msovero
JF-Expert Member
- Jun 30, 2019
- 839
- 1,472
Kwa mtazamo wangu naona haya ni maeneo ya muhimu yanayopaswa kufanyiwa marekebisho ili kuepusha changamoto zinazojitokeza wakati wa kutoa ajira.
1. Unganisheni mfumo wenu na database ya NECTA kwakuwa wao ndio wenye taarifa zote za kielimu za waombaji basi hii itasaidia pale ambapo mwombaji atagushi namba ya kidato cha nne wakati wa kuomba ajira mfumo kumkatalia moja kwa moja.
2. Kwakuwa waombaji wa hizi ajira ni wengi basi kuna haja ya kuongezea server zenu ili iwe rahisi kupokea maombi ya waombaji wengi kwa muda mfupi na hivyo kuwapunguzia hadha na usumbufu wa kimtandao wanaopata waombaji wakati wa kutuma maombi.
3. Unganisheni mfumo wenu wa ajira na database ya NIDA ili kuzuia udanganyifu wa waombaji wanaogushi au kutumia NIN za ndugu zao kuomba ajira.
4. Rekebisheni kipengele cha kujaza majina maana mfumo unahitaji majina matatu ilihali waombaji wengine wanatumia majina mawili kwenye vyeti vyao vya kitaaluma.
5. Wekeni mfumo wa kuweza kutambua (detect) masomo ya waombaji kwenye vyeti au au hati zao za matokeo(transcript). Hii itasaidia kuzuia udanganyifu wa masomo unaofanywa na waombaji. Mfano mtu kujaza Economics badala ya somo lake la kiingereza alilobobea.
Mwisho, hakuna umuhimu tena wa kuendelea kutumia kanzi data (database) ya maombi yaliyopita kwa sababu tayari imegubikwa na dosari nyingi kama zilivyo bainishwa na kuibuliwa na wadau mbali mbali. Ni vyema kuufanyia mfumo maboresho kwanza kisha kufungua upya dirisha la kutuma maombi ili kukamilisha ajira 5000 zilizosalia kama ilivyokuwa ahadi ya mheshimiwa Rais ya kuajiri walimu 13,526.
Mengine yataongezewa na wadau
1. Unganisheni mfumo wenu na database ya NECTA kwakuwa wao ndio wenye taarifa zote za kielimu za waombaji basi hii itasaidia pale ambapo mwombaji atagushi namba ya kidato cha nne wakati wa kuomba ajira mfumo kumkatalia moja kwa moja.
2. Kwakuwa waombaji wa hizi ajira ni wengi basi kuna haja ya kuongezea server zenu ili iwe rahisi kupokea maombi ya waombaji wengi kwa muda mfupi na hivyo kuwapunguzia hadha na usumbufu wa kimtandao wanaopata waombaji wakati wa kutuma maombi.
3. Unganisheni mfumo wenu wa ajira na database ya NIDA ili kuzuia udanganyifu wa waombaji wanaogushi au kutumia NIN za ndugu zao kuomba ajira.
4. Rekebisheni kipengele cha kujaza majina maana mfumo unahitaji majina matatu ilihali waombaji wengine wanatumia majina mawili kwenye vyeti vyao vya kitaaluma.
5. Wekeni mfumo wa kuweza kutambua (detect) masomo ya waombaji kwenye vyeti au au hati zao za matokeo(transcript). Hii itasaidia kuzuia udanganyifu wa masomo unaofanywa na waombaji. Mfano mtu kujaza Economics badala ya somo lake la kiingereza alilobobea.
Mwisho, hakuna umuhimu tena wa kuendelea kutumia kanzi data (database) ya maombi yaliyopita kwa sababu tayari imegubikwa na dosari nyingi kama zilivyo bainishwa na kuibuliwa na wadau mbali mbali. Ni vyema kuufanyia mfumo maboresho kwanza kisha kufungua upya dirisha la kutuma maombi ili kukamilisha ajira 5000 zilizosalia kama ilivyokuwa ahadi ya mheshimiwa Rais ya kuajiri walimu 13,526.
Mengine yataongezewa na wadau