Maoni ya mtumishi wa Mungu mwl. Mwakasege kuhusu miaka 50 ya uhuru

mchemsho

JF-Expert Member
Jun 8, 2011
3,212
867
Leo nipata Neema ya kudhuria semina ya mwalimu Christopher Mwakasege inayoendelea viwanja vya biafra kinondoni jijini Dsm, kipekee ilikuwa semina yenye Baraka na inayoashiria mwanzo Mpya wa Maisha ya Kiroho na Mahusiano Bwana Mungu. Kichwa cha somo ni namna ya kuombea maisha yako ya baadae ili yawe mazuri. Ninachotaka ku-share nanyi ni sehemu ndogo ya hotuba yake juu ya baraka ambazo mtu anaweza kupata au taifa. Akatoa mfano kuwa mwaka 2001 alitembelewa na wageni wazungu kutoka ulaya ambapo walimwelezea furaha yao kwamba nchi zao zimekubali kuongeza misaada kwa tanzania katika sekta tofauti ikiwemo afya na elimu, Wazungu hao huku wakitegemea kwamba mwalimu Mwakasege angefurahi na kuwashukuru, badala yake aliwacharukia na kuonyesha kukerwa kwake na hiyo misaada ya wazungu, aliwauliza ,hivi mnafahamu kama nchi hii imepata uhuru zaidi ya miaka 40, ni sawa kuendelea kuitwa taifa changa?? Akaendelea kusema hivi ni nani ambae anazaa mtoto anafikisha miaka zaidi ya 40 na bado akaendelea kumhudumia?? Kama yupo basi lazima aitwe kwenye vikao vya familia na ahojiwe shida nini..akahoji kwanini kipimo cha umri kiwe na maana katika social perspective lakini isilete maana kwenye umri wa nchi?? Mwisho akawaambia wale wageni wazungu waliokuwa ofisin kwake kuwa kama wanazipenda nchi masikini wangezipeleka huko wao wanapochota mali ili na waafrika wakachote wao wenyewe ili wasiwe watu wakukaa tu na kusubiri misaada. MBARIKIWE NYOTE.
 
Kwani mali zinachotwa wapi?NI AFRICA of coz,sasa wazungu wakawaonyeshe wakati kwenu ndo zapatikana?
 
Leo nipata Neema ya kudhuria semina ya mwalimu Christopher Mwakasege inayoendelea viwanja vya biafra kinondoni jijini Dsm, kipekee ilikuwa semina yenye Baraka na inayoashiria mwanzo Mpya wa Maisha ya Kiroho na Mahusiano Bwana Mungu. Kichwa cha somo ni namna ya kuombea maisha yako ya baadae ili yawe mazuri. Ninachotaka ku-share nanyi ni sehemu ndogo ya hotuba yake juu ya baraka ambazo mtu anaweza kupata au taifa. Akatoa mfano kuwa mwaka 2001 alitembelewa na wageni wazungu kutoka ulaya ambapo walimwelezea furaha yao kwamba nchi zao zimekubali kuongeza misaada kwa tanzania katika sekta tofauti ikiwemo afya na elimu, Wazungu hao huku wakitegemea kwamba mwalimu Mwakasege angefurahi na kuwashukuru, badala yake aliwacharukia na kuonyesha kukerwa kwake na hiyo misaada ya wazungu, aliwauliza ,hivi mnafahamu kama nchi hii imepata uhuru zaidi ya miaka 40, ni sawa kuendelea kuitwa taifa changa?? Akaendelea kusema hivi ni nani ambae anazaa mtoto anafikisha miaka zaidi ya 40 na bado akaendelea kumhudumia?? Kama yupo basi lazima aitwe kwenye vikao vya familia na ahojiwe shida nini..akahoji kwanini kipimo cha umri kiwe na maana katika social perspective lakini isilete maana kwenye umri wa nchi?? Mwisho akawaambia wale wageni wazungu waliokuwa ofisin kwake kuwa kama wanazipenda nchi masikini wangezipeleka huko wao wanapochota mali ili na waafrika wakachote wao wenyewe ili wasiwe watu wakukaa tu na kusubiri misaada. MBARIKIWE NYOTE.

Mkuu, nilikuwepo pia tangu J3, uwa sipendi kukosa semina za huyu Mwalimu anapokuwa Dar au nikimkuta mji wowote, alinigusa sana alipozungumzia topic hiyo ni kama alikuwa anatuma ujumbe kwa wahusika kuwa Tanzania ni mtu mzima sasa tena anaelekea uzeeni hivyo si sahihi kuendelea kuwa tegemezi la misaada toka kwa wakoloni mamboleo.
 
kweli mwalimu menigusa sana na masomo yake tanzania ina miaka 50 now inabidi ijitegemee yenyewe mwalimu mwakasege anafundisha maisha pia amenigusa aliposema kuwa tusibishane kuhusu dini ztu bali wote tuhimizane kumtolea mungu sadaka na pia hata kama ni mlutheran unaweza kuwasaidia makanisa mengine kama ukiguswa lakini sio mitume na manabiii wanahubiri juu ya makanisa yao tu
 
Mwaka jana kuhusu MZALIWA WA KWANZA nilihudhuria.This time nimekosa,hope mwakani nitahudhuria.Endeleeni kutujuza
 
Nilikuwepo nimemsikia akashangaa pia watu wanaobishania mungu anasema kama unataka mungu wako aonekane toa sadaka !kuhusu swala la nchi inamiaka hamsini lakini bado omba omba kila mtu alisikitika!ukifikiria mku wa nchi anasema asipoomba nje uchumi hauendi!
 
Back
Top Bottom