Jerry Ekky
JF-Expert Member
- May 6, 2018
- 1,682
- 5,051
Huwa nashindwa kuelewa kwann had leo lugha yetu mama (kiswahili) haijaanza kutumika kufundishia ktk ngazi zote za elimu hapa TZ kuanzia shule ya msingi had ngazi ya chuo, na si kutumika sule ya msingi pekee km ilivyo hv sasaMhe. Rais John Magufuli,
Pole sana na majukumu ya kazi ngumu ya kuliongoza taifa hili.
Nia ya uzi huu ni kukupa tu mambo ambayo nafsi yangu ingependa sana kuona vinatokea na kufanyika. Naona kama vile nikiviona vimetendeka kikamilifu, nafsi yangu itakuwa na furaha iliyoje kiasi kwamba naona kabisa uwezekano wa kusahau makosa kadhaa ya msingi kabisa niliyoyaona yametendeka katika serikali yako.
Bila kupoteza muda naomba niiache nafsi yangu iorodheshe mambo hayo:
Kwa haraka haraka, nafsi yangu imeongea hayo. Ni matumaini yangu mawazo yangu yatakufikia na utayafanyia kazi yale utakayoona yana manufaa na yanatekelezeka.
- Kujenga mji mpya kule Bagamoyo wa tafiti, sanaa na biashara. Napendekeza mji huo uwe mahususi kwa waafrika wote na uitwe John Magufuli African Renaissance. Mji huu uwe wa kukutanisha vijana na wafanyabiashara wa kiafrika katika kubuni na kujenga mawazo na biashara mpya za kiafrika zitakazokuwa na lengo la kusambaa zaidi ya nchi moja. Lengo hasa liwe kwenye sekta za sayansi na teknolojia, sanaa na viwanda vya ubunifu mpya. Ni kama uiunganishe Silicon Valley na Hollywood. VETA, BASATA, SIDO na vyuo kama cha Kilimo Sokoine na kile cha sayansi cha Arusha cha Mandela watakuwa ndiyo wadau wakubwa katika hili. Sababu moja muhimu ya kujumuisha sanaa kwenye hili ni kwa sababu ikifanyika sawasawa, sanaa inaweza kutumika vizuri kusambaza mawazo mapya mazuri pamoja na huduma na bidhaa zitakatokuwa zinatoka. Pia, mawazo hayatakuwa tu yanaishia kwenye tafiti ila viwanda na mfumo thabiti wa mtandao wa wadau wenye biashara zao Afrika nzima utakuwepo kuchukua mawazo bora na kutengeneza bidhaa, huduma na biashara mpya kabisa. Hili ni muhimu sana. Tulikuwa chachu ya ukombozi wa kisiasa wa Mwafrika, nadhani Afrika inatusubiri tuwe tena chachu ya ukombozi wetu wa kiuchumi na kifikra.
- Kujenga City Park ya kisasa na kuvutia sana itakayosambaa katika bonde la msimbazi, kuanzia huko Kigogo (au popote linapoanzia) hadi kule Jangwani, Magomeni, Kinondoni. Kama kuna mradi naweza kuunga mkono hata tukichukua mkopo kwa wachina huko ni huu hapa. Mji huu bado una changamoto, hauvutii kabisa. Kuna uzi niliwahi kuuandika humu kuhusu wazo hili, nikiupata nitauambatanisha.
- Kujenga kiwanda cha Kiswahili. Hapa namaanisha kufanya utafiti (kama bado haujafanyika) na kutoa misaada kwa makampuni na biashara za kitanzania zitakazotangaza matumizi ya kiswahili kwa njia mbalimbali. Kuna ajira lukuki na mapato yasiyo na kipimo kwenye kiwanda hiki.
- Kutambua sehemu zote zilizotengwa kwa ajili ya jamii na kujenga bustani safi, za kisasa na zitakazokuwa zina watu maalumu wa kuzisafisha muda wote.
- Kufufua na kupanua mpango wa wakati ule wa kujenga shule maalumu za michezo, kama Makongo. Njia pekee ya kupata wanamichezo bora watakaofanya hatimaye na sisi tujivunie mafanikio yao na timu zetu ni kama watatokea katika misingi bora ya elimu ya michezo na hata elimu dunia. Vilevile, tusing'ang'anie sana mpira wa miguu pekee. Kuna michezo mingi, hasa ya mtu mmoja mmoja ambayo inaweza kututangaza sana. Ukifanya hili, ndani ya miaka 15-20 tutakuwa moja ya mataifa bora Afrika katika michezo.
- Kuyaangalia masoko yetu yote ya vyakula na kuyajenga na kuyaboresha. Nadhani ungeanzisha kitengo maalumu kitakachojumuisha watu wa wizara ya kilimo, serikali za mitaa na biashara kuliangalia hili. Masoko yetu inabidi yawe siyo tu masafi na ya kisasa, ila yawe na taa za kutosha na yanafanya kazi masaa 24. Nadhani tujiongeze kidogo kwenye hili, itaboresha sana maisha ya mtanzania.
Nakutakia kila la kheri.