Mheshimiwa Rais mteuliwa, kwa heshima na taadhima hili ni ombi binafsi kwako.
Nnaomba uhakikishe huyu mrembo wa ACT Bi Anna Mughwira unamuingiza bungeni na unampa wadhifa anaostahiki, huyu mama ni kichwa adhyim na adim kabisa.
Nimemfatilia mikutano yake mingi sana ya kampeni, anatoa vitu kichwani utafikiri ana word processor inayopanga na kuchuja anachokizungumza kutoka kichwani bila kusoma.
Halikadhalika leo kanifurahisha sana alipostukizwa na kutoa hotuba pale Diamond, ilikuwa fupi na imelenga points zote nzuri na ameeleweka vyema kabisa.
Anna heko sana na nitakuunga mkono katika siasa zako.
mtu wa kukimbia matatizo na kuzira hafai. alikimbia roma, akakimbia ccm, amekimbia familia, amekimbia CDM na juzi hapa kakimbia nchi na uchaguzi.Mimi namtaka slaa,
masuala ya Zanzibar ni ya kikatiba, waliridhia wenyewe kuwa na Serikali ya umoja wa kitaifa.Kwani Maalim Seif anatekeleza ilani ipi kama Makamu wa Rais wa Zanzibar?
apewe tu kwani kazi aliyotumwa na ccm kumaliza kafulila imekwisha.Kwani Maalim Seif anatekeleza ilani ipi kama Makamu wa Rais wa Zanzibar?
Kila chama kilikuwa na ilani yake, sasa kusema ampe ubunge then cheo anachostahili Serikalini una maana gani? Je akiwa serikalini atakuwa anatekeleza ilani ipi kati ya ile ya ACT ya kwake na hii yenu ya CCM?
Ukiondoa uwenyekiti wa kamati ya PAC, huwezi kupewa uwenyekiti wa kamati yoyote ile ya kudumu ya Bunge unless uwe na undugu wa kichama na CCM yenyewe.Mkuu anaweza pewa ubunge then akawa Mwenyekiti wa kamati za bunge moja muhim...just wazo
Slaa ndo wa muhimu sana kuriko wote,