiwa mambo ambayo sikweli, Mambo mabaya yanaelezwa kwa lugha tamu, dhambi zinapambwa; Huu ni ugonjwa mkubwa, na ndio ugonjwa mkubwa wa CCM. (Call Sugar, Sugar and not something like white Sand) tuache usanii na kuipamba dhambi kwani dhambi ni dhambi tu.

Ø Inashangaza sana; kwa Tafsiri pana ushauri aliotoa Mh; Edward Ngoyai Lowasa juu ya ugumu wa maisha kwa Watanzania; ndiyo hayo hayo waliyo eleza Waheshimiwa Mbowe na Dr; Slaa katika maandamano yanayo endelea, naamini Mh. Rais anauwezo zaidi yangu wa kutafsiri mambo, Sijui nini kimekukwaza. Je, wanao kuunga mkono ni vipofu wa akili? Ebu tazama mambo yalivyo;
o Tanzania Hatuna Katiba Bora.
o Tanzania Hatuna Uongozi bora na adilifu katika Nchi yetu (ndani ya CCM) unapata heshima kwa kuipamba dhambi.
o Viongozi wetu hawana kipawa cha kutenda haki kwa umma (Waliopo wachache sana)
o Tanzania Hatuna Maendeleo Serikali haijali sauti ya umma. (Kauli ya wengi ni kauli ya Mungu)
o Tanzania viongozi wanauza haki na mali za umma kwa mafisadi na kuwamasikinisha watanzania, bila huruma (a Government without a human face) Haya ndio yanayo sababisha tuandamane. (sio kukuondoa Mh. Rais wetu).

6. Mh. Rais kumbuka maneno haya; “Maisha Bora kwa kila mtanzania”
Leo watanzania tunaishi kwa kubahatisha tu, Kutokana na watu wachache wanao kuzunguka; Kwa Shibe zao. Baba wa taifa hili, kabla hajatutoka alitambua, hataishi milele hivyo aliwaaga watoto wake (Watanzania) kwa maneno haya, “Nikifa nitawaombea kwa Mungu Watanzania”, ambapo leo CCM inawachezea kama vichuguu vya Mchwa wa kulishia kuku. Sasa ni dhahili maombi ya Baba yetu, Mungu ameyasikia. Mapema Hayati Baba yetu Mwalimu J.K. Nyerere aliwahi kusema; “Tuwe na mfumo wa vyama vingi kwani nikifa watu wangu watakosa pakukimbilia” Kauli hizi zenye Baraka tele ndio nguzo kuu ya utekelezaji wa CHADEMA. Sio kukupindua; siku zote kauli ya Umma ni kauli ya Mungu.
ü Kwa maombi na Baraka za Baba wa Taifa leo CHADEMA ndilo kimbilio la Watanzania watoto wa (Mwalimu J.K. Nyerere). Mh. Rais J.k Kikwete;
ü Achana na Mafisadi wa (CCM) kumbuka 2005 nilikuasa juu ya hao Mafisadi watakuchafua, sasa wamekuchafua. Mh. Rais Hujafika mwisho, nikuombe,
Unda Serikali iliyo sheheni watu madhubuti katika kutetea Haki na kweli.

7. Tuichambue Katiba yetu ambayo ni chanzo cha Ufisadi unaoendelea:
· Basi tuijadili katiba upya kwa pamoja kwa wakati na wakati ni sasa.
· Nchi hii ni kubwa sana kwa Km.Mraba na kwa mali za Asili ilizosheheni. Hivyo mtu mmoja kuwa Muibua uchumi na Mtatuwa shida za maendeleo Kutoka Shirati ziwa Victoria Msoma mpaka Manda Ziwa Nyasa Ludewa hakika ni muujiza tu. Lazima tutafute jibu kwani Mungu hajaumba mtu mwenye uwezo huo. (Zanzibar a case study)
· Mh. Rais elewa, Amani Tanzania haipo, ila uvumilivu ambao unamwisho. CCM isidanganyike, kwa vile Amani ni Tunda tu; Basi hakuna tunda lisilo oza bila matunzo mwafaka kwa kila aina ya tunda. Matunda yote duniani ni (Perishable).

8. Nikweli haya ni miongoni mwa matatizo ya msingi kwa maendeleo ya Watanzania hivi sasa:
a) Dowans na hatima yake.
b) Umeme na hatima yake.
c) Elimu na hatima yake.
d) Kilimo na hatima yake.

9. Mwisho Mh.Rais matatizo hayo makubwa hayawezi kutafutwa Bungeni au kwenye Halmashauri. Wewe Mh. Rais unajua vizuri kuliko mimi kwa jinsi gani Bunge letu lilivyo mali ya Vyama vya Siasa na sio wananchi (tena kikatiba) nafasi ndogo iliyo kuwepo katika Bunge la Tanzania ilikuwa ni hekima ya Mbunge mmoja mmoja tu; hivi sasa; nafasi hiyo nayo imefisadiwa na “CCM” unayo iongoza, Mh. Rais wetu. Hapo utakili kuwa ni sawa Watanzania tutafuta Maelezo hayo kwako tu. Kupinduliwa unakosema ni kutafuta Mfupa ndani ya Yai (Yai halina Mfupa)

By.
THOMAS SIMON NYIMBO
3rd March 2011.
 
Yaani ni ya kisomi kwelikweli, Mkwere badala ya kujibu hayo ye anawalaumu cdm!
 
CCM imeshindwa hata wenyewe wanajua ila kukiri hadhari inakuwa ngumu wamewaachia wananchi waamua kuwapumzisha tu. wajipanga upya kwenye ligi.
 
Gerrad, hembu nikumbushe, Nyimbo ni nani?
Mwanzilishi na Makamu mwenyekiti wa zamani wa kilichokuwa chama cha PONA, Mbunge wa Njombe Magharibi (CCM-1995-2005), Mgombea wa CCM katika kura za maoni akiibuka mshindi wa kwanza (2010) kisha akaenguliwa na Kikwete. Mgombea kupitia jimbo la Njombe Magharibi kupitia CDM akafanyiwa hujuma na sasa mlezi/Mfadhili wa CDM Wilaya ya Njombe
 
huyu ni mbunge amabae alikua sisiem akapigwa vita ndo akahamia cdm alikua mbunge wa irembula mbele ya makambako,mh Ben alimpa kauli ya kwamba by hooks or crooks nitahakikisha hautudi bungeni 2010.
 
huyu ni mbunge amabae alikua sisiem akapigwa vita ndo akahamia cdm alikua mbunge wa irembula mbele ya makambako,mh Ben alimpa kauli ya kwamba by hooks or crooks nitahakikisha hautudi bungeni 2010.
Upo sahihi kabisa Mkuu. Mkapa alimfanyia fitna za ajabu Mzee wa watu. Jimbo linaitwa Njombe Magharibi sio Ilembula
 
أطلب من جميع المسلمين في بلدي تنزانيا جيدة أن يكون جسد واحد وليكون أداة للسياسيين لتغطية ضعفهم في إدارة ستابيليتيس. أنا المحامي الدكتور jk كيكويتي لا التقاضي كاديما لأن ما يقومون به من المحتمل ما يفترض في الرجوع إلى هذه "الهياكل العظمية" الطرف الورق الرئيسية المسؤوليات إلى الحكومة الحالية
 
asanteni sana,jina mashuhuri sana ila alikuwa amenitoka kidogo. mawazo mazuri sana, yanatoa ufumbuzi kwa maswali mengi. Naskitika hayawezi kufanyiwa kazi ila thanx God ujumbe utakuwa umefika.
 
Nyimbo ni mwana CDM, aliyekuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya CDM katika moja ya jimbo la Mkoani Iringa. Ni msema kweli na haogopi mtu. Ndiye aliyeongoza harakati za kudai tanganyika miaka ya G.55 bungeni alipokuwa mbunge kupitia ccm; na kwa hila za ccm walimuona kama mwiba kwa masilahi yao. Wakawa wanamuengua kila alipogombea ubunge kupitia ccm; sasa mwaka huu akatangaza kuwa "ccm sasa basi-na kuhamia CDM". Amefungua matawi mengi sana katika jimbo lake ya CDM na kuanza kuwaandaa vema wananchi kwa ajili ya kuimarisha CDM for serikali za mitaa 2012 na uchanguzi mkuu 2015. Hongera mzee wetu Nyimbo kwa kusema ukweli wa wazi kwa jk na kwa watanzania wote. BIG UP!!
 
Nyimbo ni mwana CDM, aliyekuwa mgombea ubunge kwa tiketi ya CDM katika moja ya jimbo la Mkoani Iringa. Ni msema kweli na haogopi mtu. Ndiye aliyeongoza harakati za kudai tanganyika miaka ya G.55 bungeni alipokuwa mbunge kupitia ccm; na kwa hila za ccm walimuona kama mwiba kwa masilahi yao. Wakawa wanamuengua kila alipogombea ubunge kupitia ccm; sasa mwaka huu akatangaza kuwa "ccm sasa basi-na kuhamia CDM". Amefungua matawi mengi sana katika jimbo lake ya CDM na kuanza kuwaandaa vema wananchi kwa ajili ya kuimarisha CDM for serikali za mitaa 2012 na uchanguzi mkuu 2015. Hongera mzee wetu Nyimbo kwa kusema ukweli wa wazi kwa jk na kwa watanzania wote. BIG UP!!
Mkuu naomba nikukumbushe kwenye bold hizo. Wakati wa G.55 Nyimbo hakuwa mbunge, walichopishana na CCM ni ufisadi hasa wa NBC na mikataba michafu. Utakumbuka kwamba kati ya 1995 na 2005 alisimamishwa mara nyingi kuhudhuria viako vya bunge. Pia uchaguzi wa serikali za mitaa ni 2014
 
Asante sana mh. T.s nyimbo hakika wewe ni hazina ya taifa ambayo ccm waliichezea na sasa wanatafuta mchawi.

Mungu akupe maisha marefu tuchote hekima zako baba.

Mwenye masikio na asikie!.
 
أطلبمنجميعالمسلمينفيبلديتنزانياجيدةأنيكونجسدواحدوليكونأداةللسياسيينلتغطيةضعفهمفيإدارةستابيليتيس. أناالمحاميالدكتور jk كيكويتيلاالتقاضيكاديمالأنمايقومونبهمنالمحتملمايفترضفيالرجوعإلىهذه "الهياكلالعظمية" الطرفالورقالرئيسيةالمسؤولياتإلىالحكومةالحالية


Sasa mkuu, unatumia kiarabu ili iweje? Acha hizo!
 
Asante sana mh. T.s nyimbo hakika wewe ni hazina ya taifa ambayo ccm waliichezea na sasa wanatafuta mchawi.

Mungu akupe maisha marefu tuchote hekima zako baba.

Mwenye masikio na asikie!.
Point tupu
 
Mh. Nyimbo kama Mtanzania ana maoni haya kuhusu hotuba ya Rais kikwete- Soma mwenyewe



WATANZANIA TUNAMATATIZO JIBU ATOE NANI?
NALIKO WAPI?
HOTUBA YA MH: RAIS-FEBRUARY 2011.


Mimi ningetegemea, Hotuba yake ingesheheni mambo ambayo yanawatesa waajiri wake (Watanzania) na wanatafuta majibu usiku na mchana hawayapati. Kwa mfano:
1. Mabomu Gongolamboto (Hili nivema lichunguzwe kwa makini) yaweza kuwa hujuma na ufisadi jambo hili ni lakitaalamu;(Ufalme njozi hausaidii)

2. Kupanda kwa gharama za maisha, (Maisha magumu kwa watanzania wote)
v Umeme na Ufisadi (somo hili linaanzia 1998 TANESCO/Net group solutions) Tulishauri kucheza na Umeme ni kaburi letu.
v Mbolea bei juu.
v Mahitaji ya msingi bei juu.
v Elimu bei juu na duni.
v Ongezeko la gharama za Usafiri (Sumatra imetangaza hivi karibuni)
v Hivi kilimo kwanza kwa mimi mwana kijiji nini tafsiri yake?
v I weje CCM mgawe Kofia na Tshirts za mamilioni huku shule hazina hata chaki? Hiki ni kiina macho? Au Rushwa? Jee, Uchaguzi huru na wa haki Uwapi?

3. Umeme na Ufisadi (MH. Rais waajiri wake tunapata umasikini wa kutupwa kutokana na Mafisadi Ndani ya CCM (Ref.Mwanahalisi) Katika swala la Umeme.
I. Mh. Rais mpaka leo ameshindwa kueleza kwa nini Bwawa la Mtera halijai huku Mbeya na Makete mvua zinanyesha kila siku (Hivi ninani ameshuhudia kina cha Mtera cha sasa) Kutokana na ufidisadi unaoendelea inawezekana watu wanahamisha kielelezo cha maji na kuonekana hayatoshi (ili Matakwa yao yatekelezeke(CCM na Dowans). Watanzania hatujasahau kuwa Bosi wa Tanesco aliyepita aliitisha Nchi hii kuwa bila Dowans tutakaa gizani mpaka tukubali.

II. Mh. Rais anajua Mabwawa yote tuliyo nayo, IPTL, Dowans; Songas na hatua yeyote ile mbali na (Makaa ya Mawe Mchuchuma) ni ufisadi mtupu. Fedha zinazo liwa hivi sasa ni maradufu kuliko gharama za kuzalisha Umeme mkubwa wa Makaa Mchuchuma na mwingine tungekuwa tuna uza nje kufidia gharama za uwekezaji: Pia chuma na madini kadha ya liganga yange zalishwa nakujiletea uchumi mkubwa sana kwa nchi na watu wake. Tatizo nini? Tangu 2000 hadi leo 2011!! Kama si Ufisadi?

III. Naamini Waajiri wa Mh. Rais hatuja pata maelezo kwanini kila kitu bei juu Mbolea ingekuwa bei nafuu kipato cha mkulima kingemwezesha kumudu gharama kubwa za vitu vya msingi kama Elimu, Dawa, Vifaa vya Ujenzi, Vyakula na kadhalika.

IV. Wanafunzi wanagoma kila leo, haihitaji Usomi kujua kwamba nchi isiyo jali Elimu Duniani ni Nchi inayojenga Matabaka ya watu wake na kusimika umasikini kwa Umma.

waajiri wake Mh. Rais, tunataka kujua hatima ya tatizo la elimu ni nini? na lini mwisho. (Hapa Amani anaivuruga nani? Kama sio CCM.)

4. Amani na utulivu ni Matunda ambayo amekuwa akiyaongelea sana Mh. RAis, lakini amesahau kuwa mti wa matunda haya ni:
v Haki na utawala bora (washeria). Ni lazima Haki itangulie kwani sheria zaweza kuwa za kikandamizaji kama zilivyo sasa.
v Utulivu unazaliwa na shibe; Watanzania wana taabu ya njaa; Wana njaa kubwa ya Elimu; Njaa ya Afya; Njaa ya Umasikini, Taabu ya maradhi na Vifo. Jee Mh. Rais kauli yako ya CHADEMA inataka kupindua Nchi"; una maana gani? Jee tukidai haki zetu maana yake tunataka kunyanganya ajira yako kwa nguvu? (Mbona wote tuna kutambua Mh. Rais wetu mpendwa) Tunachodai ni haki yetu ya kuishi kwa amani ya kweli.

5. Mh. Rais ni vema ayaone yafuatayo;
Ø Chadema inaongoza mapambano ya kudai Haki ya waajiri wako; Nakumbuka Baba wa Taifa alisema (Haki yako bila kuidai kwa nguvu zote , hakuna takaye kupa haki hiyo kwenye kisahani cha Chai) kudai haki kwa Maandamano ya Amani sio tendo la vita Kamwe.
· Mh. Rais amezoea kuambiwa mambo ambayo sikweli, Mambo mabaya yanaelezwa kwa lugha tamu, dhambi zinapambwa; Huu ni ugonjwa mkubwa, na ndio ugonjwa mkubwa wa CCM. (Call Sugar, Sugar and not something like white Sand) tuache usanii na kuipamba dhambi kwani dhambi ni dhambi tu.

Ø Inashangaza sana; kwa Tafsiri pana ushauri aliotoa Mh; Edward Ngoyai Lowasa juu ya ugumu wa maisha kwa Watanzania; ndiyo hayo hayo waliyo eleza Waheshimiwa Mbowe na Dr; Slaa katika maandamano yanayo endelea, naamini Mh. Rais anauwezo zaidi yangu wa kutafsiri mambo, Sijui nini kimekukwaza. Je, wanao kuunga mkono ni vipofu wa akili? Ebu tazama mambo yalivyo;
o Tanzania Hatuna Katiba Bora.
o Tanzania Hatuna Uongozi bora na adilifu katika Nchi yetu (ndani ya CCM) unapata heshima kwa kuipamba dhambi.
o Viongozi wetu hawana kipawa cha kutenda haki kwa umma (Waliopo wachache sana)
o Tanzania Hatuna Maendeleo Serikali haijali sauti ya umma. (Kauli ya wengi ni kauli ya Mungu)
o Tanzania viongozi wanauza haki na mali za umma kwa mafisadi na kuwamasikinisha watanzania, bila huruma (a Government without a human face) Haya ndio yanayo sababisha tuandamane. (sio kukuondoa Mh. Rais wetu).

6. Mh. Rais kumbuka maneno haya; Maisha Bora kwa kila mtanzania
Leo watanzania tunaishi kwa kubahatisha tu, Kutokana na watu wachache wanao kuzunguka; Kwa Shibe zao. Baba wa taifa hili, kabla hajatutoka alitambua, hataishi milele hivyo aliwaaga watoto wake (Watanzania) kwa maneno haya, Nikifa nitawaombea kwa Mungu Watanzania, ambapo leo CCM inawachezea kama vichuguu vya Mchwa wa kulishia kuku. Sasa ni dhahili maombi ya Baba yetu, Mungu ameyasikia. Mapema Hayati Baba yetu Mwalimu J.K. Nyerere aliwahi kusema; Tuwe na mfumo wa vyama vingi kwani nikifa watu wangu watakosa pakukimbilia Kauli hizi zenye Baraka tele ndio nguzo kuu ya utekelezaji wa CHADEMA. Sio kukupindua; siku zote kauli ya Umma ni kauli ya Mungu.
ü Kwa maombi na Baraka za Baba wa Taifa leo CHADEMA ndilo kimbilio la Watanzania watoto wa (Mwalimu J.K. Nyerere). Mh. Rais J.k Kikwete;
ü Achana na Mafisadi wa (CCM) kumbuka 2005 nilikuasa juu ya hao Mafisadi watakuchafua, sasa wamekuchafua. Mh. Rais Hujafika mwisho, nikuombe,
Unda Serikali iliyo sheheni watu madhubuti katika kutetea Haki na kweli.

7. Tuichambue Katiba yetu ambayo ni chanzo cha Ufisadi unaoendelea:
· Basi tuijadili katiba upya kwa pamoja kwa wakati na wakati ni sasa.
· Nchi hii ni kubwa sana kwa Km.Mraba na kwa mali za Asili ilizosheheni. Hivyo mtu mmoja kuwa Muibua uchumi na Mtatuwa shida za maendeleo Kutoka Shirati ziwa Victoria Msoma mpaka Manda Ziwa Nyasa Ludewa hakika ni muujiza tu. Lazima tutafute jibu kwani Mungu hajaumba mtu mwenye uwezo huo. (Zanzibar a case study)
· Mh. Rais elewa, Amani Tanzania haipo, ila uvumilivu ambao unamwisho. CCM isidanganyike, kwa vile Amani ni Tunda tu; Basi hakuna tunda lisilo oza bila matunzo mwafaka kwa kila aina ya tunda. Matunda yote duniani ni (Perishable).

8. Nikweli haya ni miongoni mwa matatizo ya msingi kwa maendeleo ya Watanzania hivi sasa:
a) Dowans na hatima yake.
b) Umeme na hatima yake.
c) Elimu na hatima yake.
d) Kilimo na hatima yake.

9. Mwisho Mh.Rais matatizo hayo makubwa hayawezi kutafutwa Bungeni au kwenye Halmashauri. Wewe Mh. Rais unajua vizuri kuliko mimi kwa jinsi gani Bunge letu lilivyo mali ya Vyama vya Siasa na sio wananchi (tena kikatiba) nafasi ndogo iliyo kuwepo katika Bunge la Tanzania ilikuwa ni hekima ya Mbunge mmoja mmoja tu; hivi sasa; nafasi hiyo nayo imefisadiwa na CCM unayo iongoza, Mh. Rais wetu. Hapo utakili kuwa ni sawa Watanzania tutafuta Maelezo hayo kwako tu. Kupinduliwa unakosema ni kutafuta Mfupa ndani ya Yai (Yai halina Mfupa)

By.
THOMAS SIMON NYIMBO
3rd March 2011.

Hongera Mhe. Nyimbo kwa kuamua kuandaa rasmi maoni yako. Tatizo sisiem imekuwa sikio la kufa. Hata wakisoma maoni yako, hawatapata chochote cha maana.
 
Back
Top Bottom