Status
Not open for further replies.
Mheshimiwa Rais mteuliwa, kwa heshima na taadhima hili ni ombi binafsi kwako.

Nnaomba uhakikishe huyu mrembo wa ACT Bi Anna Mughwira unamuingiza bungeni na unampa wadhifa anaostahiki, huyu mama ni kichwa adhyim na adim kabisa.

Nimemfatilia mikutano yake mingi sana ya kampeni, anatoa vitu kichwani utafikiri ana word processor inayopanga na kuchuja anachokizungumza kutoka kichwani bila kusoma.

Halikadhalika leo kanifurahisha sana alipostukizwa na kutoa hotuba pale Diamond, ilikuwa fupi na imelenga points zote nzuri na ameeleweka vyema kabisa.

Anna heko sana na nitakuunga mkono katika siasa zako.


Slaa ndo wa muhimu sana kuriko wote,
 
Hoja ni nzuri lakini akikumbukia Mbatia alivyowageuka, CCM wenzake hawatakubali. After all nafasi ni 10 tuu na kuna wana CCM wengi waliokupigania chama. Kwani kwa kura zake 98,000 hawapewi hata kiti kimoja cha wabunge wa viti maalumu? Wakipewa achukue hicho hicho
 
Huyu mama nimemkubali sana na sijui kwanini sikuwahi kumsikia kabla ya uchaguzi! Naunga mkono hoja ila natamani ateuliwe kuwa mbunge tuu na asipewe uwaziri maana ndani ya serikali ya ccm anaweza akaonekana tofauti kutokana na mfumo.
 
haikuwa lazima kuchangia kama kungekuwa na kitufe cha like...
binafsi nazani nafasi ya ubunge tu inatosha
 
Kila chama kilikuwa na ilani yake, sasa kusema ampe ubunge then cheo anachostahili Serikalini una maana gani? Je akiwa serikalini atakuwa anatekeleza ilani ipi kati ya ile ya ACT ya kwake na hii yenu ya CCM?

Mkuu anaweza pewa ubunge then akawa Mwenyekiti wa kamati za bunge moja muhim...just wazo
 
Mama Anna ni mtu wa Singida? Huwa naona wana Singida wana akili sana, based from niliosoma nao na ninaofanya nao kazi. She is the Best. Wampe nafasi atumikie Taifa
 
Mkuu anaweza pewa ubunge then akawa Mwenyekiti wa kamati za bunge moja muhim...just wazo
Ukiondoa uwenyekiti wa kamati ya PAC, huwezi kupewa uwenyekiti wa kamati yoyote ile ya kudumu ya Bunge unless uwe na undugu wa kichama na CCM yenyewe.
 
mbagala mipango jamaa pengine kapelekwa sokoni.
maana rahisi mtu kakaa kimya
nini maana yake.
hawa wabongo wako tayari kupoteza usimamizi kwa kitu kidogo tu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom