Maoni: Tupendekeze Salaamu /Maakizi ya Kitaifa ili kuimarisha umoja na uzalendo.

JFK wabongo

JF-Expert Member
Aug 11, 2015
3,887
3,187
Wadau naamini wote tunafahamu umuhimu wa salaamu. Salamu ni kiashiria cha umoja na uungwana. Ni kawaida kusikia watu wenye vinyongo kugoma kusalimiana au watu kugoma kumsaidia mtu asiye na kawaida ya kusalimia. Salamu hujenga udugu na urafiki. Hata tuwapo kwenye hafla za kitaifa pia tunahitaji kusalimiana.

Changamoto inayotukabili kama taifa ni kuwa lugha ya kiswahili haina salamu moja kwa makundi yote. Utasikia mtu anajikanyanga kwa kusema 'wakubwa shikamoni, vijana wenzangu mambo vipi, wale ninaowazidi umri marahaba. Ni kawaida pia kusikia mtu anatumia maakizi/ salaamu kama 'Tumsifu Yesu Kristu, Bwana Asifiwe, Salama Aleyekum, CCM Oyee, Chadema Vema, Haki sawa n.k. Maamkizi haya siyo jumuishi kwani kuna watu hawana vyama wala salamu za dini zao hazisikiki popote kwenye hafla hizi. Watu hawa huhisi wanasahaulika au hawapewi umuhimu.

Kwa mtazamo wangu salamu za vikundi vikundi hazitujengei uzalendo wala umoja wa kitaifa. Hivyo basi napendekeza tuwe na maamkizi ya kitaifa. Hii itasaidia kuimarisha uzalendo na utambulisho wetu. Naomba JF tuwe wakwanza kujenga uzalendo. Tujadiliane kuhusu maamkio/salamu ya kitaifa. Je, tuendelee na salamu hizi za vikundi vikundi? Au tupate salamu ya taifa ambayo itatumika kwa watu wa vyama vyote, dini zote na makabila yote tuwapo kwenye hafla za kitaifa?
Kwa mantiki hiyo ni salamu gani (miongoni mwa zilizopo au Mpya) ambayo unafikir itawatuunganisha watanzania wote tuwapo kwenye shughuli za kitaifa? Maoni yenu tafadhali!
 
Peleka China ukomunisti huo. Kila mmoja ni ndudu ndugu, ndugu! Walichokifanya Watanzania kushusha hadhi ya kila mmoja-by CHarles Njnjo, former AG of Kenya. Ukisomea sheria UDOM unataka uwe na hadhi sawa na Havard school of law graduate! Peleka china hiyo itakubalika. Tumezoea akili ndogo kuongoza akili kubwa, naona unataka itambae kote.
Usinichukie huo ndio msimamo wangu.
 
Peleka China ukomunisti huo. Kila mmoja ni ndudu ndugu, ndugu! Walichokifanya Watanzania kushusha hadhi ya kila mmoja-by CHarles Njnjo, former AG of Kenya. Ukisomea sheria UDOM unataka uwe na hadhi sawa na Havard school of law graduate! Peleka china hiyo itakubalika. Tumezoea akili ndogo kuongoza akili kubwa, naona unataka itambae kote.
Usinichukie huo ndio msimamo wangu.
Mimi simaanishi hizo hadhi. Kama mheshimiwa aendelee kuitwa mheshimiwa. Ila huyo mheshimiwa anapotusalimia akiwa kwenye jukwaa la kitaifa basi asalimie kwa salamu moja na hadhira iitikie kwa umoja. Kama ni people's power basi iwe hiyo tu.
 
Mimi simaanishi hizo hadhi. Kama mheshimiwa aendelee kuitwa mheshimiwa. Ila huyo mheshimiwa anapotusalimia akiwa kwenye jukwaa la kitaifa basi asalimie kwa salamu moja na hadhira iitikie kwa umoja. Kama ni people's power basi iwe hiyo tu.
Kwenye vyama sawa, lakini nje hapana!
 
I do not buy that idea all together! These are petty things of no importance to our well being as a nation!
How can we foster the national well being without unit? How can we unite if we customise on our differences? For your information, the world has discovered the beauty of Mwalimu Nyerere's ideas on Secularism. America, for instance, is now mobilising Interfaith Gathering. For our case, the religious leaders have a similar movement called Interfaith Dialogue. They hold meetings and we have watched them several times holding football matches. Can you ask yourself how tricky it is to address such gatherings? Don't you think this is a clever idea to support the goodwill of our religious leaders?
 
How can we foster the national well being without unit? How can we unite if we customise on our differences? For your information, the world has discovered the beauty of Mwalimu Nyerere's ideas on Secularism. America, for instance, is now mobilising Interfaith Gathering. For our case, the religious leaders have a similar movement called Interfaith Dialogue. They hold meetings and we have watched them several times holding football matches. Can you ask yourself how tricky it is to address such gatherings? Don't you think this is a clever idea to support the goodwill of our religious leaders?
Tena usinambie hawa wanajiita viongozi wa dini,
 
Salamu hiyo ikibuniwa misamiati yake wasifundishwe kina mgambo,madereva na wale wanaofurahi kila siku.

Sent from my TECNO-Y3 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom