Status
Not open for further replies.
Hivi kitu gani kinamfanya magufuli yeye kutokukaa pembeni????

ILILIINGIZA, ANALIINGIZA NA ATALIINGIZA SN HASARA TAIFA

1. Alikamata kiholela samaki wa magufuli kesi tumeshingwa kwa ujinga wa mtu mmoja

2. Alivunja mkataba wa ujenzi kijingajinga kabisa tumeshindwa kesi

3. Alijiuzia nyumba za serikali

4. Anavunja katiba na sheria za nchi

5. Anavunja sheria za manunuzi na kujipangia matumizi ya raslimari za taifa mfano kujijengea uwanja wa ndege chato, kujinunulia bomberdier kwa maslahi yake binafsi...


MTU WA HIVI ANAFAIDA GANI KWA TAIFA? KWA NN ASIKAE PEMBENI YEYE KWANZA????
 
Amani iwe nanyi wadau.
Natumaini mu wazima na mnaendelea vizuri na majukumu yenu Ni vizuri pia kabla ya yote nikatoa pole kwa watanzania wote walioguswa na tukio la kinyama dhidi ya kiongozi wa upinzani Bw Tundu Lissu.

Nikiwa sijaonekana kitambo sana kwenye jukwaa hili leo napenda kusema kuwa kwa yanayoendelea nchini Tanzania kwa sasa, imebidi niamue kujitokeza tu na labda niamue kutoa mchango wangu wa mawazo hata kama hayatasikilzwa lakini nikiwa na Imani kuwa haya mawazo kwa kuwa ni mazuri na yanajenga basi yatasikilizwa na kufanyiwa kazi.

Sipendi kwenda kwenye hili la Lissu ila kwa kuwa nia yangu ni ya kumsaidia Mh Raisi naona kwa hili la Lissu linaweza kupata utatuzi wake humuhumu.

Kwanza nianze na maana halisi ya wasaidizi wa Mh. Raisi ni kina nani hasa- Kama hamjui kwa Tanzania hawa wanaanzia na baraza la mawaziri ambalo kisheria na kikatiba ndicho chombo kilichopewa mamlaka ya kumshauri Mh. Raisi juu ya mambo yote ya nchi. Kwa hapa Tanzania washauri wengine ni mwanasheria Mkuu wa Serikali pamoja na wasaidizi wengine wa Mh Raisi.Wengine ni viongozi wa vyombo vya ulinzi na usalama.

Kwa nini leo nimeamua kuwaelezea hawa watu na kuongea na hawa watu????

Hawa ndo watu wa kumsaidia kumwambia ukweli Mh.Raisi, ukweli wa kiuchumi, ukweli wa kisiasa hata kijamii. Bila shaka kwa hali ilivyo sasa napenda kusema kuwa wasaidizi wa raisi hamfanyi wajibu wenu ipasavyo na inapoelekea nchi itaenda kuanguka chini ya raisi Magufuli. Naomba nielezee kwa mifano hili suala.

KIUCHUMI.

Pamoja na Mh Magufuli kuwa na nia njema kwa nchi hii kiuchumi napenda kusema kuwa mmekuwa mnapotosha vibaya sana Mh. Raisi kiuchumi kiasi kwamba nchi imekuwa ikipata matokeo hasi zaidi kiuchumi zaidi ya chanya.Swali langu kwenu ni kwa nini mmeshindwa kumshauri Mh Raisi juu ya kuanza na njia ya kupiga marufuku vitu wakati mlishaona hili lilianza kuleta matokeo hasi???

Kwenye sukari wasaidizi wa raisi mlipaswa kujifunza sana kwenye suala hili kwa sababu tangu Mh.Raisi apige marufuku uingizaji wa sukari bei ya sukari haijaweza kushuka kuwa kawaida hadi leo hii. Swali langu kwenu hamkujifunza kitu kwenye suala hili???? Hamjui kuwa bei ya sukari hadi leo haijawa kawaida na hili limepelekea nia nzuri ya Mh Raisi ishindwe kuonekana hapa???

Sio tu kwenye sukari, mlishindwa kumshauri Mh Raisi vizuri kwenye pesa kuondolewa kwenye benki za biashara na hadi leo hali ya kifedha imekuwa mbaya sana nchini hasa kwenye mzunguko na upatikanaji wa mikopo.

Kubwa zaidi mliloshindwa kumshauri Mh. Raisi ni hili la Acasia. Hivi ni nani aliwaambia kuwa wazungu unapambana nao kwa mabavu na sio akili? Hamjaona hili suala la Acasia linamuweka Raisi na nchi sehemu mbaya sana kiuchumi? Hivi hamkuona haja ya kumshauri Mh Raisi angeanza na kubadili sheria tena at least kwa kujifanya anawashirikisha hao wawekezaji wa madini alafu badae kunatokea maoni ya wadau ndo tunafikia kurekebisha sheria kwa muktadha tunaoona sie??? Hamkuona hi indo ilikuwa njia sahihi ya kudeal na suala la madini bila kucreate tension kwa dunia juu ya hali ya uwekezaji Tanzania???

Mmemuacha Mh Raisi ametumia nguvu kubwa kudeal na issue ya madini kwa kuzuia usafirishwaji wa makinikia kiasi ambacho kimeleta picha mbaya sana kiuwekezaji hapa kwetu. Kusema kweli mmeiweka Tanzania sehemu mbaya sana kiuwekezaji na pia hata hifadhi yetu ya pesa za kigeni itaathilika sana kwa kuwa kuondoka kwa Acasia msidhani itakuwa raisi kwa muwekezaji mwingine kuja Tanzania kama amefikiria vizuri kwenye kucalculate risk za kuinvest Tanzania. Kwa nchi yenye miaka mingi ya uhuru hii haikuwa approach tuliyotakiwa kuitumia kwenye kudeal na hawa ngozi nyeupe.

Mnamuacha raisi atamke juu ya vita vya uchumi hadharani. Hivi mmeshindwa kumshauri Mh Raisi juu ya madhara ya nchi kutangaza hadharani vita dhidi ya maslahi yao kiuchumi?? Au mnataka siku ya mwisho nchi itapata nini??? Mnadhani kama nchi itafaidika chochote kwenye vita dhidi ya maslahi ya kiuchumi ya wanamagharibi au wanamashariki??? Hamuoni Zimbabwe?? Hamuoni Venezuela??? Hamuoni Libya na Syria???? Mnataka Magufuli aje kukumbukwa kwa sifa mbaya zaidi????

KISIASA.

Mmeshindwa kumshauri Mh Raisi vizuri kiuchumi na mbaya zaidi hadi kisiasa mnaharibu kwenye kumshauri Mh. Raisi vizuri kiasi ambacho leo adui akitumia siasa kutuvuruga anatumaliza kesho asubuhi tu. Hivi kulikuwa na haja gani ya kumshauri raisi kuwafungulia mashtaka wapinzani kila wanapomsema??? Hamuoni hili linawatengenezea huruma kwa wananchi na siku ya mwisho wananchi kuwasikiliza na kuwaamini wao zaidi kuliko wanavyoiamini serikali au Raisi wao???? Mmeshindwa nini kumshauri Mh. Raisi kuimalisha kitengo cha propaganda na uenezi cha chama chake ili kiweze kujibu kila shutuma dhidi ya Mh.Raisi na siku ya mwisho kuanzia wananchi hadi wageni waone kuwa ni game za kisiasa tu????? Hamuoni kutumia vyombo vya dola kujibu hoja za kisiasa zinamuharibia raisi kimataifa n ahata kuharibu taswira ya nchi kimataifa????

Kwako Mh. Raisi, bado nakuamini sana, kama nilivokupigania kwenye uchaguzi sitaacha kukuigania kwa nia ya kutaka uongoze vizuri. Ila naomba uchague wasaidizi wa uhakika wanaojua dunia inavyoenda na figisu zake na mwisho wape uhuru wa kukushauri kwa weredi.

MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Wewe kama ni Raiya wa Tanzania na si hawa wingine waliijipenyeza na kujivika Utz humu kwa nia ovu mbili moja ya kutambua fursa mbali mbali za kwetu. Ya pili kumanipulate na ku spin kila jema linaloongekewa au linalotreand kwa lengo la kuchafua nchi yetu na hasa Mkuu wa nchi

Nakushauri geuza thread yako hivyo hivyo ufanye updates iwe unauelekeza kwa Washauri wa wezi wanaotuibia rasilimali zetu. Ielekeze pia na kwa wapinzani ukiwashauri wamuunge mkono Mkuu wa nchi kwa mema anayofanya

Waelekeze pia wapinzani wawashauri wakuu wao wasiminye uhuru wa wanachama wao kugombea nafasi za juu
 
Hivi kitu gani kinamfanya magufuli yeye kutokukaa pembeni????

ILILIINGIZA, ANALIINGIZA NA ATALIINGIZA SN HASARA TAIFA

1. Alikamata kiholela samaki wa magufuli kesi tumeshingwa kwa ujinga wa mtu mmoja

2. Alivunja mkataba wa ujenzi kijingajinga kabisa tumeshindwa kesi

3. Alijiuzia nyumba za serikali

4. Anavunja katiba na sheria za nchi

5. Anavunja sheria za manunuzi na kujipangia matumizi ya raslimari za taifa mfano kujijengea uwanja wa ndege chato, kujinunulia bomberdier kwa maslahi yake binafsi...


MTU WA HIVI ANAFAIDA GANI KWA TAIFA? KWA NN ASIKAE PEMBENI YEYE KWANZA????


Ni kwa sababu alichaguliwa na asilimia kubwa ya watanzania, Na hakuna kiongozi perfect Duniani..

The best prez in Africa
 
Take this...sbb umeniudhi vibaya,:(:(:eek: nilidhani unaandika mambo ya msingi kumbe pumba pumbaf..

Ushauri wako & marks.

1: Kiuchumi = 00%

2: Kisiasa = 5%

Poorest advice.. Hapo kwenye Acacia wezi wakubwa unawatetea? Rubbish, ndio hovyo kabisa umeongea.. I deduct more -10%, off. :(:(:oops::oops::(:(:(
 
mie naona kila wizara iwe na independent body ya directors toka nchi mbali mbali,WENYE ELIMU,EXPIRIENCE AND EXPOSURE.................................utawalipa hela nyingi ndio,lakini utatumia utaaalamu wao kumove forward.
 
muda si mrefu atagombana na WAZANZIBAR anataka kuchukua mapato yao ya viza,,Sijui kashauriwa na nani maana kwenye hilo kama muungano haukuvunjika basi utayumba sana
 
Sizonje ndie anaewashauri washauri wake namna ya kumpa ushauri

One term

Sent using North Korean Hydrogen Bomb
 
Kuna uwezekano wa 99% kwamba waliovamia clouds ndio waliofanya jaribio la kumuua Lissu. Siro alipewa u-IGP ili kikosi cha bashite kiweze kutekeleza matendo yake bila bugudha popote nchini. Amani ya nchi hii inaondolewa na bashite.
Acha ujinga usipende kuongea vitu ili mradi umeongea ,una uthibitisho na unachoongea?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna uwezekano wa 99% kwamba waliovamia clouds ndio waliofanya jaribio la kumuua Lissu. Siro alipewa u-IGP ili kikosi cha bashite kiweze kutekeleza matendo yake bila bugudha popote nchini. Amani ya nchi hii inaondolewa na bashite.
Bashite umeishajulikana unajisikiaje?
 
Awali ya yote nawapa pole watanzania na wapenzi wote wa amani na demokrasia Tanzania. Chadema na wananchi wote waliogubujikwa na kushtushwa na shambulio lililompata Mh Tundu Lissu.

Mimi nataka kutoa maoni na sina shaka yatamfkia bwana mkubwa Raisi Dr.Magufuli.

Raisi,mimi sina chama,ila ni mkerketwa na mshabiki namba moja kwako kutokana na ari mpya na uzalendo ulionao juu ya Tanzania.

Kusema ukweli,Tanzania imechezewa na kuibiw a sana. Nakusapoti kile unachofanya na usirudi nyuma.
Lakini pia,katika tendo jema unalofanya mengine unarudi nyuma. Sitaki kukuhukumu kwa jambo lolote lakin junanmanbo yako wazi.

Suala la upinzani Tanzania limekuwa kama uadui. Upinzani sio sawa mchezo wa miguu au kuonekana wewe ni bora zaid ya yule. Tafsiri niijuavyo ya upinzani ni kusaidiana na kuelekezana pale mmoja anapokuwa anakosea kwa hoja za msingi na zenye maslahi chanya kwa Tanzania.

Upinzani sio mangumi,matusi na kejeli kaka watanzania wengi wanavyofanya.Lazima tutangulize maslahi mbele ya nchi bila kupepesa macho au kuangalia pembeni.

Kumekuwa na siasa katika mashule na kazini nk. Vikundi cya chama mashuleni,huku tunatafuta nini? tumeenda kusoma au kufanya siasa. Pamoja hii sio hoja yangu ya msingi sana naona ni wakati kutenganisha siasa na weledi na pia kutoa siasa makazini na mashuleni.

Mh Raisi Magufuli nikufahamishe tu kuwa mkuu,upo katika vita kali sana ya uchumi. Wazungu na wachina na waarabu huko wanakuangalia sana kwa macho mabaya.Hizi ghasia zinazotokea hapa na pale unaweza ukawapa mwanya mkubwa sana wa kuharibu amani iliyopo.
Pia wapo watanzania wengi ambao hawakutaki na wengine wanaona umeleta kauzibe. Nguvu yake unaweza kudharau lakini itapeleka nchi kubaya.
Tanzania ni nchi ambayo imekuwa tulivu na kipekee sana kwa muda mrefu. Kwasbabu hatukuwa tumejitambua. Huko mbele tutarajie misukosuko kwa mfano kibiti ni mfano halisi wa watu wa nje wanaotaka kuharibu amani yetu. Hawa watu wapo wazungu na middle eastern countries na ndio wafadhili wakuu.

Mh Raisi huu ni mchezo wa akili na tumia akili kuwazidi na ujue utapita wapi kabla ya matukio na baada. Wapo hawatakuelewa lakni naamini ipo siku.
Nakushauri kuongea na upinzani na kuwaweka mbele katika vita hii. Usifanye vita hii pekee yako. Hata ukifa leo,Tanzania itarudi kulekule kutokana na kwamba hujatuonyesha njia na haujatufumbua macho au kutusaidia.Ni wewe tu ndio unashika tochi na kusonga mbele.

Nafahamu nia yako ni njema. Najaribu kufikiri kuwa huna wasaidizi wanaona mbali zaidi ya matumbo yao.
 
Unakaaje na wapinzani ambao wanachotwa na haohao maaduizetu wa kiuchumi, wanaomba taarifa kutoka kwa wanyonyaji ili wazitumie kukwamisha mikakati ya taifa kujinasua katika hii mitego tuliyonasa? Kuondoa hili la wanasiasa kuzuiwa kuitisha mikutano, Magufuli yuko sahihi 100%. Upinzani wamethibitisha kuwa hawana hata chembe ya uzalendo. Sad!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom