Status
Not open for further replies.
Rais Mahufuli, tumeamua kuandika waraka huu ili tukuoredheshee mambo kadhaa.ambayo sisi wapiga kura wako tunakulilia.

1. Double Standard: Hii serikali yako imekuwa ya double standard ya hali ya juu ambayo haijawahi kuwepo katika serikali za nyuma.

Nitatoa baadhi ya mifano ifuatayo;-

Umetangaza kuwa wale watumishi wote ambao watakuwa wamefoji vyeti hutakuwa na huruma nao, kwa maana hiyo utawafukuza kazi.

Ni kweli maelfu ya wafanyakazi umewafukuza kazi bila huruma, lakini ilipofika wananchi wako tukakueleza kuwa Mkuu wako wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda ni miongoni ya watu waliofoji vyeti na jina lake halisi Mkuu huyo wa Mkoa ni Daudi Bashite, tukashangaa kuona unatwambia kuwa huyo Mkuu wa Mkoa hata kama hajui kusoma A wewe hujali ili mradi tu anakukamatia wauza madawa ya kulevya!

Hilo limetushangaza sana sisi wananchi wako kwa kuwa wapo baadhi ya wafanyakazluliowatimua kazi ambao ni wachapa kazi lakini hiyo "excuse" hijaizingatia na badala yake umewatimua kazi!

2. Dharau kwa wapiga kura wako:

Tumekusikia wakati wa ufunguzi wa barabara za juu pale Ubungo ukisema kuwa wewe huwa husikilizi kelele za wapiga kura wako, kwa kuwa ni wewe mwenyewe ndiyo ulienda Dodoma kuchukua fomu ya Urais na hukushauriwa na mtu yeyote yule!

3.Umekuwa ukisema kuwa katika serikaki yako hutakuwa na mdhaha hata kidogo juu ya watoaji na wapokeaji rushwa.

Tunakumbuka tukio la Aru Meru ambalo ulionyeshwa "video clip" ya Mkuu wako wa wilaya, Alexander Mnyeti akiwapa rushwa madiwani wa Chadema wa jimbo hilo. Badala ya kumweka "benchi" mteule wako huyo ili apishe uchunguzi, ndiyo kwanza ukampandisha cheo na kuwa RC wa Manyara!

Kwa kweli vitendo hivyo vimetukatisha tamaa sisi wapiga kura wako kiasi ambacho tumegundua kuwa kuna baadhi ya wateule wako ambao ni "vipenzi" vyako vikubwa na hata sisi wananchi tutakuja na ushahidi wa wazi kabisa wa wateule hao, kwako ni untoachables!

Kwa kuwa tunajua kuwa huko siku za nyuma ulimtumbua Waziri Nape Nnauye kwa "kosa" tu la kuunda Tume ya kuchunguza tukio la uvamizi wa Clouds Media, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda, akiwa na askari wenye silaha za moto.

4. Kumekuwa na kelele nyingi sana za kukuomba kutokana na matukio ya mfululizo ya watu kupotea, kuuawa na kupotea, basi baadhi ya wateule wako, akiwemo Waziri wa mambo ya ndani, Mwigulu Nchemba na IGP Simon Sirro wajiuzulu au uwatimue kazi ili kupisha uchunguzi wa matukio mengi mno ya mauaji wa wananchi wasio na hatia. Lakini kwa Bahati mbaya sana, umeweka "pamba" masikioni na kutotaka kabisa kutusikiza kilio chetu sisi wapiga kura wako!

Mungu ibariki Tanzania
 
Umenena vyema mkuu, nawaona wa tz wengi wameanza kuchoshwa na yey, siamini kabisa Kuwa huyu ndie magufuli yule kwa kweli, kwa hakika nyakati zinakaribia nyakati mbaya ktk taifa hili, ukiona wanyonge wameanza kutafuta njia za kujikomboa ogopa sana watu hao. Walikuwepo viongozi wa babe lakini waliondoshwa ni suala la wakat tuu.
 
Umenena vyema mkuu, nawaona wa tz wengi wameanza kuchoshwa na yey, siamini kabisa Kuwa huyu ndie magufuli yule kwa kweli, kwa hakika nyakati zinakaribia nyakati mbaya ktk taifa hili, ukiona wanyonge wameanza kutafuta njia za kujikomboa ogopa sana watu hao. Walikuwepo viongozi wa babe lakini waliondoshwa ni suala la wakat tuu.
That is very true.

Yuko wapi Gaddafi wa Libya??

Yuko wapi Hosni Mubarak wa Misri??

Yuko wapi Mugabe wa Zimbabwe??

Yuko wapi Zuma wa Afrika Kusini??

Yuko wapi yule mbabe Waziri Mkuu wa Ethiopia??

Wote hao wameondoka na kuziacha hizo nafasi zao walizokuwa kama wana hati miliki nazo!
 
Najua kitu kinachompa kiburi Rais wetu ni hivyo vifaru vya kijeshi na magari ya washawasha ambayo yamenunuliwa na sisi walipa kodi wa nchi hii

Kwa hiyo inashangaza kuona kuwa watu "tulionunua" magari hayo ya washawasha ndiyo yanaagizwa magari hayo ili kuja kutusambaratisha!

Lakini Rais wetu anapaswa kufahamu kitu kimoja muhimu sana ya kuwa hata hao marais "wababe" walikuwa na vifaa hivyo lakini wamelazimika kuachia nyadhifa zao!
 
Rais Mahufuli, tumeamua kuandika waraka huu ili tukuoredheshee mambo kadhaa.ambayo sisi wapiga kura wako tunakulilia.

1. Double Standard: Hii serikali yako imekuwa ya double standard ya hali ya juu ambayo haijawahi kuwepo katika serikali za nyuma.

Nitatoa baadhi ya mifano ifuatayo;-

Umetangaza kuwa wale watumishi wote ambao watakuwa wamefoji vyeti hutakuwa na huruma nao, kwa maana hiyo utawafukuza kazi.

Ni kweli maelfu ya wafanyakazi umewafukuza kazi bila huruma, lakini ilipofika wananchi wako tukakueleza kuwa Mkuu wako wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda ni miongoni ya watu waliofoji vyeti na jina lake halisi Mkuu huyo wa Mkoa ni Daudi Bashite, tukashangaa kuona unatwambia kuwa huyo Mkuu wa Mkoa hata kama hajui kusoma A wewe hujali ili mradi tu anakukamatia wauza madawa ya kulevya!

Hilo limetushangaza sana sisi wananchi wako kwa kuwa wapo baadhi ya wafanyakazluliowatimua kazi ambao ni wachapa kazi lakini hiyo "excuse" hijaizingatia na badala yake umewatimua kazi!

2. Dharau kwa wapiga kura wako:

Tumekusikia wakati wa ufunguzi wa barabara za juu pale Ubungo ukisema kuwa wewe huwa husikilizi kelele za wapiga kura wako, kwa kuwa ni wewe mwenyewe ndiyo ulienda Dodoma kuchukua fomu ya Urais na hukushauriwa na mtu yeyote yule!

3.Umekuwa ukisema kuwa katika serikaki yako hutakuwa na mdhaha hata kidogo juu ya watoaji na wapokeaji rushwa.

Tunakumbuka tukio la Aru Meru ambalo ulionyeshwa "video clip" ya Mkuu wako wa wilaya, Alexander Mnyeti akiwapa rushwa madiwani wa Chadema wa jimbo hilo. Badala ya kumweka "benchi" mteule wako huyo ili apishe uchunguzi, ndiyo kwanza ukampandisha cheo na kuwa RC wa Manyara!

Kwa kweli vitendo hivyo vimetukatisha tamaa sisi wapiga kura wako kiasi ambacho tumegundua kuwa kuna baadhi ya wateule wako ambao ni "vipenzi" vyako vikubwa na hata sisi wananchi tutakuja na ushahidi wa wazi kabisa wa wateule hao, kwako ni untoachables!

Kwa kuwa tunajua kuwa huko siku za nyuma ulimtumbua Waziri Nape Nnauye kwa "kosa" tu la kuunda Tume ya kuchunguza tukio la uvamizi wa Clouds Media, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dar, Paul Makonda, akiwa na askari wenye silaha za moto.

4. Kumekuwa na kelele nyingi sana za kukuomba kutokana na matukio ya mfululizo ya watu kupotea, kuuawa na kupotea, basi baadhi ya wateule wako, akiwemo Waziri wa mambo ya ndani, Mwigulu Nchemba na IGP Simon Sirro wajiuzulu au uwatimue kazi ili kupisha uchunguzi wa matukio mengi mno ya mauaji wa wananchi wasio na hatia. Lakini kwa Bahati mbaya sana, umeweka "pamba" masikioni na kutotaka kabisa kutusikiza kilio chetu sisi wapiga kura wako!

Mungu ibariki Tanzania

Nani alikwambia ccm inategemea wananchi wapiga kura, anajua kura za wananchi hazitoshi kuiweka ccm madaraki ndio maana hawasikilizi, wananchi hawajawahi kumweka madarakna awasikilize wa nn wakat aliingia kwa juhudi binafsi kwa kutunia mgongo wa tume na police.
 
Najua kitu kinachompa kiburi Rais wetu ni hivyo vifaru vya kijeshi na magari ya washawasha ambayo yamenunuliwa na sisi walipa kodi wa nchi hii

Kwa hiyo inashangaza kuona kuwa watu "tulionunua" magari hayo ya washawasha ndiyo yanaagizwa magari hayo ili kuja kutusambaratisha!

Lakini Rais wetu anapaswa kufahamu kitu kimoja muhimu sana ya kuwa hata hao marais "wababe" walikuwa na vifaa hivyo lakini wamelazimika kuachia nyadhifa zao!
 
Nani alikwambia ccm inategemea wananchi wapiga kura, anajua kura za wananchi hazitoshi kuiweka ccm madaraki ndio maana hawasikilizi, wananchi hawajawahi kumweka madarakna awasikilize wa nn wakat aliingia kwa juhudi binafsi kwa kutunia mgongo wa tume na police.
Ni kweli kabisa Mkuu Makinikia Halisi

Kutokana na kauli zake anazozitoa kwenye majukwaa ya kisiasa katika siku za karibuni, hana tena unyenyekevu wa kuwa ipo siku atakuja kuwaomba tena kura!
 
Kwa kuwa kiburi anachowapa huyu Rais wetu hao wateule wake, kinafanya wajione "miungu-watu"
 
Nchi za ulaya na marekani siku zote huwa hazina urafiki na nchi yeyote ,hasa za Afrika ambazo huzuia maslahi yao.

Nchini Tayari tumezuia maslahi ya nchi nyingi za ulaya na marekani ,hasa Canada .ukifika katika hatua hii kama kiongozi mkuu lazima ufanye lobbying ya kutosha kwa watu wako wa ndani kwani ndio watakaokusimamia dhidi ya wavamizi wa nje wanaotafuta sababu ya kukuondoa.

Ila usipokuwa na mahusiano mazuri na makundi ya kisiasa ,civil societies,na wananchi kadhaa mazingira magumu saana yanatengenezwa sababu ni hawa watu wako wandani ,unaowachukia na kuwaona maadui ndio siku xote huamua kushirikiana na maadui wa nje kupitisha agenda yao ili maslahi yao yatangulie.

Siku zote unapoharibu nje ,imarisha ndani zaidi,imarisha upendo zaidi,demokrasia zaidi,usawa zaidi watu wako wakikupenda adui wa nje hana nafasi ,watu wako ndio popular sovereignty ,watakutetea.

Aliyepita alikuwa mjanja ,aliimarisha ndani na nje pote ,alipendwa pote nje na ndani,walikufa watu ,waliuwawa watu ulisikia kelele zaidi ya hizi unazosikia,uliona BBC imeandika sababu watu waliamini ni bahati mbaya,sababu ya upendo wake, demokrasia take,usawa wake.

Ila angalia Leo Jambo lolote likitokea,utasikia kelele watu wakipiga ,utasikia BBC imetangaza unajua kwanini sababu wanajihami dhidi ya mwenendo wako yasije yakatokea mengi kesho na na makubwa zaidi ya haya sababu wanajua sio bahati mbaya ila ni tabia yako na mwenendo wako.

Halii hii hukaribisha maadui zaidi na zaidi,hupata mwanya ,Na hupelekea hata makosa usiyoyafanya mengine kuonekana umeyafanya sababu wanajua sio bahati mbaya ,ni makusudi ndio mfumo wako.
 
Wana bodi, nadhani mnaendelea vyema na mapumziko ya mwisho wa wiki....

Tangia serikali ya awamu ya tano ilipoingia madarakani chini ya raisi JPM, hakika kumekuwa na mengi yaliyoibuka kwenye nyanja za kiuchumi, kisiasa kitamaduni n.k.

kama ilivyo kawaida ni ngumu kumridhisha kila mwanachi, lakini walau utendaji wake ulionekana na umakini mkubwa sana hasa pale mwanzoni jinsi alivyokuwa akidili na mambo ambayo yalionekana yanalirudisha taifa letu nyuma mfano kutumbua viongozi waziwazi bila kujali ni nani ama alishawahi kuwa rafiki yake, mfano mzuri ni Charles Kitwanga alivyotumbuliwa, ilionesha ni jinsi gani hamwangalii mtu usoni.....

Ghafla mambo yakaja kubadilika, kukaibuka minong'ono mingi kila kona ya nchi kuhusu demokrasia, uhuru wa maoni, vyombo vya habari, mauwaji/utwekwaji wa raia, ugumu wa maisha, kudorora kwa shilingi yetu n.k huku lawama nyingi zikielekezwa kwenye serikali yake.....

je ni huyu ambaye tuliaminishwa kuwa ndiye mkombozi/mtetezi wa taifa tumempata ? je ukipata wasaa wa kukaa nae na kujadili mambo kadha kuhusu ustawi mzima wa taifa letu utamshauri nini ?

tatizo liko wapi ? viongozi wake wanamwangusha ? sera za ccm ni ngumu kutekelezeka ? hana washauri sahihi ? hazingatii/hapokei ushauri ?
 
Anatakiwa awe Situational leader. Nguvu nyingi zimetosha sasa, kama ni wezi keshawachapa.kama ni elimu ya matumizi sahihi ya fedha tumeshaanza kupractise,
Nidhamu kwenye ofisi za umma imerudi.
Vijana wanajituma sasa.
MWAMBIE ATUPE NAFASI TUTUMIE AKILI ALIZOTUPA MUNGU.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom