Status
Not open for further replies.
Hahahahaaaaa, mkuu serikali yako haitakuwa na mtumishi wa umma. Wataacha kazi wawe wananchi wa kaimwaida ili uwalipe hayo mamilioni.

Ukumbuke kuondoa kinga ya raisi kuto kushitakiwa, maana nao ni binadamu tu, as they make mistakes too.
 
Mh. Rais wa jamhuri ya Muungano-Tanzania ,
Salaam!

HONGERA KWA KAZI.

MAPENDEKEZO KUHUSU GESI ASILIA kutoka MTWARA.
-serekali iweke mkakati mkubwa kuwezesha gasi hii ITUMIKE kwenye MAGARI-

-Hii itainua sana uchumi wetu kwani licha ya gharama za gesi asili
kua ndogo (kama 1/2) lkn pia pesa itabakia nyumbani!
-Inaweza kuimarisha thamani ya shilingi yetu.
-itaongeza ajira
-serekali haina gharama kwani ikishaweka sera na sheria utekekezaji unabakia kwenye sekta binafsi.
-serekali itoe ELIMU , ihamasishe , iondoe kodi ktk vifaa vya kubadili magari yaweze kutumia gesi.
-ipunguze kodi kwa magari yanayoagizwa yanayotumia gesi
- mapato ya serekali yatakua makubwa sana kwani serekali ndio inamiliki gesi
(Angalia mawazo ya wataalam wa DIT)
Nitabaki kua mzalendo daima.
Asante!
 
Maoni ushauri kwa Dr. Magufuli inaonesha jinsi gani baadhi yetu Watanzania tunavyofikiri kwamba Rais ndiye kila kitu katika nchi hii, inasemekana Muhimbili kumeoza pamoja na juhudi zote za Rais hakuna mafanikio, mashine zimehujumiwa za kupimia wagonjwa, hiyo ni kazi ya Rais, haya kuna ujangili ni kazi ya Rais? mwandishi hakuna mahali popote anapopongeza juhudi za Rais wa awamu ya tano alizotekeleza kwa kipindi kifupi alichokaa madarakani, ana mlolongo wa mahitaji ambayo ikibidi Rais Magufuli ayatatue anahitaji kukaa madarakani zaidi ya miaka ishirini, kumbuka matatizo hayo ni malimbikizo ya miongo minne kwa awamu nne zilizopita, huenda ikahitajika miongo minne kuondokana na changamoto zote hizo za mwandishi wa makala ya ushauri kwa Rais Dr. Magufuli, pia ni muhimu Watanzania wote kuwa pamoja wakaungana kutatua hizo changamoto badala ya kumlenga Rais peke yake. Zanzibar kuna tatizo lakini linakuzwa sana kisiasa, kumekuwa na maridhiano na yalifanya kazi lakini humo ndani katika utekelezaji kunatokea mkanganyo kwa sababu ya kukiuka makubaliano ya awali upande mmoja kutaka zaidi kinyume Cha makubaliano ni shida za Kiafrika. Ni vema kwa Watanzania wote tunapochangia mawazo kuhusu mstakabali wa nchi yetu tujifunze kuzungumzia hoja zinazojenga mawazo yetu kama raia ili tushiriki katika kutatua mlolongo wa changamoto alizoainisha mshauri kwa Dr. Magufuli namna ya kuendesha nchi, badala ya kumlenga Rais peke yake. Tuna utamaduni uliojengeka miongoni mwa Watanzania kutothamini nchi yetu ndiyo sababu kuna uhamasishaji wa uzalendo na kuipenda nchi yetu, lakini bado kuna baadhi yetu hatuamini kama Tanzania ni kwetu na tunapaswa kuilinda bila kujali itikadi ya mtu.
Tubadilike.
 
Tujiulize kama wewe ungekuwa Raisi leo ungefanya nini kama nchi ilivyo leo. Mimi ningefanya hivi kwa uzoefu wangu na nina Imani kabisa nchi ingebadilika na maendeleo ya kiuchumi yangeonekana. Hivi vitu nitavitaja kwa umuhimu kwamba ninaanza na nini. Hivyo namba hapo chini ni kama hatua moja moja



  • Kwa kutumia ofisi ya CAG na kampuni za consulting za kimataifa kama (Deloitte, Ernst & Young (EY), KPMG and Pricewaterhouse) wafanye uchunguzi kwenye idara zote za serikali na watoe report ya kuongeza ufanisi mfano kuunganisha idara, kuongeza technologia na kuangalia idadi ya wafanyakazi. Lengo ni kupunguza gharama, kuongeza ufanisi na kutoa maelezo ya kila mfanyakazi anatakiwa kufanya nini na malengo yake ni yapi. Hivyo kila mtu kuanzia katibu mkuu anakuwa na malengo ya mwaka. Hii itasaidia kila mtu kuamka na kuafanya kazi bila mpangilio maalumu na kuongeza ufanisi kazini. Vilevile nitajua serikali ikoje kwa urahisi na mapungufu. Kwenye hili hakuna siasa.
  • Nitatoa uhuru kwa vyombo vya habari na wanasiasa wawe na uwezo wa kufanya mikutano wakati wowote bila kujali. Maendeleo hayajali maneno. Lakini demokrasia inaleta maendeleo. Kutakuwa na demokrasia ya ukweli
  • Mfumo wa shule kuanzia msingi mpaka form six kubadilika. Nitabadilisha mfumo wa sasa wa elimu wote. Lengo kubwa ikiwa kushindanisha watoto wetu hasa kwenye technologia. Hivyo nitahimiza technoologia iweze kutumiaka zaidi kwenye mashule na tutaongeza walimu wa technologia ngazi zote. Vilevile nitaomba misaada kutoka kwa waziri mkuu wa India, US na kwenye foundation kama Bill gate foundation kuweza kusaidia kuweka technologia kwenye madarasa. Lakini sio hilo tu nitaomba watuwekee utaratibu ili wahitimu wetu waweze kujifunza software mbalimbali ili waweze kufanya kazi kimataifa hata wakiwa Tanzania. Vilevile nitaongea na kampuni za software mbalimbali kama SAP ya German, Oracle na Cisco za USA kutusaidia kwenye hili. Kuna vitu virahisi sana mfano simu nyingi ni computer tayari ina maana kukiwa na data free basi unaweza kutafuta simu za bei rahisi zigawe kwa kila mtoto na kuweka vitabu, lecture za vyuo na kuunganisha n ahata na vyuo na shule mbalimbali duniani. Mtoto wa Tanzania anaweza kufanya homework yake akaipiga picha na mwalimu wa kujitolea ambaye yuko India anaweza kusahihisha hii inawezekana kama tunafikiria vizuri. Haya ni mambo ya kuongeza tu haina maana tusiwe na walimu lakini ni mfano tu.
  • Nitawekeza kwenye kilimo. Tukasome sera za kilimo kwanza na tufanye kama sera ilivyo
  • Mapendekezo ya kubadilisha katiba hasa kwenye mambo ya kiuchumi. Nita ruhusu watu zaidi kuja Tanzania wenye vipaji kwenye technologia, diaspora wa Tanzania na NGO za maendeleo. Mimi siamini kama tuna matatizo ya kuwa wengi au tutapoteza mashamba yetu nchi yetu ni kubwa na tunahitaji watu productive. Mimi mwenyewe niko nchi ya watu kwa sasa!. Sera za kijinga za uraia nitazitoa kwa manufaa makubwa ya nchi mfano mzuri ni katiba ya Kenya. Tofauti ni kwamba kwenye katiba hii hakutakuwa na kuongeza ukubwa wa serikali kama ilivyo Kenya. Nitabadilisha mfumo wa Ardhi ili iongeze uwekezaji lakini kutakuwa na sehemu maalumu ambazo huta ruhusu uwekezaji ni za makazi tu.
  • Bodi maalumu za ushauri. Kutakuwa na bodi za ushauri kila wizara. Hizi board ni za wasomi mbali mbali na watu wenye nia nzuri na Tanzania wanashauri kwenye sera. Hakuna kulipwa ukiwa mwana bodi wala posho ni kujitolea. Diaspora wa watu wanje wenye nia nzuri wanakaribishwa.
  • Mahakama nitaiacha huru na kuwapa watakalo kuongeza ufanisi.
  • Tutatoa elimu ya Afya kwa vijana hasa chini ya miaka 30 ya mazoezi na lishe na itaingiza kwenye elimu yetu
  • Tutakuwa na Parks za kupumzikia, kukimbia, kutembea ,kucheza watoto, na kuendesha baiskeli na kila wilaya ni lazima iwe na sehemu za wazi za hivi.
  • Nitakuwa nahutubia Taifa kila mwezi
  • Nitakuwa nafanya debate na kupokea maswali kutoka kwa wananchi kila miezi mitatu. Debate wapinzania wanaruhusiwa na itakuwa kwenye TV kwenye chuo kimojawapo live. Debate za maendeleo tu.
  • Nitaanzisha mfumo wa mobile Hospital. Yaani hospitali za magari ziende kila kijiji na Dr wa meno, kisukari, watoto nk kupunguza watu kusubiri kuzidiwan na kuja hospitali za rufaa ambazo ni chache. Yaani hii itakuwa kama kinga.
  • Ningewapa bank kuu kazi ya kuhakikisha lengo lao ni pamoja na kuongeza ajira kama ilivyo USA. Hii itasaidia Bank kuweka sera za kusaidia biashara ndogondogo ambazo ndiyo waajiri
Nitatoa mengine baadae nipe yako
Safi sana
 
Kamundu hakika una maono makubwa na mapenzi makubwa kwa nchi yako, mafanikio katika nchi yoyote hutokana na mageuzi ya kifikra ya wananchi wake, sijaona popote unapoeleza ni jinsi gani utaandaa fikra geuzi kwa wananchi hawa ili wakabiliane na maendeleo stahiki yanayotarajiwa kutoka kwako kama Rais ajaye.
Mfano rahisi tu hapa kwetu Tanzania awamu zote zilizopita za uongozi, Halimashauri zilikusanya mapato na kuyatumia kwa maendeleo ya maeneo yao, ikabuniwa miradi hewa watu wakajinufaisha sana, pesa ikaonekana pia mtaani, awamu ya sasa iliona huo udhaifu ikabadilisha utaratibu ili kudhibiti mapato na matumizi hivyo pesa yote inakwenda moja kwa moja Serikali kuu, mtaani kumekauka hakuna pesa watu watakwambia hii Serikali ni mbaya Sana watu hawana pesa, lakini Serikali imedhibiti mapato yake yasichezewe na watu,haijamnyang'anya mtu biashara yake.
Wananchi hapa wanatakiwa wabadilike kifikra kwa sababu uchumi wao wa awali ulikuwa ni wa bandia.
Kamundu ndugu yangu, kila kiongozi wa nchi katika dunia hii mwenye maono huwa ana mikakati mikubwa ya kuiletea nchi yake uchumi na heshima, Donald Trump alisema America First kwa maana kila Mmarekani aiweke nchi hiyo kwanza kabla ya kitu kingine, Wachina wana ajenda ya kutaka kuwa matajiri zaidi duniani kushinda Marekani hayo ni maono kila mtu anayetaka kukamata nafasi kubwa kabisa katika nchi yake.
Tanzania tuliambiwa wakati kampeni za uchaguzi kwamba kipaumbele ni Elimu, Afya, Miundombinu, na kupambana na rushwa na ufisadi yote yanakwenda sawia.
Nafikiri kila mtu akileta mipango yake hapa patakuwa hapatoshi,isipokuwa tusaidie Serikali itimize malengo yake iliyojiwekea ya maendeleo bila ya kuibeza bila sababu, ikiwa kuna mapungufu katika utekelezaji basi eneo hilo husika likosolewe, sio kazi yote ionekane kama haifai au Rais na mawaziri hawafai sio sahihi.
Tuipende nchi yetu na tuwe wazalendo kweli kweli.
 
Kamundu hakika una maono makubwa na mapenzi makubwa kwa nchi yako, mafanikio katika nchi yoyote hutokana na mageuzi ya kifikra ya wananchi wake, sijaona popote unapoeleza ni jinsi gani utaandaa fikra geuzi kwa wananchi hawa ili wakabiliane na maendeleo stahiki yanayotarajiwa kutoka kwako kama Rais ajaye.
Mfano rahisi tu hapa kwetu Tanzania awamu zote zilizopita za uongozi, Halimashauri zilikusanya mapato na kuyatumia kwa maendeleo ya maeneo yao, ikabuniwa miradi hewa watu wakajinufaisha sana, pesa ikaonekana pia mtaani, awamu ya sasa iliona huo udhaifu ikabadilisha utaratibu ili kudhibiti mapato na matumizi hivyo pesa yote inakwenda moja kwa moja Serikali kuu, mtaani kumekauka hakuna pesa watu watakwambia hii Serikali ni mbaya Sana watu hawana pesa, lakini Serikali imedhibiti mapato yake yasichezewe na watu,haijamnyang'anya mtu biashara yake.
Wananchi hapa wanatakiwa wabadilike kifikra kwa sababu uchumi wao wa awali ulikuwa ni wa bandia.
Kamundu ndugu yangu, kila kiongozi wa nchi katika dunia hii mwenye maono huwa ana mikakati mikubwa ya kuiletea nchi yake uchumi na heshima, Donald Trump alisema America First kwa maana kila Mmarekani aiweke nchi hiyo kwanza kabla ya kitu kingine, Wachina wana ajenda ya kutaka kuwa matajiri zaidi duniani kushinda Marekani hayo ni maono kila mtu anayetaka kukamata nafasi kubwa kabisa katika nchi yake.
Tanzania tuliambiwa wakati kampeni za uchaguzi kwamba kipaumbele ni Elimu, Afya, Miundombinu, na kupambana na rushwa na ufisadi yote yanakwenda sawia.
Nafikiri kila mtu akileta mipango yake hapa patakuwa hapatoshi,isipokuwa tusaidie Serikali itimize malengo yake iliyojiwekea ya maendeleo bila ya kuibeza bila sababu, ikiwa kuna mapungufu katika utekelezaji basi eneo hilo husika likosolewe, sio kazi yote ionekane kama haifai au Rais na mawaziri hawafai sio sahihi.
Tuipende nchi yetu na tuwe wazalendo kweli kweli.

Gunga, ukisoma vizuri utagundua mipango yangu hapo haipishani na mipangilio yeyote ya serikali bali ni kuongeza ufanisi. Sababu mojawapo inayopunguza ufanisi serikalini ni kwamba viongozi hawajui vizuri wanatakiwa kufanya nini kama wewe ni kiongozi leo au mfanyakazi wa serikali unatakiwa kujua malengo yako kikazi. Kuwe na Lengo la mwaka halafu kwenye hilo kunakuwa na malengo wa mwezi na kila mfanyakazi anajua anatakiwa kufanya nini. Kweye kampuni binafsi ndiyo wanavyofanya 'goals" Na ndiyo maana nilisema cha kwanza

"
  • Kwa kutumia ofisi ya CAG na kampuni za consulting za kimataifa kama (Deloitte, Ernst & Young (EY), KPMG and Pricewaterhouse) wafanye uchunguzi kwenye idara zote za serikali na watoe report ya kuongeza ufanisi mfano kuunganisha idara, kuongeza technologia na kuangalia idadi ya wafanyakazi. Lengo ni kupunguza gharama, kuongeza ufanisi na kutoa maelezo ya kila mfanyakazi anatakiwa kufanya nini na malengo yake ni yapi. Hivyo kila mtu kuanzia katibu mkuu anakuwa na malengo ya mwaka. Hii itasaidia kila mtu kuamka na kuafanya kazi bila mpangilio maalumu na kuongeza ufanisi kazini. Vilevile nitajua serikali ikoje kwa urahisi na mapungufu. Kwenye hili hakuna siasa. "
 
Gunga, ukisoma vizuri utagundua mipango yangu hapo haipishani na mipangilio yeyote ya serikali bali ni kuongeza ufanisi. Sababu mojawapo inayopunguza ufanisi serikalini ni kwamba viongozi hawajui vizuri wanatakiwa kufanya nini kama wewe ni kiongozi leo au mfanyakazi wa serikali unatakiwa kujua malengo yako kikazi. Kuwe na Lengo la mwaka halafu kwenye hilo kunakuwa na malengo wa mwezi na kila mfanyakazi anajua anatakiwa kufanya nini. Kweye kampuni binafsi ndiyo wanavyofanya 'goals" Na ndiyo maana nilisema cha kwanza

"
  • Kwa kutumia ofisi ya CAG na kampuni za consulting za kimataifa kama (Deloitte, Ernst & Young (EY), KPMG and Pricewaterhouse) wafanye uchunguzi kwenye idara zote za serikali na watoe report ya kuongeza ufanisi mfano kuunganisha idara, kuongeza technologia na kuangalia idadi ya wafanyakazi. Lengo ni kupunguza gharama, kuongeza ufanisi na kutoa maelezo ya kila mfanyakazi anatakiwa kufanya nini na malengo yake ni yapi. Hivyo kila mtu kuanzia katibu mkuu anakuwa na malengo ya mwaka. Hii itasaidia kila mtu kuamka na kuafanya kazi bila mpangilio maalumu na kuongeza ufanisi kazini. Vilevile nitajua serikali ikoje kwa urahisi na mapungufu. Kwenye hili hakuna siasa. "
Kamundu sijakupinga kabisa ila tu kuamusha fikra za maendeleo ni shida Sana, huko Ulaya na Marekani kuna maendeleo miaka 200 iliyopita hapa ndiyo kwanza tunaanza, tunaitwa nchi zinazoendelea, walimu wa sayansi Marekani wa high school hapa wanafundisha chuo kikuu ona tofauti hiyo, mipango yako ni mizuri angalia jinsi ya kuindaa jamii utakayokuwa nayo wakati wa utawala wako ndiyo hoja yangu, Dr. Magufuli anayo mengi sana kichwani ya kuisaidia nchi hii lakini ona katika mitandao kejeli zinazoandikwa hakika zinakatisha tamaa, lakini yeye ni shujaa anaendelea na mipango yake. Hata wewe ujifunze utamaduni wa Kiafrika katika siasa.
 
Kamundu sijakupinga kabisa ila tu kuamusha fikra za maendeleo ni shida Sana, huko Ulaya na Marekani kuna maendeleo miaka 200 iliyopita hapa ndiyo kwanza tunaanza, tunaitwa nchi zinazoendelea, walimu wa sayansi Marekani wa high school hapa wanafundisha chuo kikuu ona tofauti hiyo, mipango yako ni mizuri angalia jinsi ya kuindaa jamii utakayokuwa nayo wakati wa utawala wako ndiyo hoja yangu, Dr. Magufuli anayo mengi sana kichwani ya kuisaidia nchi hii lakini ona katika mitandao kejeli zinazoandikwa hakika zinakatisha tamaa, lakini yeye ni shujaa anaendelea na mipango yake. Hata wewe ujifunze utamaduni wa Kiafrika katika siasa.

Gunga haya si mambo ya Ulaya wala USA vitu vyote nilivyosema hakuna ugumu wowote wa kufanya ukisoma vizuri. Mfamo kuruhusu uhuru ni jambo la Ulaya na USA? kuwekeza kwenye kilimo?, afya ni vitu ambayo vinafanyika. Ujue nchi nyingi za ASIA zilikuwa kama sisi miaka 35 iliyopita hizi nchi si za Ulaya. Mambo mengi magumu tunajitakiwa au hatuna tu mpangilio mzuri. Sasa Raisi kwanini ujali mitandao kama kweli unafanya kazi vizuri! huwezi kuwa unajali maneno. Maneno yanakuwa na tija pale tu ambako ni ya kweli
 
Gunga haya si mambo ya Ulaya wala USA vitu vyote nilivyosema hakuna ugumu wowote wa kufanya ukisoma vizuri. Mfamo kuruhusu uhuru ni jambo la Ulaya na USA? kuwekeza kwenye kilimo?, afya ni vitu ambayo vinafanyika. Ujue nchi nyingi za ASIA zilikuwa kama sisi miaka 35 iliyopita hizi nchi si za Ulaya. Mambo mengi magumu tunajitakiwa au hatuna tu mpangilio mzuri. Sasa Raisi kwanini ujali mitandao kama kweli unafanya kazi vizuri! huwezi kuwa unajali maneno. Maneno yanakuwa na tija pale tu ambako ni ya kweli
Inawezekana Uhuru unaozungumzwa tunatofautiana tafsiri, mtu akishindwa jambo lake hapa hatua ya kwanza anatua kuishambulia Serikali na Rais wake, kiongozi wa Chama Cha upinzani akisimama jukwaani ni kuishambulia Serikali bila hata sababu, nikafikiri anazungumzia Sera nzuri kama ulivyoainisha wewe ulipoingiza mada ya jinsi ungefanya ungepata nafasi, hayo ndiyo mazungumzo chanya, lakini mtu anaanza kuhutubia oohh Serikali hii blabla akiacha Serikali anamvaa Rais, January hadi December ni kuponda kila kitu anachokitekeleza Rais ni shida sana, unajua huko majuu mambo hayo yalifanyika toka zamani watu wameyazoea, huku kwetu kumtukana Rais au kumdhihaki ni issue inawezekana katiba ikawekwa pembeni ili kukabiliana na hali hiyo, ili kuiondoa contempt isijengeke miongoni mwa raia dhidi ya Rais. Hakika
Kamundu umenipa changamoto za kuibua hoja mbalimbali kwa faida ya nchi yetu.
Endelea na mikakati yako siku moja ukifanikiwa tukumbukane.
 
Gunga haya si mambo ya Ulaya wala USA vitu vyote nilivyosema hakuna ugumu wowote wa kufanya ukisoma vizuri. Mfamo kuruhusu uhuru ni jambo la Ulaya na USA? kuwekeza kwenye kilimo?, afya ni vitu ambayo vinafanyika. Ujue nchi nyingi za ASIA zilikuwa kama sisi miaka 35 iliyopita hizi nchi si za Ulaya. Mambo mengi magumu tunajitakiwa au hatuna tu mpangilio mzuri. Sasa Raisi kwanini ujali mitandao kama kweli unafanya kazi vizuri! huwezi kuwa unajali maneno. Maneno yanakuwa na tija pale tu ambako ni ya kweli
Watakao kupinga wapo wengi, Libya ilikuwa paradise leo nini kinatokea, nchi zetu hizi zinataka utawala wa mkono wa chuma kama China au Urusi ili watu wawe na akili, nikiangalia sana kuongoza hapa siasa iwe kidogo utendaji ufanyike kwa vitendo sio kwa maneno.
 
Watakao kupinga wapo wengi, Libya ilikuwa paradise leo nini kinatokea, nchi zetu hizi zinataka utawala wa mkono wa chuma kama China au Urusi ili watu wawe na akili, nikiangalia sana kuongoza hapa siasa iwe kidogo utendaji ufanyike kwa vitendo sio kwa maneno.
Kwa mfano wako jiulize Ghadafi yuko wapi? Sudan vipi, Tunisia hakuna mtu asiyependa freedom na ujamaa umsshidwa tayari toka 1984 Nyerere alipoondoka
 
Mh. Rais nakusifu kwa kazi nzuri unayoifanya ya kuinua uchumi ni mzalendo no mmoja pamoja na kuwabana mafisadi na wahujumu uchumi vizuri natoa ushauri ili mizania ya uchmi ikae vizuri na haraka zaidi ili iwiane na kipato cha mwananchi basi liangazie wilayani kuja vijijini kwani huku hakujaguswa kiupotefu wa fedha kwani miradi mingi haina ukaguzi wa utekelezaji na ukaguzi wa fedha mtandao unamwaga fedha ambazo zinapigwa na viongozi wa vijiji kata na wilaya na hilo likiachiwa mizani ya uchumi haitafikia badala yake wanchi watalalama hali ngumu na kuongezewa mshahara kitu ambacho sio kizuri kimapato ushauri wangu ukaguzi wa fedha kila kijiji na miradi yote ilioko vijijini kama mfuko wa maji mfuko wa umwagiliaji n.k ili kuzuia fedha zinazotumi na wachache na kuyumbisha sarikali kwa kuhitaji ruzuku wakati miradi hiyo ingejiendesha yenyewe na kutoa gawio. Napongeza mashirika yanayotoa gawio ndio maana halisi ya miradi ya serikali ili kuinua kipato selikalini. Usiwashangae wanaobeza Reli au kununua ndege. Hawaelewi gawio au faida kupata serikali ilitokea bank ya taifa ilitoa gawio ikaleta mzozo na wengine walishanga na wengine waliwaona wafanyakazi wa Bank majuha hivo haikutoke tena kwa miradi ya selikali kuingiza faida bali kuomba fedha serikalini hadi awamu yako nakupongeza sana sana umenifanya nijisikie raha tuliyojifunza ueneshaji serkal kwa kodi na vyanzo vya mapato kwa miradi ya serikali wakati wa ujana wangu leo inafanyika asante mungu akupe maisha marefu na ukamilishe kazi ngumu amin
 
Nimeandika ushauri hu kwa rais ili aufanyie kazi husasan ukaguzi wa mapato kwa vijiji vyote na miradi iliyomo ukaguzi wa ndani . na ukaguzi wa nje ambao unafanywa na COASCO. Hakuna aliounga hoja lmani yangu kwamba wengi wetu uzalendo hatuna au sijaeleweka.
 
  • Thanks
Reactions: VMD
Tutateua sana...
Tutatengua sana...

Kwa mfano, kuna waziri aliteuliwa wakati wa sakata la korosho akiaminika kuwa atafanya vizuri, leo katenguliwa kwa sakata la wafanyabiashara hata kabla ya kufikisha miezi nane.

Mwishowe tutaona wote hawafai.
Suluhisho ni kuwa na Taasisi Imara na siyo Mtu Imara.

Na hii itapatikana kupitia KATIBA MPYA ya Watanzania. Serikali iliyo madarakani pia inahitaji katiba mpya, tukiendelea na katiba hii, tutateua sana, tutatengua sana lakini good achievement nduhu.
 
Tutateua sana...
Tutatengua sana...

Mwishowe tutaona wote hawafai.
Suluhisho ni kuwa na Taasisi Imara na siyo Mtu Imara.

Na hii itapatikana kupitia KATIBA MPYA. Serikali iliyo madarakani pia inahitaji katiba mpya, tukiendelea na katiba hii, tutateua sana, tutatengua sana lakini good achievement nduhu.
Suluhusho pekee Ni Katiba ya Watanzania,hizi teua/tengua hazisaidii na siyo sahihi.Kila ajaye atumie utashi wake kuendesha ofisi ya umma!
Lazima tutengeneze mfumo wa utawala unaowajibika kwa wananchi.Vinginevyo tusitegemee maendeleo kwa mfumo huu.
 
Status
Not open for further replies.
26 Reactions
Reply
Back
Top Bottom