Rare Sapphire
JF-Expert Member
- Jul 24, 2021
- 576
- 1,625
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda
Akizungumza na waandishi wa habari tarehe 9/5/2023, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. Adolf Mkenda amesema ya Sera ya Elimu na Mafunzo ya 2014 toleo la 2023 pamoja na Rasimu ya Mitaala Mipya ya Elimu ya Msingi, Sekondari na Vyo vya Ualimu zimekamilika, na sasa serikali imetoa rasimu hizo hadharani ili kupata maoni ya mwisho, na maoni hayo yawe yameshapokelewa kufikia tarehe 31/5/2023.
Akaongeza kuwa tarehe tarehe 10/5/2023 Wizara itafanya Semina na Wabunge kuwapitisha katika Rasimu hizo na tarehe 12/5/2023 mpaka 14/5/2023 kutakuwa na Kongamano Kubwa la Kitaifa la kujadili Rasimu hizo.
Rasimu hizo zinapatikanakatika Tovuti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia, lakini pia katika tovuti ya Idara ya Habari na Maelezo pamoja na tovuti ya Taasisi ya Elimu Tanzania.
Kwa maelezo zaidi unaweza kusoma kimbatisho hapo chini.