Maoni ya John Mnyika juu ya Kuvunjwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini

Kweli Mnyika umenena, waanze kwanza na mzee wa vijisent kama kweli wana nia ya dhati
 
Bwana Mdogo Mnyika umeshasema uamuzi wa Bi kiroboto ni sahihi na hiyo inatosha haina haja ya kueleza sana. Chadema sisi ni wepesi wa kuchanganua na kupambanua mambo. Yuko wapi January Makamba? kelele zake kumbe alikuwa anamuwinda Msukuma wa sengerema

HIZI KWENYE red NDIZO SIASA Chakavu na za kujaza matumbo. Hasikii wala haoni baada ya kutimiza ndoto zake za kupata ulaji na huo ndio mwisho wake.
 
Embu tueleze wewe Mnyika kwamba madudu haya yaliyotokea kwenye kamati yako mpaka kuvunjwa ulikuwa hujui au ulikuwa unasikilizia upepo upite.Kwa akili ya kawaida Mnyika mtu kama wewe Watu lazima wanajua ungechukulia ujiko wa kuripua maufisadi yaliyomo.Sasa kukaa kwako kimya ni dhahiri Unajua kinachoendelea kwenye hiyo kamati yenu iliyovunjwa.
 
Walimficha na walikuwa wanamzunguka walijua tu angelipuka fasta....na ameshalipuka sasa hizi blabla zingine ni utoto tu naamini ukikua utaacha labda km umetumwa na zitto
 
Embu tueleze wewe Mnyika kwamba madudu haya yaliyotokea kwenye kamati yako mpaka kuvunjwa ulikuwa hujui au ulikuwa unasikilizia upepo upite.Kwa akili ya kawaida Mnyika mtu kama wewe Watu lazima wanajua ungechukulia ujiko wa kuripua maufisadi yaliyomo.Sasa kukaa kwako kimya ni dhahiri Unajua kinachoendelea kwenye hiyo kamati yenu iliyovunjwa.

Mnyika ni mla rushwa mzuri tu na hukuwahi hata siku moja kumsikia akiishutumu TANESCO. Na hata kwenye hotuba yake ya kambi ya upinzani ukiisoma kinaga ubaga utaona mnyika ana nufaika na huu mchezo wa Muhando, iko wazi wala haihitaji digrii ya chuo kikuu ili ujue mkuu
 
Mnyika ni mla rushwa mzuri tu na hukuwahi hata siku moja kumsikia akiishutumu TANESCO. Na hata kwenye hotuba yake ya kambi ya upinzani ukiisoma kinaga ubaga utaona mnyika ana nufaika na huu mchezo wa Muhando, iko wazi wala haihitaji digrii ya chuo kikuu ili ujue mkuu
Aamewashika vibaya eh kwenye 0713... na bado mtaeleweka tu.
 
icon1.png
Maoni ya John Mnyika juu ya Kuvunjwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini


 
Huyu mnyika asipozimwa mapema anaweza kuwatishio kwenye uraisi wangu huko mbeleni!
Tutakupoteza mkuu!
 
Nikuelewa kamanda Mnyika...japokuwa kuna mpuuzi humu kadai eti CHADEMA tunadandia hoja kwani ninyi magamba tangu lini mlikuwa na hoja ya kupinga ufisadi? Pia hata sisi ni watz na tuna haki ya kutoa maoni juu ya mambo yanayotumbisha kama taifa nadhani mnajisahau kisa mmeunda serikali na magamba yenu kwamba mtatupangia ya kuongea. Acheni upuuzi wana-ccm nchi inaenda mrama kaeni chini na mjue la kumshauri J.K tena ikiwezekana ahakikishe vikosi vya usalama vinafanya kazi 24.Sasa sisi CHADEMA hatupendi namna nchi inavyoendeshwa kijinga!
 
Ee Mungu nalia mbele yako, Taifa langu Tanzania kila kukuchapo leo afadhali na jana. Taifa langu hii limekuwa kiwanja cha mpira wa wahuni hakuna jipya humu nimiendelezo ya kutufilisi. Ifike wakatati Ee Mungu wetu ututete na kuwalipizia kisasi wale wanaofanya ufedhuli huu. Uyafute majina yao katika vitabu vyako vya rehema na kuyaandika majina yao, katika vitabu vya hukumu ya jehanum wasione raha wao wala watoto wao. Uwalipizie mara elfu matendo yao maovu juu ya Taifa hii. Tumelia hawakuona huruma, tumeteta hawakusikia wala kututizama, Taifa limevamiwa na viwavi jeshi, kila kitu kinatafunwa, hakuna vinavyo sazwa hata kwa ajili ya vizazi vijavyo, Ee Mungu tukomboe macho yetu tunayaelekeza kwako.


Mpendwa maombi ya visasi Mungu hapatilizi, pia angalia sana unalaani hata kizazi cha hao wala rushwa hawana hatia na hata kama wanazo hakuna Mtanzania atakayepona. Hata wewe ni mwizi sijui kama unajua sasa ANGALIA HII LAANA SI KWA VIONGOZI HATA WEWE; Hapo ndipo ninapompenda MUNGU.
 
Safi sana kamanda, tutaifikia tu nchi ya ahadi.... Nadhani tutaongea mengi kwenye Sangara inayokuja!
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Credibility ya bunge ilisambaratika siku ile CCM walipoamua kuteua spika kwa kuangalia jinsia; "sasa ni zamu ya wanawake!!"
  • Bunge linaakisi kinachoendelea ndani ya serikali; wabunge wengi wametoka kwenye nafasi mbali mbali za utendaji serikalini ndo wakaingia bungeni! Yale waliyokuwa wakiyatenda huko serikalini, wanaendelea kuyatenda hata wakishakuwa wabunge.
  • Inaaminika kuwa "motive" kubwa ya watu wengi kuingia Bungeni ni ili waweze kushiriki kwenye "bonanza" ya rushwa; wakiwa wamechoka kuwa watazamaji wanapokuwa watendaji huko serikalini.
  • Bunge limepitisha sheria nyingi kwa kuhongwa hasa wajanja wakichomekea vipengele wanavyojua jinsi watakavyovitumia. Wabunge wakikaribishwa vikao vya ndani vyenye maposho manene manene na "kueleweshwa" sheria zinazotarajiwa kutungwa.
  • Hivi karibuni SSRA, Serikali na mifuko ya hifadhi ya jamii wamekaa na kutunga sheria ambayo inahakikisha fedha mifuko ya jamii zinakuwa kichaka cha serikali kuchezea "mdako" wa kuchota fedha za watu bila kujali; huku SSRA wakidai lengo ni kuboresha mafao; Bunge lilipitisha bila kuhoji hadi hapo wanaharakati walipowafungua macho wananchi.
Bunge hili sasa hivi ni muhuri tu, linaweza kutumiwa na yeyote mwenye maslahi yake bila kujali. Halina heshima yoyote mbele ya macho ya wananchi.

Above all they should know kwamba mwisho wa ubaya ni aibu! No stone will be left unturned....Ufisadi unahesabu muda wa maisha yake hapa Tanzania...Its so sad hata wale ambao walitakiwa kujilinda nafsi zao wakati huu tulipo jangwani kuelekea kanani hawataiona nchi ya ahadi kwakukumbuka masufuria ya nyama ya wamisri....

When it comes to ufisadi sina chama dini kabila rangi ama race kila nafsi itendayo ufisadi lazima ife....Ame the preacher still preaching the gospel kama hamuamini maneno yake basi aminini matukio!

Mnyika you are full protected hakuna atakaye kugusa na atakayejaribu atakutana na nguvu ambayo hajawahi kupata kuiona tangu ajitambue kuwepo kwenye hii dunia! Thanks for walking the talk!
 
Mara nyingi watu hupenda kutumia huu msemo wa ukiongea na kichaa nawe unakuwa kichaa tena Mshenzi. Sasa wananchi ifike mahali muelewe si kila hoja kujibu au kuongea, hata ukikaa kimya nayo ni majibu. Tumieni uwezo wenu kuimarisha chama na kuwaelimisha wananchi vilvyonyuma ya PAZIA na si kuhangaika na wale washenzi .
 
Pia ikumbukwe siku zote simba mwenda Pole ndiye mla nyama. Na debe tupu haliachi kuvuma. Tujipange Watz kutoka katika hawa wachache ambao wanasahau Yote yana mwisho. Pia Tuombeni Toba kwa ajili ya hili Taifa na wananchi, Pia tumwombe Mungu atuongoze tuombe vipi kwa Taifa hili na si kulalamika na kulaani TUNAJILAAAANI WENYEWE. Hakuna hata mmoja aliyesimama kwenye kinachomstahili wale wanaojitahidi wanauwawa je kwa Damu hiyo tutapona WAPI?
 
Back
Top Bottom