Ufunuo wa Yohana
JF-Expert Member
- Oct 9, 2007
- 318
- 67
Mimi kama Mtumishi,
Kwa Muheshimiwa Rais John Pombe Magufuli, haya ndiyo niliyofunuliwa na nikuombe unitegee sikio.
Ulitangazie Taifa zima kuwa katika hali ya maombi ya nchi nzima na Maombi haya yawe ya wiki moja na ya watu wote wenye mapenzi mema na nchi yao na yawe ya kufunga walau saa 12 kila siku na kilele chake iwe siku ya tarehe 5 Novemba 2016 mwaka mmoja baada ya kuapishwa kwako kitaifa yafanyike Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Pengine utaniuliza ni Mungu yupi tutakuwa tunamuomba watu wote hawa? Jibu ni Mungu wetu wa Taifa letu, Mungu wa Watanzania wote, tunayemuimba katika wimbo wetu wa Taifa…Mungu Ibariki Tanzania….. Ili Mungu huyu atubariki lazima Mh Rais kila mmoja wetu tumpe nafasi ndani ya mioyo yetu, tumuombe kwa nguvu zetu zote.
Maombi yetu yawe haya (Prayer Points)….Pengine na wewe utapenda kuongezea …ruksa.
1) Kumshukuru Mungu wetu kwa yote aliyotuwezesha kwa huu mwaka mzima 2016, siyo siri Mh Rais sasa hivi heshima ya Mtanzania inaonekana, tunaheshimiana maofisini, mitaani, nikupe mfano tu mmoja nilikuwa nikishughurikia transfer ya hati yangu kwa miaka 5 sasa kila nikienda naambiwa uje baada ya wiki 3 mpaka nilikata tamaa. Nimeenda mwezi wa sita mwaka huu kwanza nilipofika nilipewa kiti na wahudumu wale wale na kusikilizwa haraka sana. Na kila aliyekuwa akipita ananiuliza “Mzee umesikilizwa” na siku hiyo hiyo hati ilipelekwa kwa kamishna na kusainiwa na nikaondoka nayo, heshima ipo sasa hivi. Tumshukuru huyu Mungu aliyekutia nguvu Mh. Rais.
2) Maeneo mengi katika nchi yetu yanaingia katika msimu wa kilimo, hivyo tumuombe Mungu wetu alete mvua ya kustawisha mazao yetu kwa wingi zaidi ili tuweze kuuza nje ya nchi bidhaa za mazao nakupata kipato kikubwa kwa maendeleo ya wananchi wako wa Tanzania. Mungu huyu ninaimani atafanya na bila kuchelewa. Kilimo wanategemea watanzania wote.
3) Hofu ya Mungu huyu wetu, itufunike Watanzania wote ili dhuruma, rushwa, vurugu, mateso, wizi, yatoweke katika jamii yetu, watu waishi kwa amani na nchi yetu iwe kisiwa cha amani kweli kweli. Mh Rais watu wako wakiwa wacha Mungu ndipo itakuwa rahisi sana kuwaogoza na kufikia malengo ya maendeleo uliyoyaweka kwa watu wako. Najua unania njema na ya dhati kwa watu wako.
4) Kutokee wawekezaji ndani na nje ya nchi walio na nia njema wanaojali maendeleo ya watu wako ili tuifikie adhma yako ya kuwa Tanzania ya viwanda. Kila kijiji kiwe na kiwanda cha kuyaongezea thamani mazao yanayopatikana na kuuza kwa faida katika sako la ndani na nje ya nchi.
5) Mungu aibue vipaji katikati ya watu wako, Watanzania wenye kufikiria na kubuni mipango ya kuendeleza taifa lao. Vijana shupavu wenye mapenzi mema na nchi yao waonekane na kulitumikia taifa lao kwa moyo safi.
6) Tukemee unyonge ndani ya watu wako, wasijione kuwa hawawezi kila kitu na kuanza kulialia tu, bali Mungu huyu atujaze ujasiri wa kuwa tunaweza maana tunaye Yeye atutiaye nguvu na yuko upande wetu tutaibuka washindi katika mambo yote. Mh Rais siyo utani tukimuweka Mungu wetu juu yetu uchumi utakua kwa Zaidi ya 100% kila mwaka. Amini haya Mh. Rais
7) Mihimili yote yaani Bunge, Mahakama na Serikali zifanye kazi kwa ufanisi mkubwa na kwa hofu ya Mungu zikilenga kuleta maendeleo ya watu wako
8) Vyama vote vya siasa vihubiri maendeleo, upendo na amani kwa Watanzania wote, Mungu awafunulie wanasiasa wote kuona katika jicho la Kitaifa Zaidi, tujiviunie Utanzania wetu.
9) Jeshi letu ambalo mimi binafsi huwa nalimani sana nalo lipewe mbinu mpya za kuweza kupambana na maadui wetu wa sasa yaaani Ujinga, Maradhi na Umaskini. Hawa ndiyo maadui wetu kwa sasa Mh. Amiri Jeshi Mkuu, Mungu awape mbinu za kisasa kupambana nao hawa.
Nakuandikia mafunuo haya Mh Rais nikijua kuwa wewe ni Jemedari wetu, kiongozi wetu, uliye mstali wa mbele katika vita. Na naamini ukiwaongoza watu wako katika kumulilia huyu Mungu wetu hatakawia kushuka na kutuletea majawabu ya yale tumemuomba, napengine siku ya kilele hicho ambacho kitafanyika uwanja wa taifa akashuka kwa mfano wa mvua,, amini haya Mh. Rais.
Hatuwezi kubarikiwa kwa kuimba tu Mungu ibariki Tanzania bila ya kumtengea siku maalumu ya kuzungumza naye kumueleza shida zetu zinazotukabili. Nilazima tumtambue Mungu wetu na tuweke utaratibu wa kumshukuru na kumuomba walau mara mbili kwa mwaka kama taifa.
Ukisimama katika haya Mh. Rais nchi itaendelea kwa kasi ya ajabu mno mtu wa Mungu. Lakini ni lazima ukubali kuuwatesekea watu wako na pengine ukubali kuitwa mwendawazimu,,haya ndiyo mambo ya Mungu. Taifa lazima lijengwe kupitia hofu ya Mungu ili tuendelee.
Watangazie Watanzania wote, viongozi wa dini zote juu ya maombi ya wiki nzima na kilele chake iwe siku ya tarehe 5/11/2016 uwanja wa Taifa, kitaifa, na kila mkoa utaadhimisha katika viwanja vya mkoa husika na ikikupendeza hata vijijini.
Haya ndiyo niliyofunuliwa mimi kama mtumishi kwa Taifa lako, Uongozi wako, na watu wako yaani Watanzania.
Ahsante sana kwa kunitegea sikio.
Mungu Ibariki Tanzania.
Kwa Muheshimiwa Rais John Pombe Magufuli, haya ndiyo niliyofunuliwa na nikuombe unitegee sikio.
Ulitangazie Taifa zima kuwa katika hali ya maombi ya nchi nzima na Maombi haya yawe ya wiki moja na ya watu wote wenye mapenzi mema na nchi yao na yawe ya kufunga walau saa 12 kila siku na kilele chake iwe siku ya tarehe 5 Novemba 2016 mwaka mmoja baada ya kuapishwa kwako kitaifa yafanyike Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Pengine utaniuliza ni Mungu yupi tutakuwa tunamuomba watu wote hawa? Jibu ni Mungu wetu wa Taifa letu, Mungu wa Watanzania wote, tunayemuimba katika wimbo wetu wa Taifa…Mungu Ibariki Tanzania….. Ili Mungu huyu atubariki lazima Mh Rais kila mmoja wetu tumpe nafasi ndani ya mioyo yetu, tumuombe kwa nguvu zetu zote.
Maombi yetu yawe haya (Prayer Points)….Pengine na wewe utapenda kuongezea …ruksa.
1) Kumshukuru Mungu wetu kwa yote aliyotuwezesha kwa huu mwaka mzima 2016, siyo siri Mh Rais sasa hivi heshima ya Mtanzania inaonekana, tunaheshimiana maofisini, mitaani, nikupe mfano tu mmoja nilikuwa nikishughurikia transfer ya hati yangu kwa miaka 5 sasa kila nikienda naambiwa uje baada ya wiki 3 mpaka nilikata tamaa. Nimeenda mwezi wa sita mwaka huu kwanza nilipofika nilipewa kiti na wahudumu wale wale na kusikilizwa haraka sana. Na kila aliyekuwa akipita ananiuliza “Mzee umesikilizwa” na siku hiyo hiyo hati ilipelekwa kwa kamishna na kusainiwa na nikaondoka nayo, heshima ipo sasa hivi. Tumshukuru huyu Mungu aliyekutia nguvu Mh. Rais.
2) Maeneo mengi katika nchi yetu yanaingia katika msimu wa kilimo, hivyo tumuombe Mungu wetu alete mvua ya kustawisha mazao yetu kwa wingi zaidi ili tuweze kuuza nje ya nchi bidhaa za mazao nakupata kipato kikubwa kwa maendeleo ya wananchi wako wa Tanzania. Mungu huyu ninaimani atafanya na bila kuchelewa. Kilimo wanategemea watanzania wote.
3) Hofu ya Mungu huyu wetu, itufunike Watanzania wote ili dhuruma, rushwa, vurugu, mateso, wizi, yatoweke katika jamii yetu, watu waishi kwa amani na nchi yetu iwe kisiwa cha amani kweli kweli. Mh Rais watu wako wakiwa wacha Mungu ndipo itakuwa rahisi sana kuwaogoza na kufikia malengo ya maendeleo uliyoyaweka kwa watu wako. Najua unania njema na ya dhati kwa watu wako.
4) Kutokee wawekezaji ndani na nje ya nchi walio na nia njema wanaojali maendeleo ya watu wako ili tuifikie adhma yako ya kuwa Tanzania ya viwanda. Kila kijiji kiwe na kiwanda cha kuyaongezea thamani mazao yanayopatikana na kuuza kwa faida katika sako la ndani na nje ya nchi.
5) Mungu aibue vipaji katikati ya watu wako, Watanzania wenye kufikiria na kubuni mipango ya kuendeleza taifa lao. Vijana shupavu wenye mapenzi mema na nchi yao waonekane na kulitumikia taifa lao kwa moyo safi.
6) Tukemee unyonge ndani ya watu wako, wasijione kuwa hawawezi kila kitu na kuanza kulialia tu, bali Mungu huyu atujaze ujasiri wa kuwa tunaweza maana tunaye Yeye atutiaye nguvu na yuko upande wetu tutaibuka washindi katika mambo yote. Mh Rais siyo utani tukimuweka Mungu wetu juu yetu uchumi utakua kwa Zaidi ya 100% kila mwaka. Amini haya Mh. Rais
7) Mihimili yote yaani Bunge, Mahakama na Serikali zifanye kazi kwa ufanisi mkubwa na kwa hofu ya Mungu zikilenga kuleta maendeleo ya watu wako
8) Vyama vote vya siasa vihubiri maendeleo, upendo na amani kwa Watanzania wote, Mungu awafunulie wanasiasa wote kuona katika jicho la Kitaifa Zaidi, tujiviunie Utanzania wetu.
9) Jeshi letu ambalo mimi binafsi huwa nalimani sana nalo lipewe mbinu mpya za kuweza kupambana na maadui wetu wa sasa yaaani Ujinga, Maradhi na Umaskini. Hawa ndiyo maadui wetu kwa sasa Mh. Amiri Jeshi Mkuu, Mungu awape mbinu za kisasa kupambana nao hawa.
Nakuandikia mafunuo haya Mh Rais nikijua kuwa wewe ni Jemedari wetu, kiongozi wetu, uliye mstali wa mbele katika vita. Na naamini ukiwaongoza watu wako katika kumulilia huyu Mungu wetu hatakawia kushuka na kutuletea majawabu ya yale tumemuomba, napengine siku ya kilele hicho ambacho kitafanyika uwanja wa taifa akashuka kwa mfano wa mvua,, amini haya Mh. Rais.
Hatuwezi kubarikiwa kwa kuimba tu Mungu ibariki Tanzania bila ya kumtengea siku maalumu ya kuzungumza naye kumueleza shida zetu zinazotukabili. Nilazima tumtambue Mungu wetu na tuweke utaratibu wa kumshukuru na kumuomba walau mara mbili kwa mwaka kama taifa.
Ukisimama katika haya Mh. Rais nchi itaendelea kwa kasi ya ajabu mno mtu wa Mungu. Lakini ni lazima ukubali kuuwatesekea watu wako na pengine ukubali kuitwa mwendawazimu,,haya ndiyo mambo ya Mungu. Taifa lazima lijengwe kupitia hofu ya Mungu ili tuendelee.
Watangazie Watanzania wote, viongozi wa dini zote juu ya maombi ya wiki nzima na kilele chake iwe siku ya tarehe 5/11/2016 uwanja wa Taifa, kitaifa, na kila mkoa utaadhimisha katika viwanja vya mkoa husika na ikikupendeza hata vijijini.
Haya ndiyo niliyofunuliwa mimi kama mtumishi kwa Taifa lako, Uongozi wako, na watu wako yaani Watanzania.
Ahsante sana kwa kunitegea sikio.
Mungu Ibariki Tanzania.