Maoni ya madaktari baada ya Hotuba ya JK!-Ole wako ukiugua..utakiona!

IsangulaKG

JF-Expert Member
Oct 14, 2010
706
386
"Yani mie sahz nataka pesa tu,aniboreshee maslahi yangu,wagonjwa wakilala 60 kitanda kimoja shauri yao,na kama vifaa havipo cjigusi,hata mtindo wa kuazma bp machne wodi ya jirani naacha,yani ntatoa huduma kulingana na vitu vilivyopo mahali nilipo,hata kumconsult chf kwa kutumia vocha zangu mwisho,kumchangia mgonjwa pesa akanunue dawa ndo mwisho,yani mtanisamehe "wana ethics",kwa sasa ndipo nilipofikia,simgusi mgonjwa wa hep. B hadi nilipiwe chanjo,na leo tu m1 kafariki wodn,SIJITOI KWA AJILI YA WANANCHI TENA,hawana shukrani,hawapo tayari kujitetea,NIMECHOKA!!!"

"BeTa hata cjamckiliza...cuz naic nshakerek wt his pseudo-promise"

"eti amegawa chandarua kila kitanda.. ndo cha kujivuna?"

"Kudadadekiii bora ule mstari wa mbayuwayu kuliko hay matakataka yanayosemwa leo,kwanini haya madudu hakuyasema ijumaa walahi hadi mochwari na dispensary zingegoma kaaahhh........"

"najickia kama nimejinyea kwa jinc anavyoongea"

"Mh Rais hajataja KABISA suala la KUBORESHA sekta ya afya. Hatak watu wajue kwamba tuligoma ili wakija hospt wapate huduma bora, wapate dawa, wasilale wawili watatu kwa kitanda nk..

"Anataka watu watuoneje? Anajenga hisia gani kwa waTz?"

" Bora nyie wenye moyo wa kumsikiliza,mie keshaniboa zamaniii"

"Ngoja nimalizie haka ka proposal kangu... labda katantoa. Wakati huo huo...niendelee kuhangaikia kilimo kwanza. !"

"If this is what his speech is all about, i dnt knw what i feel... Bt its real back to square one!!!"

"Baada ya kusoma hii, nimeamua kufanya jambo!

How to 'kill' mwananchi!
www.jamiiforums.comSalamu baba yangu, Natumaini U mzima baba yangu mpendwa' Kijana wako naendela kutafuta Maisha huku mjini na usiwe na wasiwasi kwani barua yako kuhusu kibanda chako cha majani"

"Leo ndio nimethibitisha kuwa ni kichwa cha nazi.Kama ni chemistry basi leo nilikuwa nafanya confirmatory test"

"nilishasema toka mwanzo kuwa huyu jamaa haaminiki. Kimsingi udaktari umeshuka thamani sana kwani wananchi wao wanajali huduma tu. Ni bora hata kusomea uselemara"

"what if all Medical Doctors in public sector resign: only to come back after all the requirements are met?"

"ila naanza kuiona tanzania halisi, maana inawezekana vipi mtu mwenye akili timamu a vote for such a person? That means 60% of tanzanians (who voted for him) are not well upstairs? A president anahutubia watanzania mabox na mapakacha? So disappointed today...sijui kama huyu jamaa huwa anajisikiliza baada ya hotuba zake?"

"Jamani mwenye dili Windhoek,Gabarone,Kigali atuambie basi.Maana unachukua akili za kwako na unajumlisha na akili za mbayuwayu unapata akili zaidi"

"Yaani baba ridhiwani kweli disaster! Yaani mazingira bora ya kufanyia kazi ameliweka kwenye ' na madai mengine mengine'' Najaribu ku internalize hasira zangu, na hiyo ni mbaya.... I AM SUICIDAL!!!!!"


My take: kama nilivyoandika katika makala yangu ya salamu kwa mjomba daktari. Madaktari wa nchi hii wanaonewa na kudhalilishwa sana na bahati mbaya sisi wananchi hatuwapi support wakati wanapohitaji. Ubinafsi wetu wa kujali tiba tu bila kumjali mtoa tiba....unasababisha morale ya madaktari kushuka na tutarajie huduma mbovu zaidi. Kutokana na Elimu yangu ya saikolojia. Madaktari wana HAKI ya kujisikia hivyo hasa baada ya bwana mkubwa kubwabwaja katika hotuba yake na wazee!

Watanzania tutavuna tulichokipanda!

NB: Maoni mengine yameachwa kutokana na ukali wa maneno japo ni HALI INAYOELEWEKA kwa mtu katika kuonyesha hisia zake halisi baada kudhurumiwa haki yake ya msingi!



OLE WAKO UUGUE MTANZANIA!

Shukrani kwa Dr. MMIK, CJSA,NINY, POLK kwa kuniwezesha kupata maoni haya
 
Mkuu, sisi waswahili ni wapuuzi Saba, tunasahau na tunaona huduma ya afya ni favour,
Mkuu, Kama hakuna gloves Usimguse mgonjwa! Akanunue mwenyewe!!:mad:
 
sijui niseme nini, nyinyi mnao. . . . . . . . . . . . . kikwete wenu,
baada ya kufanikiwa kuipaisha rushwa kuwa chanzo mbadala cha mapato ya waserikali, wanaipigia promo hii kitu, tushindwe kuhoji kodi zetu. ulale pema peponi komredi horace kolimba.
 
@Jogi na @Bigirita, yani tutarajie tusiyoyategemea, bahati mbaya wao (wakubwa) wana ubia na India
 
Unahitaji kuwa na Moyo wa Mwendawazimu ili kuweza kumsikiliza kisha ukamuelewa JK tofauti na hapo mhhhhhhhh!!!!!!!!!!!!
 
...ukitaka kumdhamin kichaa lazima na wewe ujitoe akili kwanza ndo uweze kudhamini...madaktari poleni sana kwa kumwamini huyo m.b.a.y.u.wa.i,najua nyinyi ni wasomi mtajua jinsi ya kufanya...
 
Ee Mola nisaidie nisiugue serious mpaka mambo yatakapokuwa shwari.
Mwenye Nchi kapandisha hasira za matabibu, na machungu tutayapata wananchi
 
Kama haya ndiyo yaliyo vichwani mwa madaktari baada ya hotuba ya Kikwete, basi tunapaswa kuomba Mungu awatulize mioyo na akili zao, la sivyo, tutarajie maafa ya kimya kimya
 
Wapendwa madocta wangu, mimi nimesikiliza hotuba ya mkuu wa kaya, lakini ikani-boa nikabadilisha channel. Kwa ujumla amewadhalilisha sana, na mimi nililitegemea hili. Lakini napenda kuwaambia ukweli makosa mliyoyafanya. Mpende msipende suala hili limekwnda kisiasa japo nyie hamkutaka liende hivyo, ni jambo ambalo huwezi kuliepuka. Chadema waliwaomba kuungana nanyi ili suala hili lisukumwe na nguvu ya umma, mkakataa, sasa propaganda za ccm zimewafanya wananchi wawageukeni. Ni Chadema pek yao nchi hii walio na uwezo wa kuuamsha umma uende kinyume na utawala huu dhalimu, lakini nyie mkapuuza mkadhani nyie wenyewe mnaweza, sasa mmegeukwa na hakuna tena mgomo mtakaoufanya wananchi wawaelewe kwani tayari sumu imesha mwagwa. Utawala huu wa sasa hauwezi kwenda bila kutishiwa nguvu ya umma, sasa nyie mmefanya ujinga wa mwaka, mnatakiwa mjilauku wenyewe, na sasa fanyeni tu kazi na wala msijaribu kufanya uzembe watu wafe kwani laana itazidi kuwaandama. Fanyeni kazi kwa bidii msubiri mpaka 2015 tutakapobadili uongozi wa nchi hii. HAKIKA UKOMBOZI UNAKUJA TANZANIA, SI KWA MIGOMO BALI KWA SANDUKU LA KURA. WATU WAMEKWISHACHOKA NA CCM, NA JESHI LA VIJANA WA NCHI HII LINAKWENDA KUIBADILISHA NCHI HII MILELE. POLENI LAKINI JIPENI MOYO. THE FREEDOM IS COMING TOMORROW
 
Kama haya ndiyo yaliyo vichwani mwa madaktari baada ya hotuba ya Kikwete, basi tunapaswa kuomba Mungu awatulize mioyo na akili zao, la sivyo, tutarajie maafa ya kimya kimya

Peter muombe Mungu ampe akili za ziada rais wako na siyo madaktari. Uwezo wa JK ndio umeishia hapo. Yeye anaandikiwa na kuyasoma kama yalivyo, hujamsikia akishindwa kutamka "RADIOGRAPHER", et rais, shame on you mk..w..e..r...e.....!!!
 
Unajua ata kabla ya kuanza kuongea nilishajua atakachokuwa anaongea!
Cha msingi wazee wetu walikula good time msosi pamoja na vinjwaji kama sikosei maana nilimwona mmoja akinyuka Coke kwa mbwembwe!
 
Kweli JK ni Dokta katika siasa, maana huu mchezo unaonyesha JK ni clever na madaktari ndo wasiofikiria. Kweli, public opinion sasa iko agaist the doctors, na hii itawaumiza siku zote. Nilisikia jana ITV mtu mmoja akisema maoni yanaonyesha wananchi wanataka kuanza kuwakata madokta mikono iwapo wataendelea na mgomo.
 
Back
Top Bottom